google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 31, 2016

Kama Unajiambia Na Kufikiri Hivi Kila Wakati, Huwezi Tena Kufanikiwa.

No comments :
Mara nyingi katika maisha yetu kama tuna kawaida ya kujiambia maneno au kauli za aina fulani, ni lazima tutajihisi kwa namna ile tunavyojiambia sisi mwenyewe. Kumbuka kujiambia huku huwa tunafanya kati yetu binafsi kila siku na kila wakati vichwani mwetu ambapo mazungumzo huwa yanaendelea huko, ambayo mara nyingi ni siri zetu.
  
Kama ikatokea tuna kawaida ya kujiambia maneno au kauli za aina fulani, ni lazima tutajihisi kwa namna tunavyojiambia. Hivyo, wakati mwingine kujiamini au kutokujiamini kwetu ni matokeo ya yale yanayoenda vichwani mwetu, yaani tunajiambia nini kuhusu sisi wenyewe. Kwa kujiambia kwa namna fulani, hisia, hali na mazingira yetu yatakuwa hivyohivyo.

Naomba nikufundishe jambo moja ambalo ni muhimu sana kwako kulijua. Kama kweli unataka kujiamini, ni lazima uanze kujichunguza namna au jinsi unavojiambia wewe mwenyewe. Kujichunguza huku maana yake ni kutambua, kufahamu na kujua kwamba, huwa kuna mazungumzo ambayo unayaendesha kichwani mwako kuhusu wewe mwenyewe.

Kumbuka kwamba, kile ambacho huwa tunajiambia, yaani yale mazungumzo tunayoyafanya vichwani mwetu, ambapo mara nyingi ni kujilaumu, kujishusha, kujikatisha tamaa na mengine ya aina hiyo, yanakuwa yana nguvu sana kwetu. Kwa nini? Ni kwa sababu, tunapojiambia mambo hayo inakuwa sawa kabisa na tunavyowaambia watu wengine.


 Kasi ya kuzungumza, lafudhi na hata sauti tunayoitengeneza huko kichwani, havina tofauti sana na wakati tunapokuwa tunamwambia mtu mwingine kwa sauti tu ya kawaida ya mdomo. Ndiyo maana yanakuwa yana nguvu ya kutuathiri. Inakuwa ni kama kweli kabisa, ingawa ni ukweli kwamba hayo yote tunakuwa tumeyazungumzia vichwani mwetu.

 Hivyo, tunapojiambia huko kichwani, ‘mimi ni bwege tu siwezi kufanikiwa’ au ‘mtu mbaya kama mimi nani atanipenda!’ ama ‘nitakufa maskini tu, si nimetoka familia maskini hata hivyo’, ni wazi hayo yatakufanya ujitoe thamani na kutokujiamini. Yanakuwa ni maneno ya kukuumiza wewe ni sawa kabisa na kama vile unaambiwa na watu wengine.

Mbaya zaidi pia ni kwa sababu ni sisi wenyewe, tunaojiambia mara nyingi tena na tena na athari zinakuwa kubwa zaidi kwetu kutokana na msisitizo tunaouweka bila hata kujua. Kama nilivyosema awali, unapaswa kujua kwamba unafikiri. Ukishajua, itakuwa rahisi sana kwako kujiuliza kama yale unayojiambia kuhusu wewe mwenyewe ndiyo unayotaka au hapana.

Kama siyo unayotaka, kwa kadri unavyojiambia ndiyo utakavyokuwa unazidi kupata hisia usizozitaka. Kama ukianza kutambua kwamba huwa unafikiri, itakuwa ni rahisi sana kwako kuweza kubaini kuwa, huwa unajiambia nini juu yako mwenyewe ambacho kinaweza kukusaidia au kukuumiza na kuharibu maisha yako kabisa.

Kama unataka kujiondoa na janga la kujitia katika kutokujiamini, inabidi uchukue kalamu na karatasi, ujaribu kuandika kile usichokipenda ambacho huwa unajiambia kuhusu wewe, mara kwa mara au kile unachojiambia katika mazingira fulani. Kwa kujua kile unachojiambiwa mara kwa mara ambacho hukipendi, itakusaidia kuwa makini nacho na pengine kukiepuka kabisa katika fikra zako. 

Kwa mfano, huwa inatokea ukajiambia, ‘achia hapo usije ukaadhirika wewe’, au labda ‘usifanye tena si umeona ulivyoshindwa safari ile ‘, ama ‘ni kawaida yangu kukosea nimezoea’ ama ‘siwezi kumudu kwa sababu ni bwege basi’.

Kumbuka kwamba, maneno hayo ni mabaya na kamwe hayawezi kukusaidia kujiamini na kupata unachokihitaji. Ni maneno yenye nguvu sana ya kuweza kuingiza hisia usizozitaka ndani kabisa ya mfumo wako wa kufikiri. Kumbuka, siyo wakati huu, bali hata wakati mwingine, ukikutana na mazingira yanayokufanya ujiambie hivyo, utajihisi hovyo hivyohivyo.

Kwa kuyaandika na kuyaelewa na kuelewa ni wakati gani na kwenye mazingira gani huwa unajiambia maneno hayo, inaweza kuwa rahisi kwako kuanza polepole kudhibiti mazungumzo hayo hayaendayo kichwani mwako. Ukifanya hivyo, polepole, utaanza kujiamini. 

TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI KATIKA SAFARI YAKO YA MAFANIKIO.

IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,

Aug 30, 2016

Mambo Ambayo Watu Wenye Mafanikio Huyafanya Sana ‘Wikiendi’.

No comments :
Kimsingi, ipo tofauti kubwa sana kati ya watu waliofanikiwa na watu ambao hawajafanikiwa, husani katika suala zima la matumizi ya siku za mapumziko hasa wikiendi.
Mara nyingi watu waliofanikiwa huzitumia wikendi zao kwa manufaa zaidi ukilinganisha na wale ambao hawajafanikiwa. Kutokana na matumizi haya ya muda huo wa mapumziko ndio wakati mwingine huweza kuleta utofauti hata wa mafanikio.
Hebu tuangalie watu wenye mafanikio huzitumiaje ‘wikiendi’ zao;-  
1. Kuamka asubuhi na mapema.
Mara nyingi watu wenye mafanikio, ratiba yao ya kuamka ipo pale pale bila kujali kwwamba ni siku ya kawaida au ‘wikiendi’. Siku zote hujitahidi sana kuweza kuamka asubuhi na mapema. 

