google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 31, 2017

Nguvu Ya Nidhamu Binafsi Katika Kufikia Malengo Yako.

No comments :
Ili kufikia mafanikio yako, kati ya kitu ambacho kinahitajika sana ni uwezo wa kujenga nidhamu binafsi ambayo inaweza kukuongoza hadi kuweza kufikia malengo yako. Wapo watu ambao wanakwama sana kutokana na kukosa nidhamu binafsi ambayo inatakiwa iwaongeze katika kufikia malengo yao.
Hivyo hapa unaona, nidhamu binafsi siku zote inasimama kama daraja la kuunganisha pale ulipo na kule unakotaka kufika kutokana na malengo uliyojiwekea. Hiyo ikiwa na maana kwamba, kama huna nidhamu binafsi huwezi kufikia malengo hayo, maana utakuwa ni kama mtu ambaye anayebomoa daraja lako mwenyewe.
Kila unapojiwekea malengo yako ya aina fulani na kisha ukaamua kuweka nidhamu binafsi ya kuyafanyia kazi malengo hayo kila siku hata kama kwa kidogo sana, uwe na uhakika ni lazima utafanikiwa. Kitachokufanikisha hapo ni nidhamu binafsi uliyonayo, hasa ya kuweka juhudi kila siku ambapo umeamua kuiweka.

Unapojiwekea nidhamu binafsi ya kitu chochote na kudhamiria kwamba hutafanya kitu hiki au kitu kile mpaka malengo yako ya aina fulani yatimie, utakuwa upo kwenye uwezekano mkubwa sana wa kutimiza malengo yako. Ila unapokuwa unakosa nidhamu binafsi ni rahisi sana kuweza kushindwa.
Kuanzia leo amua kuweka nidhamu kwenye kila eneo. Weka nidhamu kwenye eneo la pesa, hakikisha pesa zako hazipotei hovyo. Weka nidhamu binafsi kwenye kazi yako. Weka nidhamu kwenye matumizi ya muda wako, ili uutumie kwa faida. Kila eneo muhimu liwekee nidhamu binafsi na utapata matokeo mazuri.
Hata hivyo ukumbuke unapojiwekea nidhamu binafsi sio adhabu au unajitesa. Huwezi kufanikiwa kama unaishi maisha kama unavyotaka wewe. Ipo misingi ambayo unatakiwa uifate ili kufanikiwa ikiwa na pamoja na swala la kujiwekea nidhamu binafsi. Kufanikiwa kwako kutakuwa lazima kama utafata nidhamu hii.
Ndio maana usishangae kuona watu wengi wanashindwa katika maisha, hii sio kwa sababu hawana uwezo au vipaji, yote hiyo ni kwa sababu ya kukosa nidhamu ndogo ndogo ambazo zingeweza kuwaongza katika kufikia mafanikio yao. Ukijiwekea nidhamu binafsi, tambua utafanikiwa tu, hakuna ubishi.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




Aug 30, 2017

Hapa Ndipo Mafanikio Yako Makubwa Yanapoanzia.

No comments :
Ni rahisi kuwaza na kutafuta sana pale mafanikio yako makubwa yanapoanzia. Hata hivyo pamoja na kuwaza huko kote bado wengi wanazunguka, hawajui sana mafanikio yao makubwa yanaanzia wapi?
Leo kupitia makala haya, nataka nikuonyeshe chanzo cha mafanikio yako makubwa yanaanzia wapi. Ni ngumu sana kuweza kufanikiwa na kufika ngazi kubwa ya kimafanikio kama huelewi vizuri mafanikio yako makubwa yanaanzia wapi.
Kwa kawaida, mafanikio yako makubwa yanaanzia kwenye ile imani uliyonayo juu ya mafanikio hayo makubwa unayoyataka. Hutaweza kufanikiwa sana zaidi ya ile imani uliyonayo. Imani yako ndio kila kitu na dawa ya mafanikio yako makubwa.

Jenga imani sahihi ya kukufikisha kwenye mafanikio makubwa.
Unapokuwa unaamini kwamba unaweza kufikia mafanikio yako fulani, unajikuta kutokana na imani hiyo unaanza kuchukua hatua za kukufikisha kwenye kile unachokiona kwenye akili yako. Imani yako inakuwa inakusukuma kufanya zaidi na zaidi hadi kufanikiwa.
Hapa imani yako naweza nikasema inasimaama kama taa ya kuweza kukuongoza wapi uweze kufika kimafanikio. Hiyo ikiwa na maana kama ukiwa na imani hafifu, imani ambayo siyo kubwa huwezi pia kufanikiwa sana.
Kumbuka ninachotaka hapa unielewe, nazungumzia imani yako kama dawa pekee ya kukufikisha kwenye mafanikio yako. Na unielewe pia hapa sizungumziii tumaini, nazungumzia imani yako.
Ipo tofauti kubwa sana kwa mtu anayeishi kwa matumaini na mtu anayeishi kwa imani. Yule mtu anayeishi kwa matumaini anaweza asichukue hatua yoyote lakini akajipa matumaini atafanikiwa kitu ambacho sio kweli.
Ili kufikia mafanikio uyatakayo, unatakiwa kuwa na imani sahihi ya mafanikio yako. Imani hii tunaweza tukasema ni imani ya kumudu, imani ya kuamini kwamba unaweza kufanya kitu fulani na kweli ukachukua hatua hata kuweza kufanikiwa kwenye kitu hicho kwa uhakika.
Unapokuwa na imani, unakua unaona mambo kwa utofauti, unakuwa unachukua hatua zako kwa utofauti na inakuwa sio rahisi kwa mtu mwenye imani inayooendana na kuchukua hatua kuweza kukata tamaa mapema. Wanaokata tamaa mapema ni wale wanaoishi kwa matumaini sana.
Kipi unachotakiwa kukifanya leo ili kujenga mafanikio yako, ni kwa wewe kujenga imani ya mafanikio. Amini kwamba unaweza kuchukua hatua sahihi, usijaribu kuishi kwenye matumani utakuwa unajitengenezea mazingira ya kushindwa.
Hakuna mafanikio makubwa yanayoanzia nje ya imani uliyonayo. Utafika tu pale kwenye mafanikio yako kutokana na imani inayokuongoza ndani mwako na sio vinginevyo.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Kila la kheri katika kufikia mafanikio  makubwa,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 29, 2017

Kama Unataka Kufikia Malengo Yako Kwa Uhakika, Fanya Mambo Haya.

