google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Sep 30, 2021

Njia Pekee Itakayokufanya Ukawa Hodari Ni Hii…

No comments :
Kuna watu ambao huwa wanatamani sana, wawe hodari katika jambo fulani. Watu hao hufika mahali hata kuwatamani watu ambao ni mahodari katika maisha yao na kujiuliza wamefikaje huko kwenye uhodari huo.
Nikwambie, ipo njia moja kubwa ya kukufanya ukawa hodari kwa kile unachokifanya, njia hiyo si nyingine bali ni kufanya kitu hicho kila siku bila kuacha. Kama utafanya jambo hilo kila siku na kwa njia tofauti za kujifunza basi utakuwa hodari.
Unapofanya jambo hilo kila siku, unatengeneza uhodari mkubwa sana ndani yako na mwisho wa siku unajikuta ni mshindi katika hilo eneo. Ukiwa unafanya jambo na kuliacha, huo uhodari utaupoteza tu.


Jiulize unataka kuwa hodari katika jambo lipi? Ukishapata jambo hili ambalo unataka kuwa hodari, anza utekelezaji wa kulifanya jambo hilo kila siku na kwa juhudi zote. Usijaribu kufanya na halafu ukaacha, hautaweza kuujenga uhodari kwa namna hiyo.
Watu wenye mafanikio, watu ambao unawaona wamefanikiwa, wamekazana kujenga uhodari kwa kuchagua kufanya kitu kimoja kwa muda mrefu na si kugusa gusa na kuacha halafu ukategemea ukawa hodari.
Angalia maisha ya wanamichezo walio hodari ni kipi wanachokifanya, angalia maisha ya wajasiriamali wakubwa ni kipi wanafanya, utagundua ni watu ambao wameamua kuweka nguvu zao kwenye jambo moja kwa muda mrefu na kutengeneza uhodari.
Acha kuwa na ndoto za kukurupuka na kusema kwamba unataka kuwa hodari, unataka kufanikiwa sana na halafu kitu hicho unachotaka kukifanya hukifanyi kila siku. Kama haufanyi kila siku sahau mafanikio hayo unayoyataka.
Kama wewe ni mwimbaji, hebu imba kila siku. Kama wewe ni mwandishi, hebu andika kila siku, kama wewe mchoraji, chora kila siku na fanya hivyo kwa miaka kumi, na huku ukijifunza tuone kama hujawa hodari.
Ukiona vya elewa ujue vimeumbwa, hivyo ndivyo wahengfa walivyosema na hawakukosea hata kidogo. Na vivyo hivyo ukitaka uhodari, acha kujidanganya, kaza buti na fanya kila siku jambo lako litakupa mafanikio tu.
Hakuna uchawi wala muujiza kwenye kutafuta uhodari. Ule uhodari unaoutafuta kila wakati upo kwenye kufanya kila siku na tena ikiwezekana unaamua kufanya maisha yako yote pasipo hata kukwama mara moja, ukifanya hivyo nakwambia utafanikiwa.
Kumbuka, uhodari unakuja kwa wewe kuamua kufanya jambo unalolitaka kila siku. Amua leo kuutafuta uhodari wako mpaka watu washangae, kumbe siri kubwa ya uhodari huo inakuwa imejificha kwa wewe kuamua kufanya kila siku.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNERS, kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kumbuka, ufalme hauji kwa maneno bali unakuja kwa vitendo,...chukua hatua. 
Nikutakie kila la kheri,
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA NDOTO ZAKO ZITUMIE,


Sep 29, 2021

Sababu Nne (4) Kwa Nini Maisha Yanazidi Kuwa Magumu Kwa Wengine.

No comments :
Kwa miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na wimbi kubwa la watu linalalamika kwamba maisha yamekewa magumu. Kwa sababu hii pia watu wengi wamekuwa wakikata tamaa na kuona maisha hayafai ni bora waishi hivyo hivyo ilimradi siku ziende.
Malalamiko ya maisha kuzidi kuwa magumu yamekuwa yakisikika sana karibu ulimwenguni kote. Na kwa hili  hiyo imekuwa ikipunguza raha ya kuona ‘utamu’ wa maisha halisi. Si vijana wala wazee kila mtu amekuwa akisema lake juu ya ugumu wa maisha.
Lakini pamoja na malalamiko hayo, kitu ambacho tunatakiwa tujiulize nini kinachopelekea kuwe na ugumu wa maisha kila kukicha? Makala haya ya leo inakwenda kukupa majibu kwa nini  maisha yanakuwa magumu kwa wengi zaidi.

