google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 7, 2022

Jinsi Ya Kukabiliana Na Kukatishwa Tamaa.

No comments :



Ili kuishi maisha yako bora, unatakiwa ujifunze JINSI YA KUKABILIANA NA KUKATISHWA TAMAA, Kimsingi, hakuna mtu ambae hakatishwi tamaa, kila mtu kwenye maisha yake anakatishwa tamaa kwa namna moja au nyingine.

Kuna wanaokatishwa tamaa na mambo madogo madogo kama kukosa karo ya shule, kushindwa kupata mkopo, biashara kushindwa kwenda vizuri au kuchelewa usafiri, kushindwa kuongezewa mshahara na kushindwa kuvuna unavyotaka.

Kuna wanaokatishwa na mambo makubwa kama kufiwa na umpendae, kupoteza kazi, kuambiwa una ugonjwa ambao huwezi kupona, nyumba au biashara kuungua, ajali, kuachishwa kazi, ndoa kuvunjika, ajali inayokupa ulemavu na mengineyo.

Kwa vyovyote vile iwavyo,  unapokatishwa tamaa na jambo lolote lile, kitu kikubwa kinachotokea kwako, IMANI YAKO INAKWENDA KUTIKISWA, Utaanza kuona kila kitu hakifai, hata kama ulikuwa na imani kubwa inashuka chini na kujikuta kushindwa kuchukua hatua.

Kitu cha kufanya hali ya kukatishwa tamaa inavyoingia ndani mwako, jitahidi sana kusahau yote yaliyokukatisha tamaa. Unatakiwa jiambie, YALIYOPITA YAMEPITA na sasa ni wakati wa kusonga mbele.

Usiruhusu YALIYOPITA yaharibu kesho yako. Usikae kwa kuendelea kuvunjika moyo kwa sababu ya matukio ambayo tayari YAMEPITA. Weka nguvu za uzingativu kwa yale unayoweza kubadilisha tu. Anzia hapo ulipo na hapo utaweza kukabiliana na kukatishwa tamaa.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno  WINNER'S FAMILY kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.