google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 30, 2016

Mabadiliko Katika Maisha Yako Hayasubiri Kitu Hiki...

No comments :
Upo uwezekano mkubwa sana kwa wewe kuamini kwamba kila mwaka unaanza utakuwa ni bora zaidi kuliko mwaka uliopita.
Upo uwezekano wa wewe kuamini sana kwamba kesho yako itakuwa ni bora sana kuliko ilivyo leo.
Pia upo uwezekano wa wewe kutokuchukua hatua  ndogo ndogo katika maisha yako na kusubiri kuchukua hatua hizo katika mwaka unaokuja.
Mipango na matumaini unayojipa naweza kusema ipo sawa kwa kiasi fulani, lakini tena wakati huo naweza nikakwambia haiko sawa kabisa. Ki vipi?
Badala ya kujipa matumaini nitafanya hili mwaka kesho au siku fulani na kuamua kutulia, hebu amua kuchukua hatua leo hii za kufanya kitu, hata kama ni kidogo.

Acha kusubiri mwaka mpya uanze, fanya mabadiliko ya maisha yako sasa.
Acha kusubiri hadi mwisho wa mwaka ndio uanze kutafakari kipi cha kuboresha na kipi sio cha kuboresha katika maisha yako. Jenga utaratibu wa kujikagua karibu kila siku na kuboresha maisha yako.
Tatizo kubwa ulilnalo unajipa muda sana wa kuahirisha mambo mengi ikiwa pamoja na mipango yako. Maisha tuliyonayo hayatusubiri hata kidogo. Kipo kitu ambacho unatakiwa kufanya kila siku ili  kufanya mabadiliko na kuboresha maisha yako.
Inawezekana ili kufanya mabadiliko ya maisha yako kuna maarifa unatakiwa uyapate. Pia inawezekana ili kufanya mabadiliko ya maisha yako kuna watu unatakiwa kushirikiana nao vizuri ili wa kusaidie kufikia ndoto zako.
Sasa kama iko hivyo ni kwa nini uendelee kusubiri hadi mwaka ujao?
Chukua muda mchache kila siku asubuhi kujiuliza ni kipi ambacho utakwenda kufanya ili kuboresha maisha yako?

Chagua jambo moja dogo tu la kufanya litakalokusaidia kuboresha maisha yako. Nimesema jambo moja tu, usichague mambo mawili au matatu, nimesema chagua jambo moja tu, ambalo unaamini litakuletea mabadiliko.
Hiyo yote inaonyesha mabadiliko ya maisha yako unaweza ukayaanza sasa na si kesho au wakati mwingine unaona ni bora zaidi kwako.
Mabadiliko katika maisha yako hayasubiri mwaka mpya uanze, mabadiliko yako hayasubiri kesho, unatakiwa kufanya mabadiliko sasa, kwani huu ndio wakati bora sana kwako.
Katika maisha, hakuna mtu ambaye ni rafiki wa kesho. Huwezi kujua kesho hiyo unayoisubiri ni nini kitatokea. Anza kufanya mabadiliko ya maisha yako sasa na si kesho au siku nyingine.
Ukichukua hatua hiyo utayapa maisha yako nguvu sana ya kusonga mbele kuliko ambavyo ungesubiri. Chukua hatua sasa. Ni muda wa kufanya mabadiliko makubwa kwenye maisha yako.
Tafakari juu ya hilo, chukua hatua na endelea kubadili maisha yako kwa kupata maarifa sahihi kupitia mtandao wako wa DIRA YA MAFANIKIO kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,

Dec 29, 2016

Hata Kama Huna Pesa, Ukiwa Na Kitu Hiki Kitakufanikisha.

No comments :
Inawezekana umekata tamaa kwa sababu unajiona mipango yako inaenda hovyo, huna pesa na hivyo unajiona huwezi kufanya kitu cha kukusaidia tena kufanikiwa kwa sababu ya hali hiyo uliyonayo.
Pengine usichokijua, kipo kitu kimoja ambacho huwa kinatoa mwelekeo na dalili ya mafanikio hata kama wakati huo huna pesa. Unapokuwa na kitu hicho ni rahisi kupiga hatua za kimafanikio. Kitu hiki si kingine bali ni matumaini.
Unapokuwa unaishi kwa matumaini ya kutambua kwamba utafanikiwa huku lakini ukichukua hatua karibu kila siku, ni rahisi kuweza kubadilika katika maisha yako na kuwa mtu wa mafanikio.
Inapotokea umeshindwa lakini ukawa una tumaini la kufanikiwa, hiyo itakupa nguvu tena ya kujaribu kitu kipya katika safari yako ya mafanikio uliyonayo.
Matumaini yanakupa nguvu ya kufanya zaidi na zaidi hata kama unachokifanya unaona kama hakilipi kwa sasa, kwa sababu una matumaini ya kufanikiwa, ni lazima utafanya hata kama upo kwenye hali ya mbaya kimafanikio.

