google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 30, 2016

Siri Nzito Za Kufanikiwa.

No comments :
Safari ya kuelekea kwenye mafanikio inahitaji ujasiri, sio ujasiri tu bali ujasiri wa hali ya juu sana, kama ilivyo ujasiri alionao simba awapo mwituni, katika kusaka riziki yake ili kuhakikisha ya kwamba halali au hafi kwa sababu ya njaa.
Ujasiri huo huo alikuwa nao simba ndio ambao unauhitaji wewe ndugu yangu, katika safari ya kujifunza, chukua muda wa kujivika taswira ya kiujasiri ili ufanikiwe zaidi.
Nafahamu ya kwamba ipo haja ya wewe kuendelea kujua mbinu ambazo zitakufanya upate ujasiri huo. Hata hivyo niweze kushukuru Mungu kwa kunipa kalama hiyo ya kuweza kutumia fikra chanya ambazo zinanifanya nikupe baadhi ya mambo yatakayokusaidia kwa namna moja ama nyingine katika kusaka mafanikio hayo.
Kama alivyo simba kuishi katika misingi ya kujiamini ,basi ndivyo ambavyo nilivyo na hasira juu ya neno mafanikio.

Laiti ungelifanya uchunguzi siku moja kumchunguza simba ungaligundua  ya kwamba simba anaishi kwa kujiamini ili aendelee kuishi miaka mingi zaidi, pia simba huyo huyo anaishi kwa hofu ambayo itafanya  asilale au afe njaa.
Kupitia hilo ifike mahali na wewe pia uishi kwa kujiamini ya kwamba unajua ambacho unakihitaji, pia uishi kwa hofu ya kushindwa katika mafanikio pia uishi kwa kuwa na hofu ya Mungu kwa kila hambo ambalo unalifanya siku zote.

Watu wengi ambao wamefanikiwa na ambao hawajafanikiwa wanafanana katika masuala ya kuishi bila hofu ya Mungu. Wapo wale ambao licha ya kwamba maisha yao ni kitajiri, lakini bado wanaishi katika misingi ya kutenda mambo yao bila kumshirikisha Mungu, maisha ambayo kiukweli yanafanya waishi kwa wasiwasi licha ya maisha yao kuwa mazuri.
Nikija upande wa pili wa shilingi ambapo  watu wengi wanaishi maisha ya duni, ambapo wengi wetu tupo pia tumekuwa ni watu wa kukata tamaa siku zote na imefiki mahali tumejikuta tunamsahau Mungu, sio kumsahau Mungu tu bali imefika kipindi mpaka tunakufuru, unaweza kusema leo nahubiri la hasha ila ukweli ubaki palepale kwa jambo lolote ambalo unalifanya ili uweze kufanikiwa unatakiwa uishi kwa kuwa na HOFU YA MUNGU.
Zifuatazo ndizo kanuni ambazo unatakiwa kuzitumia kufanikiwa;
1. Kuwa tayari kujifunza.
Moja ya njia ya kukusaidia kufanikiwa zaidi ni lazima uweze kujifunza, huenda ukawa hajanipata vizuri ila ukweli wenyewe ndio huu hapa, watu wengi wanataka kupanda ngazi ya kimafanikio, bila kujua namna ya kuitumia ngazi hiyo ya kupata mafanikio.
Kwa mfano leo hii utamkuta mtu anataka kuwa mfanyabiashara mkubwa lakini ukimwambia kuwa jambo hilo linahitaji ulazima wa kujifunza, utakuta mtu huyo hayupo tayari kujifunza juu ya biashara hiyo.
Lakini mimi huwa naamini jambo lolote ukitaka kulifanya kwa weledi ni lazima uwe tayari kujifunza, fikiria kwa umakini kisha uone ni kitu gani ambacho hauitaji kujifunza ambacho kinahusiana na mafanikio?

Ukitafakari kwa umakini utagundua ya kwamba hakuna jambo hata moja. Mambo ambayo hutakiwi kujifunza labda matendo ya hiari na yasiyo ya hiari yanayotokana na msukumo wa mwili tu yatokanayo na mawazo ya binadamu hasa hisia.
Kujifunza huku hakuhitaji wewe kukaa darasani miaka mingi, mpaka ufanikiwe ila inahitaji kujua unataka nini? Baada ya hapo ndio utagundua unatakiwa kujifunza nini.
Nikuibie siri ambayo hajawahi mtu yeyote kukuambia kwamba siri ya utajiri ipo kwenye "maandishi" siri hii usimwambie mtu bali chukua hatua pindi utakapopata ukweli juu ya jambo hilo, wengine wakikuuliza  juu ya mafanikio yako ndipo uwambia siri ya mafanikio ilipo.
2. Kuwa tayari kulipa gharama.
Mara kadhaa niwehi kuandika ya kwamba "chochote bila chochote huwezi kupata chochote" wengi walikuwa hawajanielewa ila leo ndio uwanja wako wa kuweza kunielewa juu ya jambo hilo.
Iko hivi kwa chochote kile ambacho unakitaka leo kina gharama zake, kama maelezo ya hapa juu yanavyojieleza kwamba unahitaji kuwa tayari kujifunza, basi jambo hili huenda sambamba na kulipa gharama, gharama hizi ni kama vile za kujifunza kwenye makongamono, kununua vitabu, majarida, magazeti ,vipeperushi kulipa ada za mafunzo mbalimbali ikiwemo semina au shule.
Ukiyafanya hayo utakuwa kwa ubora na weledi wa hali ya juu, utakuwa ni miongoni mwa watu ambao wanafanya mambo ya kimaendeleo kila siku, pia jamii ambayo inakuzunguka watatamani kwa kiwango kikubwa kitu ambacho unafanya wewe.
Kwa kuwa siri ya utajiri ipo kwenye mandishi endelea kufuatana nami kupitia mtandao huu wa Dira ya Mafanikio mpaka maisha yako yaimarike, nikutakie siku njema na Mafanikio mema.
Ndimi afisa mipango; Benson Chonya.(0757-909942)
(
bensonchonya23@gmail.com)

Jun 28, 2016

Tumia Njia Hizi Kujua Kipaji Chako.

