google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 24, 2019

Usipoteze Muda Wako, NI Utajiri Wa Kesho Yako.

No comments :
Muda ni mchache, maisha uliyonayo au maisha tuliyonayo ni mafupi, kwa hiyo kila muda na fursa unayoipata hata kama ni ndogo sana, tafadhari itumie vizuri na kwa uhakika mkubwa. Kutumia muda wako hovyo, hakuna tofauti na wewe kuamua kupoteza fursa za mafanikio yako tena kwa makusudi.
Ili kutumia muda wako vizuri, unatakiwa kufanya kile kinachotakiwa kufanyika kwa wakati ule  hata kama mwili wako uwe unataka au hutaki.  Moja ya kanuni ambayo inatumika na watu ambao hawafanyi kitu katika maisha, ni kutokuchukulia leo katika umuhimu wake. Kama leo yako unaiona ipo ipo tu, upo kwenye wakati wa kupoteza.
Maisha ya mafanikio yanatengemezwa na hatua ndogo ndogo sana za kila siku. Inapotokea wengine wanasita kuchukua hatua wewe unatakiwa kuchukua hatua na si kupoteza muda na kusema nitafanya siku nyingine. Muda ulionao ni wa dhahabu, ukipotea umepotea, kama ukijua thamani ya muda wako hutaweza kuupoteza tena.

Moja ya siri ya kufikia mafanikio yako ni kutumia kwa usahihi kila fursa ambayo unaipata. Muda unakwenda na kupaa, unatakiwa kuwa rubani kuendesha muda wako kwa usahihi. Jiulize,  usipotumia leo fursa za mafanikio unazozipata unataka kutumia fursa hizo lini au wakati gani, naamini unanipata vyema.
Mwanamafanikio William Ward moja katui ya maandiko anasema, “unatakiwa ujifunze kujiendeleza kwa kusoma wakati wengine wamelala, unatakiwa kuwekeza wakati wengine hawaoni fursa, unatakiwa kujiandaa kwa kila kitu wakati wengine wanacheza”. Acha kupoteza muda wa maisha yako kwa chochote, utumie vizuri.
Elewa hakuna muda bora kama huu ulionao kwa sasa. Kama utakuwa ni mtu kupoteza muda wako na kusubiri, hicho unachosubiri upo uwezekano hutaweza kukifanya tena au utakifanya kwa tabu. Wengi wanaoahirisha mambo ukumbuke huja kuyafanya tena mara nyingi huwa ni ngumu sana kwao kuweza kutokea.







Apr 23, 2019

Kama Utapoteza Jambo Hili, Hutalipata Tena Maishani Mwako.

No comments :
Katika kijiji kimoja kulikuwako na watu watatu ambao walikuwa na safari ndefu sana ya kuelekea mbali na mahali walipokuwa wanaishi, safari hii ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya kujitafutia  riziki zao za kila siku ambazo zilipatikana katika msitu fulani uliokuwa  mkubwa sana.
Watu hawa walitembea kwa umbali mrefu sana ikafika mahala wakawa wapo  katikati ya pori ambapo walianza kuingia na hofu ndani mwao, watu hawa majina yao ni, mtu wa kwanza alikuwa akifahamika kama moto, mtu wa pili alikuwa akifahamika kama maji na mtu wa tatu alikuwa hajulikani ni nani.
Wakiwa katikati ya pori wakiwa wamejawa na  wasiwasi na wanakokwenda  huku wakiwa hawaelewi watafika lini na muda gani, mmoja wao  akawambia wenzake “ jamani eeh hebu tusimame tuelezane kitu kimoja,  huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni moto, huku tukokwenda  nahisi tunaweza tukapotea.

Kama tunaweza tukapotea inabidi tuambiane ishara mapesa kabisa kwamba je, kama ukipotea utawezaje kujulikana sehemu uliyopo? yeye moto akasema  ikitokea tumeenda mahali na tukagawana kila mtu njia yake na ikawa haileweki mtu mwingine yupo wapi,  mimi kama moto ikatokea nimepotea basi msisumbuke kunitafuta ninyi angalieni ishara ya moshi popote utakapouona moshi unapotokea basi  hapo ndipo nitakapokuwepo.
Wakati huo wote moto anazungumza maji na yule mwingine ambaye hajulikani wakasema sawa mkuu sisi tumekuelewa.
Ikafika zamu ya maji naye kuzungumza, maji akasema “ moto mimi nakubaliana na wewe hata mimi nahisi kabisa kuna kila dalili zote za kupotea katika msitu huu, hivyo kama ikitokeo tumegawanyika na mimi nikapotea, mimi ili niweze kuonekana wala usisumbuke wewe angalia ishara ya kijani, ukiona sehemu ya kijani hapo ndipo utakaponipata.
Baada ya moto na maji kuzungumza hayo ikafika zamu ya mtu wa tatu ambaye hajulikani  kuzungumza, yeye akasema “jamani mimi mwenzenu sitabiriki”  mimi nikipotea sielewi mtanipataje kwa kweli maana mimi sina ishara yeyote ile nitakayoifanya ili mnione.
Sasa mimi na wewe tujiulize huyo mtu wa tatu alikuwa ni nani? Ambaye alisema hana ishara yeyote ile endapo atakuwa apotea? Endele kutafakari kisha unipe jibu.
Ila kwa kuwa umekuwa mzembe wa kuumiza kichwa basi ngoja nikupe jibu, mtu wa tatu alikwa ni muda.
Fundisho la hadithi hii ni:
Katika maisha yako poteza vitu vyote utavipata lakini usije ukapoteza muda wako huwezi kuupata, tumeona kuwa moto ukipotea ishara yake huwa ni moshi,  pia tumeona maji yakipotea ishara unaweza kuona ni ukijani katika uoto lakini muda ukipotea basi andika umeumia kwasababu muda huo hauwezi kurudi tena.
Kwahiyo tunafundishwa poteza  vingine kwenye maisha ila usithubutu kuja hata siku moja kuja kupoteza  muda wako, kwani ukipoteza muda hakuna ishara itakayokuonesha namna ya kupata ule muda ulioupoteza.
Hivyo fundisho kubwa hapa ni kuhakikisha unatumia muda wako vizuri ila kwa baadae usije ukajuta kwamba ulikuwa mjinga kwa kupoteza muda wako kwa kiasi hicho.
Nikutakie kila la kheri na tafakari njema ya hadithi hii, byee.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA AFISA MIPANGO BENSON CHONYA.


