google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 28, 2017

Wakati Bora Wa Kufikia Mafanikio Yako Ni Huu…

No comments :


Leo nimejikuta namkumbuka sana mwalimu wangu wa somo la Kiswahili, moja kati ya vitu ambavyo vimenifanya niweze kumkumbuka ni vile ambavyo alikuwa anajitoa kwa hali na mali katika kuhakikisha tunaelewa somo la Kiswahili. Ni siku nyingi kidogo zimepita lakini kile ambacho alinifundisha bado hakijafutika  akili mwangu, na sina uhakika kama kitakuja kufutika.

Mwalimu wangu huyu  sitachoka kumuombea kwa mwenyezi  Mungu kwa kila jambo ambalo analifanya aweze kufanikiwa Zaidi. Namkumbuka kwa sababu kuna somo ambalo alitufundisha kwa kutumia nguvu zote, somo hili ni somo la nyakati.

Na katika somo hili alisema zipo nyakati mbalimbali ambazo ni wakati uliopita, wakati uliopo na wakati ujao. Pia alieleza ya kwamba nyakati hizi zote humuhusu mwanadamu, katika kufanya na kusimulia mambo mbalimbali ambayo yalikwisha fanyika au ambayo yatafanyika.

Na miongoni mwa vitu ambavyo nakumbuka aliweza kutushauri kuhusu nyakati hizi alisema ya kwamba,  mwanadamu yeyote yule ili aweze kufanikiwa katika maisha yake ni lazima aweze kutambua ya kwamba katika nyakati hizo ni nyakati moja tu ndiyo muhimu kwake.

Na nyakati hiyo ni wakati uliopo na si vinginevyo, kwani wakati uliopita na wakati ujao si rafiki kwa mwadamu hata kidogo katika kutenda mambo ya msingi, kwani watu wengi wamekufa na ndoto zao kwa sababu waliamini Zaidi nyakati zijazo, wao pamoja na kuwa na mambo mazuri walijifariji na kusema nitafanya kesho, kesho hiyo ikawa kesho mpaka siku wakazikwa na neno lao nitafanya kesho.

Kwa maneno mengine kusema nitafanya kesho, kwa neno moja lenye kujifariji tunasema“nimeahirisha”. Neno hili ni baya sana kwani wale wote waliofanya kitendo hiki hawakuweza kufikia lengo lao kwa asilimia zote. Kuahirisha kufanya jambo la msingi ni kutafuta visingizio.

Hivyo kama wewe ni mtu wa kuahirisha sana mambo, hasa kwa kile kitu unachokifanya, elewa kabisa unapanda mbegu au unajitengenezea mazingira ya kushindwa kwako. Kama kuna jambo ambalo unataka kulifanya leo, hebu lifanye bila kusita sita au bila kuwa na shaka ya kitu chochote.

Hivyo kama kweli unataka mafanikio ya kweli jifunze kufanya mambo kwa wakati, huku ukikimbia visingizio visivyokuwa vya msingi. Daima ikumbukwe  ya kwamba ni heri upate ugonjwa wa malaria, kwani ugonjwa  huu utatibika,Ila ukipata ugonjwa wa kuahirisha mambo ya msingi basi jiandae kufa maskini.

Mwisho nikuache na nukuu isemayo; Kumbuka ukianza leo si sawa na kuanza kesho.

Imeandikwa na uongozi wa mtandao huu wa dira ya mafanikio,
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.