google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

DIRA YA MAFANIKIO

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 11, 2020

Je, Unahitaji Kufanya Biashara Na Hujui Ni Biashara Ipi Ya Kufanya? Soma Hapa Kujua Ni Biashara Ipi Ya Kuifanya Sasa?

8 comments :
Wapo watu ambao mara nyingi hujiuliza ni biashara gani wafanye katika maisha yao ambayo itaweza kuwaingizia pesa nyingi ya kutosha. Ni wazo ambalo hutokea kutokana na pengine kuona kila biashara wanayoitazama  kwa wakati huo kama hailipi. Hali hiyo husababisha mkanganyiko mkubwa wa mawazo ambao husababisha wabaki njia panda.
Kama imeshawahi kukutokea hali kama hii kwa namna moja au nyingine makala hi ni muhimu sana kwako kuisoma. Kwa kusoma makala hii inakuonyesha kwa uwazi orodha za biashara ambazo unatakiwa uzifanye ukiwa katika mazingira uliyopo. Karibu kila biashara ipo hapo, kazi ni kwako kuchagua mojawapo unayoipenda na kuifanya, acha kulalamika tena kuwa huelewi nini cha kufanya.
Twende kwa pamoja kuzijua biashara hizo ambazo unauwezo wa kuzifanya na kukufikisha kwenye mafanikio makubwa:-
1. Kutengeneza na kuuza chaki.
Hii ni moja ya biashara nzuri unayoweza kuifanya na soko lake liko juu. Unaweza ukanunua mashine yako za kutengeneza chaki na kisha ukaanza kuzisambaza kwenye stationary  au mashuleni. Uzuri wake mashine hizi za kutengenezea chaki gharama yake pia sio kubwa sana ni ya kawaida tu ambayo hata wewe unaweza kuimudu. Hii inaweza ikawa ni sehemu mojawapo ya kuingizia kipato chako.

