google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 31, 2017

Nguvu Ya Kimafanikio Ipatikanayo Kwenye Uchaguzi Wako Sahihi.

No comments :
Safari ya kufikia mafanikio makubwa inaanza na kufanya uchaguzi uliobora. Hakuna mafanikio makubwa yoyote ambayo yanakuja kwa bahati mbaya, mafanikio yote makubwa yanaanza na uchaguzi uliobora na tena ambao unaufanya kila siku.
Uchaguzi huu ambao nina uzungumzia hapa na ukabadilisha maisha yako si uchaguzi mkubwa sana kama unavyofikiri. Huu ni uchaguzi mdogo mdogo ambao kuna wakati unayafanya hata pengine bila kufikiri.
Uchaguzi kama leo uamke saa ngapi, uchaguzi kama leo ujifunze nini au usijifunze, uchaguzi kama leo utumie pesa zako vipi, hizi ni moja ya chaguzi ndogo ndogo sana lakini ambazo ukizitumia vizuri zinabadilisha maisha yako kabisa na kuwa wa tofauti.

Ukumbuke kabisa kile unachokipata, ni matokeo ya kile unachokifanya, na kile unachokifanya ni matokeo ya uchaguzi unaoufanya kila wakati kwenye maisha yako. Kama unafanya uchaguzi mbovu, tegemea kupata maisha mabovu pia.
Matokeo bora kwenye maisha yako yanakuja kwa kufanya uchaguzi uliobora. Hiki ndicho kitu unachotakiwa ukielewe sana na kukifatilia. Ukijifunza kuwa na uchaguzi sahihi, itakusaidia sana kuweza kutimiza ndoto zako.
Acha kuendekeza uchaguzi mbovu utakaokangusha baadae. Acha kuendekeza kufanya uchaguzi wa kufanya starehe na kusahau kufanya kazi. Acha kuendekeza uchaguzi wa kuishi maisha uyatakayo badala ya kujenga nidhamu ya mafanikio.
Uchaguzi wowote unaoufanya ni lazima ulete matokeo. Kwa chochote kile unachotaka kukifanya wewe kifanye, ila hata hivyo uelewe majibu yake lazima utayapata, yawe mazuri au mabovu lakini uyapata bila shida.
Uchaguzi ule mdogo unaoufanya leo hata kama hautilii maanani, huo ndio unajenga msingi wa mafanikio yako ya kesho. Kuwa makini usije ukaishia kuishi maisha ya hovyo kama uchaguzi wako ni mbaya na haukusaidii.
Kumbuka, maisha yako yanaweza kubadilika ikiwa kama utafanya uchaguzi na maamuzi sahihi kila siku. Elewa hiyo ndiyo nguvu kubwa ya uchaguzi sahihi inavyofanya kazi na hata kukupa mafanikio utakayo.
Kila  la kheri katika kufikia mafanikio makubwa na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com







Jul 30, 2017

Tabia Tano Muhimu Ambazo Ukizifuata Zitaboresha Maisha Yako Sana.

No comments :
Tabia ni msingi mkubwa sana wa mafanikio yako. Ukijenga tabia njema uwe na uhakika utafanikiwa na kufika mbali sana kimafanikio.
Leo nataka tuangalie kupitia makala haya, tabia ambazo ukizifuata na kuzitekeleza zitafanya maisha yako kuwa bora na  ya thamani kila iitwapo leo.

Tumia tabia bora za mafanikio zikufanikishe.
1. Usifanye kazi mbili kwa wakati mmoja.
Mawazo yako yote weka kwenye kitu kimoja unachokifanya. Ukiweka mawazo kwenye vitu viwili, utashindwa kuvifanikisha vyote kwa ufasaha na utashindwa.
2. Usigombane na mtu mpumbavu.
Kama kimetokea kitu cha kutoelewana na mtu ambaye unamwona hajielewi, achana naye ili asije akakupotezea muda wako bure.
3. Usiingie kwenye mabishano yasiyo ya lazima.
Fanya kile unachokiamini, kubishana kwingi na kujaribu kuonyeshana eti nani ni mshindi ni mambo ambayo yanapoteza muda wako pia. Epuka kubishana.
4. Usifanye maamuzi bila ya kufikiri sana.
Kama unataka kufanya maamuzi bora na ya maana kwako, yafanye kile kipindi ambacho akili yako imetulia, ukifanya maamuzi kwa haraka utajipoteza.
5. Usiende kulala ukiwa na hasira.
Unapolala huku una hasira, elewa kabisa hasira hizo utaamka nazo siku inayofuata, hivyo nenda kitandani ukiwa na amani itakusaidi sana.
Hizo ndizo tabia tano za msingi zenye uwezo wa kuboresha maisha yako ikiwa utaamua kuzifanyia kazi kwene maisha yako.
Kila la kheri katika kuboresha maisha yako na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Jul 29, 2017

Tafuta Sheria Zinazokuongoza Kwenye Maisha Yako.

No comments :

Kwa kawaida kila sehemu unayokwenda zipo sheria za kufuata. Zipo sheria za kuendesha gari, zipo sheria za kufanya biashara, zipo sheria za kuingia ‘club’,  zipo sheria za mchezo wa mpira miguu. Inawezekana unajiuliza kwa nini sheria hizi zipo? Jibu ni rahisi tu, zimewekwa ili kuleta ufanisi na mafanikio katika maeneo hayo.
Kunapokuwa na sheria zinazoongoza jambo lolote, zinafanya kwanza kunakuwa na nidhamu kubwa ya ufanyaji wa jambo hilo na mwisho wa siku huleta mafanikio. Kwa mfano, kama kungekuwa hakuna sheria ya mpira wa miguu, mchezo huo usingefanikiwa na badala yake kungekuwa na fujo tu uwanjani.
Kama kila kitu chenye mafanikio kinaongozwa na sheria, hata maisha yako yanatakiwa kuwa na sheria ambazo utazifuata kila iitwapo leo ili uweze kufanikiwa. Kama hautakuwa na sheria zinazoongoza maisha yako itakuwa ni ndoto kufanikiwa. Utakutana na changamoto nyingi bila sababu kwa sababu huna sheria zako.
Labda nikuulize kitu, je, una sheria zinazoongoza maisha yako? Kama huna tafuta sheria za kuongoza maisha yako. Unapokuwa na sheria zako, zinakufanya kutawala maisha yako na si kuishi ishi tu bila mwelekeo. Ishi kwa sheria  zako, hiyo itakufanya kila wakati utakuwa mshindi, tofauti na ambavyo kama huna. 