Hufanya hivi kwa sababu wanatambua muda ni wathamani sana. Hivyo, hawako tayari kupoteza muda kwa chochote zaidi ya kuamka mapema na kuanza kuwekeza kwenye muda huo ili uwape faida.
2. Kujisomea.
Kati ya kitu amabacho watu wenye mafanikio huhakikisha wanakifanya wikiendi ni kujisomea. Kupitia kujisomea huko hujifunza mambo mengi ambayo yanawasaidia katika kukua kimafanikio na kupambana na changamoto za maisha.
3. Kutafakari juu ya maisha.
Watu wenye mafanikio katika wikiendi zao hawaishii kujisomea tu, bali wakati mwingine kutafakari sana juu ya maisha yao. Hutumia muda huo kujiuliza wapi walipotoka, wapi walipo na wapi wanapokwenda. Maswali hayo huwasidia kupiga hatua nyingine kubwa ya kusonga mbele.
4. Kufurahia maisha na familia.
Pia wikiendi kwa watu wenye mafanikio huzitumia sana kuwa pamoja na familia zao. Ni wakati ambao hupenda kucheza na kwenda maeneo tofauti na nyumbani kama ‘beach’ au mbuga za wanyama, kufurahia maisha na familia zao.
5. Kuweka mipango sawa ya wiki lijalo.
Mara nyingi watu wenye mafanikio huzitumia wikiendi zao, kwa kupanga mipango mipya ya wiki lijalo. Hapa hukaa chini na kujiuliza ni mikakati gani ambayo wataichukua ili kufanya wiki lijalo liwe bora na la manufaa zaidi.
6. Kufunga mawasiliano yasiyo ya muhimu.
Hiyo haitoshi watu wenye mafanikio ‘wikiendi’ zao huwa hawapendi sana kuwa na masiliano mengi kama ilivyo siku za kawaida. Kama ni simu wakati mwingine huzifunga au huwa hawapendi kuwasiliana sana na wengine katika kipidi hiki kifupi cha mapumziko.
7. Kutoa shukrani.
Shukrani ni jambo lingine la pekee ambalo watu wenye mafanikio hulifanya kwenye siku za mapumzikio. Ni kipindi ambacho huweza kuishukuru jamii kwa kwa namna tofauti mfano kutoa zawadi au kutembelea wagonjwa na mengineyo.
Kwa kifupi hayo ndiyo mambo machache ambayo watu wengi wenye mafanikio huyafanya sana katika siku zao za mapumziko ya wiki.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,

Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,








Aug 29, 2016

Kama Unataka Kufanikiwa Ni lazima Uongozwe Na Jambo Hili Kwanza.

No comments :
Kisaikolojia kila binadamu anaongozwa na nafsi mbili ambazo ni hisia na Hoja .

Hisia ni hali ya utabiri isiyokuwa na uhakika wa jambo. Huenda ikawa na ukweli au uongo. Mara nyingi hisia hutawaliwa na tamaa ya macho au mwili. Hoja ni uhalisia wa jambo au mambo yanayoonekana kwa macho. Ni mambo yenye uhalisia kimtazamo. Mtu yeyote anayeongozwa na hoja hufanikiwa kwa 100% lakini mtu anayeongozwa na hisia au tamaa ni kama mcheza kamari, anaweza kupata au kuliwa au kushindwa kabisa.

Hisia kama tulivyoona ni tabia ya kimaumbile aliyonayo mtu. Kila mtu ana tamaa ya kupata mafanikio katika maisha yake. Hiyo ni hisia haina hoja ya msingi katika kuleta mafanikio. Mafanikio ili yapatikane lazima iwepo hoja ya msingi  itakayo tawala katika maneno na vitendo vya mtu katika maisha ya mtu. Kivipi kuwe na hoja za msingi?

Ukitaka mafanikio  lazima ujenge hoja za msingi na zenye mashiko. Ni lazima uwe tayari kuizishinda hisia za matamanio katika maisha. Uamue kuifanya akili yako iongozwe na hoja badala ya kuongozwa na hisia.

HOJA ZA MSINGI ZITAKUSAIDIA KUFANIKIWA.
Hoja humfanya mtu kuwa na uhakika wa kile anachokifanya. Kuwa na ‘data’ sahihi za kile anachofanya. Humfanya mtu kufanya kila kitu kwa ufanisi MKUBWA.

Hoja humfanya mtu kujiamini na kuthamini kile anachofanya. Hoja humpa heshima na kumfanya athaminike na jamii kutokana na kufanya vitu sahihi na vyenye tija kwa jamii. 

Hisia au tamaa humfanya mtu kufanya maamuzi yanayompelekea kujuta baadae katika maisha take.

Hisia zikimtawala mtu hufanya vitu vya aibu na kumdhalilisha katika jamii kama kuiba, kubaka, kulawiti, kusema uongo kwa manufaa binafsi, kula mali ya haramu bila Hofu. Hisia zikimtawala mtu hukosa kujiamini na kujiona mwenye mapungufu na kukosa ujasiri.

Katika kumalizia somo letu naomba kutoa angalizo kuwa kabla ya kufanya maamuzi katika jambo lolote unalohitaji kufanya kwanza jiulize unayotaka kufanya je, yanaongozwa na hisia au hoja? Kama yanaongozwa na hisia au tamaa kamwe usifanye jambo hilo na kama jambo hilo linaongozwa na hoja hakika lifanye maana litakufaa katika maisha yako.

Naomba tuishie hapa kwa leo tukutane muda ujao kwa ajili ya kujifunza zaidi na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza kwa kina.

Tupo pamoja,

Shariff H. Kisuda (Mzee wa Nyundo)
Simu; 0715 079 993,

Aug 19, 2016

Hatua Muhimu Za Kukusaidia Kutoka Kwenye Madeni.

