google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

May 24, 2018

Kama Unapata Pesa Halafu Zinapotea Kwa Haraka Sana, Soma Hapa.

No comments :
Najua unawajua wale watu ambao wanaweka sana juhudi katika kile wakifanyacho, kama ni pesa wanapata kweli, lakini pamoja na kupata pesa hizo baada ya muda zile pesa na  mafanikio yao  halisi yanakuwa tena hayaonekani.
Hapa ndipo wengi huanza kuwaza na kutafuta ni mchawi yupi aliyewaloga. Watu hawa wanakuwa hawaamini kama kweli wanaweza wakapata pesa halafu  mafanikio hakuna. Kinakuwa ni kitu kigumu kutokuamini zile pesa zimekwenda wapi walizozipata.
Pamoja na hayo, kwa kawaida kunakuwa ipo sababu inayopelekea hali hii kutokea sana. Ikumbukwe hali  hiyo inakuwa inatokea si kwa bahati mbaya au si kwa sababu una mkosi wa aina fulani bali inatokea kwa sababu.
Sababu hii ni kwamba watu hawa wanakuwa hawana mafanikio ndani yao, basi. Ipo hivi, huwezi kufanikiwa kama ndani yako hujafanikiwa bado. Utaweka juhudi sana na kufanikiwa kwa muda, lakini utaanguka tena kwa sababu ndani hujafanikiwa.

Siri ya kuweza kuweka mafanikio ya kudumu kwenye maisha yako ni kwa wewe kuumba mafanikio ya kutosha ndani yako. Ukiona hujaweka mafanikio ya kutosha ndani yako kufanikiwa kwa nje ni ngumu pia kwako.
Ndio maana, kabla hujaanza kulaumu kwa nje kwa nini huna mafanikio, jiulize na kujitazama mwenyewe kwa ndani yako upya, je, yale mafanikio unayoyataka unayo na unayaona ndani yako jinsi yalivyoumbika.
Kama ndani yako huoni kitu halisia yaani kile unachokitaka na una malengo ya jumla, kufanikiwa kwa nje na ukaweza kudumisha mafanikio hayo inakuwa ni ngumu sana kwako kuweza kutokea na ndio maana unatakiwa kulifahamu hili vyema.
Kwa kifupi, unatakiwa uwe na picha kamili ya kile unachokitaka ili ufanikiwe, na kama hauna picha hiyo wewe sahau kupata mafanikio hayo hata kama ukipata pesa nyinggi leo uwe na uhakika haziwezi kudumu sana, utazipoteza.
Elewa, kama unataka kujenga mafanikio ya nje ya kudumu, anza kufanikiwa ndani yako kwanza na huku nje utafanikiwa tu. Ukumbuke mafanikio yako ya nje yanategemea sana ndani yako umefanikiwa kwa kiasi gani, hakuna uchawi katika hili, tafakari.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama pia  wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

May 23, 2018

Wewe Ni Mtawala Na Mfalme Wa Maisha Yako Kwa Namna Hii.

No comments :
Kila unapoanza siku yako mpya, naomba uweke akilini hili na kutambua kwamba wewe ndiye unayatawala maisha yako kwa kila kitu. Hakuna ambacho wewe si chanzo cha kutawala. Wewe ndio unatawala na kuamua maisha yako yawe ya mafanikio au kushindwa.
Nikiongea kwa mifano, angalia, wewe unatawala matendo yako. Hakuna mtu ambaye anaweza akakuongoza, wewe ndiye unayeamua uchukue hatua hii au usiichukue kabisa na uachane nayo ufate mambo mengine.
Wewe ndiye unatawala akili yako. Hakuna anayeweza kukuamulia usome kitu fulani au uache. Hakuna anayekuamulia uangalie tv au usiangalie. Wewe ndiye mtawala wa akili yako na akili hiyo inakuongoza kufanya yale uyatakayo.
Wewe ndiye unatawala mtazamo wako. Kwa mtazamo wako ulionao, wewe ndio unaruhusu sana uwe na mtazamo wa namna hiyo. Hakuna mtu ambaye anakuamuru uwe na mtazamo wa aina fulani kama si wewe, mtazamo wako unabebwa na wewe.