2. Kufungua duka la kuuza asali.
Uzuri wa bidhaa hii muda mwingi soko lake lipo juu. Ni biashara ambayo unaweza ukaifanya kwa kuagizia asali kutoka kwa wakulima kama nilivyo mimi na kisha kuanza kuiuza moja kwa moja katika vipimo vinavyotakiwa.
Kama huwezi kufungua duka hili unaweza ukafanya mbadala wake ukaenda kutengeneza mizinga wewe mwenyewe na kuwafuga. Pia hii ni biashara ambayo ni nzuri kwako kukuingizia kipato kikubwa kwa urahisi.
3. Kuanzisha biashara ya kuuza vyakula katika matamasha mbalimbali.
Hapa siyo lazima uwe na Hotel au Mgahawa ndiyo uanzishe biashara ya namna hii. Kikubwa unahakikisha unakuwa makini na sherehe katika eneo ulilopo. Kama ni kuweka mawakala watakao kusaidia kukujulisha kuwa eneo fulani kuna sherehe ya aina fulani na siku fulani itakuwa nzuri zaidi kwako kuchangamkia tenda hizo mapema.
4. Kujenga nyumba za kulala wageni.
Kama mtaji wako unaruhusu hii ni moja kati ya biashara nzuri kuifanya. Ni biashara ambayo hahitaji kukimbizana sana ukishamaliza kujenga, zaidi unatakiwa kuweka mfumo sahihi wa kusimamia na kuanza kuingiza pesa. Na kwa bahati nzuri kwa Tanzania yapo maeneo mengi ambayo yanauhitaji mkubwa wa huduma hii. Ni Biashara nzuri kuifanya hata kama umri umeenda, kwa sababu haihitaji mkimbizano mkubwa.
5. Kutengeneza matoroli/mikokoteni na kuikodisha.
Katika hili  hapa unatakiwa kutengeneza kwa idadi unayoitaka na unamwachia kijana ambaye anaikodisha huku ukiendelea na majukumu mengine. Unaweza ukaiona ni biashara ndogo lakini fuatilia kwa waliowekeza nguvu na mawazo yao hapo wakwambie kile wanachokipata utashangaa.
6. Kuazisha huduma ya AIRTEL MONEY, MPESA, TIGOPESA, EZYPESA.
Hakuna ubishi hii ni moja ya huduma ambayo imezagaa kila eneo na watu wengi wanaihitaji. Kikubwa ni juhudi yako na kuzingatia eneo uliloweka biashara yako liwe hasa la mzunguko mkubwa zaidi kukuwezesha kufanya biashara hii vizuri.
7.  Kupamba maharusi na kumbi za harusi/sherehe.
Pia unaweza ukajiingiza hapa na kushughulika na kupamba tu maharusi. Kama hujui sana ni kitu cha kujifunza pia, kisha unachangamkia sherehe zinazojitokeza mjini.
8. Kuanzisha kilimo cha kisasa.
Wengi wanaposikia kilimo kichwa kinakataa. Lakini ikiwa utawekeza kwenye kilimo cha kisasa na cha kitaalamu ambacho unategemea kumwagilia zaidi, uwe na uhakika unatoka. Yapo mazao mengi unaweza ukalima lakini mojawapo ni kitunguu. Inaweza ikawa ni njia rahisi ya kufikia mafanikio yako  kuliko unavyofikiri.
9. Mashine za kusaga na kukoboa nafaka.
Pia unaweza ukajitengenezea kipato chako na kuwa kikubwa na cha uhakika kwa kufunga mashine hizi. Kila siku watu wanahitaji kula hivyo ukifunga mashine hizi ni rahisi sana kupata wateja wa kuwauzia unga na kupata  faida. Na uzuri mahindi ya kusaga yanapatikana maeneo mengi kwa wingi kama kule Kibaigwa (Dodoma), Gairo(Morogoro), Kiteto(Manyara) na maeneo mengine mengi kama Iringa na mbeya.
10. Yadi kwa ajili ya kupaki magari.
Kitu unachotakiwa hapa ni kununua kiwanja na kukigeuza kuwa yadi ambapo magari yanakuwa yanapaki iwe kwa kulala au kwa muda. Kila gari linalokuwa linapaki linakuwa linatozwa kiasi fulani cha pesa ambacho kinakuwa ndiyo hiyo huduma unayoitoa.
Zipo aina nyingi sana za biashara ambazo unaweza ukazifanya na kukuingizia kipato. Katika Orodha ya kipande cha makala hii kinachoendelea zimebaki biashara zaidi 110 ambazo sijaziweka hapa kutokana na ufinyu wa nafasi. Kuzijua zinazoendelea na ufafanuzi wake  unaweza ukaniandikia email kwenda diramafanikio@gmail.com nitakutumia mara moja.
ILA KAMA YOTE HAYO UTASHINDWA KUPATA LA KUFANYA WEWE UTAKUWA UMESHAPOTEA, ENDELEA NA UTARATIBU WAKO WA KUILAUMU SERIKALI.
Tunakutakia ushindi katika safari yako ya mfanikio, ila kumbuka daima tupo pamoja mpako maisha yako yaimarike.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048 035,






Jul 10, 2020

Siri Kubwa Ya Kufanya Mabadiliko Kwa Kitu Chochote.