No comments :
Wapo watu wengi ambao huwa hawafikiri sana kwamba, kujiingiza kwenye madeni mengi ni kitu cha hatari. Watu hawa huja kugundua kwamba wapo kwenye hatari hiyo mara baada ya madeni hayo kuwalemea sababu ya wingi wake.
Kutokana na madeni hayo kuwa mengi, na kushindwa kuyalipa, hapo sasa ndio majuto na kilio huanza kutanda. Na wengi huanza kujilaumu kwa nini walikopa mikopo mingi, mikopo ambayo kama inawatesa kwa sasa, kutokana na kushindwa kuilipa.
Najua umeshawahi kukutana na watu ambao wana mizigo mingi na mikubwa ya madeni. Inawezakana watu hawa walikuwa jirani zako, ndugu au pengine hata wewe mwenyewe. Je, ulishawahi kujiuliza inapokutokea hali kama hii ni kitu gani unachotakiwa kufanya?
Leo kupitia makala haya, twende kwa pamoja kujifunza hatua muhimu za kukusaidia kutoka kwenye madeni.
1. Weka mipango imara.
Hatua ya kwanza itakayokusaidia kutoka kwenye madeni yako, ni kule kuamua kuweka mipango imara ya kukutoa kwenye madeni yako uliyonayo. Utaweza kulifanikisha hili vizuri, ikiwa utakaa chini na kupitia kiwango cha pesa unachotumia, ukilinganisha na kile kinachoingia.

Weka mipango imara ya kutoka kwenye deni ulilonalo.
Kwa mfano, inawezekana kabisa upo kwenye madeni kwa sababu unatumia pesa nyingi hovyo. Kwa hali hiyo hukupelekea matumizi yazidi kipato na kukufanya kukopa. Hivyo, hakuna namna nyingine zaidi ya kuweka mipango imara ya kubana matumizi na kuweza kuondokana na madeni.
2. Tafuta chanzo kingine cha pesa.
Njia nyingine nzuri ya kuweza kuondokana na madeni uliyonayo ni kutafuta chanzo kingine cha pesa. Acha kung’ang’ania kuwa na chanzo kimoja cha pesa, hiyo inaweza ikawa ni hatari sana kwako katika harakati za kujikwamua kutoka kwenye madeni.
Kwa mfano, kama umeajiriwa tafuta namna yoyote ile uwekeze kwenye hiyo biashara. Halikadhalika, kama umejiajri kwa kufanya biashara yako mwenyewe, jitahidi baada ya muda uwe na biashara nyingine. Kwa kufanya hivi itakusaidia kuweza kutoka kwenye madeni.
3. Punguza matumizi yasiyo ya lazima.
Mbali na kuweka mipango imara na kutafuta chanzo kingine cha pesa, pia unaweza kutoka kwenye deni ulilonalo kwa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Wengi wetu mara nyingi huwa ni watu wa matumizi mengi pasipo kutarajia.
Unawezaje kutoka kwenye matumizi yasiyo ya lazima? Kwanza, unaweza kuepuka matumizi yasiyo ya lazima kwa kuepuka kununua vitu visivyo vya  lazima sana kwako. Pili, ni kuwa makini na kila pesa inayotoka kwa kuiwekea kumbukumbu. Kwa hatua hiyo, inaweza kuwa msaada kwako kukutoa kwenye madeni.
4. Anza kulipa madeni makubwa.
Kama madeni uliyonayo ni mengi, ni vizuri kuya orodhesha madeni yako na kuanza kuyalipa madeni yale makubwa. Kwa kuchukua hatua hiyo utajikuta mahali, umeweza kuuotoa mzigo wa madeni ambao ulikuwa unakusumbua kwa muda mrefu.
Kwa kuhitimisha makala haya, naomba niseme hivi; mikopo ni mizuri ikiwa itatumia vizuri kwa malengo maalumu. Endapo utaitumia vibaya inaweza ikawa ni mzigo mkubwa na kugeuka kuwa deni.
Kama mkopo uliouchukua umekuwa deni, tafadhari hizo ni baadhi ya hatua ambazo unaweza kuzitumia kutoka kwenye madeni uliyonayo. Lililo kubwa kwako, fanyia kazi hicho ulichojifunza na chukua hatua.
Nikutakie siku njema na kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa.
Chukua hatua sitahiki za kubadili maisha yako na endelea kujifunza kupitia dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com

Aug 18, 2016

Mawazo Muhimu Unayotakiwa Kuwa Nayo Ili Kukuza Biashara Yako.

No comments :
Biashara shaka naongea na wewe katika siku hii ya leo ukiwa kwenye biashara yako au pengine ukitarajia kuanza biashara hivi punde. Kama uko kwenye biashara, pengine naongea na wewe ukiwa kwenye harakati za kutafuta wazo bora litakalo kusaidia kukuza biashara yako na kuwa ya mafanikio makubwa.
Kama uko kwenye hali ya kutafuta wazo bora litakalokusaidia kukuza biashara kwa kusoma makala haya itakusaidia sana. Ieleweke kwamba kuanzisha biashara na kuikuza biashara hadi ukaiona inaleta matunda ni vitu viwili tofauti. Wengi hujitahidi sana kuanzisha biashara lakini linapokuja suala la kukuza, hushindwa kwa sababu ya kukosa mawazo muhimu.
Kwa namna yoyote ile, mfanyabiashara anahitaji kuwa na mawazo muhimu yatakayomsaidia kukuza biashara yake  wakati wote. Haijalishi udogo au ukubwa wa biashara husika, lakini mawazo bora ni nguzo muhimu ya kuifanya biashara ikaendelea mbele na kutoa mafanikio makubwa.
Leo kupitia makala haya hebu tuangalie mambo gani muhimu unayatakiwa kuwa nayo ili kukuza biashara yako.
1. Tanua soko lako.
Biashara yako itaweza kukua ikiwa utakuwa una wazo la kutanua soko lako kila wakati. Kwa mfano, kama umekuwa ukiuza bidhaa zako ndani ya mtaa mmoja, ni vyema ukafikiri namna ya kuzipeleka na mtaa wa pili. Kwa wazo hilo litakusaidia sana  kukuza biashara yako kwa viwango vya juu.

