google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 25, 2018

Jinsi Umaskini Unavyomaliza Maisha Yako.

No comments :
Na Eryne Banda, Dar es salaam.
Umaskini ni kutokuweza kumiliki kitu chochote katika maisha iwe ni nyumba, gari, shamba, ardhi na kadhalika. Ni kuishi kwa kusaidiwa na watu. Hapa mtu anakuwa hana uwezo wa kujisimamia, anaishi kwa kuombaomba.
Nikumbushe kwamba umaskini umechangia familia nyingi kutikisika kiuchumi, zingine zikisambaratika kabisa. Umaskini umesababisha afya mbaya katika baadhi ya familia huku wengine wakishindwa kuwapa elimu bora watoto wao.
Pamoja na hayo kabla hatujaingia kwenye somo jinsi umaskini unavyoweza kukumaliza, naomba tuangalie kwanza, aina mbalimbali za umaskini ambazo zimetuzunguka na zinaendelea kutesa wengi pasipo kujua chanzo chake.

Umaskini wa mawazo.
Huu ni umasikini mbaya sana. Watu wengi wana fedha lakini hawana mawazo mapya. Umaskini wa mawazo ni mbaya kuliko umaskini wa mali. Jamaa mmoja aliwahi kusema “mwisho wa mawazo yako ndio mwanzo wa matatizo yako”. Tatizo la matajiri wengi ni kutokuwa na mawazo mapya japokuwa wana fedha nyingi.
Yapo mapepo yaliyofunga akili za watu ili wasiwe na mawazo mapya. Mawazo mapya yanatoka kwa Mungu, hivyo tunapaswa kumuomba Mungu kwa bidii ili atupe mawazo mapya. Je, jiulize hapo ulipo upo tayari kujenga mawazo mapya kwa kiasi gani au bado unataka kuendelea na mawazo yako yaleyale?
Umaskini wa tabia.
Mtu mmoja aliwahi kusema; karama itakupeleka juu lakini tabia itakufanya uendelee kubaki chini. Watu wengi wana karama nzuri, vipawa vizuri lakini wameshindwa kwenye tabia. Watu wengi wamefukuzwa kazi kwa sababu ya tabia zao mbaya huku wengine wakipewa majina mabaya sababu ya tabia zao.
Ni vema sote tukaelewa kwamba; tabia yako ndiyo inayokutambulisha kwa watu; ndiyo itakayokupa kibali; ni wakati upo peke yako; yale mambo unayoyafanya wakati wengine hawakuoni. Tabia yako ndiyo itakayokufanya uendelee kuwa maskini au uwe tajiri; ndiyo inayokufanya udharauliwe au uheshimiwe.
Ni muhimu sana kumuomba Mungu abadilishe tabia yako ili iwe nzuri na ndipo utakapofanikiwa. Usiposhughulikia tabia yako, tabia itakushughulikia wewe. Watu wengi watakupenda kwa sababu ya tabia yako nzuri. Kumbuka: Utajiri wa tabia ni zaidi ya utajiri wa fedha/mali. Maisha ndivyo Yalivyo.
Umaskini wa marafiki.
Mafanikio yanahitaji uwe na watu wazuri na hakika, huwezi kufanikiwa peke yako. Watu wengi wamekosa kuwa na marafiki wazuri ndiyo maana wameshindwa kufanikiwa. Umaskini wa marafiki ni kuunganishwa na marafiki wabaya ambao ni chanzo cha kuangamiza hatma yako.
Kwa mfano, ili Daudi awe mfalme, Mungu alimuunganisha na Yonathani ili aje kuwa mfalme. Bila ya Yonathani, Daudi asingekuwa mfalme hata kama alikuwa amepakwa mafuta.
Alihitaji mtu wa kumshika mkono na kumfikisha kwenye kiti chake cha ufalme. Soma andiko la Mungu katika 1Samweli 18: 3, “Nao Yonathani na Daudi wakaahidiana, kwa kuwa alimpenda kama roho yake mwenyewe.”
Mpenzi msomaji, wapo watu ambao Mungu amewaandaa ili waweze kukufikisha kwenye hatma yako. Mungu anaweza kukuunganisha na mtu mmoja tu na maisha yako yakabadilika.
Tazama marafiki zako ulio nao, ndipo unapoweza kufanikiwa kwani huwezi kufanikiwa peke yako. Ni lazima uwe na watu wazuri wa kukusaidia. Muombe Mungu akuunganishe na marafiki wazuri, watu wenye bidii kuliko wewe.
Naamini msomaji wangu umejifunza jambo hapo. Tuishie hapa hadi wiki ijayo ambapo nitaendeleza kidogo mada hii muhimu kwa kutaja aina zaidi za umaskini ili uweze kujijua kinachokusibu hapo ulipo.
Endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kwa ajili ya kujifunza na kumasika kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Makala hii imeandikwa na Eryne Banda wa Dar es salaam, Tanzania.

