google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 28, 2018

Wanaoficha Pete Za Ndoa Hawajui Kupenda.

No comments :
Unapomkuta mwanamke au mwanaume ambaye yuko kwenye ndoa, amevua au huwa anavua pete yake ya ndoa mara kwa mara na kuiweka kwenye mkoba wake au mfukoni, utasemaje?
Ni lazima kuna namna ambayo utamfikiria mtu huyo. Je, utamfikiria kwamba ni malaya, haridhiswi na ndoa yake, au hampendi mumewe au mkewe?
Hapa nitajaribu kutoa maelezo ambayo, yatakufanya usihisi vibaya kwa kile ambacho, umekuwa ukikifikiria kuhusu mwanamke au mwanaume wa aina hiyo.
Imeelezwa kwamba, wale wanawake au wanaume ambao, huficha pete zao za ndoa, ni watu ambao hawana uwezo wa kulea watoto, yaani huwa wanawapuuza sana watoto wao.
Kwa kulinganisha, inaelezwa kwamba, wale wanawake au wanaume wenye kuvua au kupenda kuvua pete zao za ndoa na kuziweka mikobani, huwa wanawapuuza watoto wao kuliko wale ambao, huvaa pete zao muda wote.

Weka wazi pete yako ni ishara ya upendo.
Lakini pia, inaelezwa kwamba wale wanawake au wanaume wenye sura za kuvutia au nzuri sana wanapokuwa na tabia hii ya kuficha pete zao za ndoa, huwa ni wazazi wasioweza hata chembe kulea watoto wao, yaani wanakuwa ni wazazi aambao, ni watekelezaji sana, wasiojali kabisa kuhusu watoto wao.
Katika moja ya tafiti zake mwanasaikokoljia Andrew Harell wa chuo kikuu cha Alberta nchini Canada, anasema kwamba, hili sio suala la kubahatisha, kwani amelifanyia utafiti kwa wengi, kwa muda mrefu na katika mazingira tofauti.
Mwanasaikolojia huyo anazidi kudai kwamba, hata linapokuja suala la kuangalia na kutunza wagonjwa, wale watu wanaoficha pete zao za ndoa, hawana uwezo wa kuwatunza wagonjwa ukilinganisha na wale wenye kuvaa pete.
Inaelezwa kwamba, kuvua pete ya harusi na kuificha ni ishara kwamba, mwenye pete hiyo hana hisia au uwezo wa kujifunga na ndoa yake au familia yake. Kwa kukosa sifa hizo, ni wazi mtu huyo hawawezi kujifunga na watu wengine wenye kuhitaji msaada wake wa kihisia kama vile wagonjwa.
Kuvua au kuficha pete ya ndoa, kunahesabiwa kama ni dalili ya mtu kutaka kuanzisha uhusiano mpya nje ya ndoa yake. Haja hiyo inapotimizwa, uwezekano ni mkubwa kwa mwanaume au mwanamke kupunguza upendo au kujali familia yake, akiwemo mke au mume au watoto. Kwa hali hiyo, kuficha pete ni dalili ya kutokujali na kushindwa kujifunga kwenye uhusiano.
Wakati huo huo taarifa za kitafiti zinaonyesha kwamba, wazazi wenye kuvua pete huwa hawatoi uangalifu mkubwa kwa watoto wao wenye sura mbaya, ukilinganisha na ule wanaoutoa kwa watoto wao wenye sura za kuvutia au wazuri.
Katika moja ya tafiti zilizowahi kufanywa, zilihusisha  wazazi na watunza watoto walioenda na watoto hao kwenye supermarkert. Ilionekana kwamba, wale watoto wasiopendeza, waliachwa kwa umbali mkubwa bila wazazi wao kujali, wakati wale watoto wenye kuvutia, wazazi au walezi walikuwa nao karibu sana.
Tafiti zote hizo zinajaribu kuonyesha upo uhusiano mkubwa sana kati ya kitendo cha kuvua pete na suala zima la kujali. Je, hali hiyo kwako ikoje? Huu ni utafiti tu, wewe je, unasemaje?
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku. Pia chukua jukumu la kumshirikisha mwingine, ili aweze kujifunza na kunufaika na masomo yanayotolewa humu.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA ESTHER ZACHARIAH, DAR ES SALAAM.

Feb 27, 2018

Fursa Za Kunufaika Nazo Katika Ufugaji Wa Kuku.

1 comment :

Rafiki, fursa zipo nyingi ambazo zinatokana na ufugaji wa kuku leo naenda kukueleza fursa ambazo zitakusaidia wewe kukua zaidi kiuchumi huku ukiwanufaisha jamii kubwa ya watu ulionao katika maeneo yako na taifa kwa ujumla.

Rafiki tumejifunza mambo mengi kuhusu ufugaji wa kuku kila kitu unachopasa kukijua kuhusu ufugaji wa kuku tayari umekijua sasa ni wakati wa utekelezaji tu na siyo maneno tena kwa sababu mafanikio yanatokana na hatua sahihi unazochukua.
                           
Unapoweka mipango ya kufuga kuku usiishie tu kupanga kufuga kuku mia au kuku elfu moja usiishie kufuga tu fikiria kufuga na kuzalisha mayai yakutosha kwa ajiri ya kuboresha afya kwa jamii kubwa ya watu wanaotuzunguka.


Kwa Tanzania bado upo mkubwa wa mayai hasa mayai ya asili ni adimu sana hebu rafiki amka uikoe jamii kubwa ya watanzania wanaokosa mayai kwa ajili ya chakula, kwani uhitaji bado ni mkubwa.