1. Kutegemea chanzo kimoja cha mapato.
Kutokana na maisha kubadilika na gharama za maisha kupanda karibu kila siku, suala la kutegemea kipato kimoja, ni moja ya chanzo cha maisha kuwa magumu. Watu wengi wanategemea kipato kimoja, zaidi kwa wengi ikiwa ni ajira.
Kwa bahati mbaya kipato kimoja hakiwezi kukidhi mahitaji yote hata iweje. Sasa kwa sababu hiyo ya maisha kupanda mara kwa mara, ni lazima tu ugumu wa maisha uonekane. Hata siku moja usitegemee maisha yako yakawa rahisi kama bado una kipato kimoja.
2. Watu wengi wanafanya vitu wasivyovipenda.
Maisha ni magumu pia kwa watu wengi chini ya jua kwa sababu wamekuwa ni watu ambao kila siku wanafanya kazi ambazo wasizozipenda. Kama unafanya kazi usiyoipenda, unategemea nini, lazima maisha yatakuwa magumu tu.
Kufanya kazi usiyoipenda, kwa kawaida kunakuwa kunakuchosha sana na unakuwa unaifanya tu, kwa sababu eti upate pesa ya kula. Kama umechagua maisha hayo, ujue kabisa maisha hayo yatazidi kukufanya wewe uyaone magumu kila kukicha.
3. Watu wengi wanaishi juu ya matumizi.
Ugumu wa maisha pia kwa namna moja au nyingine unachangizwa na watu kuishi juu ya matumizi au vipato vyao halali. Unatakiwa kuelewa watu wengi, wanaishi juu ya matumizi kwa sababu ni watu ambao wanataka waonekane wamefanikiwa.
Watu hawa wanakuwa wapo tayari wakope au wafanye lolote lile ili waonekane mambo yao yako safi. Kwa msingi huo wanakuwa wanajitengenezea maisha magumu ambayo wanashindwa kuyamudu kwa urahisi na matokeo yake kuongeza ugumu usio na sababu.
4. Hakuna anayejali sana maisha ya wengine.
Maisha ya sasa hivi naweza kusema yamekuwa ni kama ya kuishi kisiwani, watu wamekuwa hawajali sana watu wengine kwa kiasi kikubwa, ukilinganisha na zamani. Kwa sasa ukipata changamoto kubwa wewe jua hiyo ni changamoto yako tu, inabidi ukomae nayo hadi utoke.
Kutokana na hili kuendelea kudumu kunafanya maisha yanazidi kuendelea kuwa magumu sana hadi watu wanakosa msaada ambao ungeweza kuwasaidia. Ubinafsi ambao wengi wanao imekuwa ni kichocheo kikubwa sana cha ugumu wa maisha.
Mwisho, pengine ujiulize, je, maisha yanaendelea kuwa magumu kwako kila kukicha? Jibu unalo wewe, nimekupa walau sababu chache zinazoonyesha kwa nini maisha yanazidi kuwa magumu. Wewe unaamini nini, niwekee maoni hapo chini.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE.






Sep 28, 2021

Mambo Ya kuzingatia Ukitaka Kufanikiwa Katika Masuala Ya Kifedha.

No comments :
Somo la fedha ni la muhimu sana kwa kila mmoja wetu, hii ni kwa sababu tunashindwa kupata au kudumu katika mafanikio yetu kifedha hii ni kwasababu wengi wetu hutuna uelewa wa kutosha katika suala la kipesa.

Wengi hatuelewi namna ya kupata pesa na namna ya kuzifanya pesa hizo ziendelee kuwa upande wetu, Ila ukweli unabaki palepale siku zote kwamba, ukitaka kufanikiwa kifedha na kufika mbali, unalazimika kujua mambo haya yafutayo;-


 1. Jinsi ya kutawala pesa zako.

Katika maisha yako yote unatakiwa kuwa mtalawa wa fedha zako na sio fedha zikutawale wewe. Wapo wengi wetu wanashindwa kufanikiwa kimaisha  hii ni kwa sababu fedha zimewatawala wao, yaani unaweza ukaona mtu kapata fedha lakini atataka kila kitu nachoikiona akinunue, huku ndiko kunakoitwa kutwaliwa na fedha.

Nini kifanyeke?