Jul 28, 2017

Wakati Bora Wa Kufikia Mafanikio Yako Ni Huu…

No comments :


Leo nimejikuta namkumbuka sana mwalimu wangu wa somo la Kiswahili, moja kati ya vitu ambavyo vimenifanya niweze kumkumbuka ni vile ambavyo alikuwa anajitoa kwa hali na mali katika kuhakikisha tunaelewa somo la Kiswahili. Ni siku nyingi kidogo zimepita lakini kile ambacho alinifundisha bado hakijafutika  akili mwangu, na sina uhakika kama kitakuja kufutika.

Mwalimu wangu huyu  sitachoka kumuombea kwa mwenyezi  Mungu kwa kila jambo ambalo analifanya aweze kufanikiwa Zaidi. Namkumbuka kwa sababu kuna somo ambalo alitufundisha kwa kutumia nguvu zote, somo hili ni somo la nyakati.

Na katika somo hili alisema zipo nyakati mbalimbali ambazo ni wakati uliopita, wakati uliopo na wakati ujao. Pia alieleza ya kwamba nyakati hizi zote humuhusu mwanadamu, katika kufanya na kusimulia mambo mbalimbali ambayo yalikwisha fanyika au ambayo yatafanyika.

Na miongoni mwa vitu ambavyo nakumbuka aliweza kutushauri kuhusu nyakati hizi alisema ya kwamba,  mwanadamu yeyote yule ili aweze kufanikiwa katika maisha yake ni lazima aweze kutambua ya kwamba katika nyakati hizo ni nyakati moja tu ndiyo muhimu kwake.

Na nyakati hiyo ni wakati uliopo na si vinginevyo, kwani wakati uliopita na wakati ujao si rafiki kwa mwadamu hata kidogo katika kutenda mambo ya msingi, kwani watu wengi wamekufa na ndoto zao kwa sababu waliamini Zaidi nyakati zijazo, wao pamoja na kuwa na mambo mazuri walijifariji na kusema nitafanya kesho, kesho hiyo ikawa kesho mpaka siku wakazikwa na neno lao nitafanya kesho.

Kwa maneno mengine kusema nitafanya kesho, kwa neno moja lenye kujifariji tunasema“nimeahirisha”. Neno hili ni baya sana kwani wale wote waliofanya kitendo hiki hawakuweza kufikia lengo lao kwa asilimia zote. Kuahirisha kufanya jambo la msingi ni kutafuta visingizio.

Hivyo kama wewe ni mtu wa kuahirisha sana mambo, hasa kwa kile kitu unachokifanya, elewa kabisa unapanda mbegu au unajitengenezea mazingira ya kushindwa kwako. Kama kuna jambo ambalo unataka kulifanya leo, hebu lifanye bila kusita sita au bila kuwa na shaka ya kitu chochote.

Hivyo kama kweli unataka mafanikio ya kweli jifunze kufanya mambo kwa wakati, huku ukikimbia visingizio visivyokuwa vya msingi. Daima ikumbukwe  ya kwamba ni heri upate ugonjwa wa malaria, kwani ugonjwa  huu utatibika,Ila ukipata ugonjwa wa kuahirisha mambo ya msingi basi jiandae kufa maskini.

Mwisho nikuache na nukuu isemayo; Kumbuka ukianza leo si sawa na kuanza kesho.

Imeandikwa na uongozi wa mtandao huu wa dira ya mafanikio,
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya,


Jul 27, 2017

Hatua Hizi Ni Msingi Wa Mafanikio Yako.

No comments :

Kuna yale mambo ambayo kwenye maisha huwa yanaonekana ni rahisi kabisa kufanyika na pengine kukupa mafanikio. Hata hivyo kitu cha kushangaza mambo hayo pamoja na urahisi wake wengi huwa hawayafanyi.
Hali hiyo huwa inatokea kwako kwa sababu ya kujikuta upo katika hali ya ‘easy to do…also easy not do,’ yaani urahisi kwa hali ya kawaida unauona, Lakini ndani yake kuna ugumu fulani hivi ambao unakuzuia kufanikiwa.
Ukweli wa mambo ulivyo kwenye maisha yako, iwe afya, furaha au utajiri unaweza kuvipata ikiwa utachukua hatua ndogo ndogo kila siku zile zinazowezekana ambazo zitakusogeza kwenye lengo lako bila kudharau hatua yoyote ile.
Kama ni rahisi hivyo, kwa nini watu wengi wanashindwa kufikia malengo yao? Hiyo yote ni kwa sababu ‘easy to do…also easy not do,’ kama tulivyosema. Hatua ndogo ndogo zinakuwa ni ngumu sana kuweza kutekelezwa na wengi wetu.
Jiulize ni mambo mangapi katika maisha yako ulipoambiwa fanya kitu hiki, ulisema kwamba, ‘aaah kitu hiki ni rahisi, nitakifanya tu’. Lakini mwisho wa siku unajikuta unashindwa kuchukua hatua kabisa.
Kuanzia sasa, acha kuwa mtumwa wa ‘easy to do…also not easy to do.’ Chukua hatua ndogo ndogo bila kudharau udogo wa hatua hiyo. Ukifanya hivyo utaweza kufanikiwa na kutimiza ndoto zako.