Jul 24, 2018

Mzazi Jijengee Utaratibu Huu Kwa Wanao Ili Kuleta Kizazi Chenye Tija.

No comments :
Ewe mzazi mwezangu, najua una majukumu mengi katika sayari hii, ila nakuomba  usome hili ambalo lipo katika makala haya, kwani ni la muhimu sana zaidi ya hata uzaniavyo. Lengo la kuandika walaka huu ni kwamba  mara kwa mara macho yangu yamekuwa  yakiona tabia hii ikizidi kukithiri kwa wazazi wengi.
Wazazi wengi tumekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wetu wanapata huduma zote zile za msingi. Tumekuwa tukihakikisha watoto zetu wanapata elimu, chakula pamoja malazi , halikadharika na afya bora. Katika hili niwapongeze wale wote  ambao huwa wanalitimiza hili hili kwa moyo wote pasipo kupindisha shingo.
Lakini pamoja na kuendelea kuwapa mahitaji hayo ya msingi, wengi wetu tumesahau ya kwamba watoto wetu wanahitaji mambo mengine mbali na hayo niliyoaanisha hapo juu. Wengi wetu tumekuwa tupo bize na utafutaji wa fedha muda mwingi, kuliko kukaa na familia zetu husasani watoto zetu.
Wapo baadhi ya wazazi nimekuwa nikiwasikia wakisema wapo bize katika kuhakikisha wanatafuta ugali wa watoto, wamekuwa wakitoka majumbani mwao muda wa asubuhi ambapo hata watoto hao wanakuwa bado wamelala, Hata muda wa kurudi nyumbani wamekuwa wakichekewa, na kukuta watoto wamekwisha lala, na tabia hii huenda ukaona mzazi upo sawa, lakini ukweli unakosea sana.

Walee watoto wako katika misingi iliyobora.
Kwa mtindo huu unadhani haya ndiyo malezi bora kwa mtoto? Bila shaka kama wewe ni mmoja wa mzazi mwenye tabia kama hii ni vyema ukatafakari na kuona jukumu lako kama mzazi ni lipi? Na madhara ya kufanya hivyo ni yapi?
Kwani binafsi naamini mtoto kama mtoto anahitaji muda wa kuweza kubadilishana mawazo pamoja na mzazi wake achilia mbali na marafiki zake. Kwani katika dunia hii kumekuwa na mambo mengi ambayo yamekuwa si mazuri na mengine ni mazuri. Na kwa kuwa mtoto hapati muda wa kukaa na wazazi wake ili wamueleze yapi ni mazuri na yapi ni mabaya, mtoto amekuwa akiyatenda yote kwa sababu amekuwa haoni uhimizo wowote kutoka kwa wazazi wake.
Kwa kufanya hivyo wazazi wamekuwa wanashtuka dakika za mwisho mambo yakiwa yamekwisha kuharibika kabisa, na wazazi hao hao mwisho wa siku huwanyoshea vidole watoto hao  na kusema ya kwamba wameharibika na hawafai. Huku wamesahau wazazi hao ndiyo chanzo cha kumomonyoka kwa maandili kwa watoto hao, na hii ni kwa sababu wazazi wamekuwa wakijitenga na jukumu la kufuatilia mienendo na tabia za watoto hao kiujumla.
Hivyo ni jukumu la kila mzazi kutenga muda walau hata kwa wiki mara tatu kuweza kuzungumza na mwanae elimu zote za afya, jamii, mahusiano na elimu zinginezo. Wazazi wengi wamekuwa wakiona aibu kutoa elimu hizo kwa watoto zao, huku wakiamini kufanya hivyo ni sawa nakwenda kinyume na maadili.
Lakini ukweli ni kwamba mzazi una jukumu la kumuelimisha mwanao mambo yote. Pia ewe mzazi ukumbuke ule usemi usemao ”kukonda kwa mbwa si aibu kwa mbwa bali ni kwa mfuga mbwa”.
Mwanao akajiingiza katika makundi mabaya yaliyopo hivi sasa aibu haitakuwa kwa mwanao bali itakuwa ni aibu ya kwako mzazi. Hivyo mzazi mwenzangu ni heri ukawajibika kila sekta katika kuhakikisha watoto wako unawaelea katika misingi inayoelewa, kwani pindi utakaposhindwa kuwalea watoto zako, dunia hii ipo kwa ajili ya kuwafunza wale wote ambao wameshindwa kufunzwa na mamaye.
Mwisho nimalize kwa kusema “mzazi simama imara katika kusimamaia maadili mema ya mwanao kila wakati, ili tujenge kizazi chenye tija”.
Ndimi afisa mipango: Benson Chonya,

0757909942.

Jul 23, 2018

Hivi Ndivyo Utofauti Ulipo kati Ya Mwanaume na Mwanamke Katika Hisia Za Kimapenzi.