Jenga mtandao wa kukuza biashara yako.
2. Pata maarifa ya biashara.
Kila wakati inabidi ujifunze kuunoa ubongo wako na kujifunza sana juu ya biashara unayoifanya. Maarifa ni muhimu sana katika kuikuza biashara yako, vinginevyo biashara hiyo ni lazima itadondoka. Hivyo, unatakiwa kujisomea vitabu au kuhudhuria semina mbalimbali za kibiashara ili kufanikisha hilo.
3. Toa huduma za ziada.
Unaweza ukaifanya biashara yako ikakuwa na kuwa ya mafanikio ikiwa utajifunza kutoa huduma za ziada. Kwa mfano, unaweza ukawapa wateja wako zawadi ndogo ndogo kila wanaponunua bidhaa. Hilo litawasaidia kuwavuta na kujikuta ukikuza biashara yako siku hadi siku.
4. Tengeneza mtandao wa kibiashara.
Huwezi ukasema unakuza biashara yako na kusahau kukuza mtandao wako wa kibiashara. Ni lazima kujitengenezea ‘netwek’ na wafanyabiashara wenzako ya kukusaidia kukufanikisha. Hilo litakusaidia katika kutatua changamoto na wakati mwingine hata kukuza bidhaa kwa urahisi.
5. Boresha bidhaa zako.
Mwisho, ili uweze kukuza biashara yako, kwa vyovyote vile unalazimika kuboresha bidhaa zako. Kila bidhaa unayoitoa ni lazima iwe ya viwango vya juu. Kwa hali hiyo itapelekea utapata wateja wengi kila kukicha  na kusababisha biashara yako kuweza kukua.
Ikumbukwe kwamba kutanua soko, kupata maarifa ya kibiashara, kutoa huduma za ziada, kutengeneza mtandao na kuboresha bidhaa kila wakati, ni moja ya mawazo muhimu ambayo unatakiwa kuwa nayo kila siku ili kukuza biashara yako.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku. Ila hakikisha unawashirikisha wengine waweze kujifunza zaidi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,

Aug 17, 2016

Vitu Ambavyo Wengi Hujutia Sana Wanapofika Uzeeni.

No comments :
Naamini wote tunajua tunazaliwa, tunakua na ipo siku tutakuja fikia uzeeni. Hivyo kila mtu kwa kujua hilo, hujitahidi sana kuishi maisha ambayo hatakuja kuyajutia kwa hapo baadae akifika uzeeni. Kwa kifupi, kila mtu anapenda uzee wake uwe mzuri ambao hauna lawama.
Hakuna ambaye anapenda aje achekwe na watoto au wajukuu zake eti kwa kutotimiza majukumu fulani. Kila mtu anapenda watoto au wajukuu zake wamsifie kwamba kweli babu enzi za ujana wako  ulifanya makubwa. Hilo ndilo kila mtu analolitamani litokee katika uzee wake.
Lakini hata hivyo kwa wengi waliofikia uzeeni kile wanachokitamani kiwe, huwa hawakipata kwa sababu kadhaa. Hujikuta wakiishi maisha ya kujuta sana. Majuto hayo hutokana hasa na mambo ambayo waliyafanya wakiwa vijana na kupelekea pengine maisha yao kuwa magumu.
Sitaki uwe miongoni mwa watu ambao wakifika uzeeni uje ujute kwa kulia sana. Leo nanawa mikono kwa kukuonyesha vitu vya msingi ambavyo wengi huvijutia sana kila wanapofika uzeeni. Sasa basi, vitu hivyo ambavyo wengi huvijutia sana hasa wanapofikia uzeeni ni kama hivi vifuatavyo;-.
1. “Kwa nini nilipoteza muda sana?”
Kati ya jambo la wazi ambalo wengi waliofikia uzeeni wanalojutia ni kule kupoteza muda. Huwa ni watu wa mawazo sana kutokana na lawama ambazo wanazipata kutoka kwa jamii, watoto au wajukuu zao.
Mara nyingi lawama hizi huelekezwa ni kwa nini maisha yao yako hivyo. Maswali kama babu ulikuwa wapi wakati wnzako wanawekeza huulizwa sana. kwa hali kama hiyo suala la kupoteza muda hujutiwa sana na wengi wakiwa uzeeni.

Wengi hujuta sana kwa kupoteza muda wao.
2. “Kwa nini sikuwekeza mapema?”
Si kupoteza muda tu ambapo wengi wanapofikia uzeeni hujutia. Ila wakati mwingine wanajuta kwa nini hawakuwekeza mapema wakati wa ujana wao. Hujiuliza maswali mengi kwa nini hawakununua mashamba, hawakujenga nyumba, au kwanini hawakufanya uwekezaji wa maana?
Hayo yote huibuka mara baada ya kujiona wao wapo mikono mitupu na hawana nguvu tena. Kilio, sononeko na majuto yanakuwa makubwa sana, hali ambayo inaweza kupelekea kupata magonjwa yasiyotarajiwa kama shinikizo la damu.
3. “Kwa nini sikuishi kwa kufuata ndoto zangu?”
Hili pia huwa ni jambo linaloleta majuto hasa kwa wengi wanaopofikia uzeeni. Kitu ambacho hujiuliza kila wakati kwa nini waliishi maisha ya kutimiza ndoto za watu wengine, badala ya kukaa chini na kutimiza ndoto zao. Hapa huwaza sana je, kipindi hicho walikuwa wamerogwa.
Hapa walio fikia uzeeni hujiona wana hatia na makosa makubwa sana ambayo waliyafanya wakiwa ujanani. Ukweli wote huo wanakuja kuujua baada ya kugundua kumbe hakuna hata kitu cha maana walichokifanikisha duniani zaidi ya kufanikisha ndoto za wengine na kusahau za kwao.
4. “ Kwa nini sikuwasaidia wengi kutimiza ndoto zao?”
Pia hufika mahali wale waliofikia uzeeni hutambua kwamba upo umuhimu mkubwa sana wa kuisaidia jamii, hata kwa kidogo walichonacho. Lakini kila wakiangalia hakuna msaada wa maana walioutoa. Hapo sasa ndipo huanza kuumia na kuwaza mengi.
Kiuhalisia, huwa ni kipindi kigumu sana. Hapo ndipo unapoona wanajaribu kutoa angalau msaada lakini inakuwa inashindikana kwa sababu pengine hawakujiweka vizuri kiuchumi. Majuto ya kutokuwasaidia wengine huwaumiza sana pia.
5. “Kwa nini sikujituma sana? ”
Wapo wengine ambao hujita na kujilaumu kwa sababu ya kuona kwamba walitakiwa kujituma sana hadi kufanikiwa. Sasa wanaona hawajafanikiwa na wanajua wazi hilo ni kosa lao. Kila wakati wanapata shida na kujiuliza kwa nini hawakujituma sana ili kujenga maisha mazuri zaidi.
Ikiwa kweli una kiu kubwa ya kutaka uzee wako uonekana wa maana, basi unalazimika kujituma sana kwenye kila jambo unalolifanya. Ikiwa hutajituma na kuweka misingi imara wakati ukijana, sahau kuwana mafanikio uzeeni na zaidi utalamikiwa na kujutia uzee wako wako wote.
 6. “ Kwa nini sikuishi na familia yangu kwa upendo?”
Haya ni majuto huwa yapo wale wazee ambao kila wakikumbuka waliishi na familia kwa migogoro mibgi sana. pi hali hiyo ilipelekea hata kutengana na kujikuta wakiziacha familia zao zikiteseka.
Sasa inapofika kipindi chha uzeeni hujikuta wakijuta na kujilaumu ni kwanini hayo yote yalitokea. Ni kwa nini hawakuweza kuaysuluhisha mapema na kusababisha mgogoro ambao unawasumbua hapo wakiwa uzeeni.
Kwa kawaida unapokuwa kuwa kijana unaweza ukafanya makosa mengi na ukayachukulia kawaida. Lakini inapofika uzeeni ndio unaanza kuelewa kwa nini ulikosea kufanya hivyo.
Maisha yako yapo mkononi mwako, kama bado una nguvu, jifunze kuwajibika ili baadae usije ukajuta kwenye maisha yako ya uzeeni. Ukiangalia kwa ufupi hayo ndio baadhi ya mambo ambayo wengi hujutia wakifikia uzeeni mwao.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,


