google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 6, 2021

Njia mbili ziletazo mafanikio maishani.

No comments :

 

Katika kufikia mafanikio yoyote yale, huwa zipo njia za kuweza kufikia mafanikio hayo. Hakuna mafanikio ambayo yanapatikana nje ya njia husika za mafanikio.

Na kwa kawaida, zipo njia mbili bora za kuufikia mafanikio. Hizi ni njia halali ambazo zinatumiwa na watu wote wenye mafanikio ya kweli na halali duniani.

Njia ya kwanza; Njia ya kawaida.

Hii ni njia ambayo mtu anafikia mafanikio makubwa kutokana na malengo anayoyafatilia kila siku. Hapa lazima uwe na malengo ya kuyafatilia kila siku.

Katika njia hii unakuwa na malengo yako, lakini wakati huo huo unakuwa unaenda nayo mdogo mdogo hadi kuweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Hii ni njia bora, inayoaminika, kwa sababu kuna kujifunza mengi ndani yake, ingawa inataka muda na uvumilivu, lakini mwisho wa siku utafika.

Njia ya pili; Njia isiyo ya kawaida.

Hii ni njia isiyo ya kawaida kwa sababu ndani yake kuna kuwa na hali hatarishi nyingi. Kwa mfano, kuna kuweka mtaji mkubwa ndani yake au kuchukua hatua kubwa kabisa.

Katika kutekeleza njia hii iko hivi, unakuwa unafata njia ile ya kawaida kama kawaida, isipokuwa katika njia hii kuna vitu ambavyo vinaongezeka.

Katika njia hii lazima utenge kiasi fulani cha pesa, ili kuingiza katika 'dili' ambazo zinajitokeza kati kati lakini wakati huo ukiendelea na njia ya kwanza.

Kufata njia ya pili hatumaanishi njia ya kwanza umeiacha, hapana unakuwa nayo,  isipokuwa hii unaitumia kama ziada kutengenezea pesa ndefu.

Hizi ndio njia kubwa mbili, ambazo zinatumiwa na watu wengi wenye mafanikio kuweza kufanikiwa. Ni muhimu kutumia njia zote mbili ili kujihakikishia mafanikio.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

Oct 5, 2021

Zingatia Jambo Hili Sana, Litakusaidia Kufanikiwa.

No comments :

Inapotokea kuna kitu hukijui, kuwa mtu wa shukrani, kwa sababu umepata fursa nzuri ya kujifunza juu ya kitu hicho.

Inapotokea unapitia magumu katika maisha yako, shukuru pia, kwani magumu hayo yanakufanya uwe bora na imara.

Ikiwa pia unapitia changamoto sana, huo sio wakati wa kukimbia, bali ni wakati wako wa kujiboresha kimaisha.

Unapokuwa umechoka kwa sababu ya kazi, basi pia huo ni muda wa kushukuru, kwa sababu kuna mabadiliko umefanya.

Kama umefanya makosa, pia shukuru, kwa sababu hiyo inakukumbusha ni kipi ambacho hutakiwi tena kukifanya.

Ni rahisi sana kuwa na shukrani na mambo mazuri, lakini pia jifunze kuwa na shukrani hata kwenye changamoto.

Watu wengi si wepesi sana wa kushukuru pale wanapokutana na magumu. Ni watu ambao wanakuwa hawaoni zuri lolote.

Kipo kitu chanya au kizuri unaweza kukiona pia kwenye changamoto. Usilalamike, jifunze kupitia changamoto yako.

Yapo mafanikio na  baraka ambazo zimejificha kwenye changamoto. Unatakiwa uyaone mafanikio hayo.

Changamoto unazopitia zina uwezo wa kukufanya, ujifunze, ukue na kuwa jasiri wa kufikia mafanikio yako.

Zingatia, mafanikio yako utaendelea kuyapata kama utakuwa mtu wa shukrani katika kila eneo la maisha yako. 

Kuwa na shukrani ni msingi mkubwa sana wa mafanikio yako. Anza leo kuwa mtu wa shukrani, utafanikiwa.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

Oct 4, 2021

Mawazo Kumi (10) Yatakayokupa Nguvu Kubwa Yakufikia Mafanikio Yako.