Unaweza ukawa una maumivu makubwa ya kushindwa kwa kile unachokifanya na pengine umekata tamaa kabisa, lakini matumaini yatakuamsha na kusema fanya tena.
Lakini hata hivyo, ili uweze kuwa tumaini sahihi la mafanikio yako mara nyingi tumaini  haliji hivihivi, ipo gharama ambayo unatakiwa kuilipia ili kupata tumaini sahihi la kufanikiwa kwako.
Huwezi kukaa tu, halafu ukategemea upate tumaini au kitu cha kukupa faraja ni lazima ufanye kitu cha tofauti kila siku. Ni lazima uchukue hatua ya pale ulipo na kutaka kwenda sehemu nyingine.
Ikiwa utakuwa ni mtu wa kukaa tu na bila kuchukua hatua, elewa kabisa utahangaika sana na utakuwa mtu wa kukosa tumaini karibu kila siku ya maisha yako na kuiona dunia haifai.
Hakuna kisingizio chochote katika hili, tumaini la mafanikio yako ni matokeo ya wewe kuwajibika kwako kila siku. Ikiwa huwajibiki sahau kuwa na matumaini, utakuwa ni mtu wa kukatishwa tamaa kila siku.
Watafute watu ambao ni wakata tamaa maarufu, uangalie maisha yao yalivyo, utagundua ni watu ambao mara nyingi hawachukui hatua sahihi za kuweza kubadili maisha yao.
Kitu unachotakiwa kufanya ni kujenga tumaini jipya la mafanikio yako, kufanya kitu hata kama ni kidogo ambacho lakini unaamini kitabadilisha maisha yako.
Kwa kuishi maisha hayo hiyo itakusaidia sana kujitengenezea matumaini makubwa kwa maisha yako na utapata hamasa ya kufanya mambo mengi yakuweza kubadili maisha yako.
Kitu cha kukumbuka tumaini lolote lile linajengwa kwa wewe kuchukua hatua ya kufanya kitu fulani ambacho unaamini ni msaada kwako, vinginevyo itakuwa ni ngumu sana kufanikiwa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,


Dec 26, 2016

Je, Unashindwa Kufanikiwa Kwa Sababu Ya Changamoto? Fanya Hivi…

No comments :
Ni hali ambayo hutokea kwa wengi unapokutana na changamoto au tatizo fulani kuona kwamba kila kitu ni kibaya katika maisha, ingawa ukweli hauko hivyo.
Kwa sababu ya tatizo linalokakubali ni rahisi kuona ndugu, rafiki, jamaa zako wote wa karibu ni wabaya kwa sababu huoni ule msaada wao wa moja kwa moja kukusaidia.
Usichokijua yote hayo yanapotokea si uhalisia wa maisha jinsi ulivyo. Hakuna mtu mbaya sana katika maisha yako hata mmoja. Si dunia wala ndugu zako ndio wabaya sana, vitu vyote hivyo viko sawa.
Mbaya wa kwanza katika hayo yote unayoyaona ni wewe mwenyewe, inawezekana hukusaidiwa kwa sababu ni kweli watu hao hawakuwa na uwezo. Sasa kwa nini ulalamike.
Kama hali au tatizo uliloingia limesababishwa na mwingine kwa namna moja au nyingine, jiulize wewe unamchango gani wa kusababisha hali hiyo kutokea? Kwa sababu ni lazima uwe na mchango wa aina fulani.

Hivyo unapoona una changamoto, ama tatizo fulani badala ya kulalalimikia wengine au kuumia  chukua hatua muhimu ya kuweza kutatua tatizo hilo mpaka uweze kulishinda.
Kujijengea tabia ya kuwa na lawama sana hakuwezi kukusaidia kitu hata siku moja. Unajiona una tatizo au changamoto likabili kwa nguvu zote bil kutafuta ‘mchawi’ wa tatizo lako.
Fanya kitu juu ya changamoto yako. Hakuna wa kukusaidia usipokubali kufanya kitu cha kuweza kukutoa kwenye changamoto ambayo inaweza ikawa inakukabili.
Unaweza ukawa ni kweli hujisikii vizuri, unajisikia vibaya sana kiasi cha kwamba unashindwa kuchukua hatua, lakini hebu fanya kitu ambacho kitakusaidia kutatua changamoto yako hata kwa sehemu kidogo.
Acha kuruhusu kusimama kimaisha kwa sababu ya changamoto zinazokuzunguka.
Acha kuwa chanzo cha kujiangusha mwenyewe kwa sababu ya changamoto za kimaisha.
Fanya kitu muhimu cha kukusaidia kuweza kusogea mbele kimafanikio hata ukiwa katikati cha matatizo au changamoto zinazokuzunguka.
Kutokufanya kitu, lisiwe moja ya suluhisho ambalo unaweza ukawa umechangua.
Kumbuka unao uwezo wa kubadilisha maisha yako ukiamua, changamoto zisiwe kizuizi kikubwa sana cha kukufanya ushindwe kufanikiwa.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,
dirayamafanikio@gmail.com
dirayamafanikio.blogspot.com  

Dec 20, 2016

Hiki Ndicho Kinachoitwa Kichaa Cha Mapenzi.

No comments :
Kabla mtu hajaoa au kuolewa , huamini kabisa kwamba, kabla hajafanya mapenzi au tendo la ndoa na mtu anayemwita mpenzi wake, bado hawezi kudai kwamba, huyo mtu ni mpenzi wake na kwajibika kwake kama mpenzi.
Vijana wengi huamini kwamba, baada ya kukutana kimwili, ndipo wanaweza kudai kwamba, hao ni wapenzi wao na kwamba kukutana kimwili, ndiyo mapenzi au kupenda kwenyewe.
Inapotokea wanapokutana huvutiwa na tendo la ndoa, huamini kabisa kwamba, uhusiano nao utakuwa mzuri. Kwao, tendo la ndoa ndio kipimo cha uimara wa uhusiano wao.
Baada ya kufanya mapenzi, wapenzi hao huamini kwamba, sasa wanaweza kujitolea kwenye uhusiano huo na kwamba, wanaweza kuwa na nguvu nao kwa asilimia kubwa.
Suala hili, kuna wataalamu huliita mtego wa kimapenzi. Huitwa hivyo, kwa sababu huwafanya wapenzi kutokuangalia sifa nyingine na badala yake kuweka nguvu kwenye mwili, yaani tendo la ndoa.