Wewe ndiye unatawala mwili wako, hakuna anayekuamulia ule nini au usile nini, hakuna anayekuamulia ufanye zoezi la aina fulani au usifanye, hakuna anayekuamulia uamke mapema au usiamke, mwili wako unautawala wewe na kwa kila kitu.
Wewe ni mtawala wa mahusiano yako, mahusiano hayo yanaweza yakawa ya kimapenzi au ya kawaida. Hakuna anayekuzuia kuwa na mahusiano na watu wengine. Uchaguzi wa nani ujenge mahusiano naye nae, unabaki nao wewe binafsi.
Wewe ni mtawala wa muda wako. Ni wewe ndio ambaye kila wakati unaamua muda wako uutumie zaidi kwenye jambo gani. Pengine uutumie muda wako kwenye jambo linalokupa mafanikio au uutumie kwenye jambo ambalo linakupa hasara.
Wewe ndio mtawala wa hisia zako. Tunaona hisia kama wasiwasi au woga ni wewe ambaye unaamua kuzibeba au kuzipoteza lakini wewe ni mtawala wa hayo mambo tena kwa kiasi kikubwa sana na unatakiwa uelewe hivyo.
Wewe ni mtawala wa matokeo ya maisha yako. Chochote kinachotokea kwenye maisha yako, chanzo kikubwa ni wewe. Kwa hiyo hutakiwi kulaumu kitu, utawala huo unao wewe na unatakiwa kuelewa hili kwa ufasaha na kufanyia kazi.
Ukiangalia kwa makini utagunduia wewe ni mtawala wa kila kitu kwenye maisha yako. kama iko hivyo kwa nini ulaumu wengine wamekuharibia maisha yako.  Tambua ni sehemu ndogo sana ambayo imechangia hao waharibiu maisha yako kama unavyofikiri.
Kuanzaia leo elewa wewe ni mtawala wa maisha yako na kama iko hivyo kwako, unatakiwa kukubali kuwajibika kwa sababu wewe ni mtawala wa maisha yako na chochote kinachokutokea kwenye maisha yako kinakuhusu haswa.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama pia  wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,





May 22, 2018

Hivi Ndivyo Watu Wanavyopenda Kushindwa Kwenye Maisha.

No comments :

Unaweza ukaona kama ni kitu cha ajabu au kama nimekosea vile kuandika kichwa cha habari ya makala haya, lakini elewa sijakosea na ninachokimaanisha ndicho, lipo kundi kubwa la watu linapenda kushindwa kwenye maisha.
Unashangaa, ndio, kundi hili kubwa ndilo ambalo likiulizwa, lina mipango mizuri sana ya kimafanikio, lakini maneno na vitendo vya kutaka maisha hayo haviko sawa. Kundi hili kubwa ambalo labda na wewe upo, hujikuta likipenda kushindwa kufanikiwa maishani.
Najua unajiuliza kivipi? Hebu angalia kuna watu ambao muda wao muda mwingi sana ni kuangalia Tv, utakuta zaidi ya saa tatu mtu amekaa anaangalia Tv, unategemea hapa nini kitatokea kama si kuanguka tena vibaya kwenye maisha yake.

Ule muda mwingi unaopotea kwenye kuangalia Tv, naamini ungetumuka kufanya kitu kingine kama kutafuta maarifa ya aina fulani hivi, basi mtu huyo angekuwa yupo mbali sana kimafanikio.  Kwa bahati mbaya muda huo unapotezwa mchana kweupe.
Si Tv tu peke yake, ukiwaangalia watu wengi wanaishi maisha ambayo hayana maana kabisa, ni watu wa kuishi maisha ya kuwadanganya na kuwapoteza kabisa kwa kufanya vitu ambavyo haviwastaili. Ni watu ambao dhahiri wanajidanganya.
Kwa kawaida unapofanya mambo yanayoenda kinyume  na mafanikio, hata kama unatamka mara ngapi kwamba wewe unataka mafanikio hayo, hiyo haitaweza kukusaidia kitu. Ndio maana unatakiwa usijidanganye kwenye maisha yako mwenyewe.
Unatakiwa utafute vitu vya kufanya ambavyo vinakusaidia kukupa mafanikio. Hata hivyo kwa bahati mbaya unaishi maisha ambayo kiuhalisia kwa maisha hayo hayakusogezi mbele hata kidogo kuweza kufanikiwa sana sana yanakurudisha nyuma.
Watu wengi inaonyesha wanajishughulisha na kazi ndogo ndogo ambazo haziwasaidii kupiga hatua. Kazi hizo zinaweza zikawa kama kupiga stori, kudhurura na kufatilia habari zizsizo na maana. Mafanikio hayawezi kuja kwa namna hiyo hata siku moja.
Waangalie watu waliofanikiwa, wamefanikiwa kwa sababu ya kuishi na tabia za kimafanikio. Pia waangalie watu ambao wameshindwa nao pia wameshindwa kwa sababu  ya kuishi na tabia zile za kushindwa.
Nimekwambia hata uimbe wimbo mzuri vipi ambao unajisemea kwamba unataka maisha mazuri, ila kama unaishi maisha yanayokurudisha nyuma utakwama tu. Hakuna muujiza katika kukupa mafanikio yako. muujiza ni wewe.
Anza kubadilika ishi tabia za watu wa mafanikio ili ufanikiwe. Ukiendeleza ubishi nakwambia utakwama sana. Amua kujifunza, acha kudharau yale ambayo kuna watu walipoteza muda wao kukusaidia wewe.
Kumbuka matendo yako ya kila siku ambayo unayetenda kinyume na mafanikio ndio yanayotuonyesha kwamba wewe unapenda sasa kushindwa. Hata kama hutaki kama unatenda kinyume na mafanikio, ujue basi unapenda kushindwa kwenye maisha yako.
Ishi kwa kujiamini, amua kusonga mbele kwa kuhakikisha kila unachokifanya, kiwe na matokeo ya kukusogeza wewe mbele. Ukiona kitu hicho kikimbie na hakina maana ya kuweza kukusaidia leo na hata kesho.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama pia  wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