Aug 16, 2016

Mambo Ya Kuzingatia, Ili Kuifanya Akili Yako Ifanye Kazi Kwa Ufasaha Na Mafanikio Makubwa.

No comments :
Naamini katika maisha, huwa inafika mahali kila mtu anatamani akili yake ifanye kazi vizuri na imletee mafanikio makubwa. Lakini hata hivyo, pamoja na matamanio hayo wengi bado huwa hawajui wafanye nini au wachukue hatua zipi ili kuweza kuipa akili nguvu zaidi kila siku na kufanya kazi kwa ufasaha.
Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, baada ya kufanya utafiti kwa muda, walikuja kukaa chini na kuweka vigezo ambavyo kwa mtu akiviafuta basi ni ni lazima akili yake iweze kufanya kazi vizuri zaidi na kwa mafanikio. Moja ya vigezo walivyoviweka kama unataka akili yako ifanye kazi vizuri ni kama hivi vifuatavyo:- 
1. Chakula bora.
Ili akili yako iweze kufanya kazi vizuri sana, inahitaji kwa kiasi kikubwa chakula bora, chenye virutubisho muhimu. Kwa mfano, tafiti nyingi zilizofanywa kitaalamu zinaonyesha vyakula vya jamii ya samaki ni muhimu sana katika kuipa akili yako afya ya kufanya kazi vizuri.
Hata hivyo utafiti huo haukuishia hapo tu, unazidi kufafanua mara nyingi, watoto wanao tumia vyakula jamii ya samaki sana huwa pia wana uwezekano wa kufanya vizuri hata darasani. Hivyo unaona, chakula bora ni muhimu sana katika kuipa akili yako nguvu ya kufanya kazi vizuri.

2. Mazoezi.
Kati ya kitu rahisi ambacho hakiwezi kukugharimu sana lakini ikiwa utakifanyia kazi na kitaifanya akili yako ifanye kazi vizuri, ni mazoezi. Mazoezi yana uwezo mkubwa sana wa kuipa akili yako nguvu kuliko. Wengi wanaofanya mazoezi, akili zao zipo vizuri.
Unaweza ukachukua jukumu leo la kuifanya akili yako ikafanya kazi vizuri kwa kuamua kufanya mazoezi. Pengine unaanza kuwaza unaanzia wapi? Kama ni hivyo usipate shida. Dakika 20 kwa siku iwe jioni au asubuhi zinakutosha kabisa kuifanya akili yako ikawa na afya bora.
3. Fanya kazi za kujitolea.
Si kila wakati kazi unayofanya ni lazima ikupe malipo. Kuna wakati kubali kujitolea kufanya kazi za jamii tena bure. Unapofanya kazi kama hizi kikawaida kunakufanya ujisiie vizuri na mwisho wa siku akili yako nayo inaanza kufunguka na kufanya kazi vyema hivyo hivyo.
Naona unashangaa katika hili, sikiliza. Wewe ni matokeo ya jamii uliyopo. Kwa mujibu wa kanuni za maumbile ili uweze kufanikiwa ni lazima uirudishie jamii yako kitu fulani kama shukrani. Sasa mojawapo ya vitu hivyo, ndio kazi kama hizi angalau mara moja moja. Ukifanya hivyo ujue kabisa akili itaanza kufanya kazi vyema.
4. Pata usingizi wa kutosha.
Pia usingizi wa kutosha kimetajwa kama ni kigezo kimojawapo cha kuifanya akili yako kufanya kazi vizuri. Inasemakana akili yako ili iweze kufanya kazi vizuri angalau unatakiwa kupata usingizi usiopungua angalau saa nane kwa siku.
Najua hili unalijua vizuri, lakini je huwa unalizingatia? Kama huwa ulizingatia sana, kuanzia sasa litilie mkazo na kuhakikisha lazima akili yako inapumzika na kuipa nguvu ya kufanya kazi vizuri upya kwa siku inayofuata. Ukifanya hivyo ni lazima akili yako ifanya kazi kwa ufasaha, utake au sitake.
5. Jisomee kila siku.
Chakula bora peke yake hakitoshi kuipa akili yako nguvu ya kufanya kazi kwa ufasaha. Kitu cha ziada ambacho kingine unatakiwa kukiongeza ni kujisomea. Akili inayojisomea inakuwa ina nguvu sana ya kufikiria na kufanya mambo kwa ubora.
Najua hili la kujisomea ni shida kwa wengi, lakini hakuna namna nyingine ya kuifanya akili yako ikawa ina nguvu ya kuteda kwa ubora, zaidi ya kujisomea. Unapojisomea unakuwa unaufikirisha ubngo na kuupa changamoto na mwisho wa siku unajikuta umefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Kwa kumalizia makala haya, tambua hayo ndiyo mmbo ya msingi ambayo yamezungumzwa na wataalamu kwamba yanaweza kuipa akili yako nguvu ya kufanya kazi kwa ufasaha.
Chukua hatua sitahiki za kubadili maisha yako na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 048035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Aug 15, 2016

Mambo Mawili Ya Kuzingatia Sana Ili Kufanikiwa

No comments :
Kitu kimojawapo kikubwa kinachotofautisha watu wanaofanikiwa na wale wanaoshindwa kwenye maisha ni MATENDO ama ACTION kama wenye lugha zao wanavyopenda kuita.