No comments :
Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia inasadikika hakuna kitu ambacho kina nguvu sana kama mahusiano ya mapenzi, hata hivyo kutokana na nguvu hiyo ya mahusino, watu wengi hufikiri mwanaume ndio ambao wanaathiriwa kwa kiwango kikubwa na nguvu hiyo.
Watafiti wa masuala ya mahusiano wanazidi kusema ya kwamba, mwanaume kila baada ya dakika tano ni lazima awaze masuala ya kimapenzi, hii ni kutokana wanaume wengi hupenda zaidi jinsia ya kike kwa kuona kwa macho. Ndio maana ukichunguza kwa makini wanaume huwa wanakuwa wanazingatia zaidi katika kutazama jinsia hii ya kike mahali popote walipo.
Hivi hujawahi ona wanaume wamekaa mahali wanapiga stori ghafla akapite mwanamke mzuri mbele ya macho yao ghafla stori zile zikasimama kwa muda? Bila shaka umewahi kuona. Utawasikia wakisema kwa minong'ono aaah angalia kifaa hicho, wapo wengine utawasikia wakisema mcheki chura huyo. Hii ina maana ya kwamba macho ya mwanaume ndio chanzo kikubwa cha kuingia katika mahusiano kabla ya kumjua tabia aliyonayo mtu huyo.
Lakini ukweli ambao upo nyuma ya pazia ni kwamba wanaume wengi  huingia katika matamanio ya kimahusiono kwa kuona kwa macho zaidi tofauti na mwanamke. Hata hivyo mahusiano ya kimapenzi aliyonayo mwanaume ni matokeo ya macho yako. Kwa maneno mengine tunaweza kusema matamanio ya hisia za mwanamke yapo katika kuona zaidi kuliko kitu chochote.
Lakini ukienda upande wa pili wa shilingi, mwanamke huwa yupo tofauti sana ukilinganisha na mwanaume katika suala zima la kuingia katika mahusiano. Hisia za mwanamke huwa zipo zaidi katika maneno na mguso katoka kwa mwanaume. Hisia za mwanamke huwa hazipo katika kuona kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na mwanaume.
Mwanamke huamini sana katika maneno ambayo ataambiwa na mwanaume,  kwa mfano mwanamke akiambiwa anapendwa zaidi ya kitu chochote katika dunia hii mwanamke huamini hivyo,hivyo maneno ya mwanaume yana nafasi kubwa katika kuziteka hisia za mwanamke.
Lakini pia kama hiyo haitoshi mwanamke hupata hisia zaidi pale anapoguswa na mwanaume, hivyo ndio maana kama utakutana na msichana kwa mara ya kwanza ataka usimguse katika mwili wake, hii ina maana mguso wa mwanaume una nguvu sana katika kuamsha hisia mwili wa mwanamke.
Hivyo kama ndivyo hivyo basi hii ni utofauti mkubwa ulipo kati ya mwanaume na mwanamke katika kuamsha hisia za kimapenzi. Na kitu kikubwa ambacho huongoza hamasa na kudumu katika mahusiona ya kimapenzi ni "mawasiliano", mawasiliano ndiyo chachu kubwa katika mahusiano yenu. Hivyo kila wakati ili muweze kudumu katika mahusiano yenu hakikisha unakuwa na mawasilino bora kati yako na mwenzi wako.
Asante kwa kuendelea kutembelea blog hii ya DIRA YA MAFANIKIO, TUPO PAMOJA.
Ndimi afisa mipango; Benson Chonya,
0757909942.

Jul 22, 2018

Mawazo Yakinifu Ya Mafanikio Endelevu Kwako.

No comments :
Mafanikio yoyote yanaanza na mawazo. Hakuna mafanikio yanazaliwa nje ya mawazo. Kwa jinsi unavyokuwa na mawazo bora ndivyo unavyozidi kuwa na mafanikio bora kwako. Mawazo bora unayapata vipi, unayapata kwa kujifunza.
Kupitia makala haya, nakukaribisha tujifunze pamoja mawazo yakinifu ya mafanikio yako endelevu. Naamini kupitia mawazo haya, utajifunza kitu ambacho kitakutoa hatua moja na kwenda hatua nyingine, karibu tujifunze.
1.Unaweza ukaendelea kuteseka kila siku na maisha na kuteseka kila na kila aina ya ugonjwa, lakini hiyo yote inaweza ikasababishwa na ujinga ambao  umeushikilia. Ujinga ni adui mkubwa sana wa mafanikio yako.
Fanya ufanyalo, futilia mbali ujinga wote ambao upo kwako. Ukifuta ujinga utakuweka huru na utaishi maisha ya mafanikio. Wajinga ndio waliwao na ujinga haumfanikishi mtu, tadhari usiwe kichaka cha ujinga, UTAKWAMA.
2. Kwa mawazo uliyonayo ujue kabisa yanatengeza dunia yako, yanatengeneza maisha yako au yanaumba maisha yako. Swala la kuwa makini sana kwako ni nini ambacho unakiwaza kila wakati.
Kama unawaza upuuzi mwingi, ujue kabisa ndio maisha yako unayabomoa na kuyaharibu kabisa. Kuwa makini na kile ukiwazacho maana hicho kitaleta matokeo ya maisha yako hata kama matokeo hayo huyapendi.
3. Kama unaona matokeo ya nje yanaathiri maisha yako kwa namna moja au nyingine, basi huhitaji sana kulalamikia matokeo hayo ya nje, bali unachotakiwa kufanya ni kuweka juhudi za kutawala mawazo yako.
Msingi wa maisha yako unaanza na mawazo yako, ukianza kutawaka mawazo yako kwa uhakika na vitu vingine vya nje utavitawala kwa uhakika. Anza kutawala mawazo yako kikamilifu ili ufanikiwe.