No comments :
Moja ya changamoto kubwa inayowakabili watu wengi ni kutojua kwa undani kipi  kipaji chako ambacho Mungu amekupa na ambacho unaweza ukakitumia kwa namna moja ama nyingine ili uweze kuleta mabadiliko chanya katika jamii na wewe binafsi.
Na kwa kuwa kuna watu wengi ndio wapo kundi hilo, kuna usemi unasema ya kwamba wengi wape basi ngoja nifanye hivyo kuweza kuwapa somo hilo la namna ya kujua kipaji chako  kwani hii itamsadia kila mmoja ambaye atakwenda kufuatana nami mwanzo hadi mwisho katika mukutadha wa makala haya.
Tunapozungumzia neno kipaji huenda kila mmoja akawa na maana yake ambayo anaifahamu, lakini kwa namna moja ama nyingine ni lazima mtu aweze kuzaliwa nacho hivyo Mwenyezi Mungu huhusika pia katika kumpa mtu kipaji.
Hivyo endapo mtu atakifahamu kipaji chake inampasa sasa ajue namna ya kukiendeleza kipaji hicho ili kisife. Pia ikumbukwe ya kwamba tunapozungumzia kipaji tunamzungumzia binadamu na maisha yake kwa ujumla.
Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa na  Dr. Fred Luskin kutoka Stanford university yeye aliweza kugundua ya kwamba asilimia 65 ya watu wengi hawajui vipaji vyao na katika kundi kubwa la idadi hii ya watu ndio ambao wanafanya vitu ambavyo sio vyao.
Na pia  asilimia 35 iliyobaki hawa ndio ambao wameweza kuvijua hivyo vipaji vyao ingawa haviwasadii katika maisha yao na wengine kwa asilimia 100, hii ni kutoka mafanikio yatokanayo vipaji hivyo huwa ni ya muda mrefu.
Hivyo kwa kuwa watu wengi tunataka mafanikio ya muda mfupi uvumilivu hufika ukomo na kujikuta tunaviacha vitu hivyo na kuingia kufanya vitu vingine.
Mfano mtu anakuwa na kipaji cha kucheza mpira katika timu kubwa hapa nchini na nje ya nchi,na kwa kuwa huenda amecheza kwa muda mrefu bila matarajio yake kutimia mtu huyo huacha kile ambacho hukifanya na kuamua kufanya kitu kingine ambacho sio kipaji chake mwishowe mtu huyo anajikuta anafanya hiki anakiacha mara kile nacho anakiacha.
Ukiona hicho unachokiita kipaji chako hakitoi burudani, hakifundishi, hakishangazi basi hicho sio kipaji. 
Namna ya kugundua kipaji chako.
1. Kumuomba Mungu.
Hapa huwa pananifanya nimkumbuke sana rafiki yangu Samweli Salali kwani aliwahi kuniambia ya kwamba kipaji ni kusudio la Mungu kwa kila mja wake. Kwani katika mafundisho yake katika vitabu vya dini vinasema kabla sijaumba nilikujua.
Hii inamaana kila mwanadamu aliyeumbwa na Mungu ana kipaji chake, hivyo kinauwezo mkubwa wa kubadili maisha yake na jamii kwa ujumla, ila kipaji hicho watu wengi hawahujui mpaka dakika hii kuwa kipi kipaji chake ambacho Mungu kampa.
Hivyo kama wewe ni miongoni mwa watu hao ni muda wako muafaka wa kutumia Muda huu kumuomba Mungu akuonyeshe kipaji chako hasa na kipi kwa sasa?

Tumia kipaji chako kikusaidie kufanikiwa.
2. Marafiki, ndugu na wazazi.

Hili ni kundi muhimu sana ambalo litakusaidia wewe kujua kipaji chako. Labda unaweza ukajiuliza ni kivipi? Tulia leo nipo kwa ajili yako. Watu ambao wanakuzunguka ndio wana picha kamaili juu ya maisha yako.
Kwa mfano mtu akiwa mlevi hawezi kusema mimi ni mlevi ila watu ambao wanakuzunguka ndio ambao watasema yule jamaa ni mlevi sana. Picha hiyohiyo ya kumuona mtu mwingine tabia yake ndiyo ambayo inatumika kujua kipaji chako.
Hebu waulize nyie mnanionaje, mna picha gani? Mnahisi nina kipaji Gani? Baada ya kuwauliza hayo wao ndio watakupa picha kamili juu ya kipaji chako na maisha yako kwa ujumla.

3. Matatizo.
Matatizo ni njia nzuri ya bora sana ya kugundua kipaji chako. Ulimwegu wa leo ni ulimwengu wenye changamoto nyingi sana, hata hivyo kutokana na suala hilo, pale matatizo yanapotokea na kuyapatia ufumbuzi sahihi hapo ndipo utakapojua kipaji chako.
Kwa mfano watu wengi leo hii wanapenda maisha ya kufanyiwa kila kitu. Tuchukulie leo hii unamtegemea mtu fulani ili aweze kukutimizia lengo lako. Halafu siku ya siku mtu huyo anakufukuza nyumbani kwake na kukuambia nenda kajitegemee.
Baada ya kuambiwa hivyo ndipo unakuja kugundua ni kipi kipaji chako baadala ya kuendelea kuwa tegemezi. Hebu tuone mfano mwingine unakuta mtu alikuwa ni mfanyakazi wa ofisini ila baada ya kustafu unajikita katika ufugaji mwisho wa siku unagundua wewe ulikuwa una kipaji cha ufugaji badala ya kufanya kazi za maofisini.
Hivyo wito wangu kwako ni vyema ukagundua kipaji chako mapema usisubiri changamoto fulani zitokee ndipo ugundue kipaji chako.
4. Mashindano.
Kuna baadhi ya nchi huandaa mashindano mbalimbali kwa ajili ya kusaka vipaji, hili jambo jema sana hata hapa kwetu nchini kuna baadhi ya mashindano hufanyika ambayo husaidia kujua vipaji vya watu kama vile bongo star search, fiesta, DJ compition, umiseta na mangineyo mengi.
Hivyo kama kweli unataka kujua kipaji chako endapo yatatokea mashindano yoyote yale jitahidi sana kwenda kushiriki kwani hii itakusaidia kwa kiwango kikubwa kuweza kujua ni kipi kipaji chako.
Mpaka kufikia hapo niweke nukta kwa kusema kama ukwisha kugundua hicho kipaji chako ni vyema ukajua ni namna gani ya kugeuza hicho kipaji chako kuwa pesa, kwani hapo ndipo palipo kuwa na changamoto kubwa.
Ndimi Afisa mipango Benson Chonya.
Simu( 0757909943)
bensonchonya23@gmail.com

Jun 27, 2016

Mambo Muhimu Ya Kukumbuka Kama Unataka Kuwa Mjasiriamali Mwenye Mafanikio.

No comments :
Kila kitu katika maisha ya binadamu kinaanza kama wazo. Haijalishi kitu hicho kimeleta mafanikio au la, lakini mwanzo wake huwa unaanzia kwenye wazo analokuwa nalo mtu.
Kumbuka  siku zote, mawazo yako ndiyo yanayokufanya uwe na maamuzi ya aina fulani. Maamuzi hayo pia ndiyo yanakufanya uwe na matendo ya aina fulani. Na matendo hayo ndiyo yanayotoa matokeo ya kile ukifanyacho.
Kwa hiyo, ikiwa unataka kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio, kitu cha kwanza unachotakiwa kuwa nacho ni mawazo sahihi. Unapokuwa na mawazo sahihi yatakusaidia kufanya maamuzi na matendo sahihi.
Hivyo, mafanikio utayaona kwa sababu maamuzi na matendo yako yatakuwa sawa kukusaidia kufanikiwa. Kwa sababu hiyo, ni lazima kukumbuka mambo ya msingi kama unataka kuwa mjasiramali mwenye mafanikio. Kwa vipi?
Yafuatayo  Ndiyo Mambo Muhimu Ya Kukumbuka Kama Unataka Kuwa Mjasiriamali Mwenye Mafanikio.
1. Jifunze kuwajibika.
Mjasiriamali mwenye mafanikio ni yule ambaye anawajibika na kuweka mambo sawa kila wakati na sio kusubiri hali fulani ndizo zimletee mafanikio. Mjasiriamali huyu anakuwa tayari kukabiliana na kila changamoto na kutatua.
Hili ni jambo muhimu sana la kukumbuka na kuweka kwenye akili ikiwa unataka kuwa mjasirimali mwenye mafanikio. Wakati wote usisubiri matokeo ya aina fulani bali pambana mpaka kieleweke.

Jifunze kuwajibika.
2. Jifunze kuwa mbunifu.
Ubunifu ni njia pekee itakayokufanya uwe mjasiriamali wa mafanikio. Hakuna mafanikio kwenye ujasiriamli kama wewe si mbunifu. Karibia kila kitu kinaweza kufa kwako usipochukua hatua za kuwa mbunifu.
Jifunze kufikiri tofauti na wajasiriamali wengine. Kwa mfano kila wakati unaweza ukawa unajiuliza ufanye nini cha ziada ili uongeze idadi ya wateja kwenye biashara yako? hapo ndipo unatakiwa kubuni mambo ya ziada ambayo wengine hawana.
3. Jiamini.
Vipo vikwazo vingi katika safari ya mafanikio. Lakini yote hayo yanapotokea ni wakati wa kujifunza kujiamini wewe mwenyewe na kuamini ndoto zako kuwa unaweza kuzifikia. Hakuna mtu mwingine anayeweza kufanya hivyo zaidi yako. Ni lazima ujue kujiamini kwako ndio msingi mkubwa wa mafanikio.
Wajasiriamali wenye mafanikio wana hulka au tabia ya kujiamini sana. Hicho ndicho kinachowasaidia waweze kufikia viwango vya juu vya mafanikio. Hata wewe kama usipochukua jukumu la kuweza kujiamini hakuna utakachoweza kufanikisha sanasana  utazidi kushindwa.
4. Usikate tamaa mapema.
Hakuna kitu kibaya kama kukata tamaa mapema. Unapokuwa unakata tamaa unakuwa unaitangazia dunia kwamba wewe huwezi tena. Na kimsingi hakuna faida hata moja ambayo mtu anaweza kuipata eti kwa sababu ya kukata tamaa.
Wajasiriamali wakubwa wenye mafanikio ni ving’ang’anizi wakubwa wa malengo na ndoto zao. Wanajua bila kufanya hivyo hakuna kitakachofanikiwa. Siku zote mafanikio yanakutaka usikate tamaa mapema la sivyo, utayasikia mafanikio kwa wengine.
5. Jitoe mhanga.
Je, wewe ni miongoni mwa watu wanaojitoa mhanga kuhakikisha ndoto zao zinatimia? Kama jibu ni ndiyo basi wewe ni miongoni mwa wajasiriamali wenye mafanikio makubwa.
Sifa kubwa ya wajasiriamali wenye mafanikio ni kujitoa. Mara nyingi huwa hawaangalii hasara watakazozipata zaidi sana huangalia kile watakachokipata. Hili ni jambo muhimu sana la kulielewa na kuliweka kwenye akili yako ikiwa wewe unataka kuwa mjasiriamali wa mafanikio.
6. Nenda hatua ya ziada.
Jifunze kujiongeza na kuongeza vitu vya ziada ambavyo ni tofauti na wajasiriamali wengine. Ikiwa huwezi kujitofautisha wewe na wajasiriamali wegine, basi moja kwa moja upo kwenye hatari pengine ya kushindwa kwa baadae.
Hapa unatakiwa kujitoa na kufanya kazi zako kwa uhakika na muda mrefu. Hiyo haitoshi unatakiwa kujifunza kila wakati yale ambayo wenzio wanayafanya. Kwa kwenda hatua za ziada ni silaha muhimu ya kukufanya ukawa mjasiriamali wa mafanikio.
Naamini umejifunza kitu cha kukusidia kuwa mjasiriamali mwenye mafanikio. Lakini usiishie hapa endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kupata maarifa yatakayoboresha maisha yako.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048 035,

Jun 24, 2016

Aina Tatu Za Mawazo Zinazokufanya Ushindwe Au Ufanikiwe.

No comments :
Kiasili binadamu tumepewa uwezo mkubwa wa kufikiri ukitofautisha na wanyama wengine. Uwezo huu tulionao huwa unakuja hasa kutokana na matumizi ya mawazo au kufikiri kwetu. Kufikiri huko ambapo tunafanya kila siku na kila wakati ndipo kunapotufanya tuwe na maisha ya aina fulani, haijalishi yawe ya mafanikio au kushindwa.
Lakini hata hivyo wengi wetu huwa tunafikiri au tuna mawazo ya kimazoea na kushindwa kutambua kwamba hayo mawazo yetu pia yamegawanyika. Kwa mawazo yoyote uliyonayo mara huwa yamegawanyika katika sehemu. Kwa mfano unapowaza wazo fulani, wazo hilo linakuwa lipo moja kwa moja kwenye sehemu ya kwanza, au ya pili au ya tatu ya mawazo yako.
Kivipi hili linatokea? Fuatana nami katika makala haya kujua aina tatu za mawazo zinazokufanya ushindwe au ufafanikiwe katika maisha yako.
1. Mawazo elekezi.
Haya ni mawazo yanayoleta mafanikio. Kwa lugha nyingine haya ni mawazo chanya. Mawazo yenye uwezo wa kutubalisha na kutufanya tuwe na mawazo bora. Haya ni mawazo yanakufanya uamini unaweza kufanya biashara, unaweza kuwa tajiri au unaweza kuacha chochote.
Kwa kifupi, haya ni mawazo yanayokupa mwongozo wa kufanikiwa. Unapokuwa na mawazo haya kila wakati, elewa kabisa upo kwenye njia sahihi ya kuelekea kwenye mafanikio. Ni mawazo yanayotoa hatma ya kesho yetu itakuwaje.