Kuna wakati kupenda inakuwa kama upofu.
Upofu hutokea kutokana na kuzalishwa kwa kemikali nyigi mwilini, zenye kumfanya mtu asiweze kujiuliza kuhusu maeneo mengine ya kimasha ya binadamu, zaidi  ya mwili.
Kinachotokea ni mwili kuvutwa na wale tunaowapenda kwa kuzalisha homoni inayofahamika kama ‘phenylethylamine’ au PEA kwa kifupi.
Kemikali au homoni hii pamoja na nyingine kama vile ‘depomine’ na ‘norepinephrine’ (ambazo huchochea hali za kimwili) na ‘ testosterone’(ambayo huongeza hamu ya kujaamiana), huzalishwa mara baada ya kukutana kimwili.
Baada ya kuzaliswa kwa homoni hizi, akili ya mtu huona mwili tu, yaani mapenzi na siyo sifa nyingine. Hapa ndipo ambapo, mtu hujikuta hawezi kujizuia tena kukutana kimwili na mpenzi wake, mara baada ya kukutana naye mara ya moja.
Baada ya kufanya mapenzi na kufikia kileleni, huzalishwa homoni iitwayo ‘oxytocin’ (ambayo huhusika na mihemiko), homoni hii humfanya mtu kujikuta anapenda kuwa karibu na kujifungamanisha na mtu aliyefanya naye mapenzi. Tunaweza kusema, ukaribu kwa wapenzi wawili huongezeka na unakuwa ni ukaribu wa mwili zaidi.
Kuzalishwa kwa homoni hizi, ni jambo ambalo mtu hawezi kulizuia na huwa linakuja kwa nguvu sana, kiasi kwamba, mtu kuwa kama amepoteza ufahamu wa maeneo mengineyo ya kimaisha isipokuwa mapenzi tu.
Homoni hizi humfanya mtu kuwa na hisia za kuvutiwa na mwingine, uchangamfu, ukaribu, kuvutiwa na hisia za ukamilifu zaidi. Wale waliowahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kabla ya ndoa au wale waliowahi au wanaotoka nje ya ndoa zao kwa kuvutwa kimwili na wapenzi wengine, wanajua inavyokuwa.
Lakini homoni hizi, hatimaye huanza kupungua na mtu huanza kuhisi kwamba alikosea. Huoni tena na huhisi kama ilivyokuwa awali. Sasa haoni kuwa mpenzi wake ni mzuri au anafaa kama iivyokuwa awali. Kwa sababu, homoni zile zimeshuka sana, mwili unakuwa hauna maana tena.
Kwa bahati mbaya  kile kilichokuwa kinaitwa upendo, kilikuwa kimefungiwa kwenye mwili na homoni hizo ambazo kwa sasa hazipo. Hivyo, wapenzi hawana kingine cha kushika ambacho, wataweza kukiita mapenzi.
Unajua sasa ni kwa nini, tangu kale kabisa suala la wachumba kukutana kimwili kabla ya ndoa lilikuwa likipingwa sana? ni kwamba, watu wanapokutana kimwili, uwezo wa kukaguana tabia unakuwa umefungwa kutokana na kufumuka kwa homoni hizi, ambazo hubadili hali ya mtu na hisia zake kwa ujumla.
Kwa nini unadhani watu, hasa wanaume wakishaanza mapenzi ya kimwili na mtu mpya, yaani nyumba ndogo au yeyote, inakuwa rahisi sana kwao kujisahau na kukamatwa? Sababu ni hiyo hiyo, kwamba, uzalishwaji wa homoni hizi huwa ni mkubwa kiasi cha mtu kuamini kwamba, hakuna kingine chene kufurahisha na kuliwaza kama uhusiano huo.
Kumbuka, watu wawili wanapovutana, kwa maneno mengine tunasema kuna kemia kati yao. Hii ina maana kwamba, huwa kuna mabadiliko ya badhi ya homoni kama nilivyosema. Lakini, wanapokutana, homoni hizi huwa nyingi kiasi cha kufanya upofu wa muda. Unaweza kuwa upofu wa mwezi, mwaka au miaka.
Upofu huu unapmalizika, uhusianao huwa ni wa vurugu tupu, kwa sababu kama nilivyosema awali, hqakuna mahali pengine pa kushika  siyo tabia, mienenfo waa haiba.
Upofu huu unapomalizika, uhusiano huwa ni wa vurugu tupu, kwa sababu kama nilivyosema awali, hakuna mahali pengine pa kushika siyo tabia, mienendo wala haiba.
Inashauriwa kwamba, mtu anapovutiwa na mwingine au watu wanapovutana ni vema wakawa wangalifu sana. kwanza, wajue kwamba, uhusino ambao msingi wake ni miili tu, yaani tendo la ndoa haudumu, kwani homoni zitokanazo na kukutana watu kimwili, hazina maisha, huwa zinaisha haraka.
Lakini pia inashauriwa kwamba, mtu anapoingia kwenye mapenzi ajaribu kushariana au kuukagua moyo wake, akili pamoja na hisia zake. Kuacha tu mabadiliko ya hali ya mwili yakatawala ni kutafuta maumivu.
Hebu jiulize, ni kwa nini mapenzi yanapoanza kwa moto sana, huzimika haraka  au kwa kishindo sana? ni kwa sababu yanajengwa kwenye msingi usioaminika, yaani katika mihemiko na kimapenzi. Penzi linalokua polepole ndilo lenye kushika, kwani halina msingi wa mwili.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,

Dec 19, 2016

Je, Wajua! Kila Kitu Hutokea Kwa Sababu Maalumu?

No comments :
Kijana mmoja baaada ya kuhitimu masomo yake ya chuo alipanga kwenda kumtembelea mjomba wake ambaye kwa wakati huo alikuwa anaishi kijijini. Kijana Aliamua kufanya hivyo  kwani zilikuwa zimepita siku nyingi bila kuonana kwa mjomba wake.

Hivyo siku uliyofuata kijana aliamka asubuhi na  mapema kabla jua halijaleta faraja kwa watu wake, alijiaanda kwa  kasi zaidi ya 4G   kabla ya kuanza safari ya kuelekea kijijini kwani muda haukuwa rafiki kwake.

Kwa kuwa safari ilikuwa ni ndefu sana kijana huyo aliamua kubeba chakula ambacho kingemsaidia kupungunguza njaa wakati wa safari, safari iliendelea huku kijana mawazo ya mjini akiyaacha na wenye miji yao huku akili yake ikiwa ina shuaku na msukumo thabiti kuhusu maisha ya kule kijinini. 

Ilipofika mida ya muda wa mchana kwa kuwa njaa ilikuwa inamuuma sana alichua chakula chake na kuanza kula.


Aliuamini ule usemi ambao unasema "usiudharau mkono kwa sababu ya kijiko" hivyo chakula kile alikula kwa kutumia mkono ambao anaumini zaidi, lakini kama ujuavyo wakati wa safari utaratibu wa kunawa mikono wakati wa safari huwa si zingatio sana aliamua kula bila hata kunawa mikono yake.

Baada ya dakika chache kula chakula kile, tumbo la ghafla lilimkamata huku akikaa kila aina ya mkao ujuao wewe katika siti ile, alifanya vile ili kuyanusuru maumivu ambayo yalikuwa yametawala katika tumbo. Hata hivyo kadri muda ulivyozidi kuyoyoma na tumbo nalo lilikuwa linazidi kuuma zaidi.

Aliwaza ni kitu gani ambacho kimesababisha tumbo lake kuuma, lakini kadri anavyozidi kuzama katika dibwi la halmashauri ya fikra zake aligundua ya kwamba chakula alichokula kulikuwa ni  chanzo cha kuuma kwa tumbo lake.

Hivyo safari iliendelea mpaka alipowasili katika kijiji ambacho alikuwa anaishi mjomba wake.

Mjomba alifurahi kumuona kijana yule, lakini mjomba alishtuka kumuona kijana yule akiwa hana furaha, ndipo mjomba akaamua kushirikisha mdomo katika kumuuliza swali kijana yule ni kipi ambacho kimemtoa katika ulimwengu furaha, ndipo kijana akamueleza mjomba wake tumbo lilikuwa linamsumbua kidogo.

Baada ya mjomba kusikia hayo alimueleza ya kwamba asipate tabu kwani atakuwa sawa muda si mrefu, walipofika nyumbani kwa mjomba, mjomba alimpa dawa  za miti shamba, kijana yule baada ya kula alikuwa sawa.

Baadae mjomba pamoja na kijana yule walikaa katika mkeka kwa ajili ya kupata chakula. Chakula chenyewe ulikuwa ni ugali wa mhogo pamoja nyama ya swala.

Chakula kile kilikuwa ni kitamu sana kwani kilikuwa kimepikwa kwa ustadi wa hali ya juu sana. Wakati wanaendelea kula huku hadithi mbalimbali zilikuwa zimetawala mahali pale kwani muda mrefu ulikuwa umepita bila wao kuonana. Lakini katika ya maongezi yao mjomba hakusahau kumpongeza kijana yule kwa kuhitimu masomo yake ya chuo.

Basi huku maongezi yao yakiendelea walijikuta chakula kimeisha bila hata wao kujua. Hivyo kijana yule akaona asiwe mchoyo wa fadhira hivyo akaamua kumshukuru mjomba kwa chakula kitamu, lakini zaidi alisema ya kwamba alifurahishwa na nyama ile.

Lakini mjomba alimuahidi siku iliyofuata kwamba wangeambatana pamoja kwenda kuwinda pamoja. Kijana yule alifurahi maneno hayo kutoka kwa mjomba wake kwani alitamani kujua mbinu amabazo zilitumika kuwinda. Kwani alimini ule usemi "usimpe mtu samaki" bali mpe samaki siku ya kwana siku inayofuata mpe nyavu akavue mwenye.

Ilipofika asabuhi na mapema kila mmoja aliamka akiwa ni mzima wa afya tele, kijana alimuuliza mjomba wake ni muda gani ambao wangeenda mawindoni? Mjomba akamwambia ya kwamba muda wa kufanya mawindo ni muda wa usiku ambapo wanyama wengi huwa wamechoka sana. Hivyo ingefaa waendee muda usiku.

Hivyo ilipofika usiku mjomba pamoja na kijana yule walichukua dhana za uwindaji kwa ajili ya kuelekea mawindoni. Harakati za mawindo zilikuwa zimepamba moto katikati ya msitu, lakini matarajio yao yalikuwa hayapo sawa kwani hawakupata hata mnyama mmoja lakini hawakukata tamaa waliendelea kufanya mawindo.

Muda ulizidi kwenda bila ya kupata chochote. Kijana yule alikuwa amechoka sana, kwani aliamini ya kwamba kufanya mawindo ni kitu rahisi sana. Kwa kuwa kijana yule alikuwa amechoka sana, licha ya kuchoka alikuwa tayari ana usinginzi mzito, Hivyo mjomba aliamuru washushe hema ili waweze kupumzika. Waliingia ndani ya hema na kulala ndani ya hema.

Baada ya dakika chache wote walipitiwa na usingizi mzito ndani ya hema lile, baada ya masaa machache mjomba alishtuka usingizini hivyo akaamua amuamshe kijana yule. Mjambo alimuasha kijana yule, kijana aliamka, mjomba akamuuliza kijana "unaona nini angani?"  kijana akajibu naona nyota pamoja na mwezi unaoangaza kwa mwanga mzuri.

Mjomba akauliza tena "unachokiona kinamanisha nini? Kijana akajibu ya kwamba kile anachokiona ni ishara ya kwamba  Mungu yupo pamoja nao, pia mng'ao wa nyota zinaonyesha ya kwamba siku uliyofuata ilikuwa ni njema . mjomba akasema umejibu vyema, lakini tumeibiwa hema hivyo kikubwa zaidi nilitegemea utajibu ya kwamba "tumeibiwa hema" 

Mwisho umejifunza nini kupitia kisa hiki?

Tafsiri ya kisa hicho ni;

Kisa cha hadithi hii ni kwamba wapo baadhi ya watu wamekuwa na maisha magumu kwa sababu ya kutokuwa na uwezo wa  kupambanua vitu kwa mapana, hata hivyo naweza nikasema tumekuwa tukiishi katika hali ya kimazoea. Wengi tumekuwa tukitazama mambo kwa kuanza na vitu ambavyo vinaonekana mbali kuliko kuanza na vitu vilivyopo karibu.

Kwa mfano wahitimu wengi wa vyuo huamini ya kwamba baada ya kuhitimu masomo yao ni ajira, wao hawaamini ya kwamba wanaweza kujiri. Wapo baadhi ya watu ambao wanaishi mahali fulani wanawaza kwenda sehemu nyingine huku wakiamini kufanya hivyo ni njia ya mafanikio kwao, lakini ukweli ni kwamba kila mahali ambapo leo hii upo pana fursa.

Hivyo chunguza kwa umakini na uweze kujua  fursa zile ambazo zinakuzunguka ndipo uje kuwaza fursa ambazo zipo nje na hapo ulipo.

Mwisho nimalize kwa kusema ya kwamba kiporo hakihitaji moto mwingi, maana yangu ni kwamba mafanikio yako hayahitaji mambo makubwa sana ila yanahitaji kujiongeza zaidi kwa kila kitu ambacho unakifanya.

Ndimi; Afisa mipango Benson Chonya,
0757909942

Dec 16, 2016

UTAFITI; Mwanamke Huota Tofauti Na Mwanaume.

No comments :
Wanasema mwanamke na mwanaume ni tofauti kwenye baadhi ya mambo, kimaumbile. Lakini, sio yale mambo yenye kuonekana peke yake, kwani imebainika sasa ni kwamba, tofauti huenda hadi kwenye usingizi. Ni kwamba mwanamke na mwanaume huota tofauti.
Kwa hiyo, hata wakiwa usingizini, mwanamke na mwanaume wanaendelea na tofauti zao.
Dk. Mark Blagrove, ambaye ni mtaalamu wa saikolojia, anasema kwamba, yeye pamoja na mwenzake wamefanya utafiti kwa watu zaidi ya 100,000 na kubaini kwamba, kuna tofauti kati ya mwanamke na mwanaume hasa linapokuja suala la kuota ndoto.
Utafiti uliofanywa na Blagrove na wenzake umehusisha watu wa dunia nzima, sio ulaya na marekani peke yake.
Hivyo, ni utafiti ambao unazungumzia jambo linalohusu dunia nzima, siyo upande fulani tu wa dunia.

Ipo tofauti kubwa kati ya ndoto ya mwanaume na mwanamke.
Katika utafiti huo, wamegundua kwamba, wanandoa ambao wamelala kitanda kimoja, ubavu kwa ubavu, wanakuwa na ndoto tofauti kabisa, ingawa wanaweza wakawa wanaota wakati mmoja.
Ndoto za wanawake zinaonekana wazi zinahusu kazi, zimejaa hisia sana ndani yake na huchukua muda mrefu zaidi.
Mwanamke anaweza kusimulia kuhusu ndoto yake, ukadhani imechukua saa kadhaa kuota kwa jinsi ilivyo ndefu. Huwa wanaota ndoto moja kwa muda mrefu zaidi.
Ndoto za wanawake zimejengwa kwenye msingi wa nyumbani na kuhusisha watu wengi na hasa wa familia zaidi, kuliko watu wa nje ya familia.
Kwa upande wa ndoto za wanaume, kuota wageni ni jambo la kawaida sana kwao. Wageni, ina maana watu ambao hawawafahamu. Ndoto za wanaume zimejengwa kwenye msingi wa maeneo ya barabara, magari na vurugu.
Hauwezi kupita muda mrefu kabla mwanaume hajaota kuhusu gari, barabara au vurugu za aina fulani.
Huhusisha pia tendo la ndoa na wanawake wasiowajua, mara nyingi.
Ndoto za wanaume pia zimejengwa pia kwenye mazingira ya kazi, na kuhusiana na hofu za kipato na hofu za kupoteza kazi au kufilisika. Zimejaa masuala ya kazi au shughuli.
Mwanasaikolojia aliyeandika pia vitabu kadhaa kuhusu ndoto, Veronica Tonay, anasema, utafiti huu unathibitisha tafiti za siku nyingi ambazo zilikuwa zinadai kwamba, wanawake huota tofauti na wanaume.
Hivi sasa, inaweza kusemwa kwamba, suala hilo halina utata tena. Inaonyesha pia kwamba, zaidi ya nusu ya watu wote wanapata ndoto mbaya angalau mara moja kwa wiki.
Kuna wengine ambao ndoto mbaya ni sehemu ya maisha yao ya kindoto,yaani karibu kila siku zinawatokea.
Inaelezwa kwamba, kazi anayofanya mtu inaweza kuchangia kwenye kuwa kwake na ndoto za jinamizi au ndoto mbaya.
Kwa mfano, wauguzi wahasibu na watumishi kwenye vyombo vinavyohusiana na mawasiliano, ndiyo ambao hukumbwa sana na ndoto hizi mbaya.
Kukimbizwa, meno kudondoka, kuanguka, kutegewa au kuwekewa kizuizi, ni miongoni mwa mada zinazootwa sana, hasa na wale wanaoota majinamizi.
Wanasaikolojia wanasema, ndoto zinahusiana na shughuli ambazo hatujazimaliza kwenye mpangilio wetu wa kazi wa siku au kujaribu kufanya kile ambacho tulishindwa kukifanya tukiwa macho.
Kwa mfano, kuota kupata fedha, jambo ambalo katika hali ya kawaida, limekuwa gumu kwetu.
Watafiti hapo wanazidi kuchambua ndoto kwa kusema kwamba, ndoto zinazohusu mambo mabaya ndizo ambazo zinaotwa zaidi kuliko zile zinazohusu mambo mazuri.
Hata wale watu wenye furaha maishani, wanaonekana kuota ndoto zenye mada zisizopendeza kuliko mada zenye kupendeza.
Ingawa wataalamu wa ndoto wanasema, kila ndoto ina maana kutegemea na mtu aliyeota, utafiti huu unaonyesha kwamba, pamoja na kuwa hilo ni kweli, kuna mambo ambayo mtu mmoja akiyaota , maana yake ni ile ile kwa mtu mwingine yeyote.
Kwa mfano, kuanguka, kwenye ndoto ina maana ya mtu kukosa uhakika wa usalama.
Kukimbizwa au kufukuzwa, bila kujali ni nani anaota, inaweza kuwa na maana ya kukimbia matatizo.
Ndoto ya kupoteza au kung’oka meno inahusiana na mtu kujali namna anavoonekana au sura.
Ndoto ya mtu kukimbia, lakini lakini akajikuta bado yupo pale pale, yaani hasogei, ina maana au inahusiana na mtu kuwa na kazi nyingi kumzidi uwezo.
Ndoto ya mtu kuwa uchi, ina maana kwamba, mhusika ana matamanio ya kuwasiliana na mwingine au wengine.
Kile ktiendo cha kuvua nguo ndotoni kina maana ya mtu kuondoa vikwazo vinavomkabili kwenye maisha ake.
Pamoja na kwamba, lengo la utafiti huu lilikuwa ni kuona kama mwanamke na mwanaume wanaota tofauti, bado umezaa masuala mengine muhimu ynayohusiana na ndoto. Moja ya hili lilozaliwa ni maana ya ndoto, ambazo hazibadiliki, bila kujali ni nani ameziota.
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.
TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.
Ni wako rafiki,
IMANI NGWANGWALU,








Dec 15, 2016

Ifahamu Nguvu Ya Kufikiri Na Kushukuru Katika Maisha.

No comments :
Katika vitu ambavyo wanadamu tumekuwa hatuvitilii maanani ni vitu vikubwa viwili, vitu hivyo ni kufikiri na kushukuru. Nimesema hivyo nikiwa na ushahidi tosha kwa kile ambacho nakiamini, na pia ni sahihi kwa asilimia zote ambazo unazifahamu wewe.

Unashangaa kwanini nasema kwa kujiamini? Wala usishangae bali tuendelee kusonga mbele mwanzo mpaka mwisho wa makala haya ili tuweze kwenda sawa.

Ukweli ambao upo wazi ambao hauhitaji hata mwanga wa jua ili kuonekana kwa watu wake upo bayana kabisa, ni kwamba tumekuwa tukilalamika kwa kutoa sauti au hata kutotoa sauti ya kwamba maisha ni magumu.

Yote hiyo inaweza ikawa hivyo kwa sababu watu tumeshindwa kuwekeza muda wetu katika suala zima la kufikiri, huenda nikawa nimekuacha ila nataka tusemezane bila kuoneana haya. 

Ipo sababu kubwa leo kuweza kutenga muda kwa kila siku angalau masaa mawili kwa ajili ya kufikiri, si kufikiri tu bali kufikiri vitu vipya.


Kama unafanya biashara, kilimo au kitu chochote ni vyema ukatenga angalau masaa hayo mawili kwa ajili ya "kuwaza". Kufanya hivyo kutakufanya uweze kuwa bora hatimaye kuonesha utofauti na wengine.

Ifahamu Nguvu Ya Kufikiri Na Kushukuru Katika Maisha.
Itumie nguvu a kufikiri vizuri ikusaidie kufanikiwa.
Hakuna maisha bora kama utaamua kufanya kitu kile kile, kila wakati kwa njia ambazo umezizoea. Fanya kitu cha tofauti kwa kuwa wewe ni wa tofauti.

Na kama ilivyo kauli mbiu ya mtandao huu ni kwamba badili maisha yako kwa kuwa na fikra sahihi, hivyo fikiri sana kwani fikra chanya huleta mabadiliko ya kweli hakuna jambo lolote litafanikiwa kama litakuwa katika mtazamo hasi.

Lakini tukija katika upande wa pili ni kwamba katika vitu ambavyo havipo katika tamaduni zetu ni jambo zima la kutoa "Shukrani" kutoa shukrani ni jambo la faraja sana mbele za Mungu na mwanadamu ambaye amekusaidia wewe kwa namna moja ama nyingine kuweza kufika hapo ulipo.

Elewa na tambua ya kwamba usingefika hapo ulipo kama ungesimama peke yako. Mbele ya Mafanikio yako kuna mtu nyuma yake. Swali la kujiuliza ni shukrani gani ambazo umezitoa kwa mtu huyo?


Ukifikiri kwa umakini utagundua ya kwamba hakuna hata mtu mmoja ambaye umewahi kutoa shukrani kwake, hii ni kwa sababu shukrani zetu ni za mara moja kama mla ndizi.

Naendelea kujihoji pasipo kupata majibu ni maisha gani hayo ambayo umeyachagua? Kwanini uishi maisha hayo yasiyokuwa na faida na chukizo mbele za Mungu?

Unafikiri ya kwamba ukitoa shukrani kwa Mwenyezi Mungu na mtu ambaye amekusaidia kuwa hapo utapungua uzito au utafirisika? La 
hasha binafsi naona kama ukiweka utaratibu wa kushukuru itakusaidia kuweza kufanikiwa zaidi. 

Huenda ninachokisema leo kikagusa moja kwa moja. Utajiuliza labda leo Afisa mipango kaamuka na mimi, la hasha kwa kuwa mawazo yangu hayana ukomo wa kuwaza wacha niseme tu, huenda yakagusa kwa namna moja ama nyingine na yakakusaidia.


Nguvu ya kushukuru huongeza baraka za kimafanikio kila wakati, haiwezekani wewe ukawa ni mtu kuomba tu kuliko kushukuru, kufanya hivyo ni sawa na bure hata vitabu vya dini havijakaa mbali nasi kwani vinatukumbusha ya kwamba "kila ajuaye kuomba lazima ajue na kushukuru".

Hivyo jiwekee utaratibu wa kufikiri na kushukuru ili uweze kupata amani ya moyo hatimaye kufikia ile ndoto kubwa uliyonayo. Kama umenielewa vizuri baada ya kumaliza kusoma makala hii chukua dakika chache kuwashukuru wote ambao wamekusaidia kufika hapo ulipo.

Lakini ikumbukwe kumshukuru mtu ni lazima umwambie mtu huyo. Pia utakuwa mchoyo wa fadhira kama utashindwa kujishukuru mwenyewe. Endapo nimekukwaza utanisamehe sana kwani wajibu wangu kukueleza ukweli kila nipatapo nafasi.

Ndimi :Afisa Mipango Benson Chonya,



Dec 13, 2016

Siri 6 Za Kuishi Maisha Ya Ushindi.

No comments :
Kwa kawaida zipo siri na mbinu nyingi sana za kukusaidia kuishi maisha ya ushindi wakati wote. Hakuna haja ya kulaumu au kulalamika  maisha ni magumu, zipo siri za kukusaidia kukabiliana na changamoto zako.
Leo kwa kifupi, naomba nikushirikishe mbinu au siri chache za mafanikio ambazo zitakusaidia kukupa hamasa na nguvu ya kuishi kwa ushindi na mafanikio makubwa sana.
1. Kila wakati, pambana na mambo magumu, wakati mambo hayo bado ni rahisi. Pambana na changamoto zako, wakati changamoto hizo bado ni kidogo. Pambana na kuitunza afya yako, wakati bado umzima. Pambana na umaskini, wakati bado ukijana mwenye nguvu.
Kila changamoto unayokutana nayo kwenye maisha, unaweza kuishinda ikiwa utakabiliana nayo mapema. Acha kusubiri mambo yameharibika ndio uanze kukomaa na changamoto yako. Acha kusubiri nyumba imeungua ndio utafute maji ya kuzimia moto.
Jifunze kutokuishi maisha ya zima moto. Ishi kwa mipango sahihi, ambayo mipango hiyo mwisho wa siku itakuongoza wewe kuweza kufikia katika mafanikio yako makubwa. Wengi wanashindwa katika maisha kwa sababu ya kuchelewa kuthibiti mambo ambayo walitakiwa wayathibiti mwanzoni.
Jiulize ni mara ngapi umekwama, kwa sababu ya kushindwa kuithibiti hali fulani ambayo ulitakiwa kuithibiti mapema? Acha kuendelea kuharibu maisha yako kwa kusubiri eti mpaka mambo yameharibika ndio utafute dawa yake. Changamka sasa na anza kutekeleza majukumu yako mapema.
7
Tunza na kuilea ndoto yako kwa uangalifu, ili ikupe mafanikio.
2. Siku zote katika safari ya mafanikio, kuwa makini sana na jinsi unavyoitunza na kuilea ndoto yako. Kama ndoto yako unaitunza na kuilea katika hali ya hofu na mashaka sana basi, utavuna magugu na hautaweza kufanikiwa.
Na pia kama ndoto yako unatitunza na kuilea katika matumaini makubwa ya kufanikiwa, imani ya mafanikio na kujiamini, uwe na uhakika ni lazima utafanikiwa. Wapo wengi wanaoshindwa kufikia ndoto zao kwa sababu ya kuzielea ndoto zao katika mazingira mabovu.
Kama ulivyo mmea ili ukue ni lazima umwagaliwe maji safi, halikadhalika ndoto  yako iko hivyo hivyo. Ni lazima ndoto yako ituzwe kwa matumaini na imani ya mafanikio na sio kuitunza katika hofu na woga ambapo mwisho wa siku ni lazima utakwama.
Najua hapo ulipo una ndoto ya iaina fulani, jiulize unailea ndoto yako katika mazingira yapi? Je, unajiamini utafanikisha? Au au upo kwenye mazingira ya mashaka na hofu? Mazingira yoyote yale unayoyatumia kuilelea ndoto yako yanakupa jibu kama utafanikiwa au hautafanikiwa kuifanikisha ndoto yako.
3. Ili kufikia mafanikio zaidi ya hapo ulipo, ipo haja na ulazima wa wewe kujituma na kufanya kazi kwa bidii sana nje ya yale mazoea uliyojiwekea. Kwa mfano, kama umezoea kufanya kazi kwa saa 8, ongeza masaa mengine manne ya ziada. Kama umezoea kuamka sa 12, anza kuamka saa 11 alfajiri. Fanya kitu ambacho kitakutoa nje ya mazoea yako yaani ‘comfort zone’. Kwa chochote kile unachokifanya, fanya nje ya mazoea yako. Hiyo itakusaidia sana kujenga misuri mikubwa ya kukuwezesha kufika mabali kimafanikio.
4. Kwa hali yoyote ile ambayo inatokea nje ya wewe haina mchango mkubwa sana wa kuweza kukukwamisha au kukufanya ushindwe kufikia mafanikio yako. Kitu ambacho kitakufanya ushindwe kufanikiwa ni ile hali inayotokea ndani mwako tu.
Hali hiyo inayotokea ndani mwako, ndiyo ina nguvu kubwa sana ya kubadillisha maisha yako na kuwa ya mafanikio kabisa. Hebu jiulize kila unapowaza mafanikio, ndani mwako unajionaje? Unajiona ni kwamba utafanikiwa au utashindwa? Kipi unachokiona ndani mwako?
Haijalishi watu wanasemaje au watasema nini juu yako, hata watu dunia nzima waseme kwamba utafanikiwa, lakini kama ndani yako huoni hivyo ni wazi huwezi kufanikiwa, pia hata dunia nzima iseme kwamba wewe ni wa kushindwa, lakini ikiwa ndani yako unajiona wewe ni mtu wa mafanikio, utafanikiwa.
Kiti kikubwa hapa, jifunze kutokulaumu hali yoyote ile, inayotokea nje katika maisha yako kwamba ndio imekukwamisha. Anayejizuia na kujikwamisha sio mwingine bali ni wewe mwenyewe na hali hasi nyingi ulizozibeba. Kuanzia leo amua kujenga hali bora ndani mwako itakayokupa mafanikio makubwa.
5. Kuna wakati unaweza ukajikuta unaumia sana kwenye maisha yako, hiyo yote kwa sababu ya maoni hasi ya watu wanayokutolea wewe. Sasa ili usiendelea kuumia kwa jambo hilo, kumbuka hivi, hicho ambacho kinaongelewa juu yako ni kwa mujibu wa maoni yao wao wenyewe. Uhalisia wa wewe jinsi ulivyo unaujua wewe.
Hivyo, acha kuchukua maoni ya watu na ukaamua kuyatumia kuendesha maisha yako. Alooo! Ukifanya hivyo utamuia sana na utaiona dunia chungu. Ishi wewe kama wewe kwa kufata kile ambacho moyo wako unakutuma na hiyo itakufanya uishi maisha ya ushindi na mafanikio makubwa.
6. Kitu pekee kitakacho kufanikisha si wingi wa maarifa ya mafanikio unayoyapata kila siku. Mafanikio yako utayapata kwa wewe kuamua kuyatumia maarifa hayo tena kwa uhakika.
Jiulize leo hivi, tokea uanze kujifunza juu ya mafanikio, umechukua hatua kiasi gani? Au umebakia kuwa ni mtu wa kushangilia na kuwaacha wengine wachukue hatua za kimafanikio?
Endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

Kama makala hii imekusaidia na unapenda kujifunza zaidi, karibu kwenye kundi la Whats App ili tuweze kujifunza pamoja tena kwa ukaribu. Kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S, kisha ikifuatia na jina lako kwenda 0713 048035 ili uanganishwe.

TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YA MAFANIKIO.

Ni wako rafiki,

IMANI NGWANGWALU,