Haijalishi unajua nini, haijalishi unasema nini wala haijalishi una uelewa mkubwa kiasi gani! Hivyo vyote unavyojua na kusema, kama huchukui hatua ni sawa na kelele na havitaweza kukusaidia katika safari yako ya mafanikio.

Mafanikio ya kweli kwenye maisha yako siku zote yanakuja, ikiwa utajua kile unachotaka na kuchukua hatua za kuelekea kwenye mafanikio yako kila siku. Hapa ndipo mafanikio yako yanapoanzia.

Bila kuchukua hatua, halafu ukasema eti unatafuta mafanikio, hiyo itakuwa ni sawa na kujidanganya mwenyewe mchana kweupee.

Kitu cha kufanya na kukumbuka kila siku ikiwa unataka kufanikiwa na kujitofautisha na wale walioshindwa ni KUCHUKUA HATUA KILA SIKU, HATA KAMA NI KIDOGO bila kusahau kujua kile unachotaka.

Ukijua kile unachotaka na kuamua kuchukua hatua, hapo utakuwa upo kwenye njia sahihi ya kukamata mafanikio yako. Mambo mengine ya kukusaidia kufanikiwa kama kufanya kwa ubora, nidhamu binafsi au uvumilivu yatakuja yenyewe, lakini ikiwa utajua unachokitaka na kuchukua hatua.

Haya ni mambo mawili muhimu sana ambayo ukiyazingatia ni lazima ufanikiwe. Hata kama uliwahi kuitwa huwezi kufanikiwa tena, kilaza au eti una uwezo mdogo, Lakini ukizingatia kujua kile unachokitaka na kuchukua hatua, mafanikio ni yako.

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi. Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.

Nakutakia kila la kheri,

Imani Ngwangwalu.



Aug 10, 2016

Hii Ndiyo Dozi Sahihi Ya Maisha Yako Ya Mafanikio.

No comments :
Mara kadhaa unatakuwa umekuwa shahidi kwa namna moja ama nyinyine kwa kuona ya kwamba mtu akiumwa ni lazima atafute matibabu ili aweze kupona ugonjwa  ambao unamsumbua.
Hivyo hivyo mtu huyo akipewa dawa  anatakiwa kuzitumia katika utaratibu ambao unaeleweka ili aweze kupona, utaratibu huo ndio ambao huitwa dozi, dozi hiyo lazima mtu aifuate ili aweze kupona na endapo atatumia kinyume  na alivyoelekezwa na mtalamu upo uwezakano mkubwa kuweza hudhurika zaidi au kupoteza maisha.
Kama ilivyo kwa mgonjwa ili aweze kupona na kuimarika vizuri katika afya yake hana budi  mgonjwa huyo kuweza kufuata utaratibu wa kutumia dozi ili aweze kupona.
Hata kwenye safari yako ya mafanikio ndivyo ilivyo, unahitaji kupata dozi, dozi ambayo ina misingi na utaratibu wake wa kuitumia. Wengi wetu tunamani kupata mafanikio kwa haraka zaidi, huku tukisahau ya kwamba mafanikio ni hatua kwa maana ya kwamba ni lazima tumalize dozi ndipo tupate mafanikio hayo.
Hivyo nakusihi uweze kufuatana nami ili uweze kujua namna ya kuweza kupata dozi ya mafanikio yako, pia suala si kupata dozi  tu, bali uzitumie katika maisha yako, na si kuzitumia tu bali  uzitumie ili upone ugonjwa wa dhiki,  shida na taabu za kimaisha ili uweze kupata mafanikio yako.
Vile vile nisisitize kwa kusema ya kwamba ili uweze kufika ambapo unataka ya kwenda kwa maana ya kupata mafanikio huna budi ya kuamini na kuwa mvumilivu na mbunifu wa hali ya juu  sana.
Ifuatayo ndiyo dozi sahihi ya safari yako ya mafanikio.
1. Angalia matumizi yako ya muda katika kutekeleza malengo yako.
Ipo haja leo ya kujua mambo ambayo yatakusaidia kuweza kutimiza malengo yako. Watu wengi huwa tunakosea sana hasa katika kujali na kuzingatia muda wa kutekeza mambo yetu.
Kwa mfano watu wengi licha ya kuwa na malengo huwa hatuweki ni kwa muda gani ndoto yako itakuwa imekamilika. Mfano ili uweze kufanikiwa na kutimiza malengo yako, kwa mfano unataka kuwa mfanyabiashara fulani ni lazima ujue ni muda gani  utakuwa umetiza jambo lako. Hii ni muhimu sana kuzingatia.

