google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 16, 2015

Je, Umefanya Nini Mwaka 2015?

No comments :
Mwaka 2015 unakaribia kuisha, kwani zimebaki wiki chache mwaka kuisha na kuingia mwaka mpya wa 2016. Kwa mtu mwenye busara atajiuliza sana maswali mbalimbali ya msingi kuhusiana na mwaka huu.
Maswali ya Msingi ya Kujiuliza:
·         Je nini/kipi ambacho hutasahau mwaka 2015?
·         Je mwaka 2015 umeutumia vyema?
·         Je mwaka 2015 umeutumia kivipi katika kuboresha maisha yako na kupanga malengo yako?
·         Je ni vipi unavyopaswa kubadili au kuboresha katika mwaka unaokuja?

Ni jambo la busara sana kutafakari. Lakini msingi mkuu ni kuhakikisha kuwa; katika matendo yako, maneno yako, na katika tafakari zako unapaswa kuzibadilisha kwa kuhakikisha unazidi kuendeleza hali hizo tatu na kuziboresha. Ukiweza kuboresha mawazo yako, matendo yako na maneno yako kiusahihi utaweza kubadili maisha yako vyema. Hivyo kaa na tafakari, mwaka 2015 umeutumia kivipi. Ikiwezekana andika hata katika kitabu chako au diary ya kumbukumbu itakusaidia kuhakikisha unapanga malengo mazuri na unatambua maendeleo yako ya kimaisha. 
 Makala hii imeandikwa na Apolinary Protas wa Jitambue Sasa blog  

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.