Jul 26, 2017

Kama Unashindwa Kufanya Mabadiliko Kwenye Maisha Yako, Basi Tatizo Ni Hili…

No comments :
Kuna wakati unaweza ukajikuta unataka kufanya mabadiliko kwenye maisha yako, lakini unashindwa. Je, umeshawahi kujiuliza kushindwa huko kunatokana hasa na nini au kitu gani. Najua hili linaweza likawa limekotekea.
Ikiwa kila wakati unajaribu kufanya mabadiliko ya kitu fulani na unashindwa kuleta mabadiliko hayo, basi tambua maumivu ya kushindwa hayajawa makubwa sana ndani yako hadi uweze kuleta mabadiliko hayo.
Kwa mfano, unataka kuwa na mtaji na unashindwa kila mara, basi elewa kabisa maumivu ya kushindwa kupata mtaji hayajawa makubwa vya kutosha. Tuchukulie leo hii, ukaambiwa usipokuwa na mtaji hadi mwaka huu unaisha, utapigwa risasi.
Jiulize utakubali kufa kwa sababu ya kukosa mtaji huo unaoutaka? Bila shaka haitawezekana, utafanya kila linalowezekana kufanikisha hilo. Hivyo, wakati mwingine mabadiliko yanakuja kwenye maisha yako kwa sababu ya kule kuumia sana.
Wakati ulipokuwa shule ulisoma sana na kuhakikisha unafaulu ili kukwepa maumivu ya kufeli. Pia kuna wakati umeweka juhudi nyingi sana ili kukwepa maumivu ya aina fulani na kutafuta mahala sahihi kwako.    
Tunaambiwa kitu chenye nguvu ya kubadili tabia yako na mafanikio ni maumivu. Waulize wote ambao wamefanikiwa na ambao wanafikiri chanya kuhusu mafanikio, watakwambia maumivu yamewasaidia sana kubadilika na kuweza kufika hapo walipo mpaka leo.
Hivyo basi, kila wakati tambua hasira ya kushindwa kupata kile unachokita, maumivu ya kushindwa kupata kile unachotaka kukibadili, yatumie maumivu hayo ili yaweze kukusaidia kuweza kufanikiwa.

Jul 25, 2017

Kitu Pekee Cha Kukiogopa Pale Unapohitaji Mafanikio Ya Kweli.

No comments :

Kuna wakati mwingine inabidi ujutie katika hali ambayo upo hivi sasa, nasema hivyo kwa sababu moja kati ya mambo ambayo inakubidi ujutie katika maisha yako ni kwa sababu umekuwa ni mtu wa kushangaa kuliko kutenda mambo ya msingi.
Tabia hii ya kushangaa kila kitu pasipo wewe kuchukua hatua ndiyo ambayo kiukweli inakufanya uje kujuta hapo baadae, na pia ikumbukwe wakati wewe unazidi kushangaa wapo wengine ambao wanazidi kusonga mbele katika utendaji.
Tabia hii ya kushanga ni mbaya sana katika safari ya mafanikio, kwa mfano, Utakuta wao ni watu wa kushangaa na kuhamasika sana na miradi wanayofanya watu wengine, ukija upande wao hakuna hata kitu kimoja wanachofanya.
Vilevile utakuta watu hawa kazi yao ni  kuingia kundi moja, wanashangaa kinachoendelea humo na kutoka na kuingia tena kundi lingine wanashangaa wee na kutoka tena, pia bila kuchukua hatua, endapo utachukua jukumu la kuwauliza watu hawa watakwambia wanashangaa mataa.
Tabia hii kama unayo ni vyema ukaamua kuiacha mara moja kwani dunia ya sasa hivi ni ya mwendo kasi Zaidi ya kasi ya 4G hivyo kila wakati ni lazima uweze kufanya kazi. Kama kuna fursa hata kama ni ndogo kiasi gani, itumie ikusaidie kufanikiwa na acha kubaki tu kuwa mtu wa kushangaa.  Kama ni kujifunza, jifunze kweli.
Uzuri au ubaya wa maisha hakuna ubabaishaji, ukileta ubabaishaji wa aina yoyote ile, utaumbuka tu na ni lazima utajibiwa na maisha kama vile wewe unavyobabaisha. Badilika rafiki na achana na biashara ya kushangaa, kuwa mtendaji na aamua kufanya kazi.
Hivyo amua sasa kuwa ni mtu wa kuchua hatua kuliko kubaki kushangaa, kwani kufanya hivyo ni kujichelewesha mwenyewe kumbuka ya kwamba kuendelea kushangaa ni kupoteza muda na kupoteza muda ni sawa na kuacha pesa zipite machoni mwako.
Mpaka kufikia hapo hatuna la ziada tukutakie siku njema na mafaniko mema, Mwenyezi Mungu akubariki sana kwa kusoma Makala haya.
Imeandikwa na uongozi wa mtandao blog ya dira ya mafanikio,
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya,


Jul 24, 2017

Utajiri Au Umaskini Wako, Unatokana Sana Na Maamuzi Haya.