Kunielewa vizuri ngoja nikwambie kitu rafiki najua unafahamu kuwa mimi ni mfugaji na pia unafahamu kuwa nilikuwa natangaza kuhusu watu wanaohitaji mayai, lakini kwa sasa hata sitangazi tena kuhusu mayai kwa sababu mahitaji ya watu ni makubwa.

Watu wamekuwa wakiweka oda kwa zaidi ya wiki tatu wote hao wanahitaji mayai nashindwa kuwafikia wateja wote kwa wakati uhitaji umekuwa mkubwa kuliko uzalishaji nimekuwa nikiwasiliana na wazalishaji mbalimbali ambao wanafuga kuku lakini hawajawa na uhakiki wa mayai.

Kwa wakati sahihi sasa nimefikilia kuzalisha mayai kwa wingi ambayo yatakuwa yana uwezo wa kuwafikia wengi zaidi kwa wakati, Rafiki panga na wewe kuwa sehemu ya watu watakao nufaika na mradi huu wa kuku.

Nakupendekezea kwako rafiki tumia njia ya sayansi katika kupunguza gharama ya chakula cha mifugo yako, ongeza uzalishaji wako, lifikie soko kubwa zaidi, na hapo utakuwa na uhakika mkubwa wa kipato chako.

Pia  ngoja nikwambie jambo rafiki , iwapo utafanya ufugaji wako kwa kutumia sayansi yakupunguza gharama ya chakula basi utafanya ufugaji wako kwa gharama ya chini sana baada ya kuuza kwa bei kubwa wewe uza kwa bei ya kawaida tu.

Kama sokoni mayai ya asili yanauzwa mia tano wewe uza kwa mia tatu hadi mia nne kwa sababu gharama za uendeshaji kwako zitakuwa chini sana ukilinganisha na wafugaji wengi ambao wanafuga bila kutumia sayansi hii.

Unaweza ukajiuliza kwanini mayai ya kisasa yanauzwa bei ya chini na mayai ya asili (kuku chotara) yanauzwa bei ghari? je jibu nikiwa na  mayai ya asili ni adimu kupatikana ndio maana bei yake ni kubwa ukilinganisha na mayai ya kisasa.

Naomba nikuulize rafiki nani mkombozi wa jambo hili siyo mwingine ni mimi na wewe tunajukumu la kuzalisha mayai kwa wingi yawe ya kisasa au ya asili bado yanahitajika sana kwa jamii yetu mimi  nimeanza wewe je?

Weka mipango yako sawa wewe rafiki usifikirie kuishi kufuga kuku wachache fikiria kuwa na matawi kubwa ya mayai, fikiria kusambaza mayai Tanzania nzima,  mayai yanahitajika siyo nasema uongo.

Jambo lingine utakalo nufaika nalo ni kuwa na oda nyingi kutoka sehemu mbalimbali kama vile mahotelini, kwenye mighahawa, kwenye vibanda yya chipsi, majumbani, maofisini na maeneo mengine mbalimbali.

Kwa leo nimekupa mwanga tu wa fursa za kunufaika nazo kutokana na ufugaji wa kuku. Na ukumbuke tumeongelea fursa moja tu ambayo ni kufungua matawi ya uuzaji wa mayai kwa wingi sana. Je, fursa ipi inafata itokanayo na ufugaji wa kuku? Tukutane wiki ijayo katika somo linalofuata.

Ni mimi wako katika ufugaji, 
FRANK MAPUNDA,
0656 918 243.

Feb 26, 2018

Mbinu Za Kuongeza Mauzo Katika Biashara.

1 comment :

Yapo mambo ya msingi ambayo mfanyabiashara yeyote yule ili aweze kukua katika biashara yake ni lazima ayafahamu, na mambo hayo si mengine bali ni jinsi gani anatakiwa kuongeza kiwango chake cha mauzo.
Na si kuongeza kiwango cha mauzo pekee, bali kuhakikisha anapata faida kubwa kwa kile anachokifanya. Wapo baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa hawalizingatii hili na kupelekea bidhaa au huduma wanazozitoa kutofanya vizuri sokoni.
Kwa minajili hiyo nikaona ni vyema ili kuweza kuwasadia wafanyabiashara hao ili wapone ni vyema niandike makala haya ili ikusaidie kuweza kuongeza kiwango chako cha mauzo katika biashara unayoifanya.