Apr 22, 2019

Kama Utakosa Kitu Hiki Sahau Kuishi Maisha Ya Uhuru, Furaha Na Mafanikio.

No comments :
Kama upo kwenye chombo cha usafiri, halafu ni usiku  na tena unataka kusafiri mbali na kwa haraka zaidi, kitu cha kwanza unachotakiwa kuhakikisha chombo hicho inacho ni mwanga wa uhakika. Pasipo mwanga wa uhakika safari yako itakuwa ni ya shida kidogo, unaweza ukaenda lakini si kwa kasi na mwendo ule unaoutaka wewe.
Hata kwenye maisha yako ukitaka kufika mbali kimafanikio kitu kimojawapo unachotakiwa kuwa nacho ni kujifunza kuwa na msamaha. Unapokuwa na msamaha, inakusaidia kuondoa uchungu, hasira, visasi vyote unakuwa umeweka pembeni na matokeo yake unakuwa huru kufanya mambo mengine na kusonga mbele.
Kuishi maisha ya kutokuwa na msamaha, ni sawa na kuendesha gari huku ukiwa umeshikilia breki, kwani kwa kufanya hivyo mwendo wako hautakuwa mzuri, ni rahisi kukosa mwelekeo na hata kupotea kabisa. Unatakiwa kukumbuka unapokuwa na msamaha hiyo inakuweka huru sana wewe kuweza kufikia mafanikio yako.

Unapoamua kuishi maisha ya kutokuwa na msamaha kitu kitakachofatia hapo kwako ni kwa wewe kuishi maisha ya kisasi. Inapotokea ukaishi maisha ya kisasi mwanzo inaweza ikaonekana ni maisha mazuri, lakini nikwambie maisha hayo yanakuwa ni mabaya sana kwako kwani yatakuzuia wewe kuweza kuendelea mbele sana.
Unapokosa msamaha kabisa ujue unakuwa maisha ambayo yanakuwa ya uchungu karibu wakati wote. Unatakiwa kujua ufunguo mojawapo wa furaha ni wewe kujijengea tabia ya kuwa na msamaha. Kama hautakuwa na msamaha sahau kabisa kwa wewe kuweza kuishi maisha ya furaha au maisha ya uhuru.
Kwa mujibu wa wataalumu wa saikolojia na mafanikio, inasemekana moja ya siri muhimu ya kuishi maisha marefu na yenye faida kila siku ni kwamba kabla hujalala, jifunze kumsamehe kila mtu ambae amekukosea. Unapowasamehe watu hao ambao wamekukosea hiyo ni njia ya wewe kuendelea kufanikiwa kwenye mambo yako.
Ni bora ukasamehe na kusahau kuliko ukashindwa kusamehe na kukumbuka. Elewa, kusamehe kila wakati kunaendana na Baraka, lakini kutokusamehe kunakuumiza wewe na kunakupotezea sana milango mikubwa ya Baraka ambayo inatakiwa itokee kwako. Kwa hiyo ipo haja ya wewe kuweza kusamehe kwa namna yoyote ile.
Kabla hujamaliza  siku yako unatakiwa ujue ni watu gani ambao wanahitaji msamaha wako na wasamehe hata usipowaambia. Usichome daraja moto mara baada ya kuvuka mto. Nikwambie huwezi kujua utatumia daraja hilo mara ngapi tena kwa usafiri. Ipo faida ya kuishi maisha ya msamaha, hebu anza leo kuishi maisha hayo uone faida zake.
Jiulize ni wapi unakwama hadi ushindwe kutoa msamaha, je msamaha unaotaka kuutoa kwani unalipiwa? Kama msamaha unaotaka kuutoa ni bure, hebu samehe na kisha baki huru na maisha yako. Maisha yako hayatakuwa mabaya kisa umemeshindwa kusamehe, zaidi utajenga maisha ya mafanikio makubwa kwako.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,