4. Kila kitu kinaanzia kwenye mawazo, uzuri au ubaya wa kitu unaanzia kwenye mawazo yako. Kama unaona kitu fulani ni kibaya kwako, kuna mwingine anaonaona kitu hicho ni kizuri kabisa.
Akili yako inaona kutokana na wewe jinsi unavyoamua akili hiyo iweze kuona. Kama unaiona bahari ni sehemu mbaya, wengine wanaona bahari sehemu nzuri ya kuvua samaki, ni suala  la mtazamo wako tu.
5. Furaha ni kitu ambacho unakipata kwanza ndani yako. Furaha kwa lugha nyingine ni uchaguzi ambao wewe unaamua kwamba sasa nataka kuwa na furaha ya namna hii. Furaha si kitu ambacho kinatoka nje yako. Furaha ni wewe unayoiumba ndani yako.
Kama unasubiri hadi ukamilishe mambo fulani hivi, halafu ndio uwe na furaha,  hapo utakuwa ni sawa na kujidanganya. Kwa nini ninasema hivyo ni kwa sababu, furaha ni kitu ambacho ni matokeo ya wewe na si nje yako, fikiri hili na tengeneza furaha yako.
6. Pamoja na kwamba maisha  yanaonekana ni magumu, lakini kipo kitu ambacho unaweza  ukafanya na kitu hicho kikabadili maisha yako na kuwa bora kabisa. Acha kuendelea kukazana kusema maisha ni magumu, fanya kitu.
Kuendelea kukaa tu na kujiimbia wimbo wa maisha ni magumu, hiyo haitakusaidia sana. Amka kutoka kwenye usingizi, amua kuchukua hatua kwa kufanya kitu ambacho kitakutoa kwenye ugumu wa maisha uliopo.
7. Mara nyingi mafanikio makubwa yoyote yale yanakuja kutokana na kufanya mambo ambayo watu wengi hawawezi kufanya. Kama jambo unalolifanya kila mtu analifanya, kufanikiwa kwake inakuwa ni ngumu kwa sababu ya ushindani wake unakuwa mkubwa pia.
Kuwa mtu ambaye unathubutu, kuwa mtu ambaye utajitoa mhanga kufanikisha jambo lile ambalo kila mtu anasema hawezi. Huhitaji maarifa ya ziada au kitu kingine tofauti, ni wewe tu kuamua kujitoa na kusema moyoni mwako kwamba nafanya na naweza pia, DO WHAT CAN’T BE DONE.
8.. Mara nyingi mategemeo bora ya maisha yako ya kesho yanatokana na uzoefu ulionao. Kama kwa siku za hivi karibuni umekuwa na uzoefu mbaya wa kupitia katika hali ngumu ni wazi na lazima utategemea mabaya tu katika maisha yako. Ikiwa lakini umekuwa ukipitia mambo chanya , mategemeo yako yatakuwa pia yapo vizuri.
Dawa pekee itakayoweza kukusaidia wewe uwe na mategemeo mazuri ni kuamua kujilisha dozi kubwa sana ya mambo chanya kwenye maisha kila siku. Kwa kadri unavyozidi kuwa chanya ndivyo mategemeo yako yanazidi kuwa bora. Hakuna mtu ambaye anaweza kuwa na mategemeo bora kama hayuko chanya.
Fanyia kazi mawazo haya yakinifu na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Jul 21, 2018

Zifahamu Sura Mbili Ziletazo Mafanikio.

No comments :
Habari ya muda huu mpenzi msomaji wa blogu hii ya DIRA YA MAFANIKIO bila shaka u mzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku. Naomba nikuarike jamvini tuweze kujifunza kwa pamoja sura mbili zitakazo kuletea mafanikio.

kila kitu unachokiona katika dunia hii kipo katika mwenekano wake. Na mwenekano huo ndio ambao hufanya viumbe vyenye akili viweze kutambuana kwa kutumia muonekanao huo. Pia mwonekano huo ndiyo hutumika kijenga picha kamili ya kitu halisi. 

Kama ndivyo hivyo basi katika kuyasaka mafanikio inahitajika mtu husika aweze kuvaa sura mbili ili kuyanasa mafanikio hayo. Na sura hizo mbili ndizo zitakazokufanya wewe uweze kujitofautisha na watu wengine.