No comments :
Maisha unayoishi sasa, kwa sehemu kubwa, yanatokana na maamuzi uliyoyafanya kipindi cha nyuma na maisha utakayoishi kesho pia yanategemea sana maamuzi unayoyafanya leo kwenye maisha yako.
Unauwezo wa kuboresha maisha yako kwa kufanya uchaguzi sahihi wa hatua unazozichukua kila siku. Moja ya kitu unachotakiwa uanze nacho ili uweze kuchukua hatua sahihi ni kujifunza juu ya kutawala pesa zako.
Hivi pengine nikuulize, umeshawahi kujiuliza katika maisha yako pesa ngapi zimepita mikononi mwako? Ukiangalia, ni pesa nyingi sana, lakini cha ajabu kwa wengi zimewaacha jinsi walivyo wakiwa hawana kitu.
Sasa basi, ili kuendelea kukosa pesa kusitokee kwako, unahitajika sana kujifunza juu ya kuwa na maamuzi sahihi ya kutawala pesa zako. Ukiipata elimu hii na ukaielewa vizuri, utakuwa umefanya maamuzi sahihi ya kukupeleka kwenye utajiri wako moja kwa moja.
Kwa mujibu wa uchunguzi mdogo uliofanyika unaonyesha hivi, asilimia kubwa ya watu  waliomaskini wanaweka akiba chini ya asilimi 2 na wengine hawaweki kabisa. Hiyo ikiwa na maana kipato chote kinachobakia kinaingizwa kwenye matumizi.
Mpaka hapo kwenye maamuzi hayo, ni moja ya maamuzi mabaya yanayowapeleka wengi kwenye umaskini.  Akiba au kujilipa mwenyewe kiasi kidogo cha kila pesa unayopata ni kitu cha msingi sana kama unataka kesho yako iwe ya mafanikio.
Ni kweli swala la matumizi ya pesa zako liko mikononi mwako, lakini ili uwe tajiri ni lazima ujue namna ya kutawala pesa zako. Sio kwa sababu una pesa unanunua vitu hovyo na kujikuta hakuna hata kiasi kidogo cha pesa ulichobaki nacho.
Angalia usije ukajikuta ukajuta kesho kutokana na maamuzi mabovu unayoyafanya leo juu ya pesa zako.  Fanya maamuzi leo bora yatakayokufanya kesho ukajiona shujaa mkubwa kwa kujiona ulifanya kitu cha maana kwa sababu ya pesa zako.
Ikiwa unataka kuendelea kimaisha na hata kuwa tajiri elewa vizuri juu ya kutawala pesa, yote haya unatakiwa ujifunze ukiwa bado kijana, kama hautafanya maamuzi hayo sahihi, ni wazi hautafanikiwa.
Utajiri au umaskini wako, siku zote upo mikononi mwako kutokana na maamuzi unayoyafanya juu ya pesa. Leo jiwekee kiapo kwamba, kwa pesa yoyote unayoipata ni lazima uweke kidogo kwa ajili yako.
Kwa kuanzia, anza hata na asilimia kumi ya kile unachokipata, umeshindwa kabisa, anza na kiasi chochote. Pesa hiyo kumbuka ni yako, unakuwa haujapoteza popote, hivyo usiwe na wasiwasi, chukua maamuzi sahihi leo yatakaokupa utajiri.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Email; dirayamafanikio@gmail.com.

Jul 23, 2017

KITABU; The Success System That Never Fails (Mfumo Wa Mafanikio Ambao Haushindwi)

No comments :

Kwenye  kitabu hiki mwandishi W. Clement Stone anaeleza upo mfumo katika maisha , ambapo ukiutumia mfumo huo vizuri, utayafanya maisha yako yasiwe ya kushindwa kamwe, bali yawe ya mafanikio siku zote.
Katika mfumo huo mwandishi ameongelea mfumo usioshindwa katika maisha jinsi ulivyokuwa wa muhimu katika maisha yako. Na mfumo huo umebebwa sana na mambo makubwa matatu ambayo ni;-
Hatua/vitendo (Action)
Hapa inakubidi kuchukua vitendo kwa kitu unachotakiwa kufanya. Unatakiwa kuchukua vitendo bila kujali kitu. Kitu unachokifanya kama umeamua kukifanya, kifanye. Acha kupoteza muda chochote unachokiamini, hebu kifanye bila woga.
Kujua namna ya kufanya (Know-how)
Kuchukua hatua kwenye jambo lolote yenyewe haitoshi peke yake, unatakiwa sasa kujua namna ya kufanya kitu hicho tena. Unatakiwa kujua namna ya kufanya katika hali ambayo itakupa matokeo sahihi.
Maarifa (Knowledge)
Maarifa ni kitu cha msingi katika kufanikisha jambo lolote lile. Lazima uwe umeiva kwa maarifa ya kutosha ili yakusaidie kufanya mambo yako kwa usanifu wa hali juu na kukupa mafanikio. Ukikosa maarifa ya msingi kwa jambo lolote utashindwa.
Hayo ndiyo mambo matatu ya msingi sana ambayo mwandishi ameyasititiza na kuyatilia mkazo karibu katika kitabu chake chote. Mambo mengine ya kujifunza kwenye kitabu hiki ni kama haya yafuatayo;-
1. Maamuzi mazuri katika maisha yanaendana na kuchukua hatua. Kama huchukui hatua, halafu ukasema eti una maamuzi mazuri, basi elewa unajidanganya na  maamuzi hayo hayana maana yoyote kwako kwa sababu hayawezi kukusaidia.
2. Kama umeamua kufanya kitu fulani, iwe ni biashara , masomo au kitu chochote ambacho kipo kwenye malengo yako, usirudi nyuma hadi umefanikisha kitu hicho. Haijalishi njiani umekutana na changamoto nyingi kiasi gani, pambana mpaka upate kile kitu ambacho ulikuwa umelenga kukifanikisha.
3. Unaweza ukaongeza uwezo mkubwa wa kufanikiwa ikiwa utatumia kanuni za mafanikio na kuzifanyia kazi kila siku. Unaweza pia ukapunguza hali ya kushindwa sana kwenye maisha yako, ikiwa kama utaendelea kutumia kanuni hizo hizo za mafanikio. Kama utafanya kinyume na hapo jiandae na anguko kubwa la maisha yako.
4. Mafanikio yanakuja kwa wale wote wanaojaribu hiki au kile mara kwa mara bila kujali wanashindwa kwa kiasi gani. Huwezi kuwa mshindi kama umekaa tu. Jaribu kwa jinsi unavyoweza ili kujenga mafanikio yako.
5. Kila wakati hakikisha unayatawala mazingira yako na sio mazingira yakutawale. Epuka kila hali iwe mazingira au watu wakutawale. Hakikisha unatawala mazingira yako vizuri ili yakupe nguvu ya kushinda.
7. Kufikiri peke yake hakuwezi kukafanya wewe ukashinda uoga ulionao. Kitu kitakachoweza kukufanya ukashinda uoga ulionao ni zile hatua unazochukua. Hatua au vitendo ni dawa pekee ya kuondoa hofu au woga wowote ule kwako.
8. Kama hujiwekei akiba yoyote, elewa kabisa ndani yako umekosa mbegu ya mafanikio. Wanaojiwekea akiba hata kama ni pesa kidogo sana, hiyo inawasaidia kuweza kukuza mbengu ya mafanikio iliyo ndani mwao. Angalia watu wengi ambao hawaweki akiba, maisha yao sio mazuri na kufanikiwa inakuwa ni ngumu.
9. Moja ya sifa kubwa ya mafanikio unayotakiwa kuwa nayo na kuiendeleza ni TABIA zako ulizonazo. Ukiwa na tabia sahihi, uwe na uhakika zitakuongoza hadi kuweza kufikia mafanikio yako.
10. Ukishakijua vizuri kile unachokitaka kwenye maisha yako, tafuta maarifa na mbinu za kukichimba kitu hicho ndani, nje mpaka ukielewe vizuri. Kukijua vizuri kitu hicho ndani, nje itakupa wewe uwezo wa kukifanya kwa ufasaha sana na kupata matokeo chanya.
11. Nguvu ya kuendelea kufanya jambo lolote itazidi kuchochewa ndani yako kama moto, ikiwa ndani yako pia una hasira, imani ya kufanikiwa na pengine maumivu ya kuumizwa na wengine. Kama ndani yako unavitu hivyo, itachochea nguvu kubwa iliyoko ndani yako ya kufanikiwa na utafanya kila linawezekana kuhakikisha unafanikiwa.
12. Unapokuwa una hamu na hamasa ya kufikia malengo yako, ni lazima kutafuta njia na kila aina ya maarifa yatakayokusaidia kufikia malengo yako. Maarifa hayo utayapata kutoka kwa watu ambao tayari wameshafanikisha hicho unachokitaka au hata kwenye vitabu mbalimbali vya kimafanikio.
13. Ili ukijue vizuri hicho unachotaka kukifanya ni lazima uchuke hatua. Huwezi kukijua kitu hicho kwa kusoma peke yake ni muhimu kuchukua hatua zitakazo kupa uzoefu ambao uzoefu huo utapelekea wewe kujua namna ya kufanya kwa ubora wa hali ya juu.
14. Kama kuna jambo ambalo umelianzisha hata kama linakuletea utata endelea kulifanya. Ikiwa kama utasimama inachukua muda mrefu tena kulianza jambo hilo na kuwa kwenye mwendo sahihi kuliko ungeendelea na safari. Siri ya kuendelea ipo kwenye kufanya sasa hicho unachotaka kukifanya. Acha kujisemea kuwa utafanya kesho au lini, fanya sasa.
15. Siku zote mafanikio ya mtu yanaanzia kwenye akili yake. Unachotakiwa kufanya ni kuangalia fursa zinazokuzunguka au changamoto zinazoizunguka jamii yako na kisha baada ya hapo tafutia majibu yake na utafanikiwa.
.16. Maadili bora ni msingi mkubwa wa mafanikio yoyote. Kushindwa kwingi kunaanza pale mtu anapokosa maadili na kujiingiza kwenye tabia za hovyo kama ulevi, zinaa na hata wizi. Mafanikio hayajengwi kwenye misingi kama hiyo hata siku moja.
Chukua hatua kila siku kujifunza haya muhimu uliyojifunza kwenye kitabu hiki.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Jul 22, 2017