Kwanza kabisa ili uweze kuongeza kiwango cha mauzo katika biashara ambayo unaifanya unatakiwa kuachana na mfumo wa zamani ambao ulikuwa unatumia katika kufanya biashara yako, kama inashindikana kuachana na mfumo huo wa zamani basi unachotakiwa kufanya ni kuboresha mfumo huo wa zamani ili uweze kufanikiwa kibiashara.
Jambo jingine ambalo ni muhimu kabisa ambalo unatakiwa kulikumbatia katika biashara yako ni,  kuelewa mbinu za kufanya biashara ya yako kwa kutumia mitandao ya kijamii.  Kwa wenzetu wazungu mfumo huu huitwa affiliate marketing, ambapo kwa kibantu tunaweza tukasema ifike mahala utengeneze mifumo thabiti, mfumo huu utakusadia kutenggeza pesa ukiwa umekaa tu nyumbani.
Wakati mwingine unaweza ukasema labda njia hii haiwezekani kuleta matokeo chanya, lakini ninachotaka kusema hakuna lisilo wezekana chini ya jua hii ni kwa sababu dunia ya sasa imekuwa kiganjani mwa wadamu, kila kitu ambacho unakitaka utakipata kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, kifupi dunia ya sasa inakwenda kasi sana tofauti na ilivyokuwa nyuma.
Na ili uweze kwenda sawa na kasi hiyo ni lazima jifunze mbinu mbalimbali zitakazokusaidia kuuza bidhaa au huduma kwa kutumia mitandao ya kijamii, kwani kwa sasa wanaitumia njia hiyo ndiyo ambao wanafaidi matunda ya kutumia mbinu hizo.
Jambo jingine ambalo litaweza kukusaidia kuweza kuongeza mauzo ya katika biashara unayoifanya ni kuhakikisha unakuwa mtalamu katika biashara husika. Hii mbinu muhimu sana katika kuongeza kiwango cha mauzo katika biashara kwa sababu pindi utakapokuwa mtalamu au m-bobezi wa jambo hilo itakusaidia sana kuweza kuizungumzia vizuri bidhaa au huduma unayoitoa kwa mteja wako,  kufanya hivyo kutamfanya mteja huyo ainunue bidhaa hiyo. Hivyo ili uweze kuongeza kiwango cha mauzo katika biashara yako jifunze kuwa mtalamu katika eneo husika unalolifanya.
Jambo la mwisho ambalo ni muhimu sana litakalo kusaidia kuweza kufanya biashara yenye tija ni kuhakikisha unaimarisha vizuri upande wa huduma kwa mteja, kwa sababu ule usemi wa kwamba mfalme ni mteja hakuwepo tu, bali msemo huo upo kumanisha kweli, mteja ni mfalme pindi awapo na asipokuwapo katika eneo lako la kibiashara pia.
Ufike pahala neno  mteja liwe lina maana kubwa sana katika biashara yako, yaani mfanye mteja kuwa ni sehemu ya biashara ya yako. Mfanye mteja ajisikie huru katika suala zima la kibiashara.
Mwisho nimalize kwa kusema biashara yenye tija hujengwa na vitu vitatu vya msingi ambavyo ni bidhaa au huduma nzuri+ masoko mazuri= wateja wengi.
Ndimi: Afisa Mipango Benson Chonya,
bensonchonya23@gmail.com,
0757-909942.


Feb 25, 2018

Kwa Chochote Unachokifanya Ili Ufanikiwe, Anza Hivi Na Maliza Hivi.

No comments :

Iwe wewe ni shabiki wa kuangalia mchezo wa kukimbia alimaarifu riadha au siyo, lakini kwa vyovyote najua umeshawahi kuangalia mchezo huo hata mara moja na kushuhudia wale washindi wanakuwa wanapatikanaje.
Kama utakuwa umesahau kidogo naomba nitakukumbusha hapa, washindi katika riadha, hususani zile riadha za mita mia moja, wanakuwa wanapatikana kutokana na kuanza kwao kwa kasi na kumaliza kwa kasi.
Hayupo mshindi katika riadha wa mita hasa mia moja kama nilivyosema anayeanza kukimbia kidogo kidogo halafu akawa mshindi kwa madai ya kukazana mwishoni au hakuna ambaye anaanza kwa kasi na mwishoni kukimbia kidogo kidogo na akawa mshindi.
Mchezo huu wa riadha mara nyingi kama unataka ili uwe mshindi ni lazima uanze kwa nguvu, uendelee kukimbia kwa nguvu ukiwa kwenye mbio na wakati huoho umalize kwa kukimbia kwa nguvu sana kwani washindi wanapatikana pale mwishoni.

Hiyo yote inatuonyesha mtu anayeshinda mbio, huwa hapunguzi kasi pale mwishoni bali ndio huongeza kasi, bila kujali anakutana na changamoto za aina gani iwe kuchoka au kuna hata wakati alidondoka, lakini ni lazima kuongeza kasi ili kushinda.
Halikadhalika pia kwa upande wa mafanikio, yanategemea na watu wanaonza kitu chochote kwa nguvu na kumaliza kwa nguvu pia. Kufanikiwa kwa kitu chochote kile ndio kunakuja kwa namna hiyo na sio vinginevyo.
Tatizo hapa la watu wengi wanapoanza jambo fulani wanakuwa wanaanza kwa kasi sana, lakini inapofika katikati ile pumzi yao ambayo wanakuwa wameanza nayo kwa hakika inakuwa inakata hali ambayo hupelekea kushindwa kabisa.
Na kinachokuwa kikipelekea wao kuzidi kupunguza kasi na mwisho kuweza kupotea hapa katika ni kutokana na changamoto, kutokijiamini na wasiwasi ambao wanakutana nao hapa kati kati na mwisho wa siku hujikuta wako nje  ya mstari wa mafanikio.
Unatakiwa ujue mafanikio yanategemea sana wale wote wanaoweka juhudi kuanzia mwanzo na kendeleza juhudi hizo mpaka mwisho wa mafanikio yao. Mafanikio ndivyo yanavyotengenezwa na watu wa namna hiyo.
Kitu pekee ambacho kitakufanya uanze jambo lolote kwa nguvu na umalize kwa nguvu ile ile pasipo hapa wewe kati kati kuweza kupotea kwa namna yoyote ni kujitoa kwako na kujenga mtazamo. Haya mambo yatakusaidia sana.
Unapokuwa umeamua kujitoa na kujenga mtazamo chanya, hapa kati kati hata ukikutana na changamoto nyingi, hutaweza kulalamika zaidi utaongeza mwendo kwa sababu unajua vyema ni wapi unakoenda na unatakiwa umalize vipi ili uwe mshindi.
Nikukumbushe tena washindi katika mafanikio wana anza kwa nguvu, wanaendelea kufanya kwa nguvu na wanamaliza kwa nguvu pia kila wakati. Hii ndio kanuni wanaoyoitumia na wewe unatakiwa uitumie vivyo hivyo pasipo kubabaishwa na kitu.
Kwa chochote ambacho umechagua kukifanya, kianze kwa nguvu, endelea kukifanya kwa nguvu na pia kimalizie kwa nguvu. Usije ukafanya kosa la kuanza kwa nguvu na kumalizia kwa udhaifu, hutashinda ila utashindwa ukifanya hivyo.
Chochote unachokifanya kitakupa ushindi ukiwa utakianza kwa nguvu na kukimalizia kwa nguvu pia. Hakuna hali au mazingira ambayo yatakuzuia kufanikiwa kama moto ule ule ulionanza nao na ndio huo utakaomaliza nao.
Amua sasa kuwasha moto wa mafanikio yako kuanzia mwanzo hadi mwisho, pasiwepo kitu chochote hapa kati ambacho kitaweza kujitokeza na kuzima moto huo. Wewe ni mshindi, anza kwa nguvu, endelea kufanya kwa nguvu na maliza kwa nguvu.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
MUHIMU ZAIDI; kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,