Huenda ukawa hujanielewa bado usipate shida  ipo hivi sizingumzii umbo wala muonekano ulionao ndio utaokupa mafanikio laa hasha. Bali nazungumzia ya kwamba ili uweze kupata mafaniko yako unatakiwa kuwa na sura ya Mwalimu na sura Mwanafunzi pia.

Ninapozungumzia suala la kuvaa sura ya mwalimu, kwanza tambua ya kwamba mwalimu si yule anayefundisha darasani pekee yake la hasha, bali mwalimu mzuri ni yule aliyelewa kisha kuyafanyia kazi yale ambayo amelewa kisha kuwafundisha wengine.

Hii ina maana ya kwamba kile kidogo ambacho unakifahamu kisiwe siri yako bali weka mikakati thabiti ambayo watu wengine wataweza kunufaika na hicho unakijua. Huenda kwako ukakiona ni kidogo sana ila tambua ya kwamba wapo baadhi ya watu kwa hicho unachokijua japo wewe unakiona ni kidogo kwao ni kitu kikubwa sana.  Hivyo kila wakati jifunze kuwa mwalimu kwa watu wengine.

Sura ya pili ambayo unatakiwa kuwa nayo ni sura ya mwanafunzi. Pamoja na kuwa mwalimu lakini elimu haina mwisho hivyo endelea kuwa mwanafunzi , huku ukizingatia ya kwamba mwanafunzi bora ni yule ambaye yupo tayari kujifunza katika mazingira yeyote yale.

Lakini mwanafunzi huyu ili awe mwanafunzi ni lazima pawepo na utayari kutoke ndani ya nafsi ya mtu husika, kwani kama mtu atalazimishwa kujifunza atashindwa kuyafanyia kazi yale ambayo amejifunza.

Lakini pia mwanafunzi makini ni yule mwenye kutambua ni nini maaana ya uanafunzi, yaani awe tayari kulipa gharama ya pesa na gharama ya muda kwa kitu anachotaka kukifahamu. Kufanya hii ndiyo nguzo ambayo kila unayemuona ana mafanikio imemsadia kwa namna moja ama nyingine kuwa hivyo alivyo leo.

Kila kitu ambacho unakiona mbele ya macho yako tambua kuwa kuna mtu aliwekeza gharama fulani katika kitu hivho, hadi kupelekea kitu hicho kuwa hivyo kilivyo leo.

Hivyo ndugu yangu naomba nikwambie ya kwamba mafaniko ya kweli yanajengwa na sura hizo mbili ambazo nimekwisha kukueleza yaani kuwa mwalimu lakini pia kuwa mwanafunzi. Ukiyazingatia hayo utaishi maisha yenye tija katika sayari hii ya dunia.

Ndimi: Benson Chonya


Jul 20, 2018

Dalili Tano (5) Zitakazokuonyesha Kwamba Upo Kwenye Njia Sahihi Ya Mafanikio Yako.

No comments :
Kila mtu mwenye nia ya kutafuta mafanikio, kuna wakati anakuwa ana shaka kwamba je, ‘kweli nipo kwenye njia sahihi ya kufanikiwa au hapana.’  Hali hii hujitokeza kwa sababu, njia ya mafanikio  inakuwa in changamoto nyingi sana.
Kuna wakati inafika kutokana na changamoto hizo, wengi huanza kukata tamaa na kuanza kujiuliza maswali kweli njia hiyo au hicho wakifanyacho kinawafikisha kwenye mafanikio yao, au kinawatoa nje kabisa ya mafanikio.
Hali kama hii inajitokeza kwa wengi sana si kwako tu, bali hata kwa  watu waliofanikiwa ikiwemo pamoja na mamilionea hufika wakati wakijiuliza je, kwa kile wakifanyacho kwa wakati huo kinawafikisha kwenye mafanikio mengine ya juu zaidi au hapana.
Kitu cha kujiuliza zaidi, utajuaje kwamba upo kwenye njia sahihi ya mafanikio yako? Hiki ndicho kitu ambacho nataka ujifunze kupitia makala haya ili tena usiwe na shaka. Kama utakosa dalili hizo kabisa miongoni mwa hizi ujue upo nje ya mafanikio.
Zifuatazo Dalili Tano (5) Zitakazokuonyesha Kwamba Upo Kwenye Njia Sahihi Ya Mafanikio.;-