No comments :

Tambua kile unachokitaka, hapa inabidi uelewe nini unachokitaka. Kama unataka kuongozeza uhuru wa kifedha hilo pia unatakiwa kulijua. Unatakiwa kukijua kile unachokitaka kwa uwazi sana.
Andika malengo yako chini, malengo yasiyondikwa ni kama moshi wa sigara wakati wowote ni rahisi kupotea. Malengo ambayo yameandikwa yanakuwa ya muhimu kwenye akili na utendaji unakuwa rahisi pia.
Weka tarehe ya mwisho kufikia malengo yako, kama ni malengo makubwa weka tarehe ndogo ndogo za kukamilisha malengo yako. Unapoweka tarehe hiyo akili yako inakuwa inafanya kazi kwa nguvu sana kuhakikisha malengo yanatimia.
Andika orodha ya mambo yatakayokusaidia kutimiza malengo yako, hapa andika watu, maarifa unayohitaji na hata vizuizi ambavyo vinaweza kujitokeza na jinsi ya kuviepuka ili ufanikiwe.
Weka orodha ya vipaumbele vyako, vipaumbele vinakusaidia kujua kipi cha muhimu na kipi ambacho sio cha muhimu katika kutimiza ndoto zako. Hutaleta mchezo ukishawea vipaumbele vya malengo yako.
Chukua hatua haraka sana, usichelewe katika kuchukua hatua, kuahirisha mambo ni adui mkubwa sana wa ndoto zako na unapoahirisha mambo kila wakati ni sawa na kujiibiwa mwenyewe kwenye maisha yako.
Fanya kila siku kitu cha kukusogeza kwenye malengo yako, hii ni hatua muhimu sana ambayo inakuhakikishia mafanikio yako. Fanya kitu fulani katika siku saba za wiki, fanya kitu kwa mwaka mzima, utafanikiwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 28, 2017

Utaendelea Kubaki Na Maisha Haya Mpaka Lini?

No comments :
Kati ya kitu ambacho unatakiwa ujiulize sana ni hali ya maisha yako uliyonayo sasa. Je, maisha uliyonayo unayopenda au unaishi tu ilimradi siku ziende? Kama maisha uliyonayo kwa sasa huyapendi, swali lingine la msingi, jiulize utaendelea kuwa na maisha hayo mpaka lini?
Je, kuna hatua ambazo unachukua? Je, kuna mikakati ambayo unaiweka ambayo inaonyesha kweli umechoshwa na maisha hayo? Kuendelea kusema tu peke yake bila kuchukua hatua yoyote ya msingi huko nikujichosha wewe menyewe. Unatakiwa uamue mwisho wa ugumu wa maisha yako ni lini?
Hutaki kuamua, basi kaa kimya usiendelee kulalamika au kupiga kelele zisizo za msingi, tayari jibu ambalo tunakuwa nalo kichwani ni kwamba hayo maisha unayoyaishi kuna namna unavyoyapenda, ndio maana hutaki kuchukua hatua sahihi zitakazoweza kukusadia na kukutoa hapo ulipo.

Usitegemee kutakuwa na urahisi katika kutoka hapo ulipo. Mabadiliko yoyote yahitaji nguvu tena nguvu kubwa ili kuweza kubadilisha maisha yako na yakawa na tija. Lakini kama unataka kubadilisha maisha yako halafu ukaendelea kufanya mambo yale yale, hakuna utakachoweza kukibadili.
Kubali kujikana kwa muda kubadilisha kila kitu kwenye maisha yako. Kubali kubadilisha muda wa kufanya kazi, kubali kubadilisha marafiki na hata aina ya maisha unayoyaishi, kinyume cha hapo utaendelea kubaki na maisha hayohayo na ugumu uleule karibu kila siku.
Kila kitu kinawezekana na pia unaweza kubadilisha maisha yako ukiamua kuweka juhudi za lazima. Nini kinachoshindakana kwako? hutakiwi kuwa na maisha magumu wakati wote. Ni wakati wa kubadilisha maisha yako na kuyafanya kuwa bora, hilo litafanikiwa kwa kuchukua hatua na sio kwa kuishia kusoma makala haya tu.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,


Aug 27, 2017

Sababu Mbili Zinazofanya Wengi Washindwe Katika Maisha.

No comments :
Najua unaelewa vizuri kwenye maisha kundi kubwa la watu wanaonekana wameshindwa maisha au wameshindwa kufanikiwa kwa viwango vya juu ukilinganisha na kundi dogo la watu ambalo ndilo limefanikiwa.
Kutokana na matokeo hayo ya kundi kubwa la watu kushindwa katika maisha, kundi hili kihalisia, hujikuta likianza kumwaga sumu sana kwa wengine wanaotaka kwenda juu. Sumu hizi zinaweza zikawa za maneno na kila namna ya kukatisha tamaa.
Kwa hiyo inapotokea unapingwa sana kwa kile unachokifanya, hutakiwi kushangaa wala kuhoji sana, ni kwa sababu unaishi na upo na jamii ambayo imeshindwa sana, sasa kitu cha kujiuliza unafikiri watu hao watakwambia nini zaidi ya kukukatisha tamaa?

