google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 28, 2018

Wanaoficha Pete Za Ndoa Hawajui Kupenda.

No comments :
Unapomkuta mwanamke au mwanaume ambaye yuko kwenye ndoa, amevua au huwa anavua pete yake ya ndoa mara kwa mara na kuiweka kwenye mkoba wake au mfukoni, utasemaje?
Ni lazima kuna namna ambayo utamfikiria mtu huyo. Je, utamfikiria kwamba ni malaya, haridhiswi na ndoa yake, au hampendi mumewe au mkewe?
Hapa nitajaribu kutoa maelezo ambayo, yatakufanya usihisi vibaya kwa kile ambacho, umekuwa ukikifikiria kuhusu mwanamke au mwanaume wa aina hiyo.
Imeelezwa kwamba, wale wanawake au wanaume ambao, huficha pete zao za ndoa, ni watu ambao hawana uwezo wa kulea watoto, yaani huwa wanawapuuza sana watoto wao.
Kwa kulinganisha, inaelezwa kwamba, wale wanawake au wanaume wenye kuvua au kupenda kuvua pete zao za ndoa na kuziweka mikobani, huwa wanawapuuza watoto wao kuliko wale ambao, huvaa pete zao muda wote.

Weka wazi pete yako ni ishara ya upendo.
Lakini pia, inaelezwa kwamba wale wanawake au wanaume wenye sura za kuvutia au nzuri sana wanapokuwa na tabia hii ya kuficha pete zao za ndoa, huwa ni wazazi wasioweza hata chembe kulea watoto wao, yaani wanakuwa ni wazazi aambao, ni watekelezaji sana, wasiojali kabisa kuhusu watoto wao.
Katika moja ya tafiti zake mwanasaikokoljia Andrew Harell wa chuo kikuu cha Alberta nchini Canada, anasema kwamba, hili sio suala la kubahatisha, kwani amelifanyia utafiti kwa wengi, kwa muda mrefu na katika mazingira tofauti.
Mwanasaikolojia huyo anazidi kudai kwamba, hata linapokuja suala la kuangalia na kutunza wagonjwa, wale watu wanaoficha pete zao za ndoa, hawana uwezo wa kuwatunza wagonjwa ukilinganisha na wale wenye kuvaa pete.
Inaelezwa kwamba, kuvua pete ya harusi na kuificha ni ishara kwamba, mwenye pete hiyo hana hisia au uwezo wa kujifunga na ndoa yake au familia yake. Kwa kukosa sifa hizo, ni wazi mtu huyo hawawezi kujifunga na watu wengine wenye kuhitaji msaada wake wa kihisia kama vile wagonjwa.
Kuvua au kuficha pete ya ndoa, kunahesabiwa kama ni dalili ya mtu kutaka kuanzisha uhusiano mpya nje ya ndoa yake. Haja hiyo inapotimizwa, uwezekano ni mkubwa kwa mwanaume au mwanamke kupunguza upendo au kujali familia yake, akiwemo mke au mume au watoto. Kwa hali hiyo, kuficha pete ni dalili ya kutokujali na kushindwa kujifunga kwenye uhusiano.
Wakati huo huo taarifa za kitafiti zinaonyesha kwamba, wazazi wenye kuvua pete huwa hawatoi uangalifu mkubwa kwa watoto wao wenye sura mbaya, ukilinganisha na ule wanaoutoa kwa watoto wao wenye sura za kuvutia au wazuri.
Katika moja ya tafiti zilizowahi kufanywa, zilihusisha  wazazi na watunza watoto walioenda na watoto hao kwenye supermarkert. Ilionekana kwamba, wale watoto wasiopendeza, waliachwa kwa umbali mkubwa bila wazazi wao kujali, wakati wale watoto wenye kuvutia, wazazi au walezi walikuwa nao karibu sana.
Tafiti zote hizo zinajaribu kuonyesha upo uhusiano mkubwa sana kati ya kitendo cha kuvua pete na suala zima la kujali. Je, hali hiyo kwako ikoje? Huu ni utafiti tu, wewe je, unasemaje?
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku. Pia chukua jukumu la kumshirikisha mwingine, ili aweze kujifunza na kunufaika na masomo yanayotolewa humu.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA ESTHER ZACHARIAH, DAR ES SALAAM.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.