1. Kama wewe ni king’ang’anizi.
Mafanikio kila wakati yanawapendelea na kwenda kwa watu ambao ni ving’ang’anizi  na ambao wana nidhamu ya kujua kile wakitakacho na kukifanya kwa muda mrefu. Hakuna mafanikio yanayokwenda kwa mtu ambaye si king’ang’anizi.
Mfumo na njia unayoipitia ya ung’anganizi ndio inayotabiri kwamba wewe unakwenda kufanikiwa. Nafasi yako ya kufanikiwa itakuwa kubwa sana kama ni king’ang’anizi, tofauti na yule ambaye si king’ang’anizi kwani mtu huyo lazima atashindwa.
Ukishajua kile unachokitaka vizuri, ni vyema ukawa king’ang’anizi kwani ni dalili tosha ya kwamba kitu hicho ukitakacho utakipata. Ukikosa ung’ang’anizi, ujue kabisa hautaweza kufanikiwa hata kama ungeweka juhudi kubwa sana.
2. Kama una mahusiano sahihi na pesa.
Mahusiano hayaishii tu kwa watu lakini pia ili kufanikiwa, unatakiwa kuwa na mahusiano sahihi na pesa. Si kwa sababu unapata pesa ukaamua kuzitumia pesa hizo hovyo hovyo na kufanya vitu vya ‘biashara kichaa’ ambazo hata hazieleweki.
Mahusiano sahihi yanakuja kwa wewe kutuliza akili yako, kwa kila pesa unayoipata kuiwekea akiba hata kama ni kidogo sana, kuwekeza kwa busara na mengine kama haya. Unapokuwa hauna mahusiano sahihi na pesa, huwezi kufanikiwa.
Unatakiwa ujikague na kujitathimini, je unayo mahusiano sahihi na pesa. Kila unapoangalia matumizi yako, je, yamekaa sawa? Kama ukiona una mahusiano sahihi na pesa, basi ujue upo kwenye njia sahihi ya kuweza kufikia mafanikio yako.
3. Kama una mahusiano sahihi na watu sahihi.
Kupata mafanikio kunategemea mambo mengi sana, ikiwemo mojawapo la msingi sana ni kuwa na watu sahihi. Kuwa na mahusiano na watu sahihi ni kitu cha muhimu sana katika kukupa mafanikio uyatakayo maishani mwako.
Watu sahihi wanakuwa wanakupa chachu na hamasa kubwa ya kukupeleka mbele kimafanikio. Unapowakosa watu hao unakuwa unatoka nje ya mafanikio yako na mwisho wa siku utashangaa umeshindwa vibaya sana.
Jiangalie wewe mwenyewe na ujiulize je, una timu sahihi inayokuzunguka ya watu ambao watakusaidia kukupa mafanikio yako? Kama huna timu hiyo itafute, kwani dalili mojawapo inayoonyesha kwamba utafanikiwa ni watu sahihi ulionao.
4. Kama unajua mapema kile kinachofanya kazi.
Watu wenye mafanikio wanajua mapema sana yale mambo yayofanya kazi kwao na yale ambayo hayafanya kazi. Kama kuna jambo wanalifanya, wakigundua jambo hilo linawapeleka eneo ambalo si sahihi hukimbia sana na kutafuta kitu kingine.
Kile kitakachokufanya ujijue pia uko kwenye njia sahihi ya kutafuta mafanikio yako ni kule kuwa makini na kujua kile unachokifanya kama kinafanya kazi yaani kinaleta matunda ambayo unayataka na kwa muda mwafaka unaoutaka wewe.
Ni jukumu lako kukagua kile unachokifanya na kujiuliza maswali ya msingi, je, hiki nikifanyacho kinafanya kazi au hakifanya kazi, kujiuliza maswali haya itakusaidia sana kujua njia ya mafanikio unayopita ipo sahihi au haipo sahihi.
5. Kama una imani ya kufikia mafanikio yako.
Imani ni moja ya kitu kikubwa sana ambacho kinaweza kikakufikisha kule kwenye mafanikio yako. Kila unapofikiria ndoto yako kama una imani kuna kitu ambacho unajiambia ni lazima nitafanikisha hili au ni lazima nitafanya jambo lile.
Ile imani unayojiambia wakati unatafuta mafanikio, hiyo ndio imani unayatakiwa kuwa nayo. Imani hii ya kuweza haiji kwa bahati mbaya, bali inakuja pale unapokuwa na mipango imara na kutambua jinsi unavyoweza kufikia ndoto zako.
Nikuulize hapo ulipo una imani ya kuamini kwamba utafikia ndoto zako. Imani hii hata kama huna, unatakiwa ujue jinsi ya kuweza kuimiliki ili ikusaidia kufika kule unakotaka kufika. Mafanikio yako yanahitaji sana uwe na imani hii ya msingi.
Kwa maelezo haya yakinifu, hizi ndizo dalili za msingi za kujua kama upo kwenye njia sahihi ya kuelekea kwenye mafanikio. Fanyia kazi hiki ulichojifunza na chukua hatua mathubuti zitakazoweza kukusaidia kufikia ndoto zako.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI  ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,









Jul 19, 2018

Sababu Nne (4) Kwa Nini Hutakiwi Kujilinganisha Na Watu Wengine.