Ukiwa na sababu katika mafanikio, utashindwa tu.
Ni ngumu sana kuweza kukwepa kupingwa, kubezwa, na hata kudharauliwa kwamba huwezi kitu ikiwa unaishi kwenye jamii kubwa inayokuzunguka ambayo mafanikio kwao ni msamiati au ni kitu ambacho hakiwezekani.
Kitu kingine ambacho ninatakiwa nikiulize wewe rafiki yangu, hivi umeshawahi kujiuliza nini hasa chanzo au sababu inayopelekea kuona watu wengi wakiendelea kubaki katika hali duni kwa muda mrefu sana? umeshawahi kujiuliza kwa nini hiyo iko hivyo?
Kama hujawahi kujiuliza kwa nini hiyo iko hivyo, leo nataka nikushirikishe sababu au mambo mawili tu ambayo yanawafanya wengi washindwe sana kwenye maisha. Hata kama wewe unafanya mambo hayo na utaendelea kuyafanya, hutakwepa kushindwa.
Jambo la kwanza, ni kuishi kwa kutoa sababu sana/visingizio.
Wapo watu ambao naweza nikasema maisha yao yote wameamua kuwa ni watu wakutoa visingizio. Watu hawa ni wagumu sana kuchukua hatua ila wakiulizwa kwa nini hawajafanya, wanasababu nzuri sana za kujitetea kwa nini hawajafanya hicho kinachotakiwa kufanyika.
Siku hadi siku zinasonga, lakini utawakuta watu hawa wako pale pale, watakwambia hawajawekeza kwa sababu wanasomesha, pia watakwambia hawajawekeza bado wanajipanga na sababu nyingine kama hizo.
Kwa kawaida ili kufanikiwa kila sababu unatakiwa uiweke pembeni, unatakiwa ubaki wewe kama wewe. Kuendelea kuwa na sababu ni kitu ambacho kamwe hakitakuja kukusaidia katika maisha yako zaidi kitakuangusha. Weka sababu pembeni,utimize ndoto zako.
Jambo la pili, kukosa nidhamu.
Mbali na kuishi kwa kutoa visingizio sana, wapo watu ambao wanashindwa kwenye maisha kwa sababu ya kukosa nidhamu. Watu hawa ukichunguza maisha yao karibu yote, hawana nidhamu ya kila kitu.
Utakuta wa ndio wanaongoza kwa kukosa nidhamu ya pesa, wao ndio wanaoongoza kwa kukosa nidhamu ya muda na pia wanaongoza kukosa nidhamu ya kazi. Sasa watu wa namna hii inakuwa ni ngumu au muujiza kwao kufanikiwa.
Kwa kuhitimisha tunaona, mambo makubwa yanayowaangusha wengi kufikia mafanikio ni kukosa nidhamu na kutoa visigizo sana. Ni jukumu lako yashughulikie mambo hayo ili na wewe yasije yakakuangusha kwenye maisha yako.
Nikutakie mafanikio mema na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza maisha na mafanikio kila siku.
DAIMATUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Email; dirayamafanikio@gmail.com

Aug 26, 2017

Kama Utafanya Mambo Haya, Utakumbukwa Wakati Wote Duniani.

No comments :
Yupo mtu mmoja ambaye katika wakati wake aliwahi kusema ‘haijalishi utaishi maisha ya kifahari na kitajiri kiasi gani, ila utakumbukwa tu kwa jinsi ulivyogusa maisha ya watu na wala sio pesa zako’. Ukiangalia kauli hiyo, huo ndio ukweli.
Katika maisha tunayoishi ni kweli vipo vitu ambavyo ukivifanya, ni rahisi kuacha alama ambazo alama hizo zitakumbukwa na vizazi karibu vyote hata ukiwa umekufa. Ni alama hizi hizi ambazo ingetakiwa kila mtu aziache.
Kitu cha kujiuliza je, unaweza ukaacha alama za kukumbukwa na watu duniani, au siku ukifa basi ndio historia imeishia hapo? Majibu unayo wewe, lakini najua kuna watu ambao unawajua historia zao ni kubwa sana mpaka leo, ingawa wamekufa siku nyingi.