May 21, 2018

Fanyia Kazi Mambo Haya 4, Yataleta Mabadiliko Na Mapinduzi Makubwa Ya Maisha Yako.

No comments :
Hakuna muujiza wala ramli  katika kufikia mafanikio yako.  Mafanikio yanajengwa juu ya kanuni tena wakati mwingine kanuni hizo zinakuwa ndogo ndogo sana ambapo wakati mwingine  zinapuuzwa lakini ndizo zijengazo mafanikio yako na ya mwingine.
Hakuna siri tena, ukifanyia kazi mambo ya msingi katika mafanikio utafanikiwa moja kwa moja. Ukumbuke, Yapo mambo mengi ya kufanyia kazi, lakini hapa kupitia makala haya nakupa mambo manne tu, kama ukiyafanyia kazi yataleta mapinduzi ya maisha yako.
1. Tambua ulipo sasa kimaisha na wapi unapokwenda.
Kitendo cha kujua hapo ulipo kimaisha ni hatua nzuri ya kukufanya uchukue hatua za ziada. Ila unatakiwa ujue, kujua hapo ulipo haitoshi, unatakiwa kujua ni wapi unakwenda kimaisha baada ya miaka miwili au baada ya miaka mitano.
Ukijua pale ulipo pengine upo kwenye hali mbaya sana, lakini na ikawa haujui ni wapi unakwenda kwenye maisha yako nalo hilo ni tatizo kwako. Kama hujui unakokwenda ni dalili tosha inaonyesha hautafanikiwa maana utafanya chochote ilimradi iwe hivyo.
 2. Tambua ndoto yako ni ipi.
Jiulize hapo ulipo una ndoto ya maisha yako. Je, una kitu ambacho unataka kukitimiza na tayari umeshaanza kukichukulia hatua. Kama huna ndoto yoyote ya kimaisha niseme kwa uwazi kwako hutaweza kufanikiwa.
Kutaka kuishi maisha ya kimafanikio halafu huku ukiwa mweupe, ukiulizwa kile unachokitaka kila kitu unajisemea na unakitaka huko ndiko kunaitwa kupotea. Ni lazima ndoto yako iwe wazi, hata ukiulizwa usiku wa maneno ndoto yako ni ipi, unaisema tu.
 3. Tambua ni kipi utakifanya ili kutimiza ndoto zako.
Kujua ndoto yako peke yake haiwezi kukupa uhakika wa kufanikiwa, unatakiwa ujue pia ni kipi utakifanya ili ndoto zako zitimie. Hapa ni lazima ujue kazi au shughuli ambayo utaifanya karibu kila siku ili ikusaidia kukusogeza kwenye ndoto zako. 
Ukishajua ni kipi ambacho unatakiwa kukifanya ili kuhakikisha ndoto yako inatimia, hapo ndipo kitu hicho unatakiwa kukifatilia kila siku. Tafsiri yake ni hii, kushindwa kufanya kitu hicho unajiweka kwenye wakati wa kukwamisha ndoto yako.
 4. Chukua hatua mapema.
Asikudanganye mtu mafanikio yako hayaji kwa mdomo tu au kwa kusema. Mafanikio yako yanakuja kwa wewe kuchukua hatua tena hatua za kuweza kukusaidia kufanikiwa. Ukichukua hatua utaweza kufanikiwa tena kwa kiasi kikubwa tu.
Ikiwa utaendelea kusema tu kila wakati bila kutekeleza ni ngumu sana kuweza kufanikiwa kwako. Kuchukua hatua mapema ndio mpango mzima na sahihi wa kukuwezesha wewe kufanikiwa kwa kile ukifanyacho.
Fanyia kazi mambo hayo kila siku na uwe na uhakika utaleta mabadiliko ya maisha yako kila unapofanyia kazi mambo hayo, tena mabadiliko hayo utayaleta kwa kiasi kikubwa sana mpaka unaweza ukafika wakati ukashangaa.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama pia wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,



                                                       


May 20, 2018

HEKIMA ZA MAISHA NA MAFANIKIO; Maneno Mabaya Yana Mwangwi Mkubwa Kuliko Maneno Mazuri.