No comments :
Hapo ulipo hebu jiulize swali hili? Bado unaendelea kujilinganisha na watu wengine? Inawezekana ukawa unajilinganisha na watu wa familia yako, rafiki zako au jirani zako. Tabia hii ya kujilinganisha ipo sana kwa wengi.
Kwa bahati mbaya sana tabia hii ya kujilinganisha chanzo chake kikubwa kimeanzia tokea ukiwa mtoto. Ukiwaangalia watoto wanajilinganisha sana na wenzao kwa mambo mengi kama kwenye mavazi waliyonayo, midoli wanayochezea, nyumba wanayoishi na vinginevyo.
Kwa sababu hiyo hujikuta inapelekea unapokuwa mtu mzima unaanza kusema siwezi hiki au siwezi kile au mimi si bora katika jambo lile, lakini hapa unaona yote hiyo inatokana na  kujilinganisha. Tabia hii ya kujilinganisha kwa maendeleo ya mafanikio yako si nzuri.
Kivipi tabia hii si nzuri ya kujilinganisha na wengine, zifuatazo ni sababu za msingi ambazo unatakiwa ujue kwa nini kujilinganisha hakufai.

1. Kujilinganisha na wengine, inakupozea furaha yako.
Kwa jinsi unavyozidi kujinganisha na watu wengine, hiki ni kitu ambacho kitakupotezea furaha yako pasipo kujua. Kuna maeneo ambayo unatakuwa unajiona hufai ama umepungukiwa vitu fulani hivi kwa sababu ya kujilinganisha.
Siri ya kuweza kudumisha furaha yako, acha kujilinganisha sana na watu wengine. Ishi maisha yako na kimbia mbio zako mwenyewe ambazo utaziona mbio hizo zitakusaidia kuweza kufanikiwa na kufikia mafanikio yako makubwa.
2. Kujilinganisha na wengine, inakuzuia usisonge mbele sana.
Unapokuwa unajilinganisha na watu wengine badala ya kuweka juhudi za kukusaidia kusonga mbele, juhudi hizo unazimaliza kwa kujilinganisha. Matokeo yake unajikuta unadumaa badala ya kusonga mbele sana unaishia palepale.
Hata ikitokea unajilinganisha na wengine na ukafanikiwa kusonga mbele, pia hutasogea sana, badala yake utajikuta unaishia katika eneo lile lile  ambalo wale unajilinganisha nao wamefika katika eneo hilo.
3. Kujilinganisha na wengine, hakuwezi kukubadili wewe.
Kuna watu ambao wanakuwa wanajilinganisha sana katika eneo la sura, hasa kwa wanawake. Hata ukijilinganisha vipi, lakini elewa utabaki wewe kuwa wewe. Hakuna kitakachobadilika, hautaweza kubadili sura yako.
Kama unajilinginisha kwa hivi, unatakiwa kujua unajipotezea muda. Kazana na mambo yako na usiendelee na mambo ya wengine au uzuri wao. Kazana  sana kubadili yale yaliyo yako na si kukazana kujibadili wewe kupitia wengine ni hatari kwako.
4. Kujilinganisha na wengine, kunakupotezea ubora wako.
Utaupata ubora wako na utaboresha maisha yako, kama unakazana kuwa bora wewe kuliko ilivyokuwa jana yako. Kujilinganisha na wengine utajipotezea sana ubora wako, maana utafanya kama wale unaojilinganisha nao na hautavuka sana.
Hizi ndizo sababu za msingi za kwanini hutakiwi kujilinganisha na wengine. Fanyia kazi sababu hizi na kuanzia sasa anza kuishi maisha yako wewe kama wewe. Ukumbuke kuendelea kujilinganisha na wengine huko ni kujipoteza.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

Jul 18, 2018

Kama Utatumia Mambo Haya Hovyo, Utakwama Sana.

No comments :
Muda wako ulionao, nguvu zako ulizonazo na umakini wa mambo ulionao, ni moja ya mambo ambayo yana nguviu sana katika kubadili maisha yako au kuharibu maisha yako kwa namna ambayo hata wewe inaweza kukushangaza.
Jukumu lako kubwa ulilonalo, ni kufanya juu chini na kuyatumia mambo hayo kwa ukamilifu wake ili yakupe maisha unayoyahitaji, hapa nikiwa na maana maisha ya mafanikio. Kama ila utayatumia mambo hayo hovyo, hakuna ubishi utashindwa sana.
Pengine jiulize je, kuna kitu ambacho katika hali si ya kawaida kinakuingilia na kukupotezea muda wako, nguvu zako na umakini wako wa kuelekea kwenye ndoto zako? Kama kitu hiki kipo tafuta namna jinsi utakavyoweza kuachana nacho.
Kama utaendelea kung’ang’ana na kitu ambacho kinakupotezea muda, nguvu na umakini wako pasipo manufaa yoyote, nikwambie tu hapo unajitafutia balaa au njia ya kwenda kwenye shimo la kushindwa kwako vibaya kimaisha.

