google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 30, 2018

Tabia Za Kiutendaji Zinazowatofautisha Matajiri na Maskini.

No comments :
Leo nitazungumza na wewe kuhusu tabia kuu ambazo huwatofautisha watu waliofanikiwa na wale wasiofanikiwa, hivyo naomba ukae mkao wa kula kwani chakula hiki ni adimu sana pia ni maalum sana kwako wewe msakatonge mwenzangu.
Sababu kubwa ya watu wengi waliofanikiwa na ambao wanaishi ndani ya ndoto zao ni kwamba watu huamini sana kile ambacho wanakifanya. Kuamini kile wanachokifanya ndicho kilichowapelekea watu hao waendelee kuishi ndoto zao kila jua lichomazapo.
Sababu nyingine ambayo inawafanya watu wenye mafanikio waendelee kufanikiwa ni kwamba watu hao mara baada ya kuona changamoto fulani wao walitafuta njia ya kutafuta majibu ya changamoto husika.

Hiyo ni kwa upande waliofanikiwa, ila unapokuja upande huu mwingine ni kwamba  watu wengi wameshindwa kuziishi ndota zao kwasababu, mosi ni kwamba watu hao huwa hawamini kile ambacho wanakifanya.
Hivi hujawahi kukutana na mtu fulani kisha akakwambia nafanya jambo hili kwa kujaribu tu? Bila shaka utawakuta umeshawahi kukutana na watu wengi wenye kauli kama hizi. Ukichunguza kauli kama hizi utagundua bayana ya kwamba ni wazi kabisa watu hawa hata kile wanachokifanya hawakiamini, kwa mtindo huu mafanikio yapo kweli?
Pamoja na kutoamini kile wanachofanya lakini pia watu hawa ni wazuri sana wakutafuta sababu, na sababu hizi ni zile zisizokuwa na msingi yaani watu hawa ni wazuri sana kwa kutafuta visingizio.
Ukimuuliza hivi kwani hujafanya hivi? Mtu huyo atakuja na majibu ya kwa sababu ya.........., majibu ya kwa sababu mara nyingi katika safari ya mafanikio huwa si ya majibu ya msingi bali huwa ni majibu ya kujikatiza tamaa tu.
Hivyo ndugu yangu kama ni kweli unataka mafanikio ya kweli unatakiwa kufahamu ya kwamba  kama kweli  umeamua kufanya jambo fulani wewe fanya ila kama hauhitaji mafanikio basi endelea kutafuta sababu za kutofanya.
Mpaka kufikia nukta hiyo sina la ziada nikutakie siku njema na mafanikio mema.
Ndimi: Afisa Mipango Benson Chonya.

Aug 29, 2018

Faida Tatu Muhimu Za Kuchukua Hatua Kwa Kile Unachotaka Kukifanya.

No comments :
Ili kufikia mafanikio yako, kuwa na mipango mizuri au mikakati iliyobora ni jambo zuri sana ikiwa kama utachukua hatua. Kama usipochukua hatua mipango yako hiyo mizuri haitasaidia kitu itakuwa ni sawa na kazi bure.
Kitu cha msingi kwako ili mipango yako ieleweke ni kwa wewe kuchukua hatua mapema za kukusaidia kuweza kutimiza ndoto zako. Zipo faida za wewe kuchukua hatua kwa kile unachotaka kukifanya, haijalishi umefanikiwa kwa jambo hilo au hapana.
Elewa hivi, mbali na faida kubwa ya kufanikisha lengo husika la kile unachotaka kukifanya, lakini zipo faida nyingine tatu muhimu, ambazo tu wewe utazipata kama utachukua hatua ya kufanya. Faida hizi huwezi kuzipata au kuziona mpaka uchukue hatua.

1. Utawajibika zaidi.
Kile kitendo cha wewe kuchukua hatua tu, kitakufanya wewe kuwa mtu wa kuwajibika zaidi tofauti na ambavyo kama usingeweza kuchukua hatua. Najua hutataka mambo yako yaende hovyo ila utawajibika na kujituma sana ili ufanikiwe.
Hiki ndicho kitu cha kwanza au faida ya kwanza ambayo utaipata endapo utachukua hatua. Utashangaa jinsi unavyopata shauku ya kuendelea kutaka kufanya zaidi na zaidi ukumbuke yote hayo hayaji kwa bahati mbaya ila ni kwa wewe kuchukua hatua.
2. Utajifunza kutokana na makosa.
Hauwezi kujifunza kutokana na makosa kama haujachukua hatua. Kuchukua hatua ni lazima ili ujifunze kutokana na makosa yako yaani ujue ni wapi ulipokosea na ni wapi unatakiwa kupaboresha zaidi na zaidi hadi uweze kufikia lile lengo lako.
Wengi wanaoshindwa kufanikiwa sana hawachukui hatua na ni watu wa kusitasita sana na kwa sababu hiyo inawafanya washindwe kujifunza kutokana na makosa yao. Chukua hatua leo, uone jinsi utakavyojifunza kutokana na makosa yako.
3. Utapata msaada wa ziada.
Kutokana na kile ambacho umeamua kukifanya na umeamua kuchukua hatua, hiyo itakusaidia sana kuweza kupata msaada kwa watu wengine ambao hukutegemea. Msaada huo huwezi kuupata kama umejikalia tu na huchukui hatua.
Kama unafikiri nakutania chukua hatua leo, halafu uone kama utakosa watu wa kukusaidia kwa lile lengo lako. Unakosa watu wa kukusaidia kufanikisha kwenye lengo lako kwa sababu hujachukua hatua. Ukichukua hatua watu hao utawapata.
Hizi ni faida tatu nyingine muhimu ambazo utazipata kama utachukua hatua ya kufanya jambo lile unalotaka kulifanya. Je, hapo ulipo unasubiri nini kuchukua hatua. Chukua hatua za kuwajibika ili utimize ndoto zako mapema.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