Hata hivyo kuwa na maono ya muda (time limit)kwa kila jambo lako itakusaidia kuweza kujua ni kwa namna gani utakuwa umetiza lengo lako.  Hivyo nakusihi kwa  kila jambo lako ambalo unatamani kulifanya kwa hapo baadae ni lazima uwe umelipanga  ni baada ya muda gani  lengo hilo litakuwa limekamilika. Pia mara kadhaa endelea kukumbuka msemo ule mtamu wenye kukutia hamasa ya kwamba ni ‘muda ni mali’ hivyo huna budi kulizingatia hilo.
2. Jifunze kutoka kwa watu walifanikiwa huku na wewe ukitumia njia ambazo ni za tofauti.
Mara kadhaa tumekuwa ni watu kulamika sana hasa pale ambapo tumefeli kwenye jambo fulani. Kulalamika huku mara kadhaa nimegundua ni kwa sababu kuu moja ya  kwamba tumejifunza kwa watu ambao wamefeli.
Lakini kufanya hivi mara kadhaa hutupa picha ya kwamba hata sisi hatuwezi hii ni kutokana mtu fulani alifeli. Kufeli kwa mtu  mwingine katika jambo lake kwa asilimia kadhaa hutengeneza hofu ndani yetu, hofu hiyo ni ile hofu ambayo utajiona ya kwamba hauwezi.
Hata hivyo kama unataka kupata mafanikio jambo la kuzingatia ni kwamba unatakiwa kupata ushauri kwa watu sahihi ambao wamekwisha fanikiwa kufanya hivi inakusaidia kwani wao wana taarifa sahihi kuhusiana na jambo hilo.
Kwa mfano unataka kufanya biashara ya kuuza chipsi ukiomba ushauri kwa mtu ambaye anauza mkaa, muuza mkaa huyo atakwambia biashara hiyo ina hasara sana, lakini sababu hizo sio za kweli kwa sababu hana taarifa sahihi, hivyo kama unataka kuuza chipsi ni lazima uweze kumfuata mtu ambaye amefanikiwa katika biashara hiyo kwani mtu huyo anazo taarifa kamili juu ya biashara hiyo.
Hivyo nakusihi ili uweze kupata mafanikio huna budi kuayazingatia hayo kwa hali ya juu sana, hasa katika suala la utekelezaji, kufanya hivyo kutukufanya uweze kuwa mshindi wa maisha yako. Endelea kufuatana nami katika safu hii kila wakati.
 “Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi” kwa kuendelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila siku.
Ndimi; afisa mipango Benson Chonya


Aug 9, 2016

Kinachowaathiri Wafanyabiashara Wengi Na Kufanya Biashara Hizo Kufa Ni Hiki.

No comments :
Siku zote kumbuka ya kwamba biashara ni mchakato, ninapozungumzia mchakato ni maana ya kwamba kuna kupanda na kushuka. Hapa nikiwa na maana ya kwamba kuanzisha biahara ni rahisi sana, ila endapo biashara hiyo ikifa kurudi tena katika kufanya biashara hiyo huwa ni vigumu sana.
Zipo baadhi ya sababu ambazo zinawafanya wafanyabiahara wengi wayumbe sana hasa katika biashara ambayo wanayofanya, najua wakati unaendele kusoma makala haya bado unashangaa ya kwamba nazungunza na nani?
Usishangae nazungumza na wewe, huenda ukawa unafanya biashara au haufanyi. Nazungumza na wewe ili uweze kuepukana na mambo ambayo yanafanya au yatafanya biashara yako ife.
Zifuatazo ndizo sababu ambazo zinawawathri wafanyabiashara wengi.
1. Kukosekana kwa elimu ya jinsi ya kukabiliana na ushindani katika soko.
Zipo biashara ambazo zinakuwa au ambazo tayari zimekwisha kua ambazo mara nyingi huwa zinateteleka kwa namna moja ama nyingine hasa linapokuja suala la ushindani wa bidhaa au huduma katika soko.
Wafanyabiashara walio wengi huwa wanakuwa na mtazamo mmoja tu. Mtazamo huwa ndio ambao unakuwa unawaathari kwa asilimia kubwa sana. Mtazamo huo huwa katika suala la mfanano wa utoaji wa huduma.
Kwa mfano unakuta bidhaa ambayo utanunua mahali fulani, ubora na wingi wa bidhaa vinafanana na mfanyabiashara/wafanyabiahara wengine. Kufanya hivi kunafanya kuwepo kwa kutoeleweka ni nani mmiliki au mwazilishi au huduma imenunuliwa kwa nani!

Hivyo ifike mahali kila mmoja wetu ambaye anafanya biashara kuwe na utofauti kati mfanyabiashara mmoja na mwingine, maana kufanya hivyo kutakutofautisha katika kutambulisha huduma au bidhaa kwa mteja.
Vilevile huna budi kuwa na utofauti na wengine kwa kuwa mbunifu katika biashara. Katika ulimwengu huu wa dunia ambayo inaenda kasi kuliko neno lenyewe huna budi kutumia teknolojia katika kujifunza kufanya biashara tofauti na watu wafanyavyo sasa.
Hata hivyo siri ya mafanikio ya kibiashara iliyojificha ni kwamba huna haja ya kuongeza mtaji mkubwa katika biashara ila inakupasa kuweza kuongeza thamani katika biadhaa au huduma.
Kwa  Mfano badala ya kuuza samaki ambao wateja wamezoea kwa shilingi elfu moja unaweza ukatumia teknolojia ya kuwakausha samaki, na kufunga katika vifungashio vizuri na kuuza samaki yule yule ambaye ulikuwa unamuuza kwa shilingi elfu moja na wewe ukaja ukamuuza kwa shilingi elfu tano.
Kufanya hivyo ndipo ninapozungumzia katika biashara yeyote ambayo unaifanya, fikiri kwa umakini sana na kwa jinsi gani unaweza ukaongeza thamani ya bidhaa au huduma kama ulivyoona kwa mfano wa biashara ya samaki hapo juu.
2. Kuwa na mtazamo hasi juu ya watu wanaokuzunguka kibiashara.
Biashara nyingi huwa hazikuwi au hufa kabisa hii ni kutokana na kuwa na mtazamo hasi juu ya mambo ambayo tunayafanya katika kibiashara. Watu wengi hususani watu ambao wanafanya biashara huwa ni ubinafsi sana.
Ubinafsi huu ndio ambao unazidi kujenga uhasama kwa asilimia kubwa hasa kwa wafanyabiashara wengine ambao wanakuzunguka. Ubinafsi huo ni kama ufutao.
Kwa mfano unaweza ukaenda sehemu fulani kununua bidhaa za jumla ila ghafla unakuta mtu huyo hana bidhaa fulani ila anajua kwamba jirani yake bidhaa hiyo anayo kutokana na ubinafsi wa kibiashara mfanyabiashira huyo hawezi kumuelekekeza mteja bidhaa hiyo atapata wapi? Zaidi ya kumwambia kaishiwa.
Au  mfanyabiashara huyo hawezi kwenda kumfuatia mteja bidhaa au huduma kwa jirani yake. Sasa kwa staili kama hiyo tutafanikiwa kweli? Hivyo wito wangu kwako ni kwamba ni lazima uwe na ushirikiano wa kutosha baina yako na wafanyabishara wengine ambao wanaokuzunguka.
Kufanya hivyo kutafanya kukuza biashara yako hasa katika ongezeko kubwa la wateja. Watu wengi hufanya hivi huku wakiamini ya kwamba kufanya hivi ni kuibiwa wateja wako  ila ukweli ni kwamba kufanya hivyo ni kuongeza makuzi ya kibiashara na kuongeza wateja kwa ujumla.
“Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi” kwa kuendelea kujifunza kupitia mtandao wako wa DIRA YA MAFANIKIO kila siku.
Ndimi; benson chonya

0757909924

Aug 8, 2016

Sumu Inayoathiri Mafanikio Ya Wengi.