Watu Wenye Sifa Hii…Ndiyo Wanaofanikiwa.

No comments :
Linapokuja swala la mafanikio zipo sifa na mambo mengi ambayo yanakuwa yanatajwa katika kumfikisha mtu ili aweze kufanikiwa. Mambo au sifa  hizo huwa ni za msingi sana kwa kila mtu ili kufikia mafanikio.
Hata hivyo pamoja na sifa hizo,  ipo sifa moja muhimu sana ambayo kwa mtafuta mafanikio kama unayo ni lazima utafanikiwa. Sifa hii  muhimu ya kimafanikio ambayo nataka kuiongelea hapa ni uvumilivu wako katika kuelekea mafanikio.
Unaweza ukawa unajituma kweli, una nidhamu binafsi na unafanya juhudi za kuwekeza kila wakati, lakini ukikosa uvumilivu hasa pale unapokutana na changamoto au pale unaposubiri mafanikio yako makubwa huwezi kufanikiwa.
Uvumilivu ni kitu cha muhimu sana kama umeamua kuishi maisha ya ndoto zako. Inabidi uvumilie  hali ngumu unazokutana nazo, inabidi uvumilie kuishi wakati mwingine chini ya kipato ili kutimiza malengo ya ndoto zako.
Kuna kitu najua unataka kujiuliza nitavumilia mpaka lini, mbona maisha yangu naona kama magumu, hayaeleweki na hii biashara italeta mafanikio lini? Ndio, najua yote hayo unapitia, hakuna namna zaidi ya wewe kukomaa na kukubali kuvumilia.
Sikiliza, kiuhalisia mara nyingi inachukua miaka 3 hadi 5, ili kuweza kupata mafanikio ya uhakika kwa kile ambacho umekianzisha leo. Huo sio muda mrefu sana kama unavyofikiri. Unachotakiwa kufanya ni kuwa na subira na kuweka juhudi sana kila siku.
Hebu jiulize kuna yale mambo ambayo uliyaanza miaka mitatu iliyopita, yanaonekana kama yalianza jana tu. Kama hiyo iko hivyo hata maisha yako unaweza kuyabadili. Kwa  nini usikubali kuvumulia ili kutengeneza ndoto zako za kimafanikio.
Hata kila unayemwona amefanikiwa, au kila unayemwona yupo ngazi fulani ya kimafanikio kuna mengi ambayo amepitia na kuvumulia hadi akavuna hicho alichokivuna. Kama hutaki kuwa na uvumilivu, utajiweka pembeni kwenye njia ya mafanikio wewe mwenyewe.
Huna haja ya kujiona unachelewa, hebu jipe muda wa kubadili ndoto zako. Uwe na uhakika hilo litafanikiwa na utajenga maisha ya mafanikio unayoyataka wewe. Watu wenye sifa ya kuvumilia magumu mengi na kuweka juhudi hao ndio wanaofanikiwa.
Hakuna hata siku moja mtu ambaye akipata hasara kidogo anaacha biashara eti akafanikiwa, mtu hayupo. Uvumilvu wako ni muhimu sana katika safari ya mafanikio uliyoichagua. Ukiona huna uvumilivu wa kutosha, SAHAU MAFANIKIO.
Tunakutakia kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Jul 21, 2017

Watu Wenye Hasira Na Kiu Kubwa Ya Mafanikio Wanafanya Mambo Haya Kwa Utofauti Sana.