No comments :
Mafanikio siku zote yanaanza na mawazo. Kama hakuna wazo sahihi ieleweke pia hakuna mafanikio sahihi ambayo yataweza kuchipua kwa nje, sana sana  utakuwa ni mtu wa kushindwa kila wakati. Kupitia makala haya utajifunza mawazo muhimu yatakusaidia kuweza kufikia mafanikio yako. Karibu na twende tujifunze;-
1. Usifanye maamuzi kwa muhemko kwani utaahirisha tu, ni wachache wanaofanikiwa na maamuzi ya muhemko. Kwa mfano, utakuta mtu kasikia habari kwamba biashara ya aina fulani inalipa, mtu huyo utakuta anakurupuka na kujikuta kwenye wakati mgumu sana wa kuweza kushindwa. Kabla hujafanya maamuzi, tafakari kwanza.
2. Usitake mafanikio kama unavyotaka wewe. Mafanikio yana njia yake na misingi yake pia. Kama unataka mafanikio kwa jinsi unavyotaka wewe na unategemea utayapata huo ni uongo hutaweza kuyapata. Futa njia, kanuni na miiko ya mafanikio inasema nini utafanikiwa. Ulikilazimisha kufanikiwa kama unavyotaka wewe, haitawezekana.
3. Usikae tu na kusubiri mambo yatokee, utajichelewesha sana. Amua kupambana kufanya mambo yaweze kutokea na hiyo itakusaidia sana kuweza kufanikiwa. Kuwa mtu wa kulazimisha matokeo uyatakayo na uyapate. Kusubiri subiri tu mambo yajiendee, utajikuta unasubiri sana na mambo hayawi kama utakavyo, komaa.

4. Kama unaona maisha yako ni magumu sana, rudi kwenye mawazo yako, rudi na uende ukaanze kufikiri upya tena, maana ugumu wa kila kitu unaanzia kwenye akili na si kwingine tena. Inawezekana maisha yako ni magumu kwa sababu umeshindwa kuifikirisha akili yako vya kutosha, fikiri hili na chukua hatua.                                                                               
5. Kuwa tayari kwa wakati ufaao na wakati usiofaa kwenye maisha. Kuna wakati maisha yanakutaka uwe tayari hata wakati wewe unajiona hauko tayari iwe hivyo. Unatakiwqa uwe kama mwanajeshi kwa kuamua kufanya chochote kile na wakayi wowote ule ilimradi tu kuyafanya maisha yako yasogee mbele  na kuleta mafanikio yatakiwayo.
6. Fanya ufanyalo kwenye maisha yako, lakini hakikisha uwe una kitu cha watu kujifunza kwako. Usiishie kujifunza kwa wengine ila hakikisha watu nao wajifunze kwako kupitia wewe kama wewe. Fanya vitu ambavyo watu watakuiga na wakuone kwamba wewe ni mfano wa kuigwa na wakufate nakufanya maisha yao kuwa bora.
7. Ukiwa unafanya kazi, hakikisha uwe una kitu cha kuuza yaani una bidhaa ambayo unaweza ukawauzia watu na wakanunua kwako. Fanya ufanyalo lakini hakikisha uwe na pesa ya ziada, pesa hiyo ya ziada au akiba itakusaidia. Anza kuuza kitu ambacho kitakusaidia sana kuweza kukuza uchumi wako nje ya kazi uifanyao.
8. Kila mtu anaweza akawa na wasiwasi na wewe, lakini ukijitoa na kuamua basi kila kitu kinawezekana kwako na utafanya maajabu makubwa kwako. Jiamini kwamba unaweza ukafanya mambo makubwa maishani mwako hata kama hakuna mtu anayekuamini. Jiamini wewe kama wewe na utatoboa na kufikia mafanikio makubwa.
9. Weka juhudi sana kwa kila unachokifanya pasipo kuyumbishwa na wakati unaweka juhudi ili uweze kwenda mbele zaidi kubali kujifunza kwa kukosolewa. Bila ya juhudi, kukubali kukosolewa au kuelekezwa kwa usivyojua, hauwezi kwenda. Kukosolewa si dhambi, wewe kosolewa na kubali kujifunza na utafanikiwa pa kubwa.
10. Kila jambo lifanye kwa wakati wake. Kama kwako upo kwenye muda wa kuwekeza, nikwambie tu wekeza sana na mtu asikutanie katika hilo. Usipoteze muda mwingi sana kwa kuwaza kwamba muda upo pale pale au unakusubiri, utapotea. Utumie muda wako kufanya yale yaliyo ya msingi na yale ambayo yatakusaidia kufanikiwa.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.