Fanya mambo yatakayakufanya ukumbukwe wakati wote.
Labda nikuulize unafikiri walifanya nini watu hao? au unafikiri wanakumbukwa kwa bahati mbaya. Kiuhalisia, yapo mambo ambayo walifanya ndio yanasababisha. Kwa kufanya mambo hayo, hata wewe ukiwa nayo, ni lazima utaacha alama duniani.
Kupitia makala haya ya leo, nataka tuangalie mambo ya msingi ambayo ukiyaendeleza kwa usahihi na ukawa nayo basi elewa kabisa siku ukija kuiacha dunia hii utakumbukwa kwa muda mrefu na hautayeyuka kama moshi.
Jambo la kwanza, mchango ulionao.
Hauwezi kukumbukwa au ukaacha alama duniani kama huna mchango mkubwa kwa jamii unayoishi. Je, maisha yako unayoishi sasa yana mchango kwa wengine? Maisha yako yanaleta unafuu kwa wengine? Je, unaishi kwa kusaidia wengine?
Unatakiwa ukae na kujiuliza maswali mengi na kuangalia kila eneo je, una msaada kwa wanaokuzunguka? Kugusa maisha ya wengine hata kama hauna pesa unaweza kufanya hilo. Ukiweza kugusa maisha ya wengine, utaweza kukumbukwa sana duniani.
Kama unafikiri natania, waangalie watu wote ambao wameacha historia kubwa duniani, waligusa maisha ya watu, ukiangalia kuanzia wapigania uhuru waligusa maisha ya watu wengi ndio maana nwanakumbukwa mpaka leo.
Lakini leo hii ukiwa unataka kuishi kwa ubinafsi, ukabaki wewe kama wewe, nikwambie tu siku ukitoka kwenye hii dunia ndio kwa heri, hauna alama au kumbukumbu ambayo utakuwa umeiacha ya maana, utakufa wewe kama wewe.
Jambo la pili, mahusiano.
Mbali na mchango ulionao je, mahusiano na watu wako wa karibu yakoje? Je, una mahusiano ya kubomoa au ya kujenga. Unapokuwa na mahusiano bora, elewa kabisa unajenga msingi mmojawapo wa kuacha alama duniani.
Faida ya kuwa na mahusiano bora inakusaidia wewe kuwa kiongozi bora wa maisha yako na wengine pia. Hata kama hujachaguliwa kwa kura lakini jinsi unavyowaongoza watu hiyo inatafsiriwa moja kwa moja wewe ni kiongozi kwa maisha ya watu.
Unataka kujenga jina na unataka kuacha alama za uhakika duniani, anza kujenga mahusiano  bora na watu wengine. Jenga mahusiano na watoto, jenga mahusiano na watu wazima, jenga mahusia na kila mtu, utafanikiwa.
Jambo la tatu, tabia.
Mbali na mchango ulionao kwa wengine jambo lingine ambalo linaweza likakupelekea ukaacha alama katika maisha yako ni tabia. Hapa kitu cha kuangalia tabia ulizonazo ni zipi, je zinawafurahisha wengine au kila mtu anakereka na tabia zako?
Haiwezekani ukawa na tabia mbaya na za hovyo halafu wakati huohuo ukawa ni mtu ambaye unategemea ukaacha kumbukumbu kwa wengine. Unapokuwa na tabia njema kama za kusaidia wengine ni wazi utakumbukwa.
Wengi ambao tabia zao ni mbaya sana, huishia kukumbukwa kwa muda tu lakini baada ya hapo husahaulika sana. Hivyo, unaona pia tabia ni moja ya kitu ambacho kinaweza kikamfanya mtu akaacha alama duniani.
Kwa kuhitimisha, ukiangalia kwa kina hayo ndiyo mambo ya msingi yanayopelekea moja kwa moja kwa yeyote kuweza kuacha alama duniani ikiwa atayafanya. Ni jukumu letu sote kuweza kufanyia kazi mambo haya ili tuwe na maisha ya msaada kwa wengine.
Nakutakia mafanikio mema na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza kila siku maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 25, 2017

Maumivu Haya…Yasiwe Sababu Ya Wewe Kushindwa Kabisa Kwenye Maisha Yako.

No comments :
Kwenye maisha kuna wakati unaweza ukawa na maumivu ya kushindwa, kuna wakati unaweza ukawa una maumivu ya kupata hasara, kuna wakati unaweza ukawa una maumivu ya kuachwa na mwenzi wako au hata maumivu ya kuumizwa na chochote.
Maumivu kama haya yapo sana katika  maisha yako na yanapotokea maumivu ya namna hii ni rahisi kukuchanganya na kujiona kama vile umepoteza kila kitu kwenye maisha yako na pia hata ukaona maisha hayana maana.
Kosa kubwa ambalo hutakiwi kulifanya unapopatwa na maumivu haya ni kwa wewe kusimamisha shughuli zingine zikasimama huku ukiwa umekaa ukisikilizia maumivu hayo ambayo umekuwa umeumizwa.

Maumivu yako yasizuie ndoto zako.
Kitu unachotikiwa kuelewa maisha hayasimami, maisha yanaendelea kusonga mbele bila kujali umeumizwa au hujaamizwa. Inapotokea umeumizwa na kitu, acha kusimama au kuomba ‘poo’ endelea kupambana kwa nguvu zote.
Ikiwa itatokea ukakaa chini na kusubiria maumivu yapoe utakuwa ni mtu unayejichelewesha mwenyewe. Najua ni kweli maumivu ya kuachwa au kupata hasara fulani kubwa yanauma tena sana, lakini yasikufanye ukasimamisha shughuli zako.
Endelea na shughuli zako hata kama huku unalia kwa kuugulia hayo maumivu lakini usonge mbele. Ni bora ukawa unasonga mbele kidogo kidogo kuliko kusimama kabisa na kusikilizia maumivu yako.
Ni kitu kibaya sana kuamua kutulia kwa sababu ya maumivu yako. Inapotokea umeumizwa na jambo fulani chukulia jambo hilo kama somo lakini kubali kung’ang’ania kuendelea kumbana na hadi ufikie mafanikio yako.
Hapo ulipo kaa chini angalia ni kipi kinachokuumiza, ni kipi ambacho kimekufanya ukose tumaini kabisa, usichukulie kuumizwa huko wewe ndio basi huna kitu na huwezi tena kufanikiwa, hapana haiko hivyo.
Unayo fursa ya kufanya tena hicho kilichokuumiza na ukakifanya kwa mafanikio makubwa kuliko ya hapo ulipo. Nafasi ya pili ya kurekebisha makosa yako unayo na ukaendelea mbele zaidi.
Lakini hiyo haitoshi hata nafasi ya tatu, nne na tano ya kujirekebisha unayo. Kwa nini ujute na kuamua kukaa chini kabisa. Hebu shika mkono wangu na nyanyuka hapo ulipo na ukafanye kile unachotakiwa kukifanya cha kukupa mafanikio.
Kama nilivyosema maumivu yasiwe sababu ya wewe kushindwa kabisa. Chukulia maumivu hayo kama changamoto. Na kisha amua kwa dhati kutekeleza ndoto zako bila kujali ni nini au kitu gani kinatokea ndani mwako.
Kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza maisha na mafanikio kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Email; dirayamafanikio@gmail.com

Aug 24, 2017

Misingi Mingine Ya Kuzingatia Wakati Unataka Kumjengea Mtoto Wako Nidhamu Ya Kweli.