No comments :
Wapo watu ambao ndani mwao wameamua kwa dhati kufanya mabadiliko katika maisha yao. Watu hawa wana kiu, hasira na hamasa kubwa ya kufanya kila kinachowezekana ili kuweza kufanikisha ndoto zao za kimaisha.
Watu hawa juhudi zao nyingi huzielekeza kwa kufanya mambo kwa utofauti hali ambayo huwaletea mafanikio. Inawezekana leo nitakuwa mbaya kwako, kama sitakwambia watu hawa wanafanya mambo yapi kwa utofauti na yanayowapa mafanikio.
Ni wakati sasa wa mimi na wewe kwenda pamoja katika makala yetu ya leo kujifunza kwa pamoja mambo ambayo watu wenye hasira na kiu ya mafanikio huyafanya tofauti;-
1. Wanaongozwa sana na neno HAPANA.
Watu wenye hasira na kiu ya mafanikio, kila wakati wanapoambiwa kitu ni watu wakusema sana HAPANA. Wanafanya hivi ili kufatilia ndoto zao kwa ukaribu na kuachana na kukubali kila kitu ambacho kinaweza  kuwapoteza.
Watu hawa wanajua pia kwa kusema hapana kwanza  hata kama kitu hicho walichoambiwa wakagundua kina faida kwao, ni rahisi kugeuza na kukubali pia. Kusema HAPANA ni jambo ambalo haliogopwi  na watu wenye hasira ya mafanikio.
2. Kuamka asubuhi na mapema.
Naomba nikupe tu ukweli mmoja, ukiachana na watu maskini, sijawahi kukutana na mtu mwenye mafanikio makubwa ambaye kuamka kwake asubuhi ni kwa kuchelewa. Watu wengi wenye mafanikio wanaamka mapema kabla jua halijatoka.
Asubuhi ni muda mzuri unaowawezesha kupanga mipango ya siku husika kwa uhakika na kufatilia mambo kwa ukaribu wakati wengine bado wamelala. Kuamka mapema mi kitu ambacho wengi hawapendi, kwa watu wenye hasira na mafanikio hupenda sana muda huo.
3. Kujituma sana.
Kati ya kitu ambacho watu wenye hasira na kiu ya mafanikio wanakifanya sana pia ni kujituma kwa nguvu zote. Wanajua bila kujituma itakuwa ni kazi bure tu, hakuna mafanikio yatakayojengwa.
Hujitahidi kufanya kazi kwa muda mrefu sana kuliko watu wengine ili kuleta matokeo chanya. Si ajabu kukuta usiku wa manane wakifanya kazi zao ili kufanikisha ndoto zao. Kujituma na kwenda hatua ya ziada ni kitu ambacho kinafanywa na watu hawa.
4. Wanaongozwa na roho ya ung’ang’anizi.
Watu wenye kiu ya mafanikio pia wanajaribu sana mambo mengi na kuhakikisha kila wanalolifanya linafanikiwa. Wakianzisha jambo si rahisi sana kuliachilia njiani. Hung’ang'ana na kuhakikisha mpaka kuona kutaka kuleta matokeo.
Kwa kifupi, watu wenye hasira na mafanikio ni wabishi wa mafanikio yao. Hawakubali kirahisi kushindwa. Wapo tayari kufanya mara elfu moja, ilimradi tu kuona wanafanikiwa. Hiki ni kitu kimojawapo wanachokifanya kwa utofauti pia.
5. Si walevu wa mitandao ya kijamii.
Mitandao ya kijamii ni mizuri kutusaidia kupashana habari , nafikiri hilo unalijua vizuri sana. lakini kwa watu wenye kiu na hasira ya mafanikio wanaamini sana kwamba mitandao ya kijamii imewekwa kwa ajili ya kuwapotezea au kuwaibia muda wao.
Hivyo kwa kulijua hilo wanaitumia mitandao ya kijamii kwa hesabu sana na kwa muda maalumu. Tofauti na watu wengine wanavyofanya, wao wana muda maalumu kuingia kwenye mitandao hiyo ya kijamii, lakini sio kuingia hovyo hovyo tu.
6. Kutokujali sana mambo ya wengine.
Kitu kikubwa kilicho ndani ya watu wenye kiu ya mafanikio na kinachowapelekea wafanye mambo yao kwa utofauti na kuleta mafanikio, ni kule pia kutokujali mambo ya watu wengine. Hawajali sana fulani anafanya  kitu gani.
Kila wakati ni watu ambao wanajihusisha sana na ndoto zao na kuangalia ni wapi pa kuboresha hadi kuleta matokeo. Hawajali wanakoselewa vipi na nani. Huamua kusonga mbele bila kujali vitu kama hivyo na hatimaye hufanikiwa.
7. Wasikilizaji wazuri wa mambo na kuchukua hatua.
Kila wakati watu wenye nia  ya kufikia mafanikio, ni wasikilizaji wazuri sana kwa wengine wanasema nini. Ni watu ambao wanajua kusema sana kunapoteza mafanikio, hivyo huamua kusikiliza na kuweka kumbukumbu za kimaandihi vile vitu ambavyo vinawasaidia.
Ndio maana ukiwafatilia wengi ni watu ambao wapo makini na si waongeaji sana. Huamua kujifunza kupitia maisha ya wengine, huchukua vitu vya msingi vinavyoweza kuwasaidia kufanikiwa.
Kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila siku.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com

Jul 19, 2017

Jinsi Ya Kujitoa Kikamilifu Na Kufanya Maisha Yako Kuwa Bora Na Ya Mafanikio.