Feb 24, 2018

Sehemu Sahihi Ya Kuanzia Mafanikio Yako Ni Hii Hapa.

No comments :

Bila kujali upo mbali kimafanikio kwa kiasi gani, lakini bado unayo nafasi ya kuchagua kuendelea mbele kwenye safari ya mafanikio yako.
Si kitu cha ajabu sana kwako na kwa wengine pia wanapoona wako mbali kimafanikio, hasa kwa kuwalinganisha na wengine wanaanza kukata tamaa.
Kitu ambacho watu hawa wanakuwa hawajui ni kwamba, mafanikio hayategemei sana au hayajali eti upo mbali sana, bali kinachojalisha ni mwelekeo wako.
Mwelekeo ndio kitu cha msingi sana katika safari yako ya mafanikio, hiyo ikiwa na maana pale ulipo kwa sasa unaelekea wapi kimafanikio.
Kama mwelekeo wako ni sahihi, basi hakuna shaka hata kama mwendo wako ni kidogo kama wa kinyonga lakini wakati upo utafanikiwa.

Kikubwa ambacho hutakiwi kukipoteza kwenye maisha yako ni ule mwelekeo wa kule unakoenda kwenye maisha yako. Ukipoteza mwelekeo ndio basi huwezi kufanikiwa.
Watu wengi hawafanikiwi katika maisha sio kwa sababu ya kwamba wapo mbali kwa hiyo ni ngumu kufanikiwa. Hawafanikiwi kwa sababu hawana mwelekeo.
Hata katika mazingira ya kawaida kitu chochote kikosa mwelekeo hakiwezi kufika kule kunakotakiwa kufika, lazima kitapotea hapa katikati.
Kwa mfano, ukiangalia ndege inaporuka hewani inakuwa na mwelekeo fulani unaoongozwa na rubani. Inapotokea mwelekeo huo haupo, basi ndege haiwezi kufika.
Na maisha yako hayana tofauti sana na hivyo. Maisha yako yanahitajji mwelekeo kwanza na sio wapi ulipo kimaisha ndio iamue hatma yako.
Kama umekuwa bado unasingizia kwamba eti uko mbali kimaisha na ndio maana hufanikiwi, huo sio ukweli ni uongo.
Wewe sehemu ya kuanzia kwenye safari yako ya mafanikio ni kutafuta mwelekeo. Ukiupata mwelekeo basi njia kuu ya mafanikio umeiona.
Unatakiwa sasa kujiuliza karibu kila siku, mwelekeo wa maisha yako uko wapi. Kitu gani utakachofanya ambacho kitakupa mwelekeo sahihi wa maisha yako.
Hutakiwi kulaumu hata siku moja pale ulipo, unatakiwa ushukuru kwanza, kwani sehemu ulipo hapo ndipo unatakiwa kuanza kutafuta mwelekeo wa mafanikio yako.
Hutaweza kufanikiwa kama hautaweza  kuanza kutafauta mwelekeo wako, sehemu sahihi ya kuanzia mafanikio kama nilivyosema ni kujua mwelekeo wako pale ulipo.
Hakuna kitu ambacho kitaweza kushindikana kwako, kwa sababu utakuwa umeamua kutafuta kwa dhati sehemu ya kuanza kutafuta mafanikio yako.
Amua leo iwe siku ya kuanza kutafuta sehemu sahihi ya kuanzia mafanikio yako kwa kutafuta mwelekeo wa wapi uende.
Usiruhusu mtu akwambie huwezi kufika, kule unakotaka kufika kimafanikio, wakati una uwezo wa kuanza kutafuta mweleko wako na kusonga mbele unao.
Usiruhusu mtu akakukatisha tamaa iwe kwa vitendo au kwa chochote kile kwamba wewe upo mbali sana na hautaweza kufanikiwa.
Usiruhusu tena wewe mwenyewe ndani yako ukajiambia kwamba, kwa maisha haya niliyonayo ndio basi tena siwezi kufanikiwa.
Hutakiwi kuruhusu chochote kile ndio kikawa chanzo cha wewe kushindwa kuwa na mwelekeo sahihi wa maisha yako.
Kila wakati unatakiwa kujua ule uwezo wa kufanikiwa na kufika ngazi ya juu kimafanikio unao,  kwa sababu sehemu sahihi ya kuanzia mafanikio yako umeshaiona.
Kama kuna watu wanaoendelea kukubeza, waache waendelea kukubeza na hiyo itakula kwao, wewe endelea kuchanja mbuga kutafuta mwelekeo wako kimafanikio.
Hutakiwi tena kujiuliza uliza au kumuuuliza mtu kwamba ni wapi mafanikio yanapoweza kuanzia au ni sehemu gani.
Kitu cha kukumbuka ulichojifunza hapa ni kwamba mafanikio yako, sehemu sahihi ya kuanzia mafanikio yako ni kwa wewe kuchukua hatua.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
MUHIMU ZAIDI; kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com