Aug 27, 2018

Huu Ndio Ukweli Unaouma Utakaofanya Maisha Yako Yawe Bora.

No comments :
Ni jambo la kawaida kwa watu wengi kuwa na ndoto na malengo, lakini ipo tofauti kubwa sana kati ya watu ambao wanafanikisha malengo yao na wengine wanashindwa kufanikisha malengo yaani hawa wanakuwa wanaota tu pasipo kufikia malengo.
Kwa nini hali hii inakuwa inatokea wengine wanakuwa na uwezo wa kufanikisha malengo yao na wengine wanakwama kufanikisha? Hapa ndipo unatakiwa ujue ukweli mgumu, ukweli unaouma ambao utafanya maisha yako yawe bora.
Je, nikuulize hapo ulipo upo tayari kuupokea ukweli mchungu ambao utabadilisha maisha yako? Kama uko tayari nyosha mkono, nikupe ukweli huu, ila mara baada ya kupokea ukweli huo, utakusaidia sana kukubadilisha maisha yako kwa ujumla.

1. Hatua ya kwanza ni ngumu kutekelezeka.
Inaeleweka siku zote ili kufanikisha jambo lazima kuchukua hatua. Hata hivyo kwa bahati mbaya sana siku zote hatua ya kwanza mara nyingi inakuwa ni ngumu sana kuweza kutekelezeka. Kama usipoweka juhudi na kujituma sana huwezi kuchukua hata hatua ile ya kwanza. Kuna watu wanakuwa wanakwama hata kabla hawajachukua hatua ya kwanza. Fanya ufanyalo, tumia nguvu zote na kuhakikisha unaanza.
2. Wewe ndie sababu ya kujirudisha nyuma sana.
Hakuna mtu mwenye mchango mkubwa sana wa kukurudisha nyuma zaidi yako. Unajirudisha nyuma kutokana na hofu ambazo unazo, unajirudisha nyuma kwa sababu ya kushindwa kuchukua hatua mapema na pia unajirudisha nyuma kwa sababu ya visingizio. Unatakiwa uyaepuke haya yote ili ufanikiwe.
3. Mambo makubwa yanataka muda na juhudi ili kuyafanikisha.
Hakuna jambo kubwa ambalo unaweza ukalifanikisha kwa haraka na upesi kama unavyotaka. Siku zote mambo makubwa yanataka muda na juhudi kubwa sana ili yaweze kutimia. Kama una haraka zako na hutaki kuweka muda katika kutimiza makubwa, utaishia kupata vitu vidogo sana maishani mwako.
4. Sio kila mtu yupo tayari kukusaidia.
Pamoja na kwamba unaweza ukaona unazungukwa na watu wengi wema, lakini nikwambie tu unapopata changamoto si kila mtu yupo tayari kukusaidia kufanikiwa na kufika juu. Wapo wengine watakudidimiza chini na hutaamini, ili usitape tabu weka akilini hii, si kila mtu yupo tayari kukusaidia kama unavyofikiri wewe iko hivyo.
5.  Huwezi kufanikiwa bila kujitoa mhanga.
kama unafikiri utafanikiwa tu kirahisi pasipo kuhatarisha baadhi ya mambo basi utakuwa ni mtu ambaye unajidanganya sana. Lazima ifike muda au wakati uhatarisha baadhi ya vitu kwa ajili ya mafanikio yako. Hatari haziwezi kutoka kabisa ila kama unafikiri mafanikio ya namna hiyo yapo huwezi kuyapata katu maishani.
6. Huwezi kutawala kila kitu.
Ukweli huu unakuja hasa pale unapotaka kutawala tabia na matendo ya watu. Huwezi hata siku moja kutawala tabia na matendo ya watu. Vipo vitu unavyoweza kutawala lakini si kutawala tabia zao na ukazimiliki kwa jinsi wewe unavyotaka iwe. Tawala yale unayoyaweza lakini si kutawala kila kitu utashindwa na hautaweza kufanya hivyo.
7. Huwezi kufanya kila kitu mwenyewe.
Kama ambavyo huwezi kutawala kila kitu wewe, basi huwezi kufanya kila kitu mwenyewe. Yapo majukumu inabidi uwaachie watu wakusaidaie, vinginevyo ukiwa wewe kama wewe yatakushinda. Wale wanaong’ang’ania kufanya mambo yao peke yao wanashindwa kutoka au kuweza kufanikiwa kabisa kwa sababu ni ngumu hiyo.
8. Kukosea ni lazima.
Huwezi ukafanya jambo lolote pasipo kufanya makosa. kukosea ni lazima kutokee kila wakati unapoelekea ndoto zako. Na kunapotokea kukosea kwa namna yoyote usichukie, amua kujifunza kupitia kukosea huko ambako unashindwa na si kuchukia na kuona kila kitu ndio kimeishia hapo na huwezi kufanikiwa tena.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 26, 2018