No comments :
Mbali na kanuni za kimafanikio ambazo tumekuwa tukijifunza mara kwa mara, lakini unapaswa kujua kwamba pia maisha ya mafanikio yametawaliwa sana na hekima. Hiyo yote  inaonyesha hekima ni za msingi sana katika maisha yetu pia.
Hekima zinatufunza busara, hekima zinatufunza namna ambavyo tunatakiwa kuishi na jamii inayotuzunguka na hekima pia zinatusaidia kuweza kujifunza kanuni kwa ujumla za mafanikio zilizopo kwenye maisha yetu.
Kwa mantiki hiyo, katika siku hii ya leo, nikukaribishe, tuweze kujifunza kwa pamoja baadhi ya hekima za maisha na mafanikio. Ni kusudio langu utatoka na kitu cha kuweza kukusaidia na ambacho utakifanyia kazi.


1.  Shoka halikumbuki mti lililoukata, bali mti huo huikumbuka shoka ile.
Katika hekima hii inatuonyesha katika maisha, unaweza ukamfanyia mtu kitu ambacho kitagusa maisha yake pasipo kujali kitu hicho ni kibaya au kizuri, lakini kumbukumbu inakuwa inabaki sana kwa yule aliyeguswa na alichofanyiwa.
Ndio maana unaweza ukamsaidia mtu usikumbuke, unaweza ukamfanyia mtu ubaya usikumbuke, lakini yule aliyefanyiwa ubaya huo anakuwa anakumbuka sana. Hapa ukumbuke  tunaaswa kuwa makini  yale yanayogusa maisha ya wengine.
Jiulize ni mara ngapi au kuna wakati uliwahi kumfanyia mtu kitu fulani ambacho kilimsaidia, utakuta muda unakuwa umepita na wakati huo umesahau, lakini unapokutana na mtu yule anakukumbusha na kukwambia unakumbuka ulinifanyia kitu hiki.
Mara nyingi wengi wetu hubaki tukishangaa kwa kukumbushwa kitu kile. Kwa hiyo unaona hata ubaya ukimfanyia mtu ni hivyo hivyo. Kwa wewe ukiyefanya ni rahisi kusahau lakini si kwa ,mtu aliyefanyiwa ubaya huo hata kidogo hawezi sahau.
Hapa ndipo unaweza ukapata picha kwa nini shoka halikumbuki mti liloukata na kwa nini mti uliokatwa hulikumbuka shoka. Unaona mti unakumbuka shoka kwa sababu shoka liligusa maisha ya mti huo kwa namna fulani.
2. Maneno mabaya yana mwangwi mkubwa kuliko maneno mazuri.
Ni kawaida sana maneno mabaya kuweza kuenea kwa haraka kuliko maneno mazuri. Unaweza ukafanya mengi mazuri lakini ukikosea kidogo maneno hayo yatasambaa sana kuliko ambavyo hukutarajia iwe hivyo.
Hapa kupitia hekima hii inatunaonyesha wazi kwamba maneno mabaya yana mwangwi mkubwa kuliko maneno mazuri,  hilo ni la ukweli na halina ubishi. Mwangwi wa kitu kibaya unasikika zaidi kuliko mwangwi wa kitu kizuri.
Angalia kipindi ambacho ulifanya ubaya, mwangwi wake ulisikika vipi na kipindi ambacho ulipofanya mazuri mwangwi wake ulisikikaje pia. Hapo utagundua kipindi ambacho ulifanya mabaya mwangwi wake ulionea sana.
Tahadhari kubwa unayopewa hapa ni kuwa makini sana na maneno mabaya. Kwa tafsiri nyingine inaonyesha tenda wema unavyoweza wewe ila uelewe maneno mabaya siku yakija kukuibukia yana mwangi sana kuliko maneno mazuri.
Fanyia kazi hekima hizi naamini kwa sehemu zitakuwa zimekusaidia kutoka hatua moja na kulekea hatua nyingine ya maisha yako. Kila wakati hekima zinakupa busara, hekima zinakuza uelewa wako kwa namna fulani.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama pia  wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,


May 18, 2018

Kama Utakuwa Na Kitu Hiki, Kitakufanya Uwe Imara Na Mwenye Mafanikio Ya Kudumu.