No comments :
Kumlea mtoto katika nidhamu na maadili ni mojawapo ya jukumu kubwa sana kwa mzazi. Kila mzazi anapenda kumwona mtoto wake akikua katika maadili mema yatakayomsaidia katika maisha yake yote ya kesho.
Kutokana na kiu hii ya kila mzazi kutaka kuona mtoto wake akikua katika maadili bora, hapo sasa ndio kila mzazi huamua kutafuta njia au misingi bora ya kufuata katika kumlea mtoto hadi kuleta mafanikio.
Najua zipo njia nyingi au misingi bora ya kumlea mtoto hadi kuwa katika maadili bora. Lakini leo nataka tuangalie misingi mingine ambayo unaweza kuifuta na kumlea mtoto na kumjengea maadili bora kabisa.
Tunajifunza misingi hii bora kwa sababu, usipojua njia bora mapema ya kumlea mwanao unaweza kujikuta umekuwa kama polisi kwa mtoto wako na kupelekea mtoto hata kukukimbia bila sababu na kuona nyumbani pa chungu.
Bila ya kupoteza muda, hebu tuangazie dondoo kadhaa za kutusaidia mimi na wewe kuweza kujenga msingi imara katika malezi ya watoto wetu.

Misingi Mingine Ya Kuzingatia Wakati Unataka Kumjengea Mtoto Wako Nidhamu Ya Kweli.
Mlee mtoto wako katika njia njema impasayo.
1. Usimwekee mtoto sheria nyingi sana.
Itakuwa ni kosa kwa mzazi kumwekea mtoto wako sheria nyingi sana kwa kufikiri kwamba ndio unamjengea malezi bora. Kwa jinsi unavyomwekea sheria nyingi unamjengea mtoto hofu na kujiona yupo kama jela kumbe yupo nyumbani.
Kama ni sheria weka ila zisiwe nyingi. Hata hivyo unapoweka sheria hizo ambazo unazitaka, mweleweshe mtoto vizuri aelewe ni nini anachotakiwa kufanya ili ajue kabisa akivunja kuna adhabu fulani itafuata baada ya hapo.
2. Toa zawadi na acha kuadhibu sana.
Najua ukiwa kama mzazi kuna tabia ambazo unataka mtoto wako awe nazo. Tabia zile ambazo unataka mtoto wako awe nazo jifunze kumpa hamasa kwa kumwahidi zawadi fulani ili aziendeleze na ziwe tabia za kudumu.
Kwa mfano, kama hutaki mtoto wako atembee tembee hovyo na umeamua iwe hivyo, ikitokea akienda badala ya kumpa adhabu, anza kumwambia kwamba usipoenda labda kutembea na kukaa hapa na kusoma nitakununulia hiki au kile, hiyo itamsaidia pia.
3. Kuwa mzazi kiongozi.
Mwongoze mtoto wako katika kumwelekeza kujisomea, mwongoze katika mambo mbalimbali kama michezo na mengineyo, kwa jinsi utakavyokuwa ukimwongoza katika mambo hayo, mtoto wako ataelewa vizuri unataka nini na kufuata.
Ukiwa mzazi kiongozi, hata ule msingi imara unaoutaka wa tabia, utajikuta zinajengeka taratibu na hatimaye kuwa tabia zake za kudumu. Hakuna kinachoshindikana katika malezi ila kikubwa tumia njia sahihi na sio za kumuumiza mtoto.
Nikutakie ushindi katika malezi bora ya mtoto wako na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku juu ya maisha na mafanikio.
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,





Aug 23, 2017

Matajiri Wote Duniani Wanaanza Na Kitu Hiki, Hadi Kufanikiwa Sana.

No comments :
Kipo kitu kimoja ambacho kila aliyefanikiwa anaanza nacho hadi kufikia ngazi kubwa ya kimafanikio. Kitu hicho hata wewe unaweza ukawa nacho na ukikizingatia ni lazima utafikia mafanikio makubwa na kutakuwa hakuna cha kukuzuia.
Kitu hichi ndicho ambacho matajiri karibu wote duniani huwa wanaanza nacho na ndicho kinapelekea wao kuweza kufanikiwa na kufika pale walipo leo. Hakuna mwenye mafanikio makubwa sana ambaye hajaanza na kitu hicho.
Naona umetega sikio lako kisawasawa kutaka kujua kitu hicho ni kitu gani ambacho nataka kukiongelea hapa. Nakuomba usitie shaka, kitu ambacho nataka kukiongelea hapa ni kuanzia pale ulipo na kile kidogo ulicho.
Usishangae sana, kama nilivyosema karibu matajiri wote waliopo duniani safari yao ilianza na kidogo walichonacho au hawana kitu kabisa tena wengine wakitokea kwenye umaskini na wingi wa madeni uliwaofunika.