No comments :
Hitaji lako la kwanza ambalo unatakiwa ulijue katika safari yako ya mafanikio ni kwamba, unahitaji sana kujifunza, kukua na kuendelea kufanikiwa yaani learn, grow and develop. Hilo ndilo hitaji lako la kwanza.
Kila wakati utahitaji ujue ni nini ufanye ili kuboresha maisha yako au ufanye nini cha zaidi ili hicho unachokifanya kikuletee matokeo makubwa na unayoyataka kwenye maisha yako leo na hata kesho.
Unaweza ukaanza kuboresha chochote kile hata kwa kidogo sana. Unaweza ukaanza kuboresha tabia zako,  unaweza ukaanza kuboresha biashara yako au hata maarifa yako kwa kujisomea zaidi na zaidi kila siku.
Kuendelea kujitoa kikamilifu na kuboresha maisha yako linatakiwa liwe zoezi endelevu, kila siku jiulize, ni kwa namna gani unaweza ukafanya siku yako ikawa bora, ni namna gani unaweza kuboresha maisha yako kuliko jana?
Kufanya mabadiliko na kubadilisha maisha yako, ni jambo ambalo linachukua muda( Becoming a master takes time). Unatakiwa kujifunza na kuchukua mazoezi tena na tena ili kuwa mbobezi. Hakuna kikubwa ambacho utakachofanikisha kama usipofanya hivyo.
Hakuna mpaka wa kuboresha maisha yako, hakuna mpaka unaokuzuia wewe kukua kimafanikio. Kila iitwapo leo, endelea kuboresha maisha  yako kwa jinsi unavyoweza. Ukiendelea kufanya hivyo, uwe na uhakika utafanikiwa.
Jiulize kipi kinachokuzuia ili usifanye maisha yako yawe bora? Angalia usikwamishwe na hofu wala usikwamishwe na tabia za kuahirisha mambo kila wakati. amua kufanya kitu kitakachoyafanya maisha yako yaonekane ya maana.
Kama nilivyosema mwanzoni mwa makala haya, unahitaji sana kujifunza, kukua na kuendelea kufanikiwa. Kila siku jiulize, je, umejifunza nini? Je, kutokana na kujifunza huko kuna hatua yoyote unayopiga?
Kama hujifunzi elewa hautaweza kukua, wala hautaweza kufanikiwa. Maisha ya mafanikio ndivyo yapo hivyo, yanahitajji kuweka juhudi nyingi katika .katika kila eneo ili uweze kupiga hatua za kimafanikio.
Kila la kheri katika safari ya mafanikio yako na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.comkila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Jul 18, 2017

MAFANIKIO TALK: Faida za Kushiriki Maonyesho Yoyote Yale Ya Kibiashara.

No comments :
Nikualike kwa mara nyingine tena katika kipindi hiki cha mafanikio talk ambacho kinakujia kila siku ya jumanne. Na siku ya leo tupo Patrick Kyando (star intergrated) kutoka Makambako. Licha ya kuzungumza    naye mambo mbalimbali ya kimafanikio , yeye yeye aliweza kutushirikisha faida za mfanyabiashara kushiriki katika maonesho.
Kwani wafanyabiashara wengi na wasio wafanyabiahara wamekuwa hawafahamu umuhimu wa kushiriki katika maonesho ya kibiashara ambayo yamekuwa yakifanyika ndani na nje ya Tanzania. Kama wewe ni miongoni mwa watu hao makala haya yanakuhusu, hivyo ni vyema twende sawa aya kwa aya.
Kuna  faida zaidi ya tatu kutangaza biashara ktk maonyesho yoyote :
1. Ukishiriki katika maonesho yeyote yale ya kibiashara  na ukiwa  na bidhaa ni rahisi kuuza kwa kuwa huwa kunakuwepo na watu tofauti toka sehemu tofauti ambao si rahisi sana kukutana nao ukiwa  kwenye kituo chako cha biashara. Hivyo ni muhimu kwako kuchangamkia fursa ya maonyesho kila yanapojitokeza ili kuweza kufaidika na faida hii.
2. Ukishiriki katika maonesho, ni fursa kwako kwa sababu unafungua ukurasa mpya kupata wateja wapya hata kupelekea kupata ‘network’ ya kibiashara, na ‘network’ hii huwa ni  endelevu kwa sababu utaweza kupata mawasiliano endelevu ya watu tofauti tofauti.
3. Utajifunza kutoka kwa wengine wanaozalisha au kuuza bidhaa kama zako kwasababu  wao wanakuwa na nafasi ya kuzielezea  kwa uwazi zaidi. 
4. Utajifunza vitu tofauti vya kibiashara na hasa mambo ya kiteknolojia ambayo wewe mwanzoni mwa biashara hiyo ulikuwa huijui.
5. Pia taasisi mbali mbali za serikari zinakuwepo kutoa elimu na huduma pia huwa  ni rahisi zaidi kuzipata eneo hilo la maonyesho kuliko wakiwa kwenye vituo vyao vya kazi.
6. Makampuni mengi hutangaza ofa  za maonyesho husika hivyo ni nafasi ya kupata bidhaa kwa bei  za ndogo zaidi.
Hivyo ni vyema na wasaa mzuri kwa wewe mfanyabiashara na usiye mfanyabiashara kuweza kushiriki  kwa namna moja ama nyingine katika maonyesho ya kibiashara  kwani kuna faida lukuki.
Kwa niaba ya uongozi wa mtandao huu wa dira ya mafanikio, nipende kumshukuru sana ndugu Patrick Kyando wa star intergrated kwa somo hilo zuri.
Mpaka kufikia hapo sina la ziada nikutakie siku njema na mafanikio mema. Tukutane jumanne ijayo katika kipindi hiki cha mafanikio talk. Kama unatamani siku ya jumanne ijayo tuweze kutupa somo kutoka kwako tuma neno mafaniko talk kwenda 0757 909 942 au tuma neno hilohilo kwenda e-mail yetu dirayamafaniko@gmail.com nasi tutakutafuta kwa ajili ya mahojiano mubashara.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika.
Habari njema, kama wewe ni mfugaji wa kuku, kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana na DM POULTRY FARM PROJECT, hawa ni wauzaji wa vifaranga vya kuku wa KIENYEJI ASILIA, SASSO NA KUROILER. Bei ya kifaranga kimoja ni Tsh 2000 pia kuna punguzo la bei kwa wateja watakaonunua vifaranga 500 na kuendelea. Pia tunatoa elimu ya ufugaji wa kisasa kwa wateja wa vifaranga. Hii elimu ni bure. Kwa mawasiliano zaidi tupigie simu namba 0767 04 80 35/ 0686 14 10 97. Tupo TANGA na vifaranga unatumiwa popote pale ulipo kama upo nje ya TANGA. 
Ndimi afisa mipango Benson Chonya,
bensonchonya23@gmail.com.