No comments :
Fikiria kama kila kitu unachokihitaji wewe ingekuwa unakipata kila wakati hata pasipo kuweka juhudi kubwa, pasipo changamoto, pasipo kukipigania kitu hicho  sana na wala pasipo hata kuweka kazi kubwa yoyote  ile inayohitajika, ila kitu hicho unakipata.
Najua kama itatokea hivi, wengi wangefurahi sana na kusema hiyo itakuwa safi maana mambo yao yatakuwa yamewaendea sawa tena kwa uhakika. Lakini nikwambie ikitokea hivyo kwako ujue unakwenda kuwa dhaifu sana na mafanikio yako hayatadumu.  
Nimekwambia utakwenda kuwa dhaifu na hautatengeneza mafanikio ya kudumu nikiwa na maana hii, changomoto yoyote itakayotokea hata kama ni ndogo kiasi gani hautaweza kukabilina nayo, kwa sababu mafanikio yako uliyapata kiulaini.
Mafanikio yoyote unayoyapata kwa njia rahisi sana pasipo kuyapigania uelewe hayana mizizi imara, hayana fundisho, hayana sehemu ambayo yamekukomaza na ndio maana huwezi kiuhalisia kukua kimafanikio bila kupambana kikamilifu.
Kama imetokea umepata mafanikio ya moja kwa moja pasipo kupitia changamoto, unatakiwa kuwa makini sana, la sivyo unaweza kupoteza kila kitu. Waangalie watu wanaopata bahati nasibu ni kitu gani kinawakuta baadae, wengi hufilisika tena.
Hiyo yote kama nilivyosema,  inaonyesha huwezi kuwa na mafanikio imara na ya kudumu kama hujakutana na upinzani au changamoto za kutosha. Kila unapokutana na changamoto hizo hilo si swala la kuchukia bali ni kujifunza na kusonga mbele.
Maumivu unayokutana nayo wakati huu kwa sababu ya upinzani ama changamoto, wewe yavumilie kwani ni rafiki mkubwa sana wa mafanikio yako. Unaweza usione faida yake leo, lakini kesho utakuja kugundua kile nisemacho na kina ukweli gani.
Tambua kama hujawahi kushindwa, kama hujakosea, kama hujakutana na upinzani wa kutosha, halafu ukasema unataka mafanikio makubwa unajidanganya. Hata ukipata mafanikio yataporomoka kwa sababu hakuna kitu kilichokukomaza.
Majasiri na  mashujaa katika maisha ni wale watu wote ambao wamepitia kwenye nyakati ngumu sana ambazo hata hazieleweki. Nyakati hizi ngumu ndizo ambazo zilizowajenga na kuwapa jeuri kubwa ya kuweza  kufanikiwa.
Watu hawa ukiwaona wana nidhamu na ule uchungu wa maisha. Kuna kitu ambacho unaona kinachemka ndani mwao yaani wana kiu na hamasa kubwa sana ya kufanikiwa kwao. Yote hayo yanaletwa na upinzani ama changamoto walizokutana nazo.
Huhitaji kujilaumu, huhitaji kujuta kila unapokutana na changamoto kwani hapo ndipo nguvu kubwa ya mafanikio yako ya kudumu ilipo. Changamoto na upinzani mwingi unakuja kama rafiki wa kukusaidia kukukomaza na kukupa mafanikio  ya kudumu.
Hata watu wengi katika maisha ni watu ambao hawapendi kusikia sana hadithi  za watu ambao walifanikiwa moja kwa moja kwenye maisha. Hadithi za watu, ambao walifanikiwa moja kwa moja pasipo kupitia changamoto hazina mvuto.
Kila mtu  anapenda sana kujifunza kwa watu ambao waliumia au watu ambao waliteseka juu ya changamoto fulani hivi, lakini mwisho wa siku wakaja kufanikiwa. Hivyo elewa, mafanikio ya moja kwa moja hayakupi nguvu na wala hayakukomazi .
Wewe hapo ulipo una nguvu kuliko unavyofikiri ya kukabiliana na changamoto yoyote ile. Ukiona umeshindwa wewe umeamua tu. Na changamoto yoyote unayokabiliana nayo ukiona umeishinda, tambua umepiga hatua fulani kubwa ya kimaisha.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio kwa undani, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe pia ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,


May 17, 2018

Ili Ufanikiwe, Maisha Hayataki Wewe Uwe Na Kitu Hiki…

No comments :
Kama una lengo la kujiongezea kipato, acha kuogopa kufanya kitu chochote. Kama kuna kitu fulani ambacho unatakiwa ukiuze, hebu uza kitu hicho. Acha kujisikia vibaya kwa sababu unauza kitu fulani eti ambacho hakina hadhi yako.
Maisha hayataki aibu, fanya kitu chochote cha kukukiingizia kipato ilimradi kitu hicho kiwe halali na hakiwaumizi wengine. Maisha ya kuona aibu kufanya jambo fulani yatakufanya uzidi kukosa pesa kila kukicha.
 Acha kuwa na ndoto za kufanya mambo makubwa saana na halafu ukadharau kufanya hata vidogo ambavyo huna. Kumbuka, jiwekee ndoto kubwa sana lakini anza na hapo ulipo, anza na kidogo ulichonacho pasipo kujali ni kitu gani.
Hutaki kufanya kitu kwa sababu ya kuona aibu, jiandae kufikia ndoto zako hutaweza kufanikiwa. Kwa nini uone aibu kwa kile ambacho kinakupatia kipato? Shida yako iko wapi na hapo unatakiwa ujiulize.