No comments :
Uliwahi kukaa chini na kujiuliza hivi ni kwanini baadhi ya mambo mengi hufeli zaidi kuliko kuwa katika ubora ambao mtu ametarajia? Kama hujawahi kujihoji ipo haja zaidi ya kuushirikisha ubongo wako muda huu katika kuyafakari hayo ili kujua kwa undani zaidi.

Watalamu wa saikolojia wanazidi kututabainisha ya kwamba uwezekano mkubwa wa jambo lolote ambalo unalitaka kulifanya au unalifanya upo uwezekano wa matokeo yake yasiwe kama vile ambavyo ulitarajia awali.

Hata hivyo watalaamu hao hao wanazidi kutukumbusha ya kwamba mambo mengi huwa yanafeli zaidi kuliko kuwa bora hii ni kutokana kutokuwepo kwa hamasa ya kutosha aliyo nayo mtu katika kulitenda jambo fulani. 

Hamasa hii imsukumayo mtu katika kulitenda jambo fulani, ndiyo sumu ambayo inayaathiri mafanikio ya wengi wetu kwa kiwango kikubwa sana. Ukichunguza kwa makini katika safari yeyote ya kuyasaka mafanikio mwanzoni huwa ni safari yenye utamu mwingi kuliko uchachu.

Utamu huo ambao nauzungumzia ni kwamba kila mtu wakati anaanza kulitenda jambo fulani huwa yupo katika hali ya kulipenda sana jambo hilo, hata hivyo ndipo tunapoona ya kwamba hamasa isukumayo mtu katika kulitenda jambo hilo huwa kubwa sana.


 Lakini pamoja na hamasa hiyo kuwa  kubwa huanza kupungua siku hadi siku, hii hutegemea na kiwango cha changamoto ambazo zitajitokeza. Hebu tujikite kidogo kwa kuona baadhi ya mifano itakayotusaidia kutafakari hili kwa undani zaidi.

 a) Hebu tujiulize ni mahusiano mangapi leo hii yamekufa? Huku mitazamo ya watu wengi hawakutegemea kama mahusiano hayo yatakufa?

b) Ni biashara ngapi ambazo zilianza vizuri lakini kadri siku zinavyozidi kusonga nazo zinalegalega?

c) Ni wanafunzi wangapi ambao leo wameacha kuendelea na masomo yako lakini mwanzoni wakati wanaanza masomo walikuwa wanafanya vizuri? Achilia mbali sababu za  kutokuwapo na fedha kwa masomo bali jikite zaidi katika kutafakari sababu zile za kawaida kabisa. 

c) Jiulize tena kwanini mara nyingi vipaji vingi vya watu hufa kadri siku zinavyozidi kusonga mbele? 

Kwa hayo machache kati ya mengi  ambayo umeyatafakari au unatakiwa kuyatafakari utagundua sababu za kufeli kwake ni Kutokana na muhusika huyo kukosa hamasa ya kupenda jambo hilo.

Lakini vilevile zipo changamoto kubwa na nyingi ambazo hujitokeza katika jambo hilo. Na kutokea kwa changamoto hizo ndizo ambazo zikekuwa sumu kubwa sana ambazo zinawafanya watu wengi kukakata tamaa mapema.

Nini kifanyike ile kuongeza hamasa za kiutendaji ili kufanikiwa?

1. Lifanye jambo lolote kwa upendo na sio kwa hofu au kwa kujaribu.

Upendo wa jambo lolote ambalo unalifanya linakufanya wewe kuweza kuwa katika hali ya ushindi wa mafanikio yako. Kupenda kitu kunakufanya kujua mbinu ambazo zitakusaidia kukabiliana na changamoto ambazo zitajitokeza.

Kwa mfano kama unataka kukua kibiashara lazima ipende kwa dhati biashara yako lakini ukiweka chuki kati yako na biashara yako biashara nayo itaweka chuki nawe, na kufanya hivi ni kutengeneza mazingira ya kufa kwa biashara yenyewe.

2. Zifanye changamoto kama njia za kukifikisha kwenye lengo lako.

Kila jambo lolote lina changamoto zake hivyo huna budi kuziogopa changamoto hasa chamgamoto zitakazokufanya ushindwe kufika kwenye Ndoto zako kubwa.

Jambo la msingi zifanye changamoto kama njia ya kufika kule utakako, Huna haja ya kuacha kufanya jambo lolote lenye kukuletea mafanikio ambalo unalitaka kulifanya kwa sababu  ambazo sio msingi katika kukamilisha Ndoto zako.

3. Fanya kitu ambacho unakiogopa.

Ili uweze kufanikiwa huna budi kutokugopa kufanya jambo lolote. Kuacha au kugopa kufanya jambo lako ni dalili tosha kwamba huna hamasa za kiutendaji pia kufanya hivi kunakufanya kwa asilimia kubwa kuweza kufa na ndoto zako.

Lakini nikukumbushe ya kwamba idadi kubwa ya watu ambao wamefanikiwa katika sayari ni kwamba walifanya vitu ambavyo walikuwa wanaviogopa na mambo hayo ndiyo yaliyosaidia kugeuza maisha yao kwa asilimia kubwa. Na watu hao wenye mafanikio huwa hawasimamishi masikio yao kusikiliza nani kasema nini, hususani wale wakatishaji tamaa. Tabia hii ya watu walifanikiwa ukiitumia leo itakusaidia sana.

Hivyo nikutie moyo kwa kukwambia ya kwamba ndoto zako zinakwenda kuwa kweli endapo utakwenda kuijenga misingi imara ya hamasa za kiutendaji kwa jambo lolote lile ambalo unalifanya au unataka kulifanya.

"Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi" kwa kuendelea kutembelea mtandao huu wa Dira ya mafanikio.

Ndimi; afisa mipango Benson Chonya.