Oct 3, 2021

Weka Umakini Wako Wote Kwenye Vitu Hivi Na Utafanikiwa.

1 comment :
Kila wakati zingatia kile kinacholeta mabadiliko sana kwenye maisha na unatakiwa kuachana na kile ambacho hakileti mabadiliko kwenye maisha yako. Kama unaendelea kufanya vitu ambavyo havileti matokeo chanya kwako huko ni kujipoteza.
Kwa maana hiyo, kama kuna kitu unataka kukifanya unatakiwa ujiulize je, kitu hiki kina mchango kiasi gani katika kuweza kufanikisha ndoto zangu. Kama unaona kitu hicho hakina machango wowote ni jukumu lako kuweza kuachana nacho mara moja.
Kila wakati weka nguvu zako, muda wako na umakini wako wote kwenye vile vitu ambavyo vinaleta matokeo kwako ya mafanikio tu. Haina maana kupoteza nguvu zako nyingi kwa kufanya kitu ambacho hakina msaada kwako, utakuwa unapotea sana.
Kila wakati ijaze akili yako  mawazo chanya yatakayokusaidia wewe kuweza kufikia ndoto zako. Kila wakati weka juhudi sahihi za kukusaidia kuweza kufanikiwa kwa kufanya vitu vinavyoendana na ndoto yako unayoitaka kuifanikisha.

Usijaribu kupoteza nguvu zako kwa kufanya mambo ambayo hayakusaidii kuweza kutimiza ndoto zako. Ishi kwa faida kwa kufanya mambo ambayo yanakusaidia kuweza kutimiza ndoto zako, kinyume cha hapo hutaweza kufikia ndoto zako.
Tatizo la watu wengi wanapoelekea kwenye kufikia ndoto zao, wanakuwa wanaweka umakini wao kwenye vitu ambavyo hata haviwasaidii. Kwa kufanya vitu hivyo watu hao ndio hujikuta wakipotea karibu kila wakati kwenye kufanikisha ndoto zao.
Ili uweze kufikia ndoto zako, fanya ufanyalo, lakini hakikisha unaweka umakini wako wote kwenye vitu vya msingi vinavyokusaidia kutimiza ndoto zako. Kwa kufanya vitu hivyo ni kweli ndoto zako utaweza kuzifikia hata kama unakutana na changamoto nyingi.
Usiendelee kusita, usiendelee kusubiri, kama unataka kufanikiwa weka nguvu zako zote kwenye mambo yanayoweza kukupa mafanikio. Kama nilivyosema watu wengi hawaweki sana nguvu zao kwenye mambo yaletayo mafanikio yao, zingatia hilo.

Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.


Oct 2, 2021

Jinsi Ya Kupika Tambi Za Mayai.

No comments :
Najua kila wakati tumekuwa tukikuletea makala mbalimbali ambazo kimsingi zimekuwa zikikusaidia kwa namna moja ama nyingine katika kuulisha ubongo chakula ya akili. Au kwa maneno mengine elimu ambayo umekuwa ukiipata hapa imekuwa ikikusaidia kuzaliwa upya kifikra hatimaye kutimiza kusudio lako hapa duniani.

Lakini katika makala ya leo nataka tujikite katika masuala mazima ya mapishi. Najua utakuwa unashangaa vipi leo afisa mipango kuleta somo hili. Wala usishangae kila kitu ambacho unakiona katika dunia hii ni fursa.  Inawezekana kabisa ukawa hauna lengo la kupika aina hii cha chakula. 

Ila kutokana na ulichojifunza hapa kukusaidia kutoa elimu kwa watu wengine na wao wakalipa pesa au chakula hiki unaweza ukakipika katika sehemu mbalimbali kama katika sherehe mbalimbali na wageni waalikwa na wasio waalikwa wakafurahia aina hii cha chakula. 


Au unaweza ukapika aina hii ya chakula kwa ajili ya biashara kama vile kwenye mahoteli, migahawa na sehemu nyinginezo.

Hebu tuangalie mahitaji kwa ajili ya kupika aina hii cha chakula. 

1. Tambi 1/2 paket
2. Vitunguu maji 2 vikubwa
Karoti 1
3. Vitunguu swaumu kijiko 1 cha chakula
4. Carry powder kijiko 1 cha chai
pilipili hoho 1
5. Njegere zilizo chemshwa 1/2 kikombe
6. Mafuta ya kupikia kiasi
7. Chumvi kwa ladha upendayo

MAANDALIZI YA CHAKULA HIKI

a) Chemsha maji yachemke haswaa, tia chumvi na mafuta kiasi, weka tambi katika maji yaliyo chemka ziache ziive kiasi; kisha chuja maji na uziache kavu.

b) Chukua bakuli pasua mayai kisha weka pembeni.

c) Chukua kikaango kilicho safi weka jikoni tia mafuta kiasi na utaendelelea kuweka vitunguu maji,vitunguu swaumu,hoho ,karoti na carry powder,kaanga kwa pamoja katika moto mdogo mdogo na havitakiwi kuiva sana.

d) Kisha tia tambi na njegere katika mchanganyiko wako na uendelee kukaanga kwa dakika kadhaa.

e) Chukua mayai tia katika tambi ongeza moto kiasi, ili tambi zako zichambuke ,moto hautakiwi kuwa mdogo sana ikiwa moto ni mdogo tambi zako zitashikana na kutia mabonge , mayai ya kiiva hapo chakula chako kitakuwa tayari kwa kuliwa.

Mpaka kufikia hapa chakula chako kitakuwa tayari kwa ajili ya kuliwa, chakula hiki wakati wa kula unaweza ukawa unashushia na juisi ambayo unayopendelea kunywa. 

"Mwili hujengwi kwa mawe bali hujengwa kwa kula"
 Ndimi Afisa Mipango Benson Chonya. 

Oct 1, 2021

Hiki Ndicho Kitu Kinachokuzuia Kufanya Mabadiliko Kwenye Maisha Yako.

No comments :
Ikiwa kila wakati unajaribu kufanya mabadiliko ya kitu fulani na unashindwa kuleta mabadiliko hayo, basi tambua maumivu ya kushindwa hayajawa makubwa sana ndani yako hadi uweze kuleta mabadiliko hayo.
Kwa mfano, unataka kuwa na mtaji na unashindwa kila mara, basi elewa kabisa maumivu ya kushindwa kupata mtaji hayajawa makubwa vya kutosha. Tuchukulie leo hii, ukaambiwa usipokuwa na mtaji hadi mwaka huu unaisha, utapigwa risasi.
Jiulize utakubali kufa kwa sababu ya kukosa mtaji huo unaoutaka? Bila shaka haitawezekana, utafanya kila linalowezekana kufanikisha hilo. Hivyo, wakati mwingine mabadiliko yanakuja kwenye maisha yako kwa sababu ya kule kuumia sana.

Wakati ulipokuwa shule ulisoma sana na kuhakikisha unafaulu ili kukwepa maumivu ya kufeli. Pia kuna wakati umeweka juhudi nyingi sana ili kukwepa maumivu ya aina fulani na kutafuta mahala sahihi kwako.  

Tunaambiwa kitu chenye nguvu ya kubadili tabia yako na mafanikio ni maumivu. Waulize wote ambao wamefanikiwa na ambao wanafikiri chanya kuhusu mafanikio, watakwambia maumivu yamewasaidia sana kubadilika na kuweza kufika hapo walipo mpaka leo.
Kitu kinachokuzuia wewe kufanya mabadiliko kwenye maisha yako ni maumivu, hujawa na maumivu ya kutosha kuweza kubadilisha maisha yako. Ikiwa utakuwa na maumivu hayo, hutakubali, utafanya kila njia kubadilisha maisha yako.
Tunajua sote maumivu yanauma, kama maumivu yanauma, huwezi kukubali ukabaki na maumivu hayo kwako, lazima utatafuta njia ya kubadilisha maumivu hayo. Hivyo, kila wakati pambana kuweza kuleta mabadiliko juu ya maisha yako.
Mwisho kabisa niseme kwako hivi, utabadili maisha yako, ikiwa utakuwa una uchungu na maumivu ya kutosha, maumivu ya kuchoshwa na hali mbaya uliyonayo na kutaka kubadili maisha yako kabisa, hapo mabadiliko utayaona.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kumbuka, ufalme hauji kwa maneno bali unakuja kwa vitendo,...chukua hatua. 
Nikutakie kila la kheri,
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA NDOTO ZAKO ZITUMIE.