Ukiona unaona aibu kwa kile unachotaka kukifanya ujue kabisa hujaamua kujitoa kabisa kuweza kufanikiwa. Huna sababu ya kuendelea kuona aibu, ni ukweli uliowazi wewe hapo huna kitu, sasa aibu ya nini?
Inawezekana zipo sababu ambazo zinakufanya uone aibu, sanasana pengine labda umesoma kwa hiyo unaona ukiweka genge mtaani kwako unakuwa ni mtu kama wa kujizalilisha yaani genge sio hadhi yako.
Naweza nikakubalia sawa, sasa kipi unachoweza kufanya ambacho ni hadhi yako? hapo ulipo najua unaweza ukawa una tai vizuri lakini unashindwa kutatua tatizo la shilingi elfu mbili tu, lakini na tai yako shingoni. Sasa kwa hali hiyo aibu ya nini?
Hapo yaani inaonyesha unashindwa kutatua tatizo dogo la shilingi elfu mbili na usomi wako. Jiulize tu mwenyewe je, ni akili kweli kuona aibu kufanya kitu cha faida yako? Kipi bora uendelee kulala au uzunguke mtaani na kuamua kufanya  kitu cha faida.
Nikwambie tu, kwa sasa nyakati zimebadilika sana, kuendelea kujishaua wakati maisha yanataka uyabadilishe huwezi kufanikiwa. Kama unaendelea kupaka rangi kwenye maisha yako, nakwambia endelea kupaka rangi, kuna watu wanajenga ujue na hawapaki rangi.
Mambo hayakusubiri ili yabadilike, ila wewe ndio unatakiwa kuyabadilisha mambo hayo hatua kwa hatua. Huhitaji kufanya kitu maalumu sana ili ufanikiwe, anza na kitu chochote tu, ambacho kinakuingizia kipato bila kujali ni nini, ila kiwe halali.
Acha kusikiliza maneno ya watu, funga masikio na kuamua kufanya jambo lolote mahali popote na eneo lolote, ilimradi jambo hilo liwe ni la kukuingizia kipato. Tafakari kwa kina na fanya uamuzi wa busara wa kuacha kuona aibu zisizo na msingi.

Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

May 16, 2018

Ukiwa Na Tabia Hii Moja Tu, Itakuzuia Sana Kufanikiwa Kwako.

No comments :
Zipo tabia nyingi ambazo zina mchango mkubwa sana kwa anguko la maisha ya wengi. Na kwa bahati mbaya, wengi wanakuwa hawajui kama tabia hizo ndizo zinazowaangusha na hivyo hujikuta ni watu wa kurudia tabia zile zile kila wakati.
Matokeo yake ya kutokujua tabia hizo, hupelekea wengi kuanguka kweli na kunakuwa hakuna mafanikio yanayoonekana na mwisho watu hawa hujiuliza sana ni kitu gani kilichotokea hadi maisha yao yakawa katika hali hiyo.
Leo kwa kupitia makala haya tutajiffunza tabia moja tu ambayo kama ukiwa nayo itakukwamisha sana kwenye safari yako ya mafanikio. Nasema hivyo kwa sababu, kuna watu tayari wanayo matokeo mabovu yamewapata sababu ya tabia hizo.
Tabia moja ambayo itakukwamisha sana na haitakusaidia kufanikiwa kama utakuwa nayo na kuiendeleza ni ile tabia ya kuamua kuwa mtu wa kushangaa katika maisha. Wapo watu ambao tabia zao ni kushangaa tu karibu kitu.

Kwa mfano, Utakuta wao ni watu wa kushangaa na kuhamasika sana na miradi wanayofanya watu wengine, ukija upande wao hakuna hata kitu kimoja wanachofanya au hawachukui hatua kabisa.
Pia utakuta ni watu wa kuingia kundi moja, wanashangaa kinachoendelea humo na kutoka na kuingia tena kundi lingine wanashangaa wee na kutoka tena, pia bila kuchukua hatua. Watu wenye tabia za namna hii kamwe ni watu wasiofanikiwa.
Dunia ya sasa hivi ni ya mwendo kasi, watoto wa mtaani wanakwambia hutakiwi kuuza sura’, fanya kazi. Kama kuna fursa hata kama ni ndogo, itumie ikusaidie kufanikiwa na acha kubaki tu kuwa mtu wa kushangaa.  Kama ni kujifunza, jifunze kweli.
Uzuri au ubaya wa maisha hakuna ubabaishaji, ukileta ubabaishaji wa aina yoyote ile, utaumbuka tu na ni lazima utajibiwa na maisha kama vile wewe unavyobabaisha. Badilika rafiki na achana na biashara ya kushangaa, kuwa mtendaji na aamua kufanya kazi.
Jiulize utashangaa hadi mwaka gani au hadi lini. Watu wanaoshangaa ni mara nyingi ni watu ambao hawafanikiwi. Maisha yanataka uwe mtendaji zaidi na si kuishia kushangaa ambako haukuwezi kukusaidia chochote.
Kama ulikuwa una tabia ya kushangaa basi ndoto na mipango yako mingi sana itaweza kukwama na hautaweza kufanikiwa. Wale wote wanaofanikiwa hawashangai bali wanaamua kujifunza na kuamua kuchukua hatua za kusonga mbele.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,









May 15, 2018

Njia Sahihi Ya Kupima Kama Unapiga Hatua Za Kimafanikio Au Upo Palepale.

No comments :
Hapo ulipo unao uwezo wa kupima kama unapiga hatua au hupigi hatua kwa kile ambacho ukifanyacho. Ni rahisi sana kuanza kujiuliza hivi kwa hiki nikifanyacho mimi, napiga hatua au nimebaki pale pale nilipo tu.
Mara nyingi ipo njia sahihi ambayo inaweza ikakusaidia wewe na mtu yeyote kujua kama anapiga hatua ama hapigi hatua. Njia hii si nyingine bali ni kwa wewe kukaa nje ya mazoea uliyoyazoea kila siku.
Ukiona kila siku unafanya kitu hicho kwa namna hiyo hiyo yaani hubadilishi kitu na upo kwenye mazoea yale yale si rahisi sana wewe kuweza kupiga hatua. Kama ukiona kile unachokifanya na unakifanya nje ya mazoea ujue kuna kupiga hatua hapo.
Upo uwezekano wa wewe ukawa bado hujanielewa kwa namna fulani hivi, lakini nitakupa mifano zaidi ambayo itakusaidia kuweza kuelewa. Tambua hivi, ni jambo la hatari kufanya mambo yako kwa hali ya mazoea kila siku, maana hutafanikiwa.
Niweke labda wazi kwako nakurudia hivi, hutaweza kufanikiwa kama hauko nje ya mazoea yako. Mazoea ni moja ya sumu kubwa sana inayokuzuia kufanikiwa. Ukiendelea kufanya mambo yako na mazoea utashangaa unabaki palepale miaka nenda rudi.

Wanaobadilisha maisha ni wale watu ambao wanaamua kwenda nje ya mazoea yao. Kwa tafsiri ya haraka mazoea uliyonayo ndio yaliyokupa matokea uliyonayo. Hivyo kwa kuendelea kuyang’angania utaendelea kupata matokeo yaleyale.
Hiyo inamanisha kwamba, hata kama una malengo na mipango mizuri vipi, ila kama unachukua hatua kwa mazoea, basi utaendelea kubaki pale pale karibu kila wakati kwenye maisha yako na hautaona ukipiga hatua mbele ya kukusaidia kufanikiwa.
Hivyo, kila wakati jaribu kufanya jambo jipya ambalo litakupa matokeo tofauti na yale ambayo umekuwa ukiyapata. Kwa kufanya kwako jambo jipya kuna vitu vingi sana ambavyo utajifunza na vitakubadilishia mtazamo wako kabisa.
Huhitaji kusubiri kitu, anza kujua kama unafanikiwa au hufanikiwa kwa kujipa changamoto ya kukaa nje ya mazoea yako. Hata kama kwako unaona inakuwa ngumu lakini dhamiria kukaa nje ya mazoea uliyonayo kila wakati.
Unapaswa kujua, kitakuwa ni kupimo sahihi kwako kama unapiga hatua au hupigi  hatua za kimafanikio kwa kukaa nje ya mazoea yako. Ukiona unafanya mambo yako na unaona kawaida ujue hakuna ulichobadili na hapo kufanikiwa itakuwa shida pia.
Jitahidi uwezavyo kama nilivyosema kaa nje ya mazoea yako, hiyo itakusaidia kukujengea nidhamua na hata kukupa mafanikio ambayo hukuyatarajia kwa sababu ya nidhamu yako. Hivi ndivyo unavyoweza kupima mwendelezo wa mafanikio yako.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,






May 14, 2018

Usiruhusu Maisha Yako Yatawaliwe Na Mambo Haya Kabisa.