No comments :
Kwa muda sasa, nimekuwa nikijifunza mambo mengi yanayohusiana hasa na mabadiliko ya tabia anayoweza kufanya binadamu hadi kufikia mafanikio makubwa. Kutokana na umuhimu wa hili pia nimekuwa nikiwafundisha wengine kuweza kumudu kubadili tabia zao mbaya zinazoweza kuwazuia kufikia mafanikio makubwa na kujijengea tabia bora za mafanikio katika maisha yao.
Pamoja na harakati zote hizo nzuri, lakini ugumu umekuwa ukijitokeza kwa wengi kushindwa kubadili tabia zile mbaya hasa zinazowasumbua kila siku. Tabia hizi mbaya ninazozizungumzia zinaweza zikawa matumizi mabaya ya pesa, ulevi, uasherati, uvivu, kutokujiwekea akiba, malengo na nyinginezo nyingi ambazo kwa vyovyote vile ni kikwazo kikubwa katika kufikia mafanikio makubwa.
Hata hivyo kutokana na kujifunza nilikuja kubaini kwamba tabia zote hizo mbaya kila mmoja wetu anauwezo wa kuzitawala.  Inaweza ikawa ngumu kidogo kueleweka kwako lakini uwezo huu wa kuzitawala unakuja kwako,  ikiwa tu utatambua siri kubwa iliyofichika katika mabadiliko yoyote unayohitaji katika maisha yako. Kwa kujua siri hii utaweza kubadili chochote unachokitaka katika maisha yako.
Kumbuka kila kitu duniani kina uwezo wa kubadilika. Kama mabadiliko yalikuwepo na yataendelea kuwepo. Amini maisha yako pia yanauwezo wa kubadilika na kuwa mazuri, hata kama kwa sasa upo kwenye hali ngumu kiasi gani. Kitu pengine ambacho unajiuliza utawazaje kuzitawala tabia zako zinazokutesa na kukusumbua kwa sasa?

Hiyo ni rahisi sana. Utaweza kumudu kubadili tabia zako ikiwa tu wewe utakuwa makini na tabia ile inayokusumbua. Kama unasumbuliwa na matumizi mabovu ya pesa kitu cha kufanya hapo ni kuwa makini na matumizi hayo unayoyafanya. Hapa ni lazima ujenge utaratibu wa kila shilingi unayoitumia kuiwekea kumbukumbu au kuandikia mahali.
Kama una tatatizo kubwa la kutokujiwekea malengo na kuyatimiza, hapa pia ni lazima uwajibike kuhakikisha malengo yako yanatimia kwa gharama yoyote ile. Malengo yako yataweza kutimia kwa kuyafatilia kila siku hatua kwa hatua. Kitendo cha wewe kufuatilia malengo yako hatua kwa hatua mpaka kutimia hiyo yote inaonyesha ni kwa jinsi gani uko makini na kile unachokifanya.
Kwa hiyo mpaka hapo unaona kuwa siri kubwa ya kufanya mabadiliko yoyote katika maisha yako ipo kwenye kuwa makini na kile kitu unachotaka kukibadili. Wengi wanashindwa kufikia malengo yao na kutofanikiwa kutokana na kutokuwa makini katika hili. Kwa tafsiri nyingine unapokuwa makini inamaanisha nguvu zote za uzingativu unakuwa unazielekeza hapo.
Unaweza ukaanza sasa kubadili maisha yako  na kuwa na maisha ya tofauti kwa kuwa makini kwa yale mambo ambayo hutaki yawe katika maisha yako. Hii itakusaidia kumudu kufikia ndoto zako ulizojiwekea. Bila shaka unajua ama umeshawahi kusikiwa kwamba watu wote makini mara nyingi kufanikiwa kwao ni rahisi. Na huo ndio ukweli.
Kwa kadri utakavyozidi kuongeza umakini kwa jambo ambalo hulitaki liwe sehemu ya maisha yako ndivyo utakavyojikuta unamudu kulitawala kwa sehemu kubwa tabia zako na hatimaye kufanikiwa. Hii ni siri muhimu kuijua na inanguvu ya kubadilisha maisha yako na chochote kile kinachokusumbua.
Tunakutakia safari njema katika kufikia mafanikio makubwa.
Kwa elimu na maarifa bora ya kuboresha maisha yako, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0687449428



Jul 9, 2020

Kama Hujui, Ndoa Imara Ni Tamu Kuliko Fedha.

