google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 17, 2016

Jinsi Ya Kutengeneza Tomato Souce.

No comments :
Mara kadhaa nimekuwa nikileta Makala mbalimbali ambazo zinakupa hamasa tu ila Makala ya leo ni pesa mkononi. Pesa mkononi ndiyo ambayo kila mtu anahitaji. Pia nimeamua kukuletea makala haya ili tuendane sawa na Tanzania ya viwanda.

Najua inawezekana kabisa kila mtu kuwa na kiwanda, unashangaa wala usishangae maana huo ndio ukweli maana kila kitu kinapatikana kiurahisi katika mazingira yetu.

Unajua kuwa mikono yako ndiyo itakayokupa pesa? Kama hufahamu basi nimekuja kukujuza ni kivipi utatumia mikono yako ili uweze kuwa tajiri.

Yafuatayo ndiyo mahitaji ya kutengeneza tomato source.

1. Nyanya kilo 1.
2. Vitunguu maji viwili.
3. Vinegar vijiko 3 vya chai.
4. Sukari vijiko 2 vya chai.
5. Chumvi kijiko kimoja cha chai
6. Maji ya moto kikombe kimoja cha chai.
7. Mafuta ya kula vijiko 7 ya vyakula.

Haya ndiyo mahitaji ya kutaka kutengeneza tomato souce, hata hivyo kama unataka kutengeneza zaidi ya hapo unatakiwa kuongeza uwiano wa mahitaji hayo.

JINSI YA KUTENGENEZA TOMATO SOURCE.

HATUA YA KWANZA.

a) Menya nyanya na vitunguu kisha vikate vipande vidogo vidogo.

b) Tumia Brenda kusaga mchanganyiko wako.

c) Anza kuweka malighafi namba 1 hadi namba 4 katika brenda yako kutokana na ratio (uwiano ) uliopewa hapo juu. Saga kwa dakika kadhaa hadi uone imetokea rojo laini.

HATUA YA PILI.

a) Tumia sufuria yenye nafasi kupika mseto huu.

b) Weka sufuria yako jikoni tia mafuta ya kula acha yachemke kisha mwagia mseto wako na kisha uanze kukoroga kwa dakika 30 kuelekea upande mmoja huku ukichemka.

c) Baada ya hapo epua mseto huo utakuwa tayari imeshakuwa tomato funga vizuri na kisha peleka sokoni.

Mpaka kufikia hapo wewe Tajiri, na mafanikio makubwa ambayo yatakuwa upande wako endapo utakuwa umeamua kuondokana na umaskini kwa njia ya kutengeneza vitu mbalimbali kwa ajili ya kuuza.

Nikusihi uendelee kufuatana nami katika Makala zijazo ili tuweze kufika mahali ambapo tunatamani kufika.? Endelea kufuatana nasi hapa dira ya mafanikio kwa masomo mengine yanayokuja.

Imeandikwa na Afisa mipango; Benson Chonya.
Simu; 0757-909942
Barua pepe; 
bensobchonya23@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.