Jambo muhimu la kuzingatie ni kila mmoja wetu ahakikishe hatawaliwi na pesa ila yeye ndio anayezitawala pesa hizo. Wewe ndiye unayekuwa na maamuzi sahihi juu ya kuzitumia pesa hizo na si vinginevyo.

2. Jinsi ya kutoka kwenye madeni.

Wakati mwingine madeni ni njia nambari moja imfanyayo mtu awe maskini kama hatakuwa makini mtu huyo, japo wapo baadhi ya watu, wao huamini ya kwamba mfanyabiashara wa kweli haogopi madeni, huko ni kujidanya. Kama una mkopo au madeni ni bora ukawa nayo yale ya biashara zaidi lakini si kwa ajili ya matumizi.

Nini kifanyike?

Hivyo ndugu yangu unatakiwa kuelewa ya kwamba madeni ni mabaya sana hasa ukiwa na hulka ya kujiendekeza katika michezo hii, hivyo kila wakati ili uweze kuwa na uhuru wako binafsi hususani katika uhuru wa kipesa unatakiwa kuondokana na madeni hayo mara moja, kwani madeni ni mabaya sana.

3. Jinsi ya kuongeza kipato.

Mara zote ukitegemea mfereji mmoja kama chanzo chako cha kipato basi fahamu fika maisha yako yatakuwa ni yale yale kila wakati. Ni lazima uwe na njia nyingi za wewe kuweza kukuingizia kipato ili njia hizo zikusaidie kuweza kupiga hatua. Kama una njia moja tu ya kipato, sahau kuwa huru kifedha.

Nini kifanyike?

Jambo la muhimu unalotakiwa kulikumbuka hapa ni kwamba kila wakati ni lazima uwaze kuongeza njia mbadala ya kuongeza kipato chako, na miongoni mwa njia zitakazokusaidia kuwa hivyo ni kuongeza wigo wako wa kutafuta pesa.

4. Jinsi ya kuweka akiba na jinsi ya kuwekeza kwa ajili ya baadae.

Wakati mwingine hatufahamu lile litakalojitokeza siku ya kesho hii ni kwa sababu kesho si rafiki kwetu ila tunaamini siku hiyo ipo, kama tunaamini hivyo basi tunatakiwa kujifunza kuweka akiba kwa ajili ya uwekezaji wa kesho.

Uwekaji wa akiba ni mzuri hii ni kwa sababu miongoni mwa faida itokanayo na kuweka akiba ni kwamba inasadia kutatua changamoto husika kwa muda muafaka hasa unapokuwa haupo vizuri katika suala la kifedha.

Unachotakiwa kufanya?

Ni kuhakikisha kwa kila kipato unachopata unatenga asilimia kadhaa kwa ajili ya akiba hii ni kwa sababu hatujui  likalotokea siku ya kwesho na pia ni faida kuweka akiba kwa sababu itakusaidia kuwekeza.

Hayo ndiyo mambo ya msingi unayaopaswa kufahamu kuhusu fedha.

Ndimi Benson Chonya.

Sep 27, 2021

Silaha Kubwa Ya kufikia Mafanikio Yako Ni Hii.

No comments :

Kati ya kitu muhimu sana cha kukusaidia kufanikiwa, ni akili ya utulivu. Kati ya silaha kubwa ya kukusaidia kufanikiwa, ni akili ya utulivu. Unapokuwa na akili ya utulivu inakusaidia kuona mambo mengi, na kufanikisha mambo mengi pia. 

Si rahisi sana kuweza kufanikiwa sana kama akili yako haijatulia. Unatakiwa ujue, silaha yako kubwa ya mafanikio ni matumizi ya akili yako na wala si bahati au muujiza kama uwazavyo.

Akili yako ina uwezo wa kukupa matokeo makubwa sana kama imetulia, hapa inaweza ikakupa majibu mazuri na ikaleta matokeo ya kushangaza ambayo huwezi kuyaamini.

Hivyo, unatakiwa kila wakati kuchagua mazingira tulivu yatakayoifanya akili yako ifanye kazi kwa utulivu. Unatakiwa kuishi na watu sahihi, wasio na makelele kwako.

Lakini si hivyo tu, unatakiwa kuishi na mke au mume sahihi kwako asiye na makelele. Unatakiwa kuishi na mwenzi wako ambae anaifanya akili yako itulie na isiwe ya vurugu.

Amani ya akili, utulivu wa akili, ndio chanzo cha mafanikio makubwa yote na yakutisha. Hakuna ambae aliyefanikiwa huku akili yake ikiwa haijatulia, mtu huyo hayupo.