No comments :
Karibu tena mpenzi msomaji wa mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO. Karibu tena katika siku nyingine ya kuweza kujifunza yale yote yaliyomuhimu kuweza kuboresha maisha yetu. Katika makala yetu tutaangalia umuhimu wa kuwa na ndoa bora ambayo inaweza ikatusaidia kufikia mafanikio makubwa. Kumbuka, unapokuwa katika migogoro mingi ya kifamilia itakuwa ni ngumu kwako kufanikiwa kutokana na vurugu za hapa na pale kila siku.
Je, wewe binafsi unaamini katika kuoa au kuolewa, kwamba ni muhimu sana kwa maisha ya binadamu? Kama huamini sana katika jambo hilo, huenda inabidi uanze kuamini. Kwa nini?
Tafiti za karibuni kuhusiana na furaha maishani, zinaonyesha kwamba, watu waliolewa au waliooa wameonesha kuwa na furaha zaidi kuliko wale wasiooa au kuolewa, bila kujali kipato.
Wale watu wenye kipato kizuri na ambao wameoa au kuolewa wamebainikia kuwa na furaha kwa asilimia kubwa zaidi. Wale watu ambao wameolewa au kuoa, bila kujali kipato chao, wanaripotiwa kuwa na furaha kuliko wale wasiooa au kuolewa, ambao ni matajiri.
Watu sita kati ya kumi ambao wameoa au kuolewa, wanadaiwa kuwa na ridhiko la namna maisha yao yanavyoenda, ukilinganisha na wanne kati kati ya kila kumi ambao hawajaoa au kuolewa.

Inaonyesha kwamba, kuna uhusiano kati ya fedha, ndoa na furaha na ridhiko kwenye maisha ya watu. Watafiti wengi hivi sasa wanakiri kwamba, ndoa ina thamani na maana zaidi kuliko fedha, linapokuja suala la furaha au ridhiko la maisha kwa binadamu.
Mtu mwenye ndoa ya furaha, anakuwa na ridhiko na furaha kubwa maishani, bila kujali pato lake. Yule ambaye hayuko kwenye ndoa, bila kujali pato lake, kiwango chake cha furaha huwa ni cha chini sana. Kama unafikiri natania waulize wenye ndoa ambazo zina usalama ndani yake watakwambia ukweli wa hili zaidi.
Nimesema ndoa ya furaha kwa sababu, mtu aliye kwenye ndoa ngumu, kiwango chake cha furaha kinakuwa chini kuliko kile cha mtu ambaye hayuko kwenye ndoa, bila kujali vipato vyao.
Tafiti zinaonyesha pia kwamba, karibu watu sita kati ya kila kumi walio kwenye ndoa za furaha, ambao wanapato la chini hufurahia maisha yao na wanaridhiko kubwa zaidi. Ni watu watano kati ya kumi tu ya  wale wenye pato kubwa, ambao hawako kwenye ndoa, wanaofurahia maisha.
Hata hivyo, wale walio kwenye ndoa, ambapo pia wanakipato kikubwa, wameonekana kuwa na furaha zaidi. Ni saba kati kati ya kumi kati ya watu hao, ambao wamebainika kuwa na furaha na kuridhishwa na maisha wanayoishi.
Kuna wimbo ambao nimewahi kuusikia ukisema, kwamba, watu wanashangaa wanandoa fulani maskini, kwani kila siku wanawaona wanandoa hao wakitabasamu, pamoja na ‘njaa’ waliyonayo. Ni kweli, walio kwenye ndoa imara, wanajisikia vizuri bila kujali kama wanafedha au hawana.
Wasio kwenye ndoa au wenye ndoa ngumu,  hata kama wanamamilioni ya fedha vipi, maisha yao ni mzigo mzito sana. Kwa nje wanaweza kuonekana kama ni watu walioridhika, wakati kwa ndani wanamashaka makubwa na maumivu yasiyosemekana.
Ndio maana baadhi ya wanauchumi wanasema, watu waliokwenye ndoa imara ni rahisi sana kwao kupata pesa. Urahisi huu unaletwa na ule ukweli kuwa, watu hawa wanafuraha na wameridhishwa na maisha yao, kiasi kwamba huyaona mambo kwa upana wake.
Pamoja na kwamba, watu wengine kwenye ndoa, huwa wanaamini kwamba, wakipata fedha ndipo watakapokuwa na furaha katika ndoa zao, hali ni kinyume.
Ndoa isiyo imara haiwezi kubadilishwa na kuwa imara kwa kupatikana kwa fedha, zaidi italeta matatizo mengine. Lakini ndoa imara ni nzuri na tamu kuliko kuwa na fedha.
Kwa makala nyingine nzuri zaidi endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza kila siku na kuboresha maisha yako. Pia usiache kuwashirikisha wengine kuweza kujifunza kupitia mtandao huu.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0687449428.