Anzia pale ulipo hadi kufikia kilele cha mafanikio.
Ukiangalilia matajiri kama Bill Gates, Warren Baffet, Larry Ellison, Michael Dell na Paul Allen wote hawa walianzia chini wakiwa na pesa kidogo, wakati mwingine hata ilikuwa ikiwalazimu kuishi katika madeni.
Matajiri hawa na wengineo, walipohojiwa nini siri ya mafanikio yao, wakati watu walioanza nao pamoja wamewaacha pale pale, ni wazi walidai sio kwa sababu ya akili au vipaji bali ni kujenga nidhamu binafsi na kuamua kufanya kazi kwa juhudi kubwa kuliko mtu yoyote na tena kwa muda mrefu.
Kwa hiyo unaona kwao kuanza chini sio kitu ambacho kinawaogopesha. Kuanza chini wanachukulia kama changamoto tu ya kawaida ambayo mtu yeyote mwenye nidhamu na kujituma anaweza akaanzia huko na kufanikiwa sana.
Kwa mantiki hiyo, hata wewe unao uwezo wa kuanzia hapo ulipo na kufikia mafanikio makubwa sana. Kitu gani unachokiogopa hadi ushindwe kuanzia chini? Unaogopa kuchekwa au nini unachoogopa?
Tunaona karibu historia ya watu wote duniani wenye mafanikio walianza chini. Sasa wewe ambaye hutaki kuanzia chini eti unataka kuanzia juu nani kakwambia hivyo. Kila kitu kiasili kinaanzia chini na hatimaye kufikia mafanikio makubwa sana tena ya kutisha.
Ukiangalia kuanzia mimea, viumbe hai ni vitu ambavyo vinaanzia chini na mwisho wa siku kufikia mafanikio makubwa. Kwa hiyo, usijione kuna kitu ambacho utakosa sana kama ukianzia chini, anza na ulichonacho weka nidhamu na juhudi utafanikiwa sana.                     
Kuanzia leo usiwe na shaka na kitu chochote. Anzia maisha yako pale ulipo. Ndio, naamanisha hapo ulipo. Kila mtu anayeanzia chini anapata muda wa kujifunza na kukua, hatimaye kujenga mizizi mikubwa ya mafanikio yake.
Usijisikie vibaya au kujiona hufai kwa sababu unaanzia chini, anza na ulichonacho kutafuta mafanikio yako, anza na nguvu zako, anza na vipaji ulivyonavyo upo wakati utafika juu sana kimafanikio hadi utakuwa unajishangaa mwenyewe.
Ila kama unatafuta maisha ya juu, halafu hutaki kuanzia chini, mafanikio yako yatakuwa magumu sana kuweza kufikiwa.  Ni asili ya mafanikio kuanzia chini na kukua kidogo kidogo. Hata wanaorithi mali pia huweza kufanikiwa sana kwa kuziendeleza.
Siri ya mafanikio makubwa ni kuanza na kidogo na kukikuza hadi kuwa kikubwa. Kwa hiyo hapo ulipo huna ulichokosa, anza leo kutafuta safari yako ya mafanikio kiuhakika na ukifanya hivyo utafanikiwa na kuwa huru.
Tunakutakia kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 22, 2017

Hivi Ndivyo Utandawazi Na Teknolojia Vinavyofanya Kazi Katika Sayari Hii Ya Wasakatonge.

No comments :
Ukuajaji wa utandawazi pamoja na teknolojia kwa namna moja au nyingine umetusaidia kuweza kupima kiwango cha maendeleo ya dunia na jamii kwa ujumla. Kiwango hicho cha maendeleo kitokanacho na utandawazi kimekuwa kikipimwa siku hadi siku.
Utandawazi huo huo pamoja na teknolojia umesadia kuweza kuipambanua dunia ya zamani na dunia ya sasa. Kutoka na mabadiliko hayo ndipo tunapopata hadithi zama za kale za mawe, na sasa tupo zama za tekolojia na ukuaji wa utandawazi.
Kiuhalisia ni kwamba zama hizi za tekinolojia na ukuaji wa utandawazi zina faida lukuki sana hasa kwa wale wenye kujua namna ambavyo wanaweza kuendana na zama hizi, lakini wengi wate ambao hatuwezi kuendana na zama hizo, tumekuwa wakipata hasara tu.
Tunaweza tukajikita hata kwa dakika chache kuwaza, hivi kwa mfano ugunduzi wa simu, kompyuta za kisasa pamoja na ujio wa mitandao ya kijamii inakusaidia wewe na kwa kiwango gani? Au unaiona ipo ipo tu.

Hivi Ndivyo Utandawazi Na Teknolojia Vinavyofanya Kazi Katika Sayari Hii Ya Wasakatonge.
Tumia teknolojia vizuri ikufanikishe.
Bila shaka wengi hatujui ni kwanamna gani vitu hivyo vitavyoweza kutusadia sisi kuweza kufika mbali kimafanikio, wengi tunachukulia ujio wa teknolojia ni kama kuifurahisha tu akili zetu.
Wakati mwingine tunadhani ya kwamba ugunduzi wa mambo mbalimbali katika sayari hii ni kwa ajili ya watu wachache tu, la hasha kila kitu ni kwa ajili ya watu wote madharani wewe unayesoma makala haya. Hivyo kila kitu kilichopo zama hizi lazima ukiwazie kinakupaje wewe fedha.
Kila kitu ambacho unakiona katika ulimwengu huu wa utandawazi kina faida na hasara zake, ila wengi wetu tumekuwa tunavitumia vitu hivyo kwa upande wa hasara zaidi huku tukipumbazwa na kuona hasara hizo ndizo faida.
Kama upo katika katika upande wa kuona hivyo, tafadhari nakuomba ufanye mapinduzi kwani dunia ya sasa imebadilika sana, kile ambacho unakijua leo, upo uwezekano  kitakuwa hakina thamani siku ya kesho.
Ukuaji wa wa utandawazi ndio ambao umeleta maana hiyo. Hebu tujiulize kidogo na kuona maajabu ya teknolojia jinsi ambavyo yanafanya hicho ambacho unakijua leo kinavyokuwa hakina thamani siku ya kesho.
Hebu tujiulize wale waliokuwa wanafanya kazi kwa kutumia ‘typwriter’ na leo utandawazi umeleta kompyuta, wale watu waliofanya kazi kwa ‘typwriter’ wanafanyakazi gani? Bila shaka utagundua ya kwamba watu wa ‘typwritter’ watashindwa kuendana na kasi hii ya teknolojia.
Tuendelee kujihohoji wale ambao walikuwa wanafanya kazi za uhasibu hapo awali, ambapo kazi hii kila mtu akipeenda na leo hii karibu kila kampuni watu wanafanya miamala kwa kutumia simu, hawa wahasibu wanafanyakazi gani? Bila shaka utagundua ya kwamba kazi nyingi ambazo zilikuwa zinafanywa na watu mbalimbali kwa sasa zinapungua na kufanywa na mashine.
Zipo kazi nyingi sana ambazo leo zimerahisishwa sana, badala ya kufanywa na watu , zimekuwa zikifanywa na mashine, kwa mtindo huu naendelea kuwaza kwa sauti hivi hicho ambacho unakijua leo kesho kitakuwa na thamani tena? Bila shaka majibu unayo mwenyewe.
Hivyo kwa kuwa mabadiliko makubwa yanayoendelea kufanyika katika sayari hii yanafanya mambo makubwa kutokufanywa na wewe, unachotakiwa kufanya ni kujiongeza kwani zama zimebadilika sana.
Hivyo jijengee mifereji mingi ya kuweza kujua vitu vingi zaidi ya hicho ambacho unakijua sasa, kujua vitu vingi kutakufanya uweze kujua namna ya kuweza kuishi kesho.
Maisha yanabadilika sana hivyo ni heri kila wakati kuweza kuwa bora zaidi kwa kile ambacho unachokifanya acha kung'ang'ana na mambo ya mwaka 47, kwani hayana tena thamani tena mbele ya sayari hii, na hata kama yatakuwa na thamani kinachohitajika ni kuweza kujifunza namna ya kukiboresha kitu hicho ili kuendana na kasi ya sayari hii.
Mpaka kufikia hapo sina la ziada, tukutane siku nyingine.
Ndimi afisa mipango, Benson Chonya,