Waangalie vizuri watu waliofanikiwa, utajifunza kitu kimoja kwao ni watu ambao akili zao zimetulia. Unasema nimejuaje, angalia jinsi wanavyoongea, wanaongea kwa utulivu mkubwa sana, hiyo ni ishara akili zao zimetulia.

Ili kufukia mafanikio yako makubwa, haina haja na maana kuishi na watu au katika eneo ambalo linakunyima utulivu wa akili. Jiulize, ya nini kuishi na mpenzi ambaye anaifanya akili yako isitulie na kuanza kumwaza yeye. Tafuta utulivu wa akili utaona matokeo yake makubwa jinsi utakavyo yapata.

Unapokuwa na utulivu wa akili inakusaidia sana wewe kupangilia mambo na mikakati yako kwa ukamilifu, tofauti na ambavyo ukikosa utulivu akili yako haiwezi kuwaza kitu cha maana na kukupa matokeo makubwa. 

Zingatia sana, utulivu wa akili, ni silaha ya kwanza katika kufikia mafanikio yako. Kila siku, jitahidi, utafute eneo lilotulia na tafakari maisha yako, na utaona matokeo mazuri yakija kwa upande wako. 

Unatakiwa ujue, silaha kubwa katika kufikia mafanikio yako ni utulivu wa akili. Ukituliza akili zako, utafanya mambo makubwa sana na ya kushangaza wengi na pia wengi hawataamini je, kweli ni wewe. Kumbe siri, ipo kwenye kutuliza akili, basi.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

Sep 26, 2021

Chagua Mwendo Upi Unakusaidia Kufanikiwa.

No comments :

Kuna wakati unaweza ukakamilisha mambo mengi sana, kama utaamua kwenda kwa taratibu. Unatakiwa usikimbize mambo yako, ila unatakiwa kwenda taratibu na kufanya kwa uhakika na ufanisi mkubwa wenye faida. 

Kwa mfano, kama kuna majukumu ambayo unayafanya kila siku, basi, majukumu hayo yafanye kwa utaratibu, kwa utulivu mkubwa na utajikuta unakamilisha mambo mengi ambayo hukutegemea.

Kuna watu wanafikiri ili kukamilisha mambo mengi unatakiwa kwenda kwa haraka zaidi, kitu ambacho si kweli. Unaweza kwenda taratibu na ukakamilisha mambo mengi, unaweza kwenda haraka halafu ukaharibu.

Ni wajibu wako unatakiwa ujue ni wakati upi unatakiwa uende taratibu na wakati upi unatakiwa uende haraka. Si kila wakati wa kwenda kwa haraka ikiwa utafanya hivyo huwezi kukamilisha mambo mengi zaidi unajiharibia wewe.

Kama nilivyosema, kwenda haraka hakuwezi kukusaidia kukamilisha mambo mengi kwa sababu, akili yako inakuwa haijatulia yaani inayumba yumba. Kama akili yako inayumba hivyo, kufanikisha mambo mengi ni ndoto.

Unatakiwa kila wakati kujiuliza, hapo ulipo ni wakati wa kwenda haraka au wakati wa kwenda kwa kasi. Kisha ukishapata majibu, fanya uamuzi sahihi. Maisha sio mashindano na wengine, angalia mwendo wako.

Hapa ndio upo ule umuhimu wa kuchagua mwendo upi unakusaidia kukamilisha mambo mengi. Je, mwendo wa kasi au mwendo wa taratibu, lakini kaa ukijua kila mwendo una sehemu yake.

Suala hili, lipo kama vile unavyoendesha gari. Si kila wakati unatakiwa kukimbiza gari, yapo mazingira yake. Na kwenye maisha iko hivyo hivyo, kuna wakati wa kwenda kwa haraka na wakati wa kwenda taratibu.

Kufanikiwa kwako kunategemea sana uchaguzi wako wa mwendo upi uutumie na katika eneo lipi. Fanyia kazi hili, na utaona matokeo makubwa kwa upande wako.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

Sep 25, 2021

Mambo muhimu ya kuzingatia unapotaka kufanya uwekezaji.

No comments :

Ipo hivi unapofanya uwekezaji katika jambo lolote unatakiwa kuelewa kwamba hakuna faida utakayoipata papo hapo. Bali uwekezaji huchukua muda fulani mpaka uje uone uwekezaji wa jambo hilo.

Wengi wanapoambia wawekeze katika jambo fulani hukurupuka katika kuwekeza mwisho wa siku hujikuta wanapata hasara au kutokuona faida ya uwekezaji waliofanya.