  

Jul 8, 2020

UTAISHI MAISHA GANI BAADA YA UONGOZI,MAISHA YA MBABE YAHAYA ADBULY JAMMEH BAADA YA KUONDOLEWA MADARAKANI KWA NGUVU ZA KIJESHI

No comments :

Watu walikuwa wamesimama Baada ya maisha marefu ya shida na mateso hatimaye watu wa Gambia mapema January 2017 walipata kushudia kitu ambacho pengine hawakukitegemea katika maisha yao kwamba yangetokea ,ilikuwa ni siku ambayo wanagambia walikuwa wanafungua ukurasa mpya wa maisha yao na hii ni baada ya kuishi maisha ya Utumwa kwa mda wa miaka 22 chini ya utawala wa Yahaya Jameh (54) ilikuwa ni siku ya furaha na majonzi kwa wengine pia.

Waandamanaji wakina mama, vijana kwa wazee walikuwa wamejazana uwanja wa ndenge wa taifa la Gambia na wengi walikuwa wanalia na kukubujikwa na machozi wengine walikuwa wanatabasamu kuashiria yamekwisha maana waliokuwa wanayashuhudia waliona kama ndoto kwao ,wengi wa wandamanaji walikuwa wamebeba mabango yaliyosomeka "GO AND FEEL THE PAIN "ulikuwa ni Ujumbe wao wa mwisho wakimaanisha Nenda na wewe ukaonje utamu wa jiwe . 

TAZAMA SIMULIZI NZIMA KATIKA CHANNEL YETU YA YOUTUBE VIDEO IPO HAPO CHINI.
USIACHE KU LIKE, SUBSCRIBE NA KUSHARE

Mpoki Buyah kaminah
 Contacts:0762155025 
Contacts:0624027362 Email:mpokibuya@gmail.com



Jul 7, 2020

Hii Ndiyo Silaha Kubwa Ya Mjasiriamali Katika Kufikia Mafanikio Makubwa.

1 comment :
Wahenga walisema: “Maisha ni kuona mbele.” Huu ni usemi unaompa mjasiriamali matumaini ya kusonga mbele pasipo kutumia muda mwingi kuwaza yale aliyokwishafanya.
Katika maisha ya kila siku kwenye ujasiriamali, wajasiriamali wanakumbana na changamoto nyingi. Changamoto hizi wakati mwingine huwasaidia kuona mbele na hatimaye kuwa watu wenye mafanikio.
Kwa mfano, kama mtu anajishughulisha na ujasiriamali halafu akawa anasumbuliwa na mamlaka zinazohusika na urasimishaji wa biashara kwa sababu za kutorasimisha shughuli zake, akiamua kurasimisha biashara yake atafanya shughuli zake bila kubughudhiwa.
Mwisho wa siku atakua kibiashara, hivyo kuchangia maendeleo ya nchi yake kwa kulipa kodi na kuajiri watu. Kwa mjasiriamali wa aina hii hatakuwa na muda tena wa kuanza kuwaza yale yaliyotokea bali atakuwa anaiona dunia yenye matumaini kesho yake.
Atakuwa anafikiria zaidi juu ya siku za baadaye. