google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 13, 2017

MREJESHO; Zijue Faida Za Kumheshimu Kila Mtu Katika Kazi Yeyote Uitendayo-03

No comments :
Habari za muda huu mpenzi msomaji wa mtandao huu wa dira ya mafanikio, ni matumaini yetu u mzima wa afya tele, kwa upande watu sisi hatujambo kabisa. Wiki iliyopita tulipata kusoma kisa kimoja mahala hapa ambacho kilimuhusu mfalme Mhavila pamoja na mama mjane. Kisa hiki kilikuwa ni cha kusisimua sana.
Ambapo tulikisimulia kwa siku mbili na watu wengi walitutumia ujumbe mzuri ya kwamba wamejifunza mengi sana kupitia kisa kile. Hivyo kwa kuwa tunatambua mchango wako kwetu , hivyo tukaamua kukupa nafasi wewe msomaji wetu uweze ulichojifunza kutokana na hadithi ile;
Watu wengi sana walitutumia maoni yako miongoni mwa maoni hayo ni;
Naitwa FURAHA  MWIKOMBO kutoka Uyole Mbeya.
Kwanza kabisa nipende kuwapongeza waheshimiwa kwa elimu mnayotupatia katika kundi la whatsapp, facebook na blog yenu ya DIRA YA MAFANIKIO.
Mimi nilichojifunza kwenye hadithi hii ni;
1.      Kudharau kazi ya mtu hakuna faida yeyote.
2.      Kushukuru kwa kile kidogo unachokipata na kuwasaidia wengine. Ni jambo la busara.
3.      Mungu anapotupima heshima na upendo wetu huwatumia wale walio chini yetu, mfano viwete, vilema, vichaa na wenye shida kama ambavyo alitumia njia hii mfalme mhavila.
4.      Mara nyingi bahati, riziki na mafanikiohuwa ni vitu vilivyojificha sana, tukivumilia na vitatokea baadae sana.

Karibu tuongee mafanikio kila JUMANNE hapa DIRA YA MAFANIKIO.
Naitwa SHABANI SAIDI kutoka Dodoma
Mambo makubwa matatu ambayo nimejifunza kutoka kwenye hadithi hii ni;
1.      Anayewashweshea wengine kwa ukarimu na yeye pia atanyweshwa kwa ukarimu.
2.      Usiwanyime watu mema watu wanayostaili ikiwa mkono wako una uwezo wa kufanya.
3.      Usimwambie mwenzako nenda kasha urudi na kesho nitakupa kumbe una kitu unachokihitaji.

Naitwa SIMONI MAPUNDA kutoka mbinga.
Mimi nilichojifunza kwenye hadithi hii ni;
Kwamba  kuwa mkarimu kwa watu wote ni siraha, hata kama huna kitu fanya kitu kwa msaada wa wengine, kupitia ulichonacho hajalishi wewe ni maskini, mjane, yatima, kilema au una madaraka amini una uwezo wa kufanya makubwa.
Naitwa ISRAEL NDANG, kutoka Mwanza –Tanzania
Kupitia hadithi ya mfalme mhavilia nimejifunza  mambo yafutayo;
1.      Nimejifunza kutoa pasipo kutegemea malipo, hivyo kila wakati toa mazuri kwa wengine kadri uwezavyo huku ukijua Mungu ndiye mlipaji wa fadhira zako.
2.      Fursa zinaweza kukujia kwenye hali ngumu na utata mwingi ama katika mazingira magumu, hivyo usiyatilie maanani mazingira hayo bali wewe pambana mpaka uweze kupata mafanikio.
3.      Tuwe wakarimu, wanyenyekevu na hata wasikivu pia ili kuelewa hisia za binadamu mwenzetu pia.
TANGAZO MUHIMU
Asante sana kwa wale wote ambao walituma maoni yao kwa namna moja ama nyingine, maoni yako tuliyapenda  na kuyapokea kwa mikono miwili. Tulichokigundua ya kwamba watu wengi wana mambo mengi sana ambayo yatausaidia sisi pamoja na wewe kuweza kufanikiwa na kufika mbali zaidi..
Hivyo kwa kulitambua hilo uongozi wa mtandao wa DM tumeamua kuanzisha kitu kinachoitwa Mafanikio Talk (M.T), hiki ni kipindi maalumu kabisa ambacho kitakuwa kinahusisha mahuzungumzo baina ya uongozi wa mtandao huu wa dira ya mafanikio  pamoja na wewe msomaji wetu.
Tutakochokifanya ni kwamba tutakupigia simu na kufanya mazungumzo na kile ulichokizungumza tutakwenda kukiweka hapa siku ya jumanne Ili watu wengine wajifunze kutoka kwako.
Je ungependa kuwa wa kwanza kufanya kipindi hicho cha Mafanikio Talk (M.T) siku ya jumanne ijayo? Kama jibu ni ndiyo tuma ujumbe mfupi wa maandishi ukianza na neno Mafanikio Talk kisha jina lako  na mahali ulipo kwenda-0757909942/ au email yetu dirayamafaniko@gmail.com nasi tutakutafuta kwa ajili ya kufanya mazungumzo hayo.
Imeandikwa na uongozi wa mtandao huu wa dira ya mafanikio,
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya,
bensonchonya23@gmail.com,
dirayamafanikio.blogspot.com.


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.