Kitu pekee ninachopaswa kukumbusha ni kwamba unapotaka kuwekeza katika jambo fulani, unatakiwa kuzingatia mambo haya machache;

·        Uwekezaji unakutaka uweze kulielewa jambo unalotaka kuliwekeza kwa undani zaidi.

·        Faida ya uwekezaji  huchelewa sana kuonekana.

·        Uwekezaji huitaji uvumilivu mkubwa ndani yake.

·        Uwekezaji unahitaji umakini wa hali ya juu ili kuepukana kupata hasara ya jambo husika.

Hivyo ni vyema ukayazingatia hayo machache kati ya mengi kabla hujaamua kuwekeza katika jambo lolote lile ulitakalo.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Ndimi: Afisa Mipango Benson Chonya.

0757-909942

 

Sep 24, 2021

Jinsi Ya Kupata Wazo Bora La Biashara.

4 comments :
Kisaikolojia kila mtu ana mawazo bila kujali ni mazuri au mabaya. Wakati mwingine binadamu huwa na mawazo mazuri ambayo kama atayaendeleza na kuyafanyia kazi yanaweza kubadili kabisa maisha yake.

Mawazo humfanya mtu awe alivyo, aonekane vile anavyoonekana. Mwenye akili, mpole, mkorofi,mwema au mkatili. Haya yote ni matokeo ya mawazo aliyonayo mtu kichwani mwake.

Kila siku tunasikia watu wanasema nina pesa ila sijajua nifanye biashara au mradi gani. Wakati mwingine utasikia mtu akisema nina wazo zuri la kufungua biashara au mradi tatizo langu mtaji sina.

Katika kuwaza kwao watu hawa mwisho hujikuta muda umeenda, umri umesonga bila hata kutekeleza wazo moja alilopanga. Mwenye pesa amekaa na pesa hadi  imekwisha kwa kutatua matatizo ya aina mbalimbali.


Mwenye wazo kawaza mpaka kawazua mtaji hana na wazo limechina mwisho anakata tamaa na kuamua kufanya kazi asiyotaraji kuifanya ili kujikimu na mahitaji ya kila Siku katika maisha.

Ni Kitu gani kifanyike ili watu hawa waweze kufanikiwa? Mwenye wazo na mwenye pesa? usiumize kichwa Kisuda nitakupa siri yake leo. Kabla sijaeleza namna gani ufanye nikudokezee siri moja muhimu katika mafanikio.

Tafuta wazo sahihi la kukufanikisha.
Ili mtu yeyote iwe mimi au wewe uweze kufanikiwa unahitaji vitu vinne.

1. MAARIFA/UJUZI juu ya jambo unalotaka kufanya.

2. WAZO BORA NA  ZURI la kukuongoza hatua kwa hatua lenye taarifa sahihi juu ya mradi au biashara husika.

3. WATU WAZURI wa kushirikiana nao. Hakuna kazi au mradi unaoweza kuufanya peke yako ila kushirikiana na watu. Hivyo ni lazima upate watu makini na sahihi wa kushirikiana nao.

4. MTAJI /PESA ya kuanzishia mradi lakini zingatia kuwa pesa si chochote katika mradi au biashara hata uwe na mamilioni ya shilingi kama huna hivyo vitu vingine wazo,maarifa na watu sahihi sahau kuhusu MAFANIKIO utaangukia pua tu.
Kisaikolojia  pesa haileti mawazo, bali mawazo ndiyo huleta PESA. Na hii ndio Imani yangu na falsafa yangu Kisuda  katika maisha yangu ya mafanikio.


Sasa nitoe njia 5 za kuweza kukusaidia wewe rafiki yangu katika kupata wazo la biashara ili uweze kufanikiwa kirahisi kwa wewe mwenye pesa na mwenye wazo:-

1.Tafuta uhitaji wa watu/ tatizo linalowasibu watu kisha tafuta namna ya kuwatatulia shida /tatizo lao utapata pesa nyingi sana.

2. Boresha wazo la mwingine. Hapa ni kuangalia tu mapungufu ya mtu katika kazi au biashara halafu una boresha utendaji kazi na utaona mabadiliko makubwa katika kazi au biadhara yako. Kamwe usiige wafanyavyo wengine utapata matokeo yaleyale wapatao wao badili njia.