Aug 21, 2017

Hata Kama Mambo Kwako Ni Magumu…Bado Hujachelewa Kufikia Mafanikio Yako.

No comments :
Kama unafikiri umechelewa kufanya kile unachotakiwa kukifanya elewa hivi…
Mpaka sasa kitabu kizuri bado hakijaandikwa…
Mpaka sasa nyimbo nzuri kuliko zote duniani bado haijaimbwa,..
Mpaka sasa jengo zuri zaidi duniani bado mpaka dakika hii halijajengwa…
Mpaka sasa chakula kizuri kuliko vyote bado hakijapikwa…
Mpaka sasa ugunduzi mkubwa kuliko yote duniani bado haujafanyika unasubiriwa…
Mpaka sasa mashine safi na ya kisasa bado haijagunduliwa…
Mpaka sasa mfanyabiashara mkubwa kuliko wote duniani wa karne bado hajatokea…
Mpaka sasa mwandishi bora wa vitabu kuliko wote na wakati wote bado hajaibuka…
Mpaka sasa mafanikio yote makubwa yapo yanakusubiri wewe…
Narudia mpaka sasa mafanikio hayo makubwa yapo yanakusubiri wewe…
Huhitaji kutilia shaka uwezo wako, tumia maarifa yako kutoa yaliyobora…
Hakuna kinachoshindikana chini ya dunia, ikiwa utaamua…
Ndani mwako una nafasi ya kutoa mafanikio yoyote ukiamua…
Kipi kinachokuzuia, mafanikio makubwa wakati wote bado hayajatokea…
Je, unataka kujiona unakata tamaa na kujiona tena basi…
Usijione uko hivyo, unayo nafasi ya kubadilisha kila kitu kwenye maisha yako…
Unayo mbegu ya mafanikio makubwa ndani mwako, itumie…
Wewe ni bora na unaweza kuibadilisha dunia…
Usikubali kufa kifo cha mende miguu juu kwa kufikiri huwezi…
Unaweza, huo uwezo unao, na inawezekana…
Bado hujachelewa hata kama mambo ni magumu...
Tumia muda wako vizuri...tumia nafasi uliyonayo vizuri...utafanikiwa...
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
 Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 20, 2017

Acha Kuharibu Hatma Ya Maisha Yako Yote, Kwa Sababu Ya Kitu Hiki Tu.

No comments :
Kwa kawaida vipo vitu vingi vinavyopelekea maisha ya mtu kuharibika na kuwa ya kushindwa kabisa. Vitu hivi kuna wanaovijua kwa uwazi na pia kuna ambao hawavijui au hawana habari kwamba ndio chanzo cha kushindwa kwao.
Kama nilivyokwambia  vipo vitu vinavyopelekea kushindwa kwa wengine katika maisha. Lakini leo kupitia makala haya, nataka nikwambie kitu kimoja tu, ambaco kama utakibeba sana,utake usitake utashindwa na  kuharibu maisha yako yote.
Kitu hicho sio kingine bali ni kukata tamaa mapema. Kama unakata tamaa mapema tambua kabisa unakua umeamua kuharibu hatma ya maisha yako mwenyewe. Hakuna mtu aliyefanikiwa mwenye sifa ya kukata tamaa mapema.
Watu waliofanikiwa ni wabishi, wanakomaa na ndoto zao hadi kuweza kufanikiwa. Lakini kama una ndoto yako, halafu kutokana na changamoto ukaamua kuachana na ndoto hiyo, elewa kinachotokea sio tu unajiumiza sasa, bali pia unapoteza kesho yako sana.