Jul 17, 2017

Muda Ulionao Ndio Kila Kitu Kwenye Maisha Yako.

No comments :

Moja ya kitu cha thamani sana maishani  mwetu ni muda. Hata hivyo ingawa huwezi kuona muda, huwezi kuugusa muda, lakini muda unaongoza maisha yetu na kuamua maisha yetu yaweje yaani ya mafanikio au ya kushindwa?
Muda unaweza kufanya chochote kwenye maisha yako. Kama leo hii ukitumia dakika 20 tu kufanya mazoezi baada ya miezi sita mwili wako unakuwa umebadilika. Leo pia ukiamua kujifunza vitu kwa nusu saa tu, baada ya muda unakuwa mtaalamu.
Kipi ambacho hakiwezi kuleta matokeo mbele ya muda, ikiwa muda huo utatumiwa kwa busara? Muda ndio mwisho wa kila kitu, muda unasawazisha kila kitu, ‘time is a greater equalizer’. Kama unaona maisha yako magumu, jipe muda na fanya kazi kweli, kila kitu kitabadilika.
Leo hii pengine unaitwa mtu wa kushindwa, au pengine unaitwa ni mtu usiyeweza kitu, usiumie juu ya hilo, amua sasa kutumia muda wako kwa busara kuwekeza kwa uhakika katika eneo unalotaka. Miaka mitatu au mitano mbele utakuwa mtu wa tofauti sana.

Jifunze kuufanya muda wako ukupe matokeo chanya. Jifunze kuufanya muda wako ukufanyie kazi kwa faida, PUT TIME TO WORK.’ Ukizingatia hilo maisha yako yatabadilika hata kama hayataki, ila usiwe na haraka sana na mabadiliko hayo, JIPE MUDA.

Jul 16, 2017

Yafanye Maisha Yako Yawe Ya Mafanikio Kwa Kuanza Kuchukua Hatua Hii…

No comments :
Kama unakumbuka kupitia historia ujenzi wa piramidi kubwa za Misri, haukuanza kwa kujengwa na mawe mengi kwa pamoja, bali zilianza kujengwa kwa jiwe moja tu, tena jiwe hilo ambalo liliwekwa na mhudumu mmoja katika siku hiyo ya kwanza ya ujenzi.

Hilo jiwe moja liloanza kujenga piramidi hizo kubwa kihistoria na kupelekea mamilioni ya watu leo hii kutembelea Misri, lilionekana jiwe hilo ni la kawaida tu na wala halina chochote na wala mchango wake haukuweza kuonekana mara moja.

Hata yule mfanyakazi mtumwa ambaye aliweza kuweka lile jiwe la kwanza katika kujenga piramidi hizo hakuweza kutambuliwa wala kuonekana ana mchango wowote zaidi alizidi kuonekana ni mtumwa tu na asiye na maana yoyote.

Pamoja na kwamba umuhimu wa kujenga piramidi haukuonekana na mtu yeyote, na pia wala hakuna aliyejali ni nini kinaendelea, lakini kutokana na nguvu ya kuanza mwisho wa siku piramidi zilisimama na kushangaza watu wengi.


Kama nilivyotangulia kusema, leo mamilioni ya watu duniani wanasafiri tena kwa gharama kubwa kwenda kuangalia piramidi hizo za kihistoria ambazo ni matokeo ya kazi iliyoanzishwa na uwekaji wa jiwe moja moja.

Hata kwenye maisha yetu inabidi tuelewe kwamba, siku zote kuanza jambo lolote ni kitu kigumu sana. Mara nyingi inahitjika juhudi sana ili kuanza jambo, vinginevyo huwezi kuanza kabisa na pia najua unaelewa vizuri hili kuwa kuanza ni kugumu.

Kama wewe usipokuwa makini, utakuwa unatumia muda mwingi sana kufikiria kuhusu kuanza hasa ukifikiria ukubwa wa jambo unalotaka kulifanya na kujikuta unakata tamaaa au kuahirisha kwamba nitafanya siku nyingine.

Ni rahisi sana kupata msisimko na hamasa mara tu pale unapojiwekea malengo yako,  lakini kwa wengi linapokuja suala la kuchukua hatua hapo ndipo ugumu unapoanza na wengi husau kabisa kwamba siri ya mafanikio yao ipo kwenye kuanza.

Ili ufanikiwe unatakiwa uelewe hivi, chochote kitu kikubwa unachotaka kukitimiza, kinaanza na wewe kuchukua hatua ya kufanya au kinaanza na wewe kuchukua hatua  ya kuweka jiwe la kwanza ili kukamilisha  piramidi ya mafanikio yako.

Mwanzoni unapoanza kujenga mafanikio yako, unaweza ukaonekana si kitu wala huna chochote na hakuna unachofanya, lakini elewa huo ni mwanzo. Maajabu ya maisha yako ndipo yanapoanzia hapo kwa wewe kuamua kufanya.

Hutasogea na hautafanya mabadiliko yoyote ya maisha yako, ukiamua kutulia bila kufanya kitu. Fanikisha maisha yako na kuwa ya mafanikio kwa kuanza kitu kitakachokusogeza kwenye maisha yako.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio  makubwa na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kwa ajili ya kujifunza na kuhamasika kila siku.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,

Ni wako rafiki katika mafanikio,

Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog, dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com