google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 10, 2015

Hivi Ndivyo Kufikiri Kimazoea Kunavyoweza Kuharibu Maisha Yako.

No comments :
Kuna wakati katika maisha yetu huwa tunajikuta ni watu wa kutenda mambo yetu kwa mazoea zaidi na kudhani tupo sahihi, wakati tupo kwenye makosa matupu ambayo huwa yanatuumiza, badala ya kutusaidia kama tunavyofikiri. Makosa haya huwa tunayafanya kutokana na matendo ama mienendo ambayo tunakuwa nayo binafsi katika maisha yetu ya kila siku bila kujijua sisi wenyewe kuwa tunakosea.

Makosa haya mara nyingi huwa yanatokana na kufikiri kimazoea. Kufikiri huku kimazoea kwa kawaida huwa ni jambo baya sana ambalo huweza kuathiri  maisha yetu. Tunapoamua kufikiri kimazoea maana yake huwa tunalazimika kufikiria kwa mujibu wa kile tulichofundishwa utotoni katika malezi au mazingira tulimokulia, bila kujiuliza wala kuchukua hatua zozote muhimu zenye uwezo wa kuleta mabadiliko tofauti kwetu.

Hebu fikiria kuhusu kulalamika au kunung’unika. Watu wengi huwa hawajui kwamba, tunaponung’unika tunasema au kujiambia kwamba hili tatizo ambalo tunalinung’unikia hatuwezi kulikabili au kulitatua, bali kuna wengine wanaoweza kulitatua. Kulalamika, iwe tunajua au hatujui, lakini kuna maana ya sisi walalamikaji kukosa uwezo, kushindwa kumudu, hivyo kutegemea wengine kumudu au kufanya kwa niaba yetu.

Kwa kulalamika, tunaamini kwamba, kwa hizo kelele zetu tunawachochea wengine  ambao tunaowaamini kwamba wana uwezo wa kukabiliana na yale matatizo yanayotukabili kwa wakati huo. Badala ya kulalamika, tunatakiwa kupeleka nguvu zetu zote kwenye suluhu ya tatizo. Kulalamika kuna maana kwamba, nguvu zetu tumezipeleka kwenye kuamini kwamba tatizo ambalo linatukabili hatuliwezi na hatuoni suluhu yoyote.


Hebu fikiria juu ya kulaumu kwako. Hii ni tabia ambayo wote tunaiona ni sahihi kabisa kwa sababu ya mazoea tu. Tunapolaumu, bila kujua tunaiambia dunia pamoja na sisi wenyewe kwamba, hatuna nguvu, bali kuna wenye nguvu zaidi kuliko sisi ambao wameshindwa kutuwezesha au kutugawia. Fikiria tena tokea umeanza kulaumu katika maisha yako ni kati kikubwa ambacho umevuna, zaidi ya kuharibu maisha yako?

Kwa kulaumu, tunatupa nguvu na uwezo uwezo wetu wa kubaki watupu. Kwa kuwa kila binadamu anapaswa kuwajibika kwa maisha yake, kulaumu tuna maana kwamba tumeshindwa wajibu wetu. Tunaamua kwa kusudi kabisa kuwa wahanga wa maisha yetu, uamuzi ambao haupendezi. Badala ya kulaumu sana, jifunze kukaa chini na kuchukua hatua ambazo zitakusaidia kuelekea kwenye kubadili maisha yako.

Kuna kujilaumu au kujikosoa, tabia ambayo pia ni ya kimazoea. Kumbuka, kile kinachoenda ndani, kwenye kufikiri kwetu, ndicho chenye kujionesha nje. Kwa kuwa maisha hutupatia kile tunachokihitaji, kwa kujilaumu au kujikosoa, tunachopata ni maumivu ya jambo tunalojilaumu kwalo. Tunapojiambia kwamba, sisi ni wajinga kwa sababu tumeshindwa  biashara fulani, ni lazima tutakuwa wajinga kweli, kwani hicho ndicho tunachokitaka.

Badala ya kujikosoa tunapofanya jambo kinyume na matarajio yetu na tunakuta tunataka kujilaumu, inabidi tuchukue kalamu na karatasi na kuandika yale yote ambayo ni mazuri kwa upande wetu. Tunayo mazuri mengi, kila mtu ana mazuri mengi. Hivyo, hatuna haja ya kujikosoa kwa mabaya yetu, kwani hayo siyo tunayoyahitaji. Unachohitaji wewe ni kuachana na kujikosoa sana na kusonga mbele.

Kila tunapojikosoa, tunapaswa kujua kwamba, tunazuia nguvu nyingi chanya kuweza kutufikia na kutusaidia tunakotaka kwenda. Hii ni kwa sababu tunayaambia mawazo ya kina kwamba, hatustahili kupata mema au mazuri. Kumbuka, maishani huwa tunakipata kile tunachokitaka au kukitarajia. Kama utakuwa tu wewe ni wa kujikosoa sana, itakuwa ni sawa na kujiambia hutaki mafanikio makubwa maishani mwako.

Kunakuwakosoa wengine kimazoea. Kwa mazoea, tabia hii huwa tunaiona kuwa ni ya kawaida sana na haina madhara kwetu. Huwa tuaamini kwamba, tuna haki ya kukosoa wengine na jambo hilo haliwezi kutudhuru. Kwa kuwahukumu wengine vibaya au kuwakosoa , tunatengeneza vurugu na ukosefu wa amani kwenye mfumo wetu wa kufikiri na ufahamu. Hii ni kwa sababu, tunaupeleka uzingativu wetu kwenye jambo ambalo hatulitaki.

Kijicho ni tabia ambayo wengi tunadhani au kuamini kwamba, ni lazima tuwe nayo. Lakini kijicho ni dalili ya mtu kuamini kwamba yeye hawezi kama huyo anayemwonea kijicho na hatakuja kuweza. Kuwa na kijicho ni moja ya tabia ya kimazoea ambayo huwa inauwezo mkubwa wa kuharibu maisha yetu wenyewe bila kujijua.

Jaribu kufikiria au kutazama ule uzoefu mzuri kuhusu maisha na siyo usioutaka. Jaribu kuangalia yale tu unayoyapenda kwa watu kuhusu watu wengine.  Kisha jenga tabia nzuri ambazo zitakusadia katika maisha yako na achana na kufikiri kimazoea ambako hakuwezi kukusidia kitu zaidi ya kukupa maumivu tu. Hivyo ndivyo kufikiri kimazoea kunavyoweza kuharibu maisha yako.

Nakutakia mafanikio mema, ansante kwa kutembelea matandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO na endelea kwashirikisha wengine kujifunza mambo mazuri yanayoendelea hapa.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE.

IMANI NGWANGWALU,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.