\



Feb 23, 2018

Huu Ndio ‘Ugonjwa’ Mpya Hatari Usipothibitiwa Mapema, Utaangamiza Familia Nyingi.

No comments :
Inafahamika yapo magonjwa mengi sana, ambayo yamekuwa tishio kwa familia na jamii inayotuzunguka kwa muda mrefu. Magonjwa hayo yapo ambayo yamekuwa yana dawa na yapo ambayo hayana dawa, lakini yapo.
Kwa kuwa mimi si daktari hapa katika makala haya sitataja sehemu ya magonjwa hayo ambayo yamekuwa ni hatari kwa familia, pengine na taifa kwa ujumla, bali hapa mimi nitazungumzia ugonjwa mmoja tu ambao naufahamu ila ni hatari sana.
Ugonjwa huu ambao nauzungumzia hapa na ambao ikiwa hauathibitiwa mapema, basi tujiandae kupoteza familia nyingi na kuzipeleka kubaya zaidi, ni ugonjwa wa mmonyoko wa maadili, ndio nimesema ni mmonyoko wa maadili.
Kwa miaka ya hivi karibuni ukifatilia kwa makini, utagundua swala la kuporomoka kwa maadili kadri siku zinavyokwenda mbele nalo limekuwa likiongezeka kwa kasi. Watoto wa sasa, wamekuwa  si watoto wa miaka ile, mambo yamekuwa yametofautina sana.

Malezi bora kwa watoto yanatakiwa kusimamiwa vizuri.
Hilo unaweza ukaliona vizuri kwa watoto wa sasa, kama si wa kwako basi wa jirani na kama si wajirani basi ni wa ndugu. Lakini kitu ambacho kipo na kinaendelea kutokea katika jamii zetu tunamoishi kila siku.
Najua walezi wa watoto kama wazazi, walimu pia ambao kwa sehemu wanajukumu la kukaa na watoto kwa muda mrefu, hapa wanaweza wakawa wananielewa kwa uzuri sana kwamba mmomonyoko wa maadili tayari limekuwa ni tatizo au ugonjwa ambao unakuja kimya kimya.
Kwa bahati mbaya sana kila mtu anakazana na kinga ya nyumbani kwake na wengine hata hiyo kinga hawaijui, matokeo yake watoto wanakuwa wanalelewa tu kama kibahati, na mwisho wa siku ni hatari kubwa ambayo inapelekea mmonyoko wa ukweli.
Kiuhalisia ukiangalia  yapo mengi yanayosababisha ‘ugongwa’ huu wa mmonyoko wa maadili kwa sasa kutokea kwa kasi kuliko wakati mwingine. Moja ya msingi mbovu inaweza ikawa ni malezi mabovu ya wazazi na walezi kwa watoto na hata pia mitandao ya kijamii.
Hivi ni vitu ambavyo vinaweza vikawa na mchango mkubwa sana kupelekea mmonyoko wa maadili kwa watoto wetu. Na pasipo vitu hivi au swala hili la mmomonyoko wa maadili kudhibitiwa basi taifa la kesho tutakalokuwa nalo litakuwa ni bovu sana.
Unaona mpaka hapo ni jukumu la kila mmoja wetu kusimamia kwa umakini swala la mmonyoko wa maadili kutokuendelea, vinginevyo tutakuwa na taifa ambalo litakuwa halina maadili kwa siku za huko baadae.
Ni imani na mategemeo yangu wazazi na walezi watajitahidi kuziba mianya yote inayopekeleka mmonyoko wa maadili. Hayo yote hayawezi kufanikiwa pasipo kutoa ushirikiano kwa wazazi wote.
Pia walimu wetu inatakiwa washirikishwe na watiwe moyo na wazazi katika kuhakikisha watoto wanalelewa katika maadili mazuri na bora. Kila mtu akisimama katika nafasi yake mabadiliko yatawezea kutokea.
Lakini ikiwa tukishindwa kuthibiti kwa sasa mmomonyoko wa maadili, basi tujiandae kuwa na kizazi ambacho kitakuwa  kipo kipo tu. Mpaka hapo ieleweke hatujachalewa, uwezo wa kuthibiti ‘ugonjwa’ huu wa mmonyoko wa maadili inawezekana.
Inawezekana unajiuliza tunaanzia wapi, anzia hapo ulipo, ‘mtoto wa mazazi mwezio ni mtoto wako pia.’ Kama unaona mtoto amekosea kitu hata kama sio wako, chukua jukumu la kumuonya.
Pale mtoto atakapogundua alaa kumbe anaweza kuonywa na mzazi ambaye si wake, najua atajirekebisha na vivyo hivyo tutajikuta tuna kizazi chema, kizazi ambacho tutakifurahia siku za usoni kwenye maisha yetu.
Watengenezaji wa maisha ya watoto wetu ni sisi wenyewe, jukumu ni letu sote. Tuchuke hatua za kuweza kubadili sisi kwa kuwa wazazi au wazazi wawajibikaji na kwa kufanya hivyo tutaweza kuthibi ‘ugonjwa’ huu wa mmonyoko wa maadili.
Fanyia kazi ujumbe huu, linda kizazi cha kesho kwa kukipa maadili bora na ya manufaa leo na si kesho.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
MUHIMU ZAIDI; kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




