google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 27, 2017

Hatua Hizi Ni Msingi Wa Mafanikio Yako.

No comments :

Kuna yale mambo ambayo kwenye maisha huwa yanaonekana ni rahisi kabisa kufanyika na pengine kukupa mafanikio. Hata hivyo kitu cha kushangaza mambo hayo pamoja na urahisi wake wengi huwa hawayafanyi.
Hali hiyo huwa inatokea kwako kwa sababu ya kujikuta upo katika hali ya ‘easy to do…also easy not do,’ yaani urahisi kwa hali ya kawaida unauona, Lakini ndani yake kuna ugumu fulani hivi ambao unakuzuia kufanikiwa.
Ukweli wa mambo ulivyo kwenye maisha yako, iwe afya, furaha au utajiri unaweza kuvipata ikiwa utachukua hatua ndogo ndogo kila siku zile zinazowezekana ambazo zitakusogeza kwenye lengo lako bila kudharau hatua yoyote ile.
Kama ni rahisi hivyo, kwa nini watu wengi wanashindwa kufikia malengo yao? Hiyo yote ni kwa sababu ‘easy to do…also easy not do,’ kama tulivyosema. Hatua ndogo ndogo zinakuwa ni ngumu sana kuweza kutekelezwa na wengi wetu.
Jiulize ni mambo mangapi katika maisha yako ulipoambiwa fanya kitu hiki, ulisema kwamba, ‘aaah kitu hiki ni rahisi, nitakifanya tu’. Lakini mwisho wa siku unajikuta unashindwa kuchukua hatua kabisa.
Kuanzia sasa, acha kuwa mtumwa wa ‘easy to do…also not easy to do.’ Chukua hatua ndogo ndogo bila kudharau udogo wa hatua hiyo. Ukifanya hivyo utaweza kufanikiwa na kutimiza ndoto zako.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.