Tumia muda ulionao, nguvu ulizonazo na umakini wako kukusaidia kufanikiwa.
Waangalie watu wote wanaoshindwa kwa kitu chochote. Watu hao wanaoshindwa wanasifa moja kubwa sana ambayo ni kufanya mambo ambayo yanapoteza muda wao, nguvu zao na umakini wao katika kuelekea mafanikio wayatakayo.
Haya ni mambo yanaonekana kwa juu juu hayana athari kubwa katika maisha yako, lakini kiuhalisia mambo haya ndio yanaua ndoto za watu wengi na kujikuta ni kilio cha kuishi maisha yasiyo ya mafanikio sana karibu wakati wote.
Ukitaka kubadili hali hii na iwe ya manufaa kwako, kuanzia leo anza kutumia muda wako, nguvu zako  na umakini wako wote katika mambo ambayo unaamini yatakusaidia wewe kukubadilisha na kukupeleka sehemu nyingine ya mafanikio.
Ikiwa unachukua hatua, hakikisha unachuka hatua ambazo hazikupozei muda wako, nguvu zako na umakini ulionao katika kuelekea mafanikio yako. Ikitokea unachukua hatua ambazo zinakupotezea mambo hayo, basi kushindwa kunakuhusu sana wewe.
Ikiwa pia unawaza, una panga mikakati yako, hakikisha sana,  kuwaza kwako kusiwe unawaza tu kwa sababu wewe ni binadamu. Jitahidi kuwaza  kule ambako kunakuletea manufaa na si kukupotezea muda wako, nguvu zako na umakini.
Kitu ninachotaka unielewe hapa kwa umakini ni kwamba muda ulionao, nguvu ulizonazo na umakini ulionao, ndivyo vitu ambavyo vitakutambulisha wewe kama unafanikiwa au unashindwa na hiyo yote inatokana na jinsi unavyovitumia vitu hivyo.
Kila wakati, tumia vitu hivi viwe daraja la kukusaidia kufanikiwa kwako na si kukuangusha. Kama nilivyosema mwanzoni, kama utatumia vitu hivi hovyo kwenye maisha yako ya sasa, basi andika utashindwa sana na hautafanikiwa kwa sehemu kubwa maishani mwako.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




Jul 16, 2018

Maisha Yatakuwa Bora Na Mazuri Sana Kwako Kama Utafanya Mambo Haya…

No comments :
Maisha yatakuwa mazuri kwako, kama utajiruhusu kuishi maisha mazuri kwa kufanya yale yaliyo ya msingi na yanayoweza kujenga maisha yako yakawa mazuri.
Maisha yatakuwa mazuri kwako, kama nguvu zako nyingi za uzingativu unaziweka kwenye mambo chanya na ambayo yanaleta mabadiliko kwako na kwa wengine.
Maisha yatakuwa mazuri kwako kama unaweka nguvu zako za uzingativu pia katika kutoa matokeo chanya, ambayo yanakubadilisha wewe na yanawabadiisha watu wengine pia.
Maisha yatakuwa mazuri kwako kama utaondoa mitazamo yako potofu uliyonayo, pamoja na kinyongo kwa wengine na kuanza kuuona usawa kwa wote.
Maisha yatakuwa mazuri kwako, kwa sababu, leo hii unayo tena nafasi na fursa ya kuishi na kufanya chochote ukitakacho pasipo kuzuiliwa na kitu cha aina yoyote.

Maisha yatakuwa mazuri kwako, kwa kuona mazuri kwa wengine na kubali kujifunza kutokana na mazuri hayo na si kubaki wewe kama wewe.
Maisha yatakuwa mazuri kwako, ikiwa utakubali kujifunza kutokana na makosa na kukubali kujirekebisha na kisha kusonga mbele kwa mafanikio.
Maisha yatakuwa mazuri kwako, kwa wewe kukubali kuwasaidia watu wengine kuweza kufikia ndoto zao na kwa kufanikiwa kwao na wewe utajikuta ukipiga hatua.
Maisha yatakuwa mazuri kwako na ya Baraka, kama utaamua kuwa mtu wa shukrani na sio mtu wa kunung’unika kila wakati kama ilivyo mazoea ya wengi.
Ruhusu siku ya leo iwe maalumu kwa ajili ya kutengeneza maisha yako ya kesho na yakawa bora na ya mafanikio makubwa.
Hata siku moja usikubali kubaki hapo ulivyo kwa kuwa king’ang’anizi kwa mambo yanayoharibu maisha yako ya leo na kesho.
Nguvu ya kuumba maisha yako na kuwa bora unayo. Kikubwa kwako ni kuweka juhudi na kujiruhusu ili uwe na maisha ya namna hiyo kwako.
Ikiwa utajiruhusu kufanya maisha yako yawe bora na huku ukichukua hatua, ndivyo itakavyokuwa na maisha yako yatakuwa bora vivyo hivyo siku zote.
Boresha maisha yako, kwa kuruhusu yale yaliyo mema yatokee kwako, na amini hilo unaweza na hakuna shaka, anza sasa.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama pia  wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,