No comments :
Ikiwa upo kwa ajili ya kutaka maisha ya mafanikio makubwa, yapo mambo ambayo hutakiwi kuyaruhusu kabisa yatawale maisha yako. Unapokuwa unaruhusu mambo haya yatawale maisha yako, hiyo inakuwa ni sawa na kuamua kuharibu maisha uliyonayo.
Ni wajibu na jukumu lako kuyajua mambo haya ambayo tunakwenda kuyajadili na kuyafanyia kazi. Je, mambo haya ni mambo gani ambayo hutakiwi kuyaruhusu yatawale maisha yako? twende pamoja tujifunze;-
Mambo yaliyopita.
Kwenye maisha yako usifanye kosa ukaruhusu maisha yako ya sasa au yajayo yakatawaliwa na mambo ambayo yamepita. Mambo ambayo yamepita ni tayari yamepita pasipo kujali yamekuumiza au hayajakuumiza.
Achana na kila kitu cha nyuma ambacho tayari kimeshapita, kwani hata ukiendelea kukibeba sana hakitakusaidia kitu zaidi utaendelea kuumia na kuharibu kesho yako. iwe kuna makosa ulifanya, ulifanyiwa kitu kibaya na wengine, achana na hiyo habari.
Kuendelea kukumbuka mambo ambayo tayari yameshapita hiyo ni sawa na kuendelea kuyapa nguvu mambo hayo. Kikubwa maisha yako anza kuyatengeneza hapo ulipo na mambo yaliyopita usiruhusu yatawale maisha yako tena.

 
Maoni ya watu wengine juu yako.
Jambo la pili, usiruhusu maisha yako yatawaliwe na maoni ya watu wengine. Watu wanaweza wakawa na maoni juu ya maisha yako ambayo hayaendani kabisa na malengo yako, kwa hiyo ikiwa utaamua kuyafata basi utakuwa unajipoteza wewe.
Ndio maana kabla hujafanya kitu unatakiwa kujiuliza unakifanya kitu kwa sababu yako au kwa sababu ya maoni ya wengine? Wapo watu ambao hawawezi kufanya kitu mpaka wasikilize maoni ya wengine wanasema nini.
Umezaliwa kwa sababu ya makusudi maalumu ambayo unatakiwa uyatimize. Sasa  makusudi hayo huwezi kuyatimiza kama maisha yako unayeendesha kwa kutumia maoni ya watu. Usijaribu kuishi kwa ajili ya maoni ya wengine sana, utakwama.
Mawazo yako hasi.
Yapo mawazo ambayo unayo na mawazo hayo yamekuwa yakikuzuai kwa muda mrefu sana kuweza kufanikiwa. Pengine umekuwa na mawazo ya kusema kwamba siwezi kufanikiwa kwa sababu hii au ile.
Ukiangalia mawazo hayo hayana ukweli ila yamekuwa yakikuzuia kufanikwa kwa sababu unavyojiwazia. Kama unajiwazia kwa ndani huwezi kufanikiwa  kwa sababu umezaliwa kwenye ukoo haujiwezi au kwa sababu huna bahati ni dhahiri hutaweza kufanikiwa.
Kwa jinsi ilivyo, kama hakuna kinachokuzuia ndani yako kuweza kufanikiwa, basi na hata nje hakuna kitu ambacho kitaweza kukuzuia kufanikkiwa hata iweje. Uamuzi unabaki kwako, kutokuruhusu mawazo ya kutokufanikiwa yakutawale, basi.
Mahusiano.
Kati ya kitu kimojawapo chenye nguvu sana katika maisha ni mahusianao. Ni hatari sana kujihusisha na mahusiano na mtu yeyote eti kwa sababu huna mtu. Hiyo nikiwa na maana unaingia kwenye mahusiano kwa sababu furaha pekee unaipata huko.
Kama wewe unaona mahusiano ndimo sehemu pekee ya kupata furaha na huwezi kupata furaha mpaka uwe kwenye mahusiano basi utakuwa kwenye wakati mgumu sana maana utakuwa unatawaliwa na mahusiano.
Ninachotaka kusema hapa ni kwamba, unatakiwa uwe imara na kutengeneza furaha yako wewe mwenyewe bila kujali upo kwenye mahusiano au la. Ni rahisi kuingia kwenye mahusiano mabovu na kuharibu maisha ikiwa utakuwa na mahusiano ya hovyo.
Pesa.
Tunaposema usiruhusu pesa itawale maisha yako tukiwa na maana hii, si kwamba pesa ni mbaya au kwamba hutakiwi kuitafuta, hapana. Hapa kinacholengwa usije ukakubali ukafanya maamuzi kwa sababu una pesa.
Unachotakiwa kuelewa ni kwamba usiruhusu pesa, ikawa ndio inatawala maamuzi yako. Fanya mambo yako si kwa sababu ya pesa. Ifanye pesa ibaki kwako kama kitu cha kukusaidia na si kwa sababu una pesa kichwa kinaanza kuyumba hovyo hovyo.
Haya ndio mambo ya msingi ambayo hutakiwi kuyaruhusu kabisa yatawale maisha yako. Unaporuhusu mambo haya yakatawala maisha yako kuna namna ambayo unakuwa una haribu maisha yako, kuwa makini na fanyia kazi.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,