google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 22, 2017

Hiki Ndicho Kitu Cha Muhimu Sana Kuzingatia Katika Mafanikio.

No comments :
Upo ushauri mwingi sana ambao umekuwa ukitolewa juu ya namna gani mtu afanye ili aweze kufanikiwa. Waandishi na vitabu vingi vya mafanikio vimekuwa vikiandika sana na kutoa ushauri wa kipi kifanyike ili mtu kuweza kufanikiwa.
Pamoja na ushauri wote huo mzuri ambao umekuwa ukitolewa, lakini kipo kitu kimoja cha muhimu sana ambacho mtu akiamua kukifatilia na kukifanyia kazi hicho ndicho naweza kusema ndio mafanikio yote yaanzia hapo.
Kitu hicho si kingine bali ni kujitoa/‘commitment.’ Mafanikio yote yanaanza kwa wewe kuamua kujitoa na kuamua kweli kufikia mafanikio yako. Hakuna unachoweza kukifanikisha usipojitoa kikamilifu.

Kuwa na malengo, shauku ya kufikia malengo yako na hamasa hivyo kweli ni vitu muhimu, lakini huwezi kufanikiwa hata kama una vitu hivyo ikiwa hautaweza kujitoa. Kujitoa kwako ndio kila kitu katika kufikia mafanikio uyatakayo.
Ni kweli ili kufanikiwa unahitaji kufanya kazi kwa juhudi, unahitaji kuwa na nidhamu, unahitaji kuwa na shauku ya mafanikio yako, lakini lililo muhimu kwako ambalo unatakiwa ulizingatie sana ni kwa wewe kujitoa kwako.
Angalia maisha ya watu waliofanikiwa au angalia vile vitu ambavyo umewahi kuvifanikisha katika maisha, sina shaka utapata jibu kwamba kwenye vitu hivyo ulijitoa sana na ndio maana ukaweza kufanikiwa.
Kujitoa kunakuja kwa wewe kuamua kufanya kila linalowezekana hadi kuweza kutimiza ndoto zako. Hata kitokee kitu gani au kizuizi kipi kwa kuwa umeshaumua kujitoa utaamua kwa chochote kile utafanya hadi uweze kufanikiwa.
Wataalamu wote waliobobea katika fani mbalimbali duniani wametokana kwa sababu ya kujitoa. Ugunduzi wowote duniani umetokeaa kwa sababu ya kujitoa. Kuna watu walikuwa hawalali hadi wakawa wa wataalamu au wagunduzi wa kitu fulani.
Unapoona mafanikio ya aina fulani yametokea pia hayo ni matokeo ya kujitoa. Kuna vitu lazima vilipotea au vilitolewa sadaka ili mafanikio hayo yaonekane. Pasipo kujitoa kwa nguvu zote ni rahisi tu kusikia mafanikio yakionekana kwa wengine lakini sio kwako.
Kwa hiyo huhitaji kukwepa kiujitoa unapotafuta mafanikio. Kama ni kazi unatakiwa kazi ufanye haswa. Swala la kujionea huruma huko ni sawa na kuamua kuyapa mafanikio mkono wa kwaheri kwamba hutaki tena.
Hata kila mtu mwenye mafanikio ukimwona ujue kabisa kuna vitu ambavyo aliamua kujitoa hadi akaweza kufanikiwa. Kwa namna yoyote ile kama unataka kufanikiwa angalia unajitoa kwenye vitu gani.
Kujitioa ni kitu pekee ambacho kitakuhakikishia mafanikio yako wakati wote. kwa sababu utakapoanza kujitoa basi juhudi, kufanya kazi kwa moyo, kuwa na nidhamu hivyo ni vitu ambavyo vitakuja vyenyewe kwenye safari yako ya mafanikio.
Kuanzia leo, amua kujitoa kwa chochote kile unachokifanya kwenye maisha yako. hiyo itakusaidia sana kuweza kufika katika kilele cha mafanikio makubwa uyatakayo katika maisha yako kwa sehemu kubwa.
Kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji kuuziwa vifaranga bora na kwa bei nafuu, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 14. Wote mnakaribishwa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.