3. Hamisha wazo kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Hapa na maanisha ukiona mradi au biashara sehemu si lazima nawe ukafanyie pale unaweza anzisha wazo kama hilo sehemu tofauti na ukafanikiwa sana.

4. Rahisisha mchakato au upatikanaji wa huduma au bidhaa fulani badala ya watu kuifuata sokoni au mjini wapelekee wewe nyumbani kwao watakulipa pesa nyingi na gharama ya usafiri kwa nini wakulipe? Umewaokolea muda wao ili wafanye mambo mengine na pia wamepata wanachotaka kwa wakati.

5. Tengeneza uhitaji kwa watu. Hapa ni kubuni Kitu cha ziada ambacho watu wanakihitaji lakini kutokana na muda au umbali wanaona kama hakina umuhimu sana kwao. Mfano simu za mkononi zimekuja baada ya barua kuonekana kuchelewa kuwafikia wahusika leo hii taarifa ya dakika 10 imeshasambaa nchi nzima.

Haya sisi wataalamu tunaita ni kutengeneza mahitaji ya ziada kwa watu ili wakulipe pesa. UWEZO WAKO WA KUJA NA MBINU AU WAZO JIPYA TOFAUTI NA MAZOEA YA WATU NDIO CHANZO CHA MAFANIKIO YAKO.

Ansante kwa kutembelea DIRA YA MAFANIKIO na endelea kujifunza hapa bila kuchoka.

Sep 23, 2021

Vizuizi Katika Maisha Yako, Vipo Kwa Ajili Ya Kukuandaa Na Jambo Hili.

No comments :

Vizuizi katika maisha, huwa havipo kwa ajili ya kukuzuia wewe eti ushindwe kufanikiwa. Vizuizi katika maisha huwa vipo kwa ajili ya kukuandaa uwe bora kwenye mafanikio yako.

Piga picha, ingekuwa vipi mtoto wa miaka 10 angekuwa yupo chuo Kikuu, hiyo isingekuwa na maana yoyote. Elimu yake ingeonekana bure na kukosa ule uthamani mkubwa.

Lakini, vizuizi vya miaka takribani 14 ya kupitia shule ya msingi, sekondari, kufanya majaribio, hivyo vyote vinamkomaza na kumfanya aione digrii ya chuo Kikuu ni ya thamani.

Piga picha pia, kama mafanikio unayoyataka yangekuwa rahisi tu, pasipo kupitia changomoto au vizuizi vyovyote vile, hayo mafanikio naamini yasingekuwa na raha kubwa zaidi.

Kuna wakati unaweza ukawa unalaumu sana kutokana na vizuizi unavyokutana navyo, lakini ukiangalia vinakukomaza na kukufanya ukawa bora kwenye mafanikio yako.

Unapokutana na vizuizi, ni wakati wako wa kujifunza maisha yanasema nini juu yako na si wakati wa kulaumu. Jifunze kitu kutokana na vizuizi hivyo. Usikae kizembe jifunze kitu.

Acha kuona vizuizi ni kama tatizo kwako, ona vizuizi ni kama njia ya kuweza kukukomaza wewe na kukufanya ukawa bora. Utafanikiwa sana kama vizuizi vyako utaviona kwa jicho hilo.

Kama unapitia kwenye changamoto kubwa, kaa ukijua unaandaliwa, unakomazwa hasa kwa kule unakoenda. Unajengewa misuri ya ukomavu itakayokufanya ufanikiwe.

Shukuru kama unakutana na changamoto. Shukuru kwa sababu ndio saa ya kukomazwa. Unatakiwa kukumbuka, vizuizi havipo kwa ajili ya kukuzuia bali kukuandaa kuwa bora.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

Sep 22, 2021

Ujasiri Unaohitajika Katika Kusaka Mafanikio Yako.

No comments :

 

Tunaaminishwa ya kwamba mnyama mwenye ngozi ngumu kuliko wote huenda ikawa ni mamba, japo hakuna uthibitisho kamili juu ya hilo. Uwezo wa mnyama mwenye ngozi ngumu ni mnyama mwenye uwezo wa kuvumilia mengi ikiwemo uwepo wa jua kali wakati wa kingazi.

Kama ilivyo kwa mnyama mamba basi hata sisi tunaambiwa ili tuwe na ngozi ngumu katika kufanya mambo mbalimbali, hii ikiwa na maana ya kwamba tunapaswa kuvulimia kila changamoto ambazo zitakuwa zinajitokeza kwenye kukamilisha mambo mbalimbali.