Usikate tamaa mapema.
Kila maamuzi unayoyachukua kwenye maisha yako, yanamuathiri mtu mmoja muhimu sana kwenye maisha, ambaye ndiye wewe. Hata uamuzi wa kukata tamaa na kuacha ndoto zako zisifike mwisho, pia ni uamuzi ambao ni hatari na unaharibu kesho yako.
Hatma ya maisha yako ya kesho, inategemea sana maamuzi unayofanya leo. Inapotokea ukafanya maamuzi ya kukata tamaa kwa kitu unachokifanya, elewa unajitengenezea mazingira ya kuharibu sana maisha yako kesho.
Hivyo kutokana na kukata tamaa mapema unajikuta unakuwa ni mtu wa kuanza jambo hili leo, tena kesho unaanza lingine. Kwa maisha hayo unashangaa unapoteza muda na pia unapoteza mafanikio yako ya kesho kwa sababu ya kukaa tamaa.
Kama una wewe ni mtu wa kukata tamaa sana, ukumbuke katika maisha yako hakuna kitufe cha kubonyeza kurudisha maisha yako yakarudi nyuma, maisha yanavyosonga mbele, hayarudi nyuma hata kidogo.
Kikubwa unachotakiwa kujua ni kwamba ili kufanikiwa unatakiwa kukomaa na kuvumilia kila hali. Hakuna anayepitia mteremko wa maisha, kila mtu anachangamoto zake. Ukifanya mchezo na ukaendeleza  kukata tamaa hutafanikiwa.
Kama unaona maisha ni magumu, elewa huo ugumu ndio unatakiwa kukomaa nao na kuushinda. Hata hivyo ukiangalia nani aliyekupa ahadi kwamba maisha ni mepesi? Changamoto kwenye maisha zipo toka enzi za mababu, kuwa mvumilivu ili kufanikiwa.
Jaribu kukaa chini na kujiuliza, kesho yako itakuwaje ikiwa kila kitu unakata tamaa mapema? Nikwambie kitu rafiki yangu, usikubali hata kidogo kuharibu hatma yote ya maisha yako kwa sababu ya kukata tamaa, nimesema kuwa mvumilivu utashinda.
Nakutakia mafanikio mema na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila siku kwa ajili ya kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Aug 19, 2017

Kama Usiposhinda Kwenye Vitu Hivi, Sahau Mafanikio.

No comments :
Kitu ambacho natamani kila mtu angalau aelewe, ni kwamba huwezi kupata ushindi mkubwa kama haujawahi kupata hata ushindi kidogo. Hiyo ikiwa na maana, ili uweze kushinda makubwa lazima ushinde kwanza madogo.
Unapokuwa unapata ushindi mdogo, ni rahisi kukupa hamasa, mzuka, nguvu na hata jeuri ya kuendelea kufanya mambo mengine kwa uhakika ambapo utashangaa mambo hayo yanakupa mafanikio hata bila kutarajia.
Hali hii ndio tunayoiita nguvu au majabu ya mafanikio madogo madogo. Kuna nguvu sana ya kufanikiwa kwa vitu vidogo vidogo na kuweza kukusaidia kufanikiwa. Kile unachokiona ni kidogo kwako, lakini kina nguvu ya kuweza kukuvusha na kukupa mafanikio.

Ushindi mdogo, ni nguzo ya mafanikio makubwa.
Unatakiwa utulie na uelewe ili kuweza kutawala makubwa, kwanza unatakiwa kutawala mambo madogo. Ili kutawala biashara kubwa unayoitaka, ni lazima na muhimu sana kwanza kutawala biashara ndogo tena kwa mafanikio.
Mafanikio  makubwa yanakuja kutokana na nguvu ya kufanikisha mambo madogo madogo. Sasa nguvu hii haiji kwa bahati mbaya bali ni kutokana na ushindi mdogo unaoupata. Hivyo unaona ili uweze kuwa mshindi kwa chochote kikubwa, ushindi mdogo ni muhimu sana.
Huhitaji kujiuliza sana ushindi mdogo utaupata vipi wakati huna hata kitu cha kufanya. Sikiliza, kuamka asubuhi na mapema yenyewe na kufanya majukumu uliyojiwekea na ukafanikisha huo ni ushindi. Kusoma kitabu angalau kurasa 20 kwa siku pia huo ni ushindi.
Au labda nikueleze hivi haijalishi  hapo ulipo una kazi maalumu au huna, lakini kama unafanya vitu fulani hata kama ni vidogo sana na ukavifanikisha huo ni ushindi pia ambao unatakiwa kuuzingatia.
Inawezekana ukawa huoni maendeleo ya ushindi wako kwa sababu hufatilii, lakini hebu leo anza kufatilia ushindi wako mdogo. Utashangaa unavyofatilia unazidi kupata nguvu ya kufanya tena na tena.
Mafanikio wakati mwingine yana kawaida ya kuja kwa ‘rekodi’ zake. Kwamba kutokana na umekuwa ukishinda hili na lile basi upo uwezekano na hili hata kama linaonekana gumu sana, uwezo wa kulishinda unalo kwa sababu tu ya ‘rekodi zako’ zinaonyesha hivyo.
Kuelewa vizuri hapa angalia timu mbili za mpira kabla hazijaanza kucheza, kwanza zinawekwa kumbukumbu za michezo waliyowahi kucheza na nani ameshinda mara ngapi na kuna matarajio gani.
Kama si hivyo hata mchezo wa ngumi uko hivyo hivyo zile ‘rekodi’ za nyuma zinaanza kuwekwa kwanza kabla mchezo haujachezeka. ‘Rekodi’ hizo zinawekwa kuangalia nani alikuwa mshindi kwenye mapambano mangapi na upo uwezekano wa nani leo kushinda.
Mpaka hapo, sina shaka sasa kwa sehemu unanielewa juu ya umuhimu wa kuweka kumbukumbu juu ya ushindi wako mdogo anaoupata. Kumbuka, ushindi mdogo unaoupata unaweza kutumika kama ngazi ya kukupeleka kwenye mafanikio ya juu.
Elewa unaposhinda kwenye vitu vidogo, unapata nguvu ya kujiamini na kuamini alaa kumbe inawezekana. Pia unapokosa ushindi mdogo ni ngumu sana kufanikiwa kwani ndani mwako zinajengeka fikra za kuona kwamba huwezi kufanikiwa kwa kila kitu.
Nikutakie siku njema, endelea kusheherekea ushindi mdogo unaoupata kwenye maisha yako kila wakati, lakini elewa ushindi mkubwa unakusubiri na unakuja pia.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,