Jinsi Unavyoweza Kuboresha Maisha Yako Hatua Kwa Hatua Kila Siku.

No comments :
Kuboresha maisha yako kila siku na kwa kidogo kidogo ni jambo la muhimu sana kwako kuliko kuharibu maisha yako kila siku hata kama ni kwa kidogo pia. Kuboresha maisha yako kila siku ni jambo la muhimu sana kulifanya.

Unapoanza kufikiria juu ya kuboresha maisha yako, acha kuwaza juu ya kuchukua hatua kubwa sana itakayoleta matokeo ya ghafla na ya kushangaza  wengi. Unachopaswa kufikiria ni kuleta mabadiliko ya kila siku hata kama ni kidogo.

Kwa mfano, kubadilisha maisha yako kwa asilimia moja kla siku ni kitu ambacho unaweza usikione kina faida, lakini ukifanya mabadiliko hayo kila siku na kwa muda mrefu mabadiliko hayo huanza kuonekana tena kwa uwazi.

Hapo unaona kilicholeta utofauti ni yale mabadiliko kidogo kidogo na maamuzi kidogo sana na ndivyo unabadilisha maisha yako na kuwa ya tofauti na kuwaacha watu wengine wakikushangaa eti ulifanyaje hadi hayo yakatokea.

Kama kuboresha maisha yako kila siku ni jambo la mujimu na ambalo linaweza kukufikisha kwenye kilele cha mafanikio, je, ni kitu gani kifanyike ili uwe na uhakika wa kuweza kuboresha maisha yako hatua kwa hatua na kila siku.


1. Fanyia kazi zaidi mambo yaletayo matokeo chanya.

Usijajidanganye kufanya mambo ambayo hayakupi matokeo mazuri. Yale mambo yanayoleta matokeo mazuri yafanye zaidi. Hata kwenye mpira kikosi kinacholeta matokeo bora hicho ndicho kinachopangwa kila wakati.

Kaa chini na angalia ni mambo gani ambayo yanaleta matokeo mazuri kwako na yafanye mambo hayo kila siku. Nasema hivi, usipoteze muda wako kufanya mambo ambayo hayakupi matokeo chanya, utakwama, kabisa.


2. Epuka kufanya makosa madogo madogo yasiyo ya lazima.

Unaweza usione matokeo yake kwa sasa, lakini makosa madogo madogo yanaathari kubwa sana katika kujenga au kuharibia maisha. Unatakiwa kujua kuepuka kupoteza pesa ndogo ulizonazo, muda kidogo ulionao na kila siku.

Kwa kadri jinsi unavyomudu kuepuka kufanya makosa madogo madogo, ambayo kwa dhahiri hayawezi kukupa matokeo chanya, ndivyo unajikuta upo kwenye wakati sahihi wa kufanikiwa. Makosa madogo au ‘tinny losses’ ni lazima kuyaepuka.


Kwa kuepuka kufanya mambo yasiyo leta matokeo na pia kuepuka kufanya makosa madogo madogo kila siku utajikuta unaboresha maisha yako na mwisho wa siku utajikuta unatengeneza maisha yako na kuwa bora zaidi na zaidi.

Kikubwa ambacho unatakiwa kukumbuka hapa, ni kuamua kuvaa jukumu la kuboresha maisha yako kila siku. Ukiamua kuboresha maisha yako na kwa kila siku uwe na uhakika utafanikiwa hata kama mabadiliko hayo hayaonekani leo, kesho yataonekana.

Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,





Aug 25, 2018

Mambo Matano (5) Muhimu Yatakayokusaidia Kufikia Kilele Cha mafanikio Yako

No comments :
Siri kubwa iliyopo katika kuyafikia mafanikio yako ipo katika kuzifahamu mbinu zitakazokusaidia kuweza kuyafikia mafanikio hayo. Wengi tumebweteka kimwili na kiakili huku tukizani labda mafanikio chanzo chake huwa  ni bahati nasibu, uchawi na mengineyo mengi yasiyokuwa na ukweli wowote ndani yake.
Hata hivyo ukweli ni kwamba yapo mambo muhimu ambayo yatakusaidia kuweza kufikia kilele cha mafanikio, na mambo hayo ni:
1. Chukua hatua kila siku.
Mafanikio ni mchakato usiokuwa na mwisho, hivyo basi kwa kila kitu ambacho unadhani kinakupa mwanga wa kuelekea kwenye kutimiza malengo yako ni vyema ukachukua hatua za utekelezaji wa jambo hilo.
Watu wengi sana ni wazuri sana wa kuwaza mambo mengi sana ya msingi ila linapokuja sula la kuchukua hatua wamekuwa ni watu wavivu sana wakuweza kufanya hivyo na matokeo yake watu hayo wamekuwa wakijitengenenezea ukata wao wenyewe. Hivyo kila wakati jifunze kuchua hatua sahihi kwa kile unachokifanya au unachotaka kufanya.

2. Jifunze kuweka viupambele.
Kazi yeyote  inayofanywwa isiyokuwa na vipaumbele ni uchafua, kama ulivyo uchafu mwingine, unashangaa wala usishangae huo ndio ukweli.
Watu wengi wanashindwa kutuliza kiu ya umaskini hii ni kwa sababu watu hao wameshindwa kutambua ni kwa namna gani wanaweza kupanga viupembele kwa vile vitu wanavovifanya.
Kupanga vipaumbele humsaidia mtu husukia kufahamu na kutambua ni kazi gani ianze kufanyika na ipi ifuate. Hivyo kama kweli umeuchoka umaskini jifunze kupanga vipaumbele kwa vitu unavyofanya kwa kuangalia nini kianze kufanyika, lini na kwa wakati gani.
3. Jifunze kuyaweka malengo yako katika nyakati.
Malengo uliyonayo ni lazima uyaweke katika nyakati kabla hujaanza kufanya, na nyakati hizi ni lazima uwe ni wakati uliopo na wakati ujao.
Jambo hili linahitaji maamuzi magumu, yaani amua kwamba jambo hili ni lazima nitafanya wakati huu au aumua jambo hili ni lazima nitalifanya muda fulani. Katika kipengele hiki ugopa sana tabia ya kugharisha kufanya kwani ndiyo inayoendelea kukuua taratibu bila wewe kujua.
4. Andika kila kitu ulichokifanya au unachotaka kufanya.
Kuandika mambo yako uliyoyafanya au unayotaka kufanya humpa mtu hamasa za kiutendaji kwani mara kwa mara anakuwa anakumbuka ni kitu natakiwa kufanya na kwa wakati gani? .
Ogopa kufanya mambo ya msingi kwa kukurupuka kwani hii ndiyo ambayo husababisha watu wengi kutokufanya maumizi sahihi. Hivyo kila nyakati jifunze kuweka kila kitu  katika maandishi ili uweze kujijengea fikra thabiti.
5. Fahamua kile unachokitaka.
Maisha sio bahati nasibu bali maisha ni vile unavyotaka kuwa na muamuzi wa mwisho ni wewe, hivyo kaa chini na tafakari kwa makini ni nini hasa unachokitaka kisha uanze kuchua hatua stahiki juu ya jambo hilo.
Lakini pia ikumbukwe kufahamu kile unachokitaka pasipo kuchukua hatua za kiundeji ni sawasawa na bure, hivyo amua sasa kubadilika kwa kuchukua hatua za kiutendaji kwa kile unachokifanya.
Mwisho naomba nihitimishe kwa kusema ya kwamba endapo ukiyazingatia hayo yote niliyokwisha yaeleza jiandae kuishi maisha yenye tija katika hii dunia.
Ndimi Afisa Mipango Benson Chonya

Aug 24, 2018

Hii Ndiyo Kanuni Ya Mafanikio Iliyosahaulika Na Wengi.

No comments :
Mafanikio hayatengenezwi na kanuni moja tu, bali ni mjumuiko wa kanuni za kimafanikio tofauti tofauti na hizi ndizo ziletazo mafanikio. Zipo kanuni za wazi kabisa za kimafanikio ambazo zinafahamika na wengi na zipo ambazo hazifahamiki.
Kwa mfano, kufanya kazi kwa bidii, kuwa na nidhamu, kutengeneza nguvu ya uzingativu, naweza kusema ni moja ya kanuni za mafanikio au misingi ya mafanikio ambayo inaeleweka na wengi kwamba ukiifata lazima ufanikiwe.
Hata hivyo inabidi ieleweke hivi, zipo kanuni nyingi za kimafanikio ambazo unatakiwa uzifanyie kazi sana ili ufanikiwe, na kwa bahati mbaya zipo ambazo huzijui au umezisahau kwa kutokujua lakini zipo na zinafanya kazi kwa matokeo makubwa.
Na mojawapo ya kanuni rahisi ya mafanikio ambayo wengi hawaijui au wameisahau, ni kanuni ya kuwa na shukrani. Inaeleweka kwamba kwa mtu yeyote ambaye ana shukrani, na huku akawa ni mtu wa kuchukua hatua kufanikiwa ni lazima kwake.
Sasa linakuja tatizo la watu wengi ni wabinafsi na hawana shukrani, kama unafikiri natania nianze na wewe, je, wewe ni mtu wa shukrani, je, wewe ni mtu wa kukumbuka kule ulikotoka na kushukuru hapo ulipo na kwa maisha uliyonayo.
Mara nyingi utakuta watu wengi hawana shukrani sana, si watu wa kukumbuka watu wale waliowasaidia na wapi, hata kama ni kwa kidogo na matokeo yake wanajikuta ni watu ambao wanaiweka kanuni hii pembeni na mwisho wake hushindwa kufanikiwa sana.
Kama nia yako ni mafanikio makubwa kweli, pia unatakiwa kuchukua shukrani kama mojawapo ya kanuni ya kimafanikio. Kila wakati unapochukua hatua za kiutendaji, lakini  hakikisha shukrani iwe karibu na kinywa chako kwa chochote kitakachotokea.
Kuna watu wana midomo kama ya ‘laana’ wanapochukua hatua, kwa mfano kufanya biashara ya aina fulani halafu wakapata hasara, midomo yao inakuwa inaongea mengi sana na kulalamika, sasa hii sio nzuri na haikusadii, shukuru kwa chochote.
Unaweza ukawa upo kwenye wakati mgumu shukuru kuna kitu cha kujifunza, unaweza ukawa umepata hasara kweli shukuru, hii ni kanuni ya kimafanikio na ambayo pia ni kanuni ya kiroho, pasipo kushukuru mambo yako hayawezi kwenda sawa saana.
Inawezekana sasa unajiuliza nashukuru kwa mambo yapi, hilo lisikupe tabu. Yapo mengi sana ambayo unaweza ukaanza kuwa na shukrani nayo lakini kwa kuanza tu, unaweza ukaanza na kushukuru kwa mambo haya na yatakusaidia sana kufanikiwa.

1. Shukuru kwa uhai ulionao.
Kwa sababu ile tu unaishi, kwa sababu ile tu umepewa uwezo wa kuishi unatakiwa kushukuru sana kwa hilo kwanza. Amka asubuhi na sali kwa kwa sababu umepewa uwezo wa kuishi na muumba wako na hicho ni kitu kizuri sana.
Kitendo cha kushukuru kwa uhai ulionao kitakupa nguvu hata ya kutenda mambo mengine makubwa maishani mwako ambayo moja kwa moja yatakusaidia kuweza wewe kufanikiwa kwenye maisha yako moja kwa moja.
2. Shukuru kwa afya yako.
Tofauti na kushukuru juu ya uhai ulionao, huna budi kushukuru kwa sababu ya afya uliyonayo. Sote tunajua afya ni msingi mkubwa sana wa mafanikio yako, hiyo ikiwa na maana kama huna afya ujue kabisa na mafanikio huna.
Shukuru kwa afya uliyonayo, kama kuna sehemu unaona unaumwa shukuru pia kwa sehemu zingine za mwili ambazo huumwi. Kwa kushukuru huku uponyaji una uwezo wa kusambaa na sehemu zingine za mwili kwa njia ambayo hata wewe huijui.
3. Shukuru kwa fursa zilizopo.
Tunaishi katika dunia kwa sasa ambayo fursa zipo nyingi sana. Nakwambia hivi ni kwa sababu tunaishi katika dunia ya habari. Kama  upo hapo na huoni fursa basi ujue kuna shida sehemu kwako au ‘umepigwa upofu’, macho yako hayaoni.
Shukuru kwa sababu ya fursa zilizopo, ukishindwa kuchukua hatua fursa hii basi elewa ipo fursa nyingine kule, kikubwa ni kutuliza sana akili yako na kutumia fursa hizo za kimafanikio ziweze kukusaidia wewe na wengine wanaokuzunguka.
4. Shukuru kwa watu wanaokuzunguka.
Unalazimika kuwa na shukrani kwa watu wanaokuzunguka, watu hawa wanaweza kuwa ni ndugu, rafiki zako au jamaa zako lakini watu hawa wanamchango mkubwa wa kubadili maisha yako na inabidi uwatumie vizuri kukusaidia katika hilo.
Kama huna shukrani na watu wanaokuzunguka basi utakuwa unakosea na unajiweka katika wakati mbaya wa kutokuendelea kufanikiwa. Haujaja duniani wewe kama wewe,unaishi na kuzungukwa na watu, basi kuwa na shukrani na watu hao.
5. Shukuru kwa wakati mgumu.
Ni vyema pia ukawa na shukrani hata katika kipindi kigumu cha maisha yako. Kipindi kigumu cha maisha yako ni mwalimu mzuri wa kukufundisha na kukupa uzoefu wa wewe kukusaidia wewe kuweza kufanikiwa.
Unaweza ukawa hupendi sana nyakati hizi ngumu lakini kumbuka kipindi kigumu, hicho ndicho kinachokukomaza wewe na kukusaidia kuweza kufanikiwa. Unatakiwa uelewe nyakati ngumu hazipo kukuangusha bali kukusaidaia wewe kusimama kimafanikio.
Haya ndio mambo ya msingi unatakiwa uanze kuwa na shukrani nayo ili kanuni ya shukrani ifanye kazi kwako vizuri. Hata maandiko matakatifu yameandika juu ya shukrani. Wale walioshukuru walipokea muujiza zaidi maishani mwao.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,



Aug 23, 2018

Mambo Ambayo Umekuwa Ukidanganywa Sana Kuhusu Pesa Na Uwekezaji.

No comments :
Kati ya kitu ambacho kinatafutwa sana na wengi hapa duniani ni pesa. Pesa imekuwa ikitafutwa usiku na mchana karibu na watu wote. Hali hii imekuwa iko hivyo kwa sababu ya umuhimu wa pesa katika kutusaidia kufikia malengo yetu.
Lakini pamoja na pesa kutafutwa hivyo, bado watu wengi wamekuwa wana hadithi nyingi za uongo kuhusiana na pesa hata swala la uwekezaji kwa ujumla.  Kila inapotajwa pesa au uwekezaji wakati mwingine kumekuwa na uongo mwingi sana wa kupotosha.
Ni lengo la makala haya kukuwezesha kutambua mambo ambayo umekuwa ukidanganywa juu ya pesa na uwekezaji. Mambo hayo ni yepi? Fuatana nami katika makala haya mwanzo hadi mwisho tuweze kujifunza kwa pamoja:-
1. “Unahitaji pesa nyingi ili kuwekeza”.
Wengi wetu bado tunaendelea na fikra mgando za kuamini kwamba ili uweze kuwekeza ni lazima uwe na pesa nyingi. Kutokana na uongo huo, tumekuwa tukisubiri tupate mitaji na pesa nyingi ili tuweze kuwekeza.
Kwa taarifa yako huo ni uongo ambao umekuwa ukidanganywa. Kwa dunia ya sasa jinsi ilivyo, kitu kikubwa unachohitaji ni wazo na taarifa sahihi za mafanikio ili kuwekeza. Kama ni mtaji unahitajika sio lazima uwe mkubwa sana kama unavyofikiri.

Kwa hiyo kama umesimama na huwekezi kwa kisingizio cha kukosa mtaji, unajichelewesha mwenyewe. Zinduka kwenye huo usingizi na anza kutumia kidogo ulichonacho kufanya uwekezaji unao faa kwako. Naamini kipo kitu ulichonacho hata kidogo cha kukusaidia, hauwezi kukosa vyote.
2. “Uwekezaji ni hatari”
Jambo la pili ambalo wengi wamekuwa wakidanganywa sana kuhusu pesa na uwekezaji kwa ujumla ni kwamba, uwekezaji ni ‘risk’ kubwa sana. Nafikiri umeshawahi kusikia hadithi za namna hii sana kuwa uwekezaji ni hatari.
Kutokana na wengi kupokea hadithi za namna hii na kuzikubali kupelekea kutokufanya uwekaji wowote ule. Unajua ni kwa nini? Kwa sababu wameshaambiwa uwekezaji ni hatari na ni ‘ risk’ kubwa sana.
Huu ni uongo ambao umekuwa ukidanganywa kwa muda mrefu. Na kwa bahati mbaya umekuwa ukijisahau pia kwamba uwekezaji sio hatari kubwa sana kama unavyofikiri, ila unachangamoto zake na ni njia mojawapo nzuri ya kukufikisha kwenye uhuru wa kipesa.
3. “Mshahara ndio kila kitu”
Acha kuendelea kuugua na kuamini hadithi za kwamba wale wanaolipwa mshahara ndio kila kitu. Kama hicho ndio kilio chako na unaamini tosha kabisa kwamba eti kwa sababu wewe hukusoma na hulipwi mshahara basi maisha yako yameharibika.
Sikiliza nikwambie rafiki, maisha ni mipango. Jiwekee taratibu zako za kutengeneza kipato na jiamini zaidi, utafanikiwa. Kama unafanya kazi acha kuwadanganya wengine kwamba ukiwa na mashahara ndio uhakika wa mafanikio.
Mafanikio ya kweli hayaji kwa sababu ya mshahara unaolipwa. Mafanikio makubwa na ya uhakika yanakuja kutokana na mipango yako imara uliyojiwekea na kuifata kila siku.
Ukiangalia na kufuatilia hizo ndizo hadithi ambazo una danganywa sana kuhusu pesa na uwekezaji. Mengi yamekuwa yakisemwa sana kuhusu pesa na wekezaji kitu ambacho sio kweli.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Napenda pia kuchukua fursa hii kukukaribisha kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja na kwa ukaribu zaidi. Kujiunga tuma neno MAFANIKIO YANGU, kisha ikifutia na namba yako kwenda 0713 04 80 35 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,

Aug 22, 2018

Jambo Hili Ni Muhimu Sana Katika Ukuaji Wa Biashara Unayoifanya.

No comments :
Katika biashara yeyote ile unayoifanya ni lazima uweze kujifunza mbinu maridhawa zitakazokufanya uweze kukua katika biashara hiyo, hii ni kwa sababu moja kati ya changamoto kubwa ambayo inawakumba wafanyabiashara wengi kutofanya vizuri katika biashara wanazozifanya ni kwamba wanashindwa kujifunza mbinu mpya za kibiashara zitakazowasaidia wao kuweza kukua katika biashara husika.

Kama na wewe ni miongoni mwa  watu watu ambao wanakumbwa na sakata hilo basi nakuomba  usipepese macho mahala pengine bali endelea kusoma makala haya kwani leo nimekusogezea makala muhimu sana kwako itakayokufanya wewe uendeleee kufanya vizuri katika biashara ambayo unaifanya.

Tunafahamu fika ulimwengu wa sasa ni ulimwengu wa biashara hivyo bila kujiongeza katika biashara tunayoifanya tutashindwa kufikia malengo yetu ya kibiashara, hivyo ndugu yangu kwenye biashara yeyote ile ili uweze kufanikiwa ni lazima ujifunze kujitengenenezea soko lako maalamu.


 Soko maalumu, hii ni kanuni muhimu sana katika biashara kwani ndiyo utambulisho wa biashara unayoifanya, huenda ukawa bado hujanielewa ipo hivi unapofanya biashara ni lazima uweze kutengeneza alama, na alama hizi ziwakae wateja wako akili mwao.

Pia ninapozungumzia alama nina maana ubobezi katika eneo fulani, yaani kwa mfano  mtu akisikiaa neon  “kwa Beny fashion” basi ajue moja kwa moja huyu anahusika na  nini. Kama wewe ni muuzaji wa viatu vya dukani basi hata jina lako likitamkwa mbele ya masikio ya watu basi watu hao wajue fika wewe ni muuzaji wa viatu.

Kufanya hivi ndiyo kitendo ambacho huitwa kutengeneza soko lako maalum. Pia kitendo hiki kinapochukuliwa hatua stahiki ndicho kinawafanya wafanyabiashara wengi waliofanikiwa waendelee kuyakumbatia mafanikio ya biashara zao.

Hivyo mpenzi msomaji wetu  kila wakati ni lazima uweze kujifunza kutengeneza soko lako maalumu katika kila eneo unalolifanyia kazi, ni lazima wateja wako watambue kuwa wewe ni mbobezi zaidi katika eneo gani? Kitendo hiki kitawafanya wateja wako wasambaziane taarifa kwa haraka sana kwa kile unachokifanya.

Lakini pia ni lazima ikumbukwe ya kwamba neno mafanikio sio uchawi kama wengi wazaniavyo, bali ni matokeo ya vitu vidogovidogo ambavyo wengi huvipuuza. Hivyo kuanzia sasa jifunze kuchua hatua kwa vitu vidogo vidogo ambayo unaona fika havina mchango wowote wa kufanikiwa kwako, kwani vitu hivyo ndivyo vitavyokupa mafanikio unayoyataraji.

Hivyo kila wakati ni vyema ukajifunza kujitengenezea soko lako maalum ili uweze kufanikiwa katika biashara.

Ndimi; Afisa Mipango: Benson Chonya

Aug 21, 2018

Huu Ndio Uongo Unaokuzuia Ushindwe Kuchukua Hatua.

No comments :
Uwe unajua au hujui unatakiwa kujua kuna wakati upo uongo unaojijaza mwenyewe na kwa bahati mbaya sana uongo huo  ndio unaokuzuia ushindwe kuchukua hatua za kuelekea kwenye mafanikio yako uliojipangia kuyafikia
Inawezekana unajiuliza inawezekanaje na kivipi mtu ukajijaza mwenyewe uongo, ndio inawezekana kabisa kwamba ukajidanganya mwenyewe na ukajipoteza kutokana na mawazo ambayo unajisemea mwenyewe kila wakati.
Hapa kupitia makala haya nataka nikuonyeshe uongo ambao unajiambia wewe mwenye na kwa uongo huo unakuzui wewe kuweza kuchukua hatua za kufikia mafanikio yako. Je, uongo huo ni upi unaojiambia?

1.”Siko tayari kufanya jambo hili kwa sasa.”
Kuna watu ambao wanajidanganya katika hili nakuona kile wanachotakiwa kukifanya kwa sasa hawako tayari, nikiwa na maana watu hawa wanakuwa wanadai maandali mengine zaidi bado yanahitajika ili waweze kuchukua hatua.
Matokeo yake watu hawa huendelea kujiandaa wee na mwisho hushindwa kuchukua hatua kabisa. Sasa huu ni uongo ambao wengi wanajidanganya, wakati unatakiwa kuchukua hatua hata kama unajiona hauko tayari lakini wewe chukua hatua.
2. “Natafuta wazo bora zaidi.”
Moja ya kizuizi kinachowazuia watu wengi kushindwa angalau kuchukua hatua ya kwanza tu kwa kile wanachokifanya ni kutokana na wao kuendelea kutafuta wazo bora zaidi la kibiashara badala ya kulifanyia kazi lile walilonalo.
Utakuta mtu ana mawazo mazuri tu ya kibiashara lakini unaona mtu huyo anaendelea kutafuta wazo lingine bora na kuacha kutumia hata lile wazo walilonalo. Huo ni uongo mwingine wa kuamini lipo wazo bora zaidi la kufanyia kazi.
3. “Nimeshachelewa kwenye mradi huu.”
Kati ya mojawapo ya wazo linalopoteza wengi ni kule kwa wengine kuamini mradi wanaoufanya tayari wameshachelewa wakiwa na maana kwamba mradi huo tayari unafanywa na watu wengi na jambo ambalo si sahihi.
Kuendelea kuwa na mawazo haya ni kujidanganya tu, hakuna kitu ambacho umechelewa wewe kufanya kwa sehemu yako na weka juhudi vya kutosha na kuhakikisha hadi unaweza kufanikiwa vya kutosha.
Kwa kumaliza makala haya, tambua huo ndio uongo ambao wengi wanajidanganya na unawafanya washindwe kuchukua hatua za kufikia mafanikio yao.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 20, 2018

Yajue Mambo Ya Muhimu Katika kurahisisha Safari Ya mafanikio Yako.

No comments :
Shughuli zote zifanywazo na mwanadamu katika sayari hii ya dunia, kila mmoja baada ya kufanya shughuri hilyo ni lazima mtu huyo anategemea kupata pesa, unashangaa wala usishangae huo ndio ukweli halisi. Na miongoni mwa siri ambayo hujawahi kuijua kuhusu mafanikio ni kwamba kwa kila kitu ambacho unakifanya ni lazima uwaze kwa kina kitu hicho kinakuing’iziaje pesa?
Hii ni kwa sababu wapo baadhi ya watu hufanya vitu visivyo vya msingi hii ikiwa ni kigezo cha  kuiburudisha  nafsi basi jiandae kupata tabu sana. Nimesema hivyo kwa sababu mambo yamebadilika sana hivyo habari za kuufariji moyo katika jambo unalolifanya pasipo kuingiza kitu chochote katika maisha yako kunajipoteza mwenyewe.

Lakini pia unatakiwa kufahamu ya kwamba Maisha yako ni mjuimuko wa mambo madogo madogo ambayo wewe kama dereva unapaswa kuyafahamu vyema mambo hayo ili kuhakikisha maisha yako yaweze kusonga mbele kimafanikio, au kwa maneno mengine siku zote ni lazima ufahamu ya kwamba hatma ya maisha yako unayo wewe na si mtu mwingine.
Pia ikumbukwe ya kwamba unavyoonekana hivi leo ni matokeo ya kwako mwenyewe ndiye uliyeamua kuwa hivyo ulivyo, usiruhusu nafsi pamoja na kinywa chako kumlam mtu mwingine kukusababishia ugumu wa maisha, kwani nimeshasema hapo awali ya kwamba wewe ndio dereva halisi wa maisha yako na si vinginevyo.
Wewe ndiye mwenye maamuzi sahihi ya kufanya jambo fulani au usifanye. Mara nyingi watu wengi sana wanashindwa kukidhi matakwa ya maisha yao kwa sababu wameruhusu watu wengine ndio wawe waamuzi wa kile wanachokifanya na kitendo hiki ndicho kinachowapeleea watu hawa wazidi kulalama maisha ni magumu, na kitendo hiki ndicho kinachotupoteza wengi.
Vile vile watu wengi wanashindwa kufanikiwa kwa sababu wao pia wameshindwa kufanikiwa katika maisha yao hii ni kwa sababu wameshindwa pia hata kuchagua hata marafiki sahihi wanaopaswa kuongozana nao katika maisha yao.
Ni ninii kinatakiwa kufanyika ili kuishi maisha yenye tija katika safari hii ya dunia katika kuyasaka mafanikio?
Mosi,  unachopaswa kukizingatia katika dunia hii ili uweze kuishi maisha ya mafanikio ni kuhakikisha unakuwa ni mtu mwenye maamuzi  yako sahihi ambayo yatakufanya uweze kutimiza kusudio lako hapa duniani ili mradi usivunje sheria za nchi na sheria za Mwenyezi Mungu.
Jambo la pili, kwa kila jambo unalolifanya ni vyema ukawa ni mtu wa kujiuliza hivi jambo hili lina manufaa yeyote yale kwangu? Na je napateje pesa kupitia jambo hili?
Jambo la tatu na la mwisho, ni vyema ukajifunza kuchagua marafiki sahihi wataokusaidia kupiga hatua za kimafanikio za kule ambako unataka kuelekea na si vinginevyo.
Kwa leo sina mengi, naomba niishie hapo nikutakie siku njema na mafanikio mema.
Ndimi Afisa Mipango; Benson Chonya