Feb 22, 2018

Hizi Ndizo Biashara Ambazo Haziwezi Kufa.

No comments :

Mara nyingi inapotokea uchumi umeyumba au uchumi mbovu kunakuwa na idadi kubwa ya biashara kuweza kuyumba na zingine kuweza kufa kabisa. Hali hii hupelekea watu hasa wafanyabishara kuanza kupata tabu kwa kuyumba kiuchumi pia.
Ndio maana kabla hujafanya biashara unashauriwa kufanya utafiti wa kutosha na kuangalia ni biashara zipi ambazo zina mahitaji mengi au zinaweza zikadumu kwa muda mrefu pasipo kuteteleka au kufa kabisa hata kitokee kitu gani.
Pegine unajiuliza kweli kuna biashara ambazo haziwezi kufa? Katika mazingira ya kawaida unaweza ukakataa ukasema kwamba, kila biashara inaweza kufa. Lakini hapa leo nataka ni kukuonyesha biashara chache tu ambazo haziwezi kufa.
Katika makala hii, biashara hizo sitazichambua kwa kina bali nitakuonyesha tu mwanga au njia kisha utatafakari na kuangalia ukweli na uhalisia wa biashara hizo ambazo zinafanywa kwa vizazi na vizazi, na zinaleta mafanikio kwa wengi

Kwa mtu ambaye ameamua kufanya biashara hizi na akabobea kweli, ni ngumu sana kuweza kumtoa kwa sababu zinalipa, labda wewe mwenyewe uamue kwamba sasa siwezi kuifanya tena biashara hii, ukaamua kukaa kwa kubweteka.
Lakini biashara ambazo nakwenda kukushirikisha hapo ni biashara ambazo zinafanyika katika mazingira yoyote yale. Zinafanyika kijijini na zinafanyika mjini, lakini ni biashara ambazo hazichagui kitu ilimradi tu wewe uamue kufanya kwa ufanisi na utafanikiwa.
Biashara ambazo haziwezi kufa au hata kama zikifa ndio zitakuwa za mwisho ni biashara za vyakula kama vile unga  wa sembe, unga wa ngano, mchele, mafuta ya kula, sukari, maharage, dagaa, pamoja  na chumvi. Hizi ni biashara ambazo zinadumu sana.
Ukiangalia hivi ni vitu ambavyo vinagusa matumizi ya watu ya kila siku. Hakuna siku ambayo itapita pasipo watu kufanya matumizi ya hivi vitu. Kila siku kwa mfano, unga eidha uwe wa sembe au wa dona unahitajika sana kila siku.
Watu wenye mashine au wanaojihusisha na biashara hii kwa mfano ya uuzaji wa unga wanajua ni biashara ambayo haiwezi kudorola sana, ni biashara ambayo ipo wakati wote, iwe njaa au kusiwe na njaa lazima watu wale.
Ni jukumu lako wewe kuangalia kwa mfano ni kipindi gani mahindi yanapatikana kwa urahisi na kusaga ili kupata unga huo na kuusambaza mtaani. Kuuza ni lazima utauza hata bila kujali kama utauza kwa faida ndogo au kwa faida kubwa.
Mbali na unga wa sembe ukiangalia upande mwingine maharage nayo, yanatumika sana kwenye familia zetu karibu kila siku na uzuri wake yapo maeneo mengi ambayo maharage haya yanapatikana kwa bei nafuu hususani hasa kipindi cha mavuno.
Unaweza ukanunua na kuyauza moja kwa moja au ukasubiri kipindi yakiadimika ukaanza kuyauza moja kwa moja na ikakusaidia kupata pesa. Uzuri soko lake liko wazi ukizingatia familia nyingi, zinatumia maharage kila siku.
Hali hiyo hiyo ndio inayoenda mpaka kwenye sukari, dagaa, mafuta ya kula, halikadhalika na ngano. Ni biashara ambazo zinawalaji wengi. Na watu wengi wametoka kupitia biashara hizo na kuwa na pesa nyingi sana.
Ukiwauliza watu wenye maduka ya reja reja ambayo yanauza vitu mchanganyiko, watakwambia vitu vinavyoendesha duka la reja reja au roho ya duka la reja reja ipo kwenye hivyo vitu na ndivyo vyenye faida.
Kama utaamua kufanya, kwa sababu pia wengi wanafanya, ni jukumu lako wewe kuingia na kufanya kwa akili, au kuongeza kitu cha ziada ili ufanye kwa ufanisi ikiwa ni kuanzia kwenye vifungashio na hilo litakusaidia kupata wateja wengi.
Kumbuka sijasema kwamba biashara hizi hazina changamoto. Kila biashara ina changamoto zake, lakini hata hivyo ni biashara ambazo walaji wake ni wengi na wanapatikana kila siku.
Mpaka hapo angalau umepata mwanga wa kile ambacho nilikuwa nataka kukuonyesha biashara ambazo haziwezi kufa au hata kama zikifa zitachukua muda mrefu sana kudondoka. Usichelewe kuchukua hatua, ndoto zako zinawezekana.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
.DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,








Feb 21, 2018

Huu Ndio Ukweli Kuhusu Maisha Ya Mafanikio Unaotakiwa Kuufahamu Vizuri.

No comments :

IIi kufikia mafanikio, kuna wakati inatakiwa uujue ukweli wa aina fulani hivi na kwa kuujua ukweli huo utakusaidia kufanikiwa. Lakini kuendelea kuishi kwa kujidanganya na huku ukiwa hujui mbele wala nyuma juu mafaniko utajidangaya tu, hutafanikiwa.
Najua utaweka juhudi hii au ile kufikia mafanikio, lakini hutaweza kufikia kwa sababu utakuwa bado unaishi kwenye dunia ya giza ambayo inakuwa imekufunika na ushindwe kutafuta mafanikio yako kama inavyotakiwa iwe kwako.
Kupitia makala hii ya leo, tunakuangazia kweli tano ambazo unatakiwa uzijue na ili zikusaidie kufanikiwa. Ni matumaini yangu, utafaidika vya kutosha na kuweza kubadilisha maisha yako kwa kufanyia kazi kweli hizi. Kweli hizi ni zipi, karibu ujifunze.

1. Ni kazi ngumu kufikia mafanikio.
Asije akakudanganya mtu kwamba kufikia mafanikio ni kazi rahisi, huyo atakuwa ni mtu mwongo kabisa. kufikia mafanikio inahitaji uweke juhudi na maarifa ya kutosha ili kufikia mafanikio hayo. Kama huweki juhudi huwezi kufanikiwa.
Kwa lugha nyepesi tu bila kukuficha kitu naomba nikwambie kufikia mafanikio ni kazi ngumu na sio nyepesi kama wengine wanavyowezza wakawa labda wanakudanganya kwamba ni kitu rahisi tu na cha mara moja.
Lakini hata hivyo haimaanishi kwa kuwa ni kazi ngumu kufika mafanikio, basi haiwezekeni kuyafikia. Kufikia mafanikio ni kweli ni kazi ngumu, lakini inawezekana kuyafikia kwa asilimia zote na hilo halina ubishi. Huu ni ukweli unaotakiwa uumeze kama ulivyo bila kutema.
2. Unahitaji msaada kufikia mafanikio.
Hakuna mafanikio ambayo unaweza ukayapata ukiwa wewe kama wewe. Unahitai msaada ili kuweza kufikia mafanikio yako. Pasipo kuweza kupata msaada huwezi kupata mafanikio yoyote, kwani mafanikio yapo kwa watu.
Kwa hiyo utaona unahitaji msaada kutoka kwa rafiki zako, utahitaji msaada kutoka kwa ndugu zako wa karibu na hata pia utahitaji msaada kutoka kwa wale watu wanaokusaidia kazi zako na ambao wanakuwa wana mchango fulani kwako.
Huhitaji hapa kutunisha kifua kusema mimi ndio mimi, mafanikio ni muunganiko wa misaada tofauti tofauti kutoka kwa watu wengine pia. Ukweli huu unatakiwa kuujua kwamba mafaniko yanahitaji msaada wa wengine pia, hivyo heshimu watu.
3. Makosa ni ngazi ya kufikia mafanikio.
Imezoeleka kati ya kitu kinachowaangusha wengi katika safari ya mafanikio ni yale makosa ambayo wanakuwa wanayafanya wakati wanatafuta mafanikio yao. Watu hao wamekuwa wakisahau kwamba makosa ni kama shule.
Unapokuwa unatafuta mafanikio ya aina fulani, kukosea ni kitu cha kawaida sana. Kwa hiyo hutakiwi kujilaumu kwa chochote kwamba kwa nini umekosea katika eneo la aina fulani, badala yake unatakiwa ujifunze kusonga mbele.
Utakwama sana kwenye maisha yako, kama makosa utakuwa unayachukulia  kwa umakini sana na inakupelekea mpaka kushindwa kufanya vitu vingine. Yafanye makosa yawe shule yako ya kukuwezesha wewe kuweza kusonga mbele zaidi na si kukurudisha nyuma.
4. Kuwa king’ang’anizi.
Sifa mojawapo kubwa ya watu ambao wamefanikiwa ni wabishi. Ni watu ambao hawakubali kushindwa kirahisi, ni watu ambao wanaamua liwalo na liwe, lakini wanapigana mpaka kuhakikisha ndoto zao zinaweza kutimia.
Hata wewe ili uweze kufanikiwa unatakiwa uwe king’ang’anizi sana. Kwa kifupi unatakiwa uwe na roho ngumu, roho ambayo haikubali kushindwa kirahisi, inayotaka lazima mabadiliko yaweze kutokea kwenye maisha yako.
Ukiujua vyema ukweli huu kwamba unatakiwa kuwa mbishi hilo litakusaidia sana kuweza kuweza kung’ang’ana kufanya kila linalowezekana na kuongeza juhudi zote kwa kufanya kila kilicho cha msingi, ilimradi tu ufanikiwe.
5. Jipe hamasa ya mafanikio kila siku.
Usifanye kosa la kusubiri hali au kitu chochote kikupe hamasa ya kufanya kile unachotaka kufanya. Jipe hamasa hiyo wewe mwenyewe kila siku. Kama huoni hamasa ikitokea usitulie, wewe endelea kufanya, hamasa itakuja mbele ya safari wakati unaendelea.
Washindi katika mafanikio hawasubiri hamasa ili kuweza kusonga mbele. Ni watu wa kufanya na mwisho wa siku hamasa inayofuata. Kwa hiyo hata wewe unaweza ukaanza kujihamasisha wewe mwenyewe.
Hakikisha unafanyia kazi kweli hizi muhimu kwako na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
MUHIMU ZAIDI; kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Feb 20, 2018

Usitegemee Kufanikiwa Kama Hautafanya Jambo Hili Mapema.

No comments :
Kufanya maandalizi ya kitu chochote kile ni jambo la muhimu sana kwako na pia ni moja ya dalili nzuri kwamba unajiandaa kuwa mshindi kwa kitu hicho unachokifanya. Kama haufanyi maandalizi ni rahisi tu kushindwa na hilo halina ubishi.
Ndio maana unaona mwanafunzi ni lazima ajiandae mapema ili aweze kufaulu mtihani wake, ndio maana unaona mkulima anaandaa shamba lake mapema pia ili wakati wa kilimo ukifika ili aweze kufanikisha kilimo chake.
Hiyo haitoshi unaona pia, mwana riadha anaanza kufanya mazoezi mapema  ya kukimbia ili wakati ukifika aweze kushinda mbio hizo, hiyo yote inaonyesha maandalizi ni kitu cha muhimu sana kwa ushindi wowote ule.
Hakuna mshindi anayetokea au kuibuka tu kiholela pasipo kuwa na maandalizi yale ya mwanzo ya kuweza kujifua haswaa ili kutengeneza ushindi huo. Kila ushindi unaouona umetokezea kwa nje, ujue kabisa ushindi huo umeandaliwa na haujaja kwa bahati.
Unapaswa ukumbuke pia hata wakati ule wa Nuhu. haikuwa kipindi cha mvua au gharika wakati Nuhu anajenga safina, bali Nuhu alifanya maandalizi ya mapema na gharika inayokuja mbele yake na hilo kweli lilikuja kutokea.

Halikadhalika na wewe unatakiwa kujenga maisha yako kwa ubora sana kipindi ambacho mambo yako hayajaanza kuharibika au mambo hayajaanza kubanana na mpaka ukasombwa na gharika ya changamoto.
Unatakiwa kujua kwamba wakati wa kutengeneza maisha yako ni sasa wakati bado una nguvu za kutosha ni si baadae. Huu ndio wakati wa kutengeneza safina ya maisha wakati hali, nguvu na muda wako bado vinakuruhusu.
Kitafika kipindi ambacho hautakuwa na uwezo huo yaani muda utakuwa huna, na wala nguvu utakuwa huna. Angalia sana usije ukaanza kulia kama wale watu waliokuwa wakimlilia Nuhu wafungulie kwenye safina, lakini akawaambia hakufunga yeye mlango.
Hata wewe angalia usije ukafika muda ambao utaanza kuwalilia watoto wako, ukaanza kuwalilia wajukuu wako wakati utakapoanza kusombwa na maji na ukiangalia ulishindwa kujenga safina yako mapema. Wakati wa kufanya na kukazana ni sasa na si kesho.
Kwa nini usubiri mabaya ya kukute ili upambane nayo wakati una uwezo wa kujindaa sasa mapema na kuyaepuka. Huhitaji kusubiri kitu, unahitaji kufanya kitu kwa ajili ya maisha yako ya kesho bila kujali hli uliyonao kwa sasa ni ipi.
Hebu nikuulize kitu, kama utashindwa kutengeneza maisha yako sasa na yakaonekana yana maana, je, utaweza kweli ukishazeeka. Hapo ulipo ni kijana umeshindwa je, ikifika uzeeni utaweza? najua hutaweza hata ufanyaje.
Ndio maana unatakiwa kuweka juhudi sana za kuhakikisha unafanya kila kinachowezekana wakati bado damu yako ina chemka, wakati bado una nguvu ili ufanikiwe. Nikwambie tu ukisubiri, jiandae kusombwa na gharika ya changamoto za maisha.
Na ubaya wa gharika inakuwa haina msamaha au hakuna kupona, ikikukuta ujue ndio tayari umeshaenda. Kwa hiyo usikubali kupoteza maisha yako ya mafanikio kwa sababu ya kushindwa kufanya maandalizi mapema.
Kuanzia sasa fanya maandalizi mapema kwa kila kitu ambacho unachokifanya. Usipofanya maandalizi mapema utaanguka na utajiangusha wewe mwenyewe na kutakuwa hakuna mtu ambaye ataweza kukuamsha tena.
Ndiyo maana, unatakiwa uweke akiba mapema kipindi ambacho kabla hujaishiwa. Unatakiwa uzime moto mapema, kabla moto haujawaka vya kutosha. Ni muhimu kufanya maandalizi mapema ya chochote kile ukifanyacho ili ikusaidie kuwa mashindi.
Kama hautafanya maandalizi ya mapema kwa chochote unachokifanya kushindwa hautaweza kukwepa hata kidogo. Kumbuka hata Nuhu alijenga safina mapema, kabla hata gharika haijafika. Tafakari na chukua hatua.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com