2. Mawazo ya kuharibu.
Kama huna mawazo chanya au mawazo elekezi ya kukusaidia basi elewa utakuwa na mawazo ya kuharibu. Mawazo haya wakati mwingine yanafahamika kama mawazo hasi. Haya ni mawazo ambayo  kila wakati yanakwambia huwezi kufanikiwa au huwezi kufanya hili.
Haya ni mawazo yanayoua na kuharibu maisha ya wengi. Jaribu kujiuliza utakuwa ni mtu wa aina gani ikiwa kila unalolifanya unaona kama haliwezi kufanikiwa? Ukiwa na mawazo haya, tambua una mawazo ya kuharibu ambayo hayawezi kukusaidia kwa chochote.
3. Mawazo ya hovyo.
Unapokuwa na mawazo haya mara nyingi yanakuungoza katika vitu kama kupoteza muda au kufanya mambo yasiyo na faida. Utakuta badala ya kukaa chini na kufanya mambo ambayo yanaweza yakakusaidia kufanikiwa, badala yake unajikuta unafanya mambo ambayo hayana msaada kama kupiga soga na marafiki.
Kumbuka, aina hizi za mawazo ndizo zinazokufanya ufanikiwe au ushindwe katika jambo unalolifanya. Jambo kubwa kwako la kujiuliza je, ni aina gani ya mawazo uliyonayo ambayo inakutawala sana? Kwa aina hiyo ya mawazo uliyonayo ndiyo itakayoamua maisha yako yaweje.
Nikutakie siku njema na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila siku. Hakikisha pia usikose kuwashirikisha wengine waendelee kujifunza kupitia mtandao wako huu. 
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Jun 23, 2016

Je, Unahitaji Mafanikio Ndani Ya Muda Mfupi?

No comments :
Kuna wakati inakupasa uweze kuondokana kwenye jopo la watu ambao wanalalamika na kuingia kwenye kundi la watu ambao ni watu wasaka mafanikio daima na sio walalamikaji. Kuna baadhi ya watu huelekeza mawazo yao hasi katika kulaumu watu wengine kuliko kuwaza ni kwa jinsi gani wataweza kuyasaka mafanikio kiurahisi kabisa.

Mara nyingi sana tunatumia muda mwingi katika kufanya mambo ambayo hayana manufaa katika maisha yetu. Kwa mfano, tumekuwa tukipoteza muda kwenye mitandao au kupenda mazungumzo yasiyo na msaada kwetu. Kwa kuwa tunapoteza muda huo mwingi katika mambo yasikuwa na tija inafika mahali tunakuwa ni watu maisha ya kawaida kila siku.

Na ili kutoka hapo kwenye kuishi maisha ya kawaida, hakuna dawa nyingine zaidi ya kuacha kufanya mambo yasiyo na manufaa kwetu. Ukiweza kufanya hivyo, mafanikio utayapata tena kwa muda mfupi. Siri kubwa ya kupata mafanikio kwa muda mfupi ipo kwenye kufanya mambo yenye manufaa kwako kila siku na si kinyume cha hapo.


Najua unakuna kichwa unawaza “daaaah! sasa Afisa mipango kama nikitaka mafanikio kwa muda mfupi nafanyaje tena?” Kama ni hivyo na unataka kusikia jibu kutoka kwa afisa Benson nisikilize. Ili kupata mafanikio kwa muda mfupi, mbali na kutokufanya mambo ambayo hayana manufaa kwako pia zingatia sana yafuatayo:-

1. Amini nguvu iliyopo ndani yako kwamba unaweza.
Watu wengi hawaamini nguvu ambazo zipo ndani yao. Wengi huamini ya kwamba mafanikio huja kwa watu mafisadi peke yao. La hasha mafanikio yapo kwa kila mtu ambaye anamini ya kwamba yeye ni mshindi katika maisha yake, bila kuangalia ni changamoto ngapi ambazo amezipitia.

Unapokuwa unaamini uwezo na nguvu kubwa uliyonayo ndani mwako, inakusaidia sana kufikia mafanikio yako kwa muda mfupi. Kwa kadri utakavyozidi kuamini na kutumia vipawa na nguvu zilizopo ndani yako, utajikuta mambo mengi yanaenda vizuri tofauti na ulivyokuwa ukiwaza.

Tumia muda sahihi, kufikia mafanikio yako.
2. Kuwa na kusudi maalamu kwa chochote anachotaka kufanya.

Moja ya changamoto ya watu wengi ambao walifeli kimaisha ni kwamba watu hao walifanya vitu bila kujua ni nini kusudio lao maalumu, hata hivyo ikawapelekea watu hao kuweza kuwa na malengo ambayo hayana tija. Unakuta mtu anafanya biashara ukimuuliza kusudio la kufanya biashara hiyo utakushanga ya kwamba hata mfanyabiashara huyo huenda ukawa hajui pia.

Unahitaji kuwa na picha kamili ya jambo ambalo unalifanya kwa miaka ya mbeleni. Picha hii ndiyo ambayo itakuonesha utaweza kufanikiwa kwa kiasi gani? Au utashindwa kwa kiasi gani. Kama ni biashara ni lazima uwe na mlolongo mzima wa biashara yako jinsi itakavyokuwa kwa siku za mbeleni.

3. Usichukue ushauri wa kila mtu.

Kimsingi maneno ya watu yapo ambayo yanajenga kwa namna moja ama nyingine. Ila maneno ambayo hajajengi ndiyo yapo mengi zaidi, kwa mfano leo hii utaka kufanya biashara utakwenda kumshirikisha mtu ambaye yupo karibu yako unakwenda kuomba ushauri, mtu huyo atakwambia biashara hiyo hafai.

Utakapoambiwa biashara hiyo haifai mwishowe unajikuta unawabadilisha mawazo na kufanya jambo jingine na kwa kuwe wewe haujia amini unajikuta huna hata jambo hata moja ambalo unalifanya kwa uhakika. Mwishowe unakosa hata jambo moja ambalo lina manufaa kwako.


4. Fanya jambo la kwako.

Ili kufanikiwa kwa muda mfupi ni lazima kujua u wewe wako ndio siri ya mafanikio kwani moja ya watu wengi walioshindwa katika maisha ni kwamba waling'ang'ana kufanya vitu visivyokuwa vya kwao. Nikuache na swali la kujiuliza je jambo ambalo unalifanya ni lako?

Pia kumbuka maisha ya mwanadamu yanafanana na miiba ya michongoma kwa maana ya kwamba kila wakati uwe tayari katika kupambana na changamoto ambazo zinajitokeza kama ilivyo kwa miiba ya michongoma, maana miiba hii kila wakati upo  tayari kwa ajiri ya upambanaji tu.

Mwisho Afisa nimalizie kwa kusema akili ikiamua kufanya jambo inawezekana hivyo inahitajika nguvu ya mwili katika kuisaidia akili katika utekelezaji. Naamini ukifanya mambo hayo yatakusaidaia kufikia mafanikio yako kwa muda sahihi  unaohitajika.

Tunakutakia siku njema na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila wakati. Karibu sana na tupo pamoja.


ANGALIZO; Lengo la makala hii ni kukuhamasisha kufikia mafanikio yako kwa muda sahihi kama inavyotakiwa iwe. Lakini usije ukafikiri makala hii inakutaka utumie njia za mkato ili ufikie mafanikio yako kwa muda mfupi. Makala hii inahitaji uachanae na mambo yote yatakayokupelekea uchelewe sana kufanikiwa. 

Imeandikwa na afisa mipango: Benson Chonya.

Jun 22, 2016

Kijana Wa Umri Wa Chini Miaka 30 Anayemiliki Kampuni Yake Binafsi.

No comments :
"Endapo utafika miaka 25 hujui unapoelekea ujue fika umekwisha potea"

Hayo ni maneno ambayo aliwahi kuniambia mama yangu mpendwa, hivyo kila nikikaa huwa yanajirudia sana  kichwani mwangu. Maneno hayo ndiyo ambayo yananipa hamasa kwa kila jambo ambalo nalitenda siku zote, pia hunifanya niongeze juhudi na maarifa zaidi kwa kila jambo ambalo nalifanya.
Kwani juhudi nilizonazo hunifanya niwe mbunifu kila jua lichomazapo. Ubunifu huu huwa unanijenga hasa pale ninapoyakumbuka maneno ya mwalimu wangu wa somo la brand Tanzania Mr. Nduku Jr kwani mara kadhaa alikiwa ananiambia ya kwamba kwa kuwa zama zimebadilika hauhitaji kupeleka hirizi kwenye biashara bali unahitaji ubunifu utakao kutofautisha na watu wengine.

Hivyo katika kuthibisha juu ya kauli hizo ambazo nimezieleza, mara namuona kijana kwa mbali ambaye amevalaa tisheti nyeupe ambaye yupo ofisini kwake ila kadri nivyozidi kusogea nagundua ya kwamba wapo na vijana wenzake, huku kijana huyo aliyevalia tisheti ya nyeupe akiwa anazungumza.
Loooh! Kadri ninavyozidi kusogea na gundua ya kwamba tisheti hilo limeandikwa Tim success ltd. Mmh kama ilivyokuwa kawaida yangu nikiona neno success (Mafanikio) huwa mishipa ya aldenalini huwa inashutuka kama nimepita sehemu yenye giza huku nikiwa na hofu fulani.

Hivyo kwa kuwa nimeona fulana imeandikwa success (Mafanikio) nikataka kujua mawili matatu kutoka kwao na kuwaomba nifanye mazungumzo japo ya dakika chache na kijana huyo.

Baada ya kujitambulisha mimi, kisha kijana huyo akaanza kujitambulisha kwa kusema; "Kwa jina naitwa Tamimu ni kijana ambaye mnamo mwaka 2008 niliweza kuhitimu chuo kilichopo mkoani morogoro, pia pale morogoro niliweza kusomea masomo masuala ya tekinolojia ya habari ya mawasiliano(IT).
Baada ya kumaliza niliungana na wanafunzi wengine mbalimbali katika kuandika barua kwa ajili ya kuomba ajira kama wafanyavyo vijana wengi baada ya kumaliza vyuo.

Muda mwingi ulipita bila kuona mafanikio ya kupata ajira, kila tangazo ambalo lililotoka kuhusiana na ajira ambalo lilikuwa linahusu ilikuwa ni lazima niweze kutuma barua ya maombi. Mara kadhaa nilikuwa nachaguliwa mpaka kufanya usaili lakini matokea yake nilikuwa ninaishia kufanya usali tu, licha yakuwa nilihitimu na kuwa nawastani mkubwa wa alama. Ilifika mahali mpaka nikaanza kulaumu ni kwanini nilikwenda kusoma?

Miaka mitatu ilikatika bila mafanikio yeyote ya kupata ajira, mnamo mwaka 2012 nilikutana na kaka mmoja huko maeneo ya kwetu songea, ambaye alikuwa ni rafiki wa kaka yangu ambaye alikuwa anaishi huko jijini Dar-es-salaam.
Hivyo kwa kuwa nilikuwa naamini ya kwamba Dar-es-salaam ni  njia panda ya kuelelekea ulaya hivyo niliamini ya kuwa huko kila kitu kipo, hii ni kutokana jinsi ambavyo huwa nasikia na kuona habari mbalimbali juu ya jiji hilo hivyo niliamini kupitia huyo rafiki yake kaka, nitakwenda kupata jawabu tosha juu ya tatizo langu la ajira.

Hivyo nilimueleza changamoto kubwa ambayo ilikuwa inanisibu, baadae kaka huyo(jina limehifadhiwa) alinimbia ya kwamba kutoka na kitu ambacho nimesomea nina uwezo kufanya kitu kikubwa na kutengeneza kipato changu ambacho  kitasaidia kutatua changamoto zangu binafsi pasipo kutegemea suala la ajira ambalo ni changamoto sana kwa wengi.

Baada ya siku chache tangu siku ambayo tulizungumza maneno yale, tuliweza kusafiri kwenda Dar, huko niliweza kujifunza masuala ya kutengeneza mabango ya kutangaza biashara mbalimbali, bussiness card yaani kwa ufupi naweza sema nilijifunza masuala yote yanayohusiana na designing kwa ujumla.
Pia nilijikita zaidi zaidi katika kuweka alarm za magari, muziki kwenye magari pamoja na stika za magari na ufundi mwingine. Kufanya hivi kukanifanya niweze kupata kipato ambacho nilijitahidi kuweka akiba, akiba ambayo ilinifanya nije nimiliki kampuni yangu  ambayo inaitwaTim success Ltd kama unavyoona kwenye tishiti hii.

Kijana Tamimu katikati,
akiwa na mwandishi wa makala haya Benson Chonya,
 Kushoto kabisa.
Pamoja na misukosuko mingi ambayo nilikuwa naipata wakati wa kusajili kampuni hii nilijipa moyo pasipo kuwa na hata chembe ya kukata tamaa. Ilifika kipindi hata pesa ya kuendesha maisha yangu ilikuwa ngumu kwa kuwa pesa nyingi zilitumika katika nauli pamoja na usajili wa kampuni.

KUHUSU KAMPUNI
Kwa kifupi ni kwamba mimi kama ndiye mwazilishi wa kampuni niliwaza ya kwamba katika nchi yetu lina jopo kubwa ni vijana. Na kwa kuwa asilimia kubwa ya vijana hao ni wale wasomi na wasio wasomi, lakini changamoto kubwa ambayo inatukabili ni suala la ajira, nikaona ni vyema kwangu niifanye kama fursa ili niweze kuwasaidia vijana wenzangu, hivyo nikawakusanya vijana wenye ujuzi na wasio na ujuzi tukajifunza pamoja kuweza kufanya mambo mbalimbali.
Mambo hayo ni kama vile umeme , mapambo ya nyumba, kufunga kamera za ulinzi majumbani, kufanya designing, kupima viwanja(land survey),kuandika miradi mbalimbali na kuwashauri vijana wengine ambao wamekata tamaa na Maisha haya.

Kama timu ya mafanikio mnaleta suluhisho na changamoto gani ambayo inaihusu jamii kwa ujumla? Kama timu tumeamua kuja na suluhisho la changamoto ya maji. Kwa kuwa tunasema kwa kuwa maji ni uhai, hivyo tukaona ni vyema tuweze kuja na majibu kwani changamoto ya maji ni kubwa.
Unajua ndugu mwandishi licha ya kuendelea kusema ile sera ya kilimo kilimo kwanza lakini tunashidwa kufikia sera hiyo kwa kiwango cha juu, hii ni kutokana hatuna kilimo cha umwagiliaji, hivyo tunajikuta tunafanya kilimo kilekile miaka nenda miaka rudi. Pia ukijaribu kufanya uchunguzi mdogo utagundua ya kwamba majimbo mengi yana changamoto ya maji.
Hivyo sisi kama vijana wachapa kazi tumeamua kuja na suluhisho ambapo tunatengeneza visima ambavyo maji mengi yatavunwa kwa kutumia nguvu ya upepo, hapa ndugu mwandishi haitaji uwepo wa Umeme, au kupungua kwa maji kwenye chanzo bali mashine hii itatoa maji muda wote, nafikiri hii itasaidia sana hasa maeneo ya mjini na vijini ambayo kiuhalisia yana changamoto ya maji, wito wetu kwa viongozi Wa serikali na watu wengine hii ni fursa ambayo itabadili Tanzania kwa asilimia kubwa sana, kwani tutakwenda kuwa wakulima bora ambao hatutegemei misimu kufanya kilimo chetu tu.

Neno langu la mwisho ni kwamba kupata maendeleo kwa kiwango kikubwa inawezekana lakini jambo la msingi la kuzingatia ni kwamba inahitajika ushilikishwaji wa wananchi katika kutoa maamuzi yao kwani ni muhimu sana, mwisho kabisa nawashauri sana vijana ambao hawana ajira ni kwamba wazipe nafasi bongo zao kuweza kufikiri kwa umakini ni jinsi gani wataweza kuondokana na adhaa hii ya ajira kama tulivyofanya sisi

Kama una swali lolote kwa Mr tamimu piga au sms kwenda
0714-800922.
Kama una hadithi kama hizi zenye ukweli na ubunifu wasiliana na afisa mipango Benson chonya (0757-909942
).

Jun 21, 2016

Malezi Mabaya Ya Familia Ni Adui Wa Mafanikio.

No comments :
Miongoni mwa sababu kubwa iliyonifanya leo kuchukua kalamu  kuweza kumwaga wino wangu juu ya karatasi ni kwamba uvumilivu umenishinda ndani ya moyo wangu. Mambo yamenifika shingoni ni lazima niyaseme leo kabla umri wangu hajaelekea jioni (uzeeni). Hata nikiangalia saa nayo bado mishale inazunguka pia hata siku nazo hazijawahi kumsaliti lady jay dee kwamba siku zinaganda.
Siku chache zilizopita tuliadhimisha siku ya mtoto wa Afrika kama ambavyo  huadhimishwa kila mwaka kitu hiki ni kizuri ambacho kinafaa kiendelezwe katika jamii tunazoishi kwenu kufanya hivi ni kudumisha amani na upendo kwa watoto wetu.
Tuachane na hayo kwani hayo yamekwishapita na wala haina haja tena kuzungumzia masuala ya maadhimisho hayo.  Ila leo nimeona ni vyema tuzungumzie kwa uchache juu ya MADILI BORA YA FAMILIA.  Jamii ya leo imekosa elimu tosha juu ya malezi bora kwa familia.
Hebu jaribu kuzunguka mtaa wa kwanza utagundua kati ya watoto 9 kati ya 10 wanazungumza lugha za matusi zaidi  kama wanaimba nyimbo za injili au bongo fleva. Ukitoka mtaa wa kwanza pita mtaa wa pili huko nako utastajabu ya Musa maana huko watu wazima na akili zao wanacheza nyimbo za vigodoro, baikoko pamoja na watoto wao.
Watu wazima hao ukichungunza kwa umakini utagundua nguo ambazo wamezivaa ni fupi mithili ya mabawa ya nzi, watu hao nguo ndefu na za heshima kwao huwa ni zenye upupu. Mmmh tunakwenda wapi?

Tena toka mtaa pili ingia mtaa wa tatu huko nako utashangaa kuokota dhahabu mchangani, watoto wadogo wamekuwa ndio wanaigizwa kununua bia, madawa ya kulevya na mengineyo mengi. Ukitoka mtaa huo jaribu kuingia mtaa mwisho huko nako kweli utaamini dunia inaelekea ukiongoni maana kuna mambo ya ajabu sio kawaida ya nchi, kama Tanzania huko utakutana na watoto ambao ni omba omba wengi ambao waliletwa duniani na wazazi wenye akili timamu kabisa, wazazi hawa huwa napenda kuwaita "sura ya mzee akili ya mtoto" maana hawafai hata kidogo.
Tunasema mara kadhaa kuwa kijana ni taifa la kesho. Maneno hayo yatadhibitisha ukweli huo kwa malezi mtindo huo? Ya kuwalea watoto malezi yasikuwa na heshima wala utukufu Mbele za Mungu. Kiukweli najaribu kujiuliza kwa umakini bila hata kupata majibu sahihi tunaelekea wapi kwa maisha ya aina hiyo?
Kimsingi ni kwamba ugumu wa maisha haya tunayasababisha sisi wenyewe walezi wa familia zetu kwa namna moja ama nyingine. Mara kadhaa tumekuwa tukiwatamkia maneno mabaya sana watoto zetu hata hivyo kupelekea madili mabovu kwa jamaii hii. Mfano wa maneno hayo wapo wale wanaowambia kuwa watoto wao ni wezi au vibaka.

Kila kukicha watoto wa mitaani wanaongezeka kwa idadi kubwa, ukichunguza kwa umakini juu ya hilo utagundua ya kwamba chanzo la ongezeko hilo ni mateso na mihangano mingi ya kifamilia ambayo kila baada ya sekunde  inafanya ongozeko la watoto hao.
Wapo pia baadhi ya wazazi huwakatisha tamaa watoto wao kwa namna moja ama nyingi pindi wakiwa wadogo na kusababisha maisha magumu kwa watoto na kuwapotezea dira ya maisha. Watoto yatima wanaachwa katika mazingira magumu sana ambayo kila mwanajamii hufumba macho pindi anapo watoto wa aina hiyo na kuona mtu huyo hausiki. Tunaelekea wapi?

Ikiwa tunasema ya kuwa dalili ya mvua ni mawingu kwa methali hiyo tunaweza tukafananisha na kusema ya kwamba dalili ya umaskini wa nchi ni mateso, chuki na migogoro ya kifamilia inaandaa kizazi chenye maisha duni ambacho kinaamini katika misingi ya kuombaomba, wizi, utumiaji wa madawa ya kulevya na tabia nyingine ambazo hazipendezi machoni pa Mungu na kwa watu wenye heshima zao. Nauliza tena tunaandaa kizazi cha aina gani?
Hebu kabla sijaenda kuweka nukta tuangalie malezi ya watoto katika baadhi ya familia nyingi. Katika kufanya utafiti nimegundua ya kwamba malezi ndiye ambaye yanaandaa kwa kiasi kikubwa mafanikio ya mtu kwa namna moja ama nyingine. Wazazi wengi hawana muda wa kukaa na kuzungumza na watoto wao, ili kujua watoto wao wanahitaji nini katika maisha yao, wazazi wengi wamekuwa wanafahamu ya kuwa mtoto ni lazima aende shule, apete mahitaji mengine kama kula, malazi pamoja na chakula huku wamesahau watoto wanahitaji zaidi ya hayo.
Hebu tujiulize ya kwamba ni mara ngapi umekaa na watoto wako kuongea nao kuhusu mambo mbalimbali yatakayomjenga kwa hapo baadae? Tujiulize tena hili tatizo na ongezeko la watoto yatima chanzo chake ni nini? Halafu kwa nini kila huwa  hatujali juu ya jambo hili.
Wito wangu ni kwamba tuache kuchukulia vitu katika taswira ya kawaida, najua suluhu juu ya jambo hili lipo payana kabisa, tuache kupita na gari kwa mwendo wa kasi ili tuone mambo haya yanavyowadhuru watoto wengi katika nchi yetu. Kuna usemi unasema mtoto wa mwenzio ni wako.
Ukweli juu ya kauli hii upo wapi? Kauli hiyo ipo kwa baadhi ya vituo vya kulelea watoto yatima na mazingira magumi ila katika taasisi na watu wengi kauli hiyo imekuwa haikuhusu. Tafadhari najua ujumbe umefika mahali pake hivyo ni wakati muafaka wa kuchukua hatua mahususi kuondokana na suala hili.
Ndimi, Afisa mipango Benson chonya.

Jun 20, 2016

Mambo 8 Ambayo Watu Wenye Mafanikio Hawapotezi Muda Kuyafanya.

No comments :
Katika harakati za kutafuta maisha si ajabu sana kukutana na watu walio kata tamaa au watu wenye msongo wa mawazo inayotokana hasa na kuona ndoto na malengo yao hayatimii. Ni jambo ambalo huwa linatokea sana miongonii mwetu na kufikia mahali kuona maisha kama hayafai.
Lakini kitu nilichokuja kugundua, kipo chanzo kikubwa kimoja tu ambacho hupelekea kuona ndoto au malengo ya wengi kutokutumia na kusababisha msongo wa mawazo au kukata tamaa. Chanzo hiki si kingine bali ni kupoteza muda kwa mambo madogo madogo.
Ukiwa kama mjasiriamali ni muhimu sana kujua thamani ya kila sekunde unayoitumia. Sasa wengi hawalijui hili, wanapoteza muda hovyo na kujifanya wanatafuta mafanikio. Wajasiriamali waliofanikiwa hawapotezi muda wao kwa mambo yasiyowasadia.
Ni wakati umefika wa kujua kila thamani ya muda wako unaoutumia kuanzia dakika, saa mpaka siku nzima. Usipoteze muda kufanya mambo yanayokurudisha nyuma. Anza sasa kuishi kwa mafanikio, kwa kujifunza mambo ambayo wajasiriamali wenye mafanikio hawapotezi muda kabisa kuyafanya:-
1. Hawapotezi muda kwenye mitandao ya kijamii.
Kuingia kwenye mitandao ya kijamii kama face book, twitter au instagram kuangalia taarifa za hapa na pale ni moja ya sehemu ya maisha yetu ya sasa. Lakini ikiwa utashindwa kutawala muda wako na kujikuta wewe ni mtu wa kuperuzi utapoteza muda mwingi sana ambao ungekusaidia kwa mambo mengine.
Watu wenye mafanikio wana nidhamu kubwa sana juu ya hili, na wakati wote huwa makini na mitandao hii ili isiwapotezee muda. Kama wewe ni mlevi wa mitandao ya kijamii, jiwekee muda wa kuingia huko na kuangalia mambo yako. Usiingie tu kwa kuwa unao muda. Yapo mambo mengi ya kufanya na muda ikiwa pamoja na kujisomea.

2. Hawapotezi muda kufikiria makosa yaliyopita.
Kila mtu anafanya makosa kwenye maisha yake, halikadhalika hata watu wenye mafanikio wanafanya makosa pia. Siri kubwa ya mafanikio ni pale unapokosea jifunze juu ya makosa hayo na ya kusaidie kuweza songa mbele zaidi ya pale ulipokuwa.
Inapotokea unafanya kosa, huhitaji kulia sana zaidi ya kujifunza na kuchukua hatua za kukusaidia kufanikiwa. Hata watu wenye mafanikio katika maisha yao wanapokosea, huwa hawapotezi muda kufikiria makosa yao na kikubwa wanachokifanya ni kuhakikisha wanajifunza na kuendelea mbele.
3. Hawapotezi muda kuanza siku yako bila kuipangilia.
Watu wenye mfanikio wana mipango ya kuwaongoza kufanikiwa kila siku. Ni watu wa kuandika mipango yao ya kesho siku moja kabla. Hivyo, wanapoianza siku wanakuwa wanajua ni wapi wanapotakiwa kuanzia na wapi wanapotakiwa kuishia kwa siku inayofuata.
Kimsingi, hakuna kitu kizuri kama kuianza siku yako kwa kuipangilia kwanza kabla hujaifikia. Ni utaratibu mzuri sana ambao haukupotezei muda na unakufanya uishi kwa ushindi. Watu wenye mafanikio hawapotezi muda kuainza siku yao bila kuipangilia, nawe pia unatakiwa kujifunza juu ya hilo.
4. Hawapotezi muda kufikiria mambo yanayofanywa na wengine.
Watu wenye mafanikio ni mara nyingi hawapotezi muda wao wa thamani kujilinganisha na watu wengine. Kwa kifupi, ni watu ambao hawaangalii sana wengine wanafanya nini ili nao wafanye. Ni watu ambao wana misimamo yao wenyewe na kuamini kile wanachokifanya kwamba kitawasaidia kufanikiwa hata kama ni kidogo.
Hata hivyo kumbuka si vibaya kuangalia au kushindana na yale ambayo wengine wanayafanya. Mtu pekee ambaye unaweza kushindana naye kwa yale unayoyafanya ni wewe mwenyewe. Kila siku unatakiwa kuwa bora zaidi ya jana ili kuyaweka maisha yako katika nafasi nzuri ya kufanikiwa.
5. Hawapotezi muda kuwa na watu hasi.
Kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya mafanikio wanatuambia kwamba, tabia na mienendo yako kwa ujumla inaathiriwa sana na watu wanaokuzunguka. Watu wanaokuzunguka wana athari kubwa sana juu ya maisha yako, haijalishi athari hizo ni chanya au hasi.
Kwa kulijua hilo watu wenye mafanikio, huwa ni watu ambao hawapotezi muda wao kabisa kuwa na watu hasi. Kwa sababu wanajua watu hao watawakatisha tamaa na kuwafanya washindwe kufikia malengo yao waliyojiwekea. Hivyo hicho ni kitu amabacho huwasaidia sana kufanikiwa.
6. Hawapotezi muda kwa mambo wasiyoyaweza kuyatawala.
Katika maisha ya binadamu huwa yapo mambo na matukio ambayo katika hali ya kawaida huwa si rahisi kuyatawala. Matukio haya yanaweza yakawa kama ajali, ugonjwa, kufikiwa au hali mabaya ya uchumi. Haya ni baadhi ya matukio ambayo binadamu huweza kukutana nayo na sio rahisi kwake kuyatawala.
Kwa watu wenye mafanikio, wanapokutana na matukio ya aina hii, kwao huwa si rahisi sana kupoteza muda na kuendelea kuyafikiria. Kitu wanachokifanya yanapowakuta matukio kama hayo ni kuyapokea kama yalivyo, kisha baada ya kuyatatua basi huachana nayo na si kuendelea tena kuyafikiria kila wakati.
Kwa kuhitimisha makala haya, naamini umejifunza kitu kuhusiana na mambo amabayo watu wenye mafanikio ambayo hawapotezi muda wao kuyafikiria sana. Kitu cha kufanya chukua hatua za kuelekea kubadilisha maisha yako.
Tunakutakia kila la kheri katika safari ya maisha yako. Kitu kikubwa ambacho kama DIRA YAMAFANIKIO tunakuomba ni kwamba endelea kuwashirikisha wengine ili waweze kujifunza kama wewe unavyofanya sasa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,

Jun 17, 2016

Jinsi Ya Kutengeneza Tomato Souce.

No comments :
Mara kadhaa nimekuwa nikileta Makala mbalimbali ambazo zinakupa hamasa tu ila Makala ya leo ni pesa mkononi. Pesa mkononi ndiyo ambayo kila mtu anahitaji. Pia nimeamua kukuletea makala haya ili tuendane sawa na Tanzania ya viwanda.

Najua inawezekana kabisa kila mtu kuwa na kiwanda, unashangaa wala usishangae maana huo ndio ukweli maana kila kitu kinapatikana kiurahisi katika mazingira yetu.

Unajua kuwa mikono yako ndiyo itakayokupa pesa? Kama hufahamu basi nimekuja kukujuza ni kivipi utatumia mikono yako ili uweze kuwa tajiri.

Yafuatayo ndiyo mahitaji ya kutengeneza tomato source.

1. Nyanya kilo 1.
2. Vitunguu maji viwili.
3. Vinegar vijiko 3 vya chai.
4. Sukari vijiko 2 vya chai.
5. Chumvi kijiko kimoja cha chai
6. Maji ya moto kikombe kimoja cha chai.
7. Mafuta ya kula vijiko 7 ya vyakula.

Haya ndiyo mahitaji ya kutaka kutengeneza tomato souce, hata hivyo kama unataka kutengeneza zaidi ya hapo unatakiwa kuongeza uwiano wa mahitaji hayo.

JINSI YA KUTENGENEZA TOMATO SOURCE.

HATUA YA KWANZA.

a) Menya nyanya na vitunguu kisha vikate vipande vidogo vidogo.

b) Tumia Brenda kusaga mchanganyiko wako.

c) Anza kuweka malighafi namba 1 hadi namba 4 katika brenda yako kutokana na ratio (uwiano ) uliopewa hapo juu. Saga kwa dakika kadhaa hadi uone imetokea rojo laini.

HATUA YA PILI.

a) Tumia sufuria yenye nafasi kupika mseto huu.

b) Weka sufuria yako jikoni tia mafuta ya kula acha yachemke kisha mwagia mseto wako na kisha uanze kukoroga kwa dakika 30 kuelekea upande mmoja huku ukichemka.

c) Baada ya hapo epua mseto huo utakuwa tayari imeshakuwa tomato funga vizuri na kisha peleka sokoni.

Mpaka kufikia hapo wewe Tajiri, na mafanikio makubwa ambayo yatakuwa upande wako endapo utakuwa umeamua kuondokana na umaskini kwa njia ya kutengeneza vitu mbalimbali kwa ajili ya kuuza.

Nikusihi uendelee kufuatana nami katika Makala zijazo ili tuweze kufika mahali ambapo tunatamani kufika.? Endelea kufuatana nasi hapa dira ya mafanikio kwa masomo mengine yanayokuja.

Imeandikwa na Afisa mipango; Benson Chonya.
Simu; 0757-909942
Barua pepe; 
bensobchonya23@gmail.com