Ni muhimu kuwa na ngozi ngumu kwa sababu wengi wetu tumekuwa ni watu wa kukata tamaa sana, hasa pale zinapojitokeza changamoto mbalimbali kwenye mambo tuyafanyayo.

Ila ukweli ambao napaswa kukumbusha siku ya leo  ni kwamba pamoja na changamoto zote zinazojitokeza kwenye mambo mbalimbali tunakumbushwa ya kwamba tunapaswa kuwa wavumilivu kwani mvumilivu ndiye ambaye atakula mbivu, au kwa maneno mengine anayevulia ndiye atakayefanikiwa zaidi.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Ndimi, Afisa Mipango Benson Chonya

0757909942

 

Sep 20, 2021

Nguvu Ya Changamoto.

No comments :

 

Kuna wakati unajikuta upo kwenye siku ambayo una vitu vingi sana vya kufanya, lakini cha ajabu huwa ni siku ambayo pia unaweza kukamilisha mambo mengi ambayo hukutarajia.

Pia kuna siku ambayo unajikuta una vitu vichache vya kufanya, lakini huwa ni siku ambayo hukamilishi mambo mengi pia. Unashangaa unajikuta, mambo mengi hujafanya.

Hiyo inamaanisha nini, kila unapokuwa kwenye changamoto, akili yako inakuwa na nguvu na uwezo wa kufanya mambo mengi na kufanya kazi vizuri na ufasaha mkubwa. 

Unatakiwa ujue, changamoto unazokutana nazo,  zinakuwa zina uwezo mkubwa wa kuamsha akili yako na kuifanya ifanye kazi kwa njia ya maajabu na kuleta majibu ya kushangaza. 

Hivyo, fundisho kubwa hapa ni kwamba, hutakiwi kuogopa changamoto, kwani changamoto zinakukomaza na kukusaidia kukamilisha mambo mengi. Changamoto ni msaada kwako.

Kila unapokutana na changamoto, jiulize, utawezaje kufanya na kupata majibu sahihi. Hakuna kinachoshindikana kila kitu kinawezekana hata ukiwa kwenye changamoto. 

Ipo nguvu kubwa sana ndani ya changamoto, kama utaelewa vizuri. Yale ambayo ulikuwa huwezi kuyafanya unaweza kuyafanya ukiwa kwenye changamoto kubwa na za kutisha.

Kuanzia leo, acha kuhuzunika unapokutana na changamoto, jifunze juu ya changamoto hizo. Kazi ni kwako, weka akilini changamoto wakati wote ni msaada kwako, zitakuimarisha na kukufanikisha.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

Sep 19, 2021

Hii Isiwe Sababu Ya kukuzuia Kufanikiwa...

No comments :

Kuna watu hawafanikiwi kwa sababu, wanafanya kazi zao nusu nusu na zinaishia kati, hawafiki mwisho kule wanakotakiwa kufika. Watu kama hawa kufanikiwa ni ngumu.

Kwa mfano, ilitakiwa watu hao wafanye kazi zao zianze kuwalipa, kwa sababu hawafiki mwisho yaani wanaishia kati, basi hujikuta wafikii yale mafanikio yanayotakiwa.

Utakuta mtu ni mwimbaji mzuri sana, lakini hafanikiwi, kwa sababu, hajaweza kurekodi, hafanikiwi kwa sababu hajaweza kujiweka wazi akajulikana na kusaidiwa na watu wengine. 

Pia utakuta mtu ni mwandishi mzuri sana, lakini anakuwa hafanikiwi kwa sababu, mtu huyo anakuwa bado hajachapa kazi zake zikaonekana, hivyo kazi zake zinakuwa ni nusu hazijafika mwisho wa kumpa faida.

Wapo watu wa aina hii wengi, utakuta wengine wanafanya kilimo, lakini hawaweki ule ubora unaotakiwa ili wafanikiwe. Kwa kuishia kwao kati inaleta shida sana kwao na kuwazuia kufanikiwa.

Ili kufanikiwa kwa chochote kile unachokifanya, unatakiwa kufanya kitu hicho mpaka mwisho. Hutakiwi kuishia katikati, utakuwa unajipoteza wewe kwa kupoteza muda na nguvu zako bure.

Kwa chochote ukifanyacho, kifanye hadi mwisho na ukione kinakupa  mafanikio makubwa. Hapo ndipo ilipo siri ya mafanikio yako, yaani kufika mwisho. Kama hufiki mwisho, itakuwa kazi sana kwako kufanikiwa.

Kufanya kazi nusu nusu na kushindwa kufika mwisho isiwe hata sababu ya kukuzuia kufanikiwa. Kwa chochote ukifanyacho, nenda mazima mazima, hakuna kufanya kazi nusu nusu, hutafanikiwa.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

Sep 18, 2021

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuipa Akili Yako Ushawishi Na Ikupe Mafanikio.

No comments :

Wataalamu wengi wa mafanikio wanasisitiza sana umuhimu wa kupitia malengo yako kila siku ili iwe rahisi kwako kuweza kuyatimiza. Unajua ni kwa nini hili linasisitizwa sana? Umeshawahi kujiuliza kwa nini?

Hiyo yote ni kuufanya ubongo wako uamini kwamba malengo yako yanawezekana. Hiyo iko hivyo pia kwa sababu kabla hujafikisha miaka mitano unakuwa umekataliwa mara 40,000 kwa vitu tofauti na ni mara 5000 tu ndio unakuwa umekubaliwa.

Mpaka hapo unaona kama umekataliwa mara nyingi hivyo, tafsiri yake ni rahisi kuona kila kitu hakiwezekani. Ili mambo hayo yawezekane sasa, inabidi uushawishi ubongo wako kuamini kwamba inawezekana. 

Kumbuka mafanikio yanaanza na sisi wenyewe kwanza, yaani zile imani tulizonazo ndani mwetu, ndizo zinajenga mafanikio. Hivyo unatakiwa kujilisha vitu chanya na kujiaminisha kwamba inawezekana kwa lolote lile kwako, pitia malengo yako kila siku utafanikiwa.

Hakuna namna utakayoweza kuifanya akili yako iamini kuwa utafanikiwa zaidi ya kuandika malengo yako na kuyapitia kila siku. Ukifanya zoezi hilo kila siku la kuyapitia malengo yako, utaipa akili yako ushawishi mkubwa sana na utafanikiwa.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.

 

Sep 17, 2021

Usipotumia Mambo Haya Vizuri, Utakwama.

No comments :

Unatakiwa kutumia kila ulichonacho kwa uhakika na vizuri kabisa. Acha kujidanganya kwamba unataka mafanikio makubwa wakati hata ile misingi ya kutengeneza mafanikio makubwa unaiharibu hovyo hovyo.

Haiwezekani eti unasema unataka mafanikio makubwa wakati unatumia muda, pesa na nguvu zako hovyo, ambapo vitu hivyo kwa pamoja vingekusaidia kufikia mafanikio makubwa kama ungevitumia vizuri na kwa busara. 

Pesa unazozipata hazijiamulii zenyewe kwamba ‘sasa mimi pesa ninakwenda kununua kitu hiki au kile.’ Wewe ndie mwenye jukumu la kupanga pesa zako zitumike wapi na kwa sababu ipi.

Sasa kama hiyo iko hivyo, kwa nini unafanya maamuzi mabovu ambayo yanakupotezea pesa nyingi na kwa kiasi kikubwa? Kuwa makini sana na matendo yako ili yasikupotezee pesa ambayo ni moja rasilimali muhimu kukusaidia kufanikiwa.

Hapo ulipo najua una pesa za kiasi fulani hata kama ni ndogo, najua una muda na nguvu fulani, sasa kwa nini hivi vitu usivitumie kwa uangalifu ili viweze kukusaidia kukupa mafanikio makubwa na badala ya kuvipoteza tu kiholela.

Watu matajiri, wanajua namna ya kutunza pesa zao vizuri, kwa nini wewe usiwe miongoni mwao? Huna pesa si kwa sababu pesa zinakukimbia bali ni kutokana na matendo yako yanayofukuza pesa.

Kitu cha kufanya jiulize, ni hatua zipi utaweza kuzichukua ili kuweza kulinda rasilimali zako za kukusaidia kufanikiwa ambazo ni pesa, muda na nguvu zako.  Kama hujui tafuta watu wenye mafanikio kisha wafatilie.

Kama utatumia muda, nguvu na pesa zako vizuri, utafanikiwa. Usipotumia mambo hayo vizuri, nakuhakikishia itafika utakwama na hautaweza kupiga hatua kubwa. Muda wako, pesa zako na nguvu zako, ni vitu vya msingi sana katika mafanikio yako.


Kila la kheri katika kufikia mafanikio yako.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya kimafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2021 Imani Ngwangwalu. Haki Zote Zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Ruksa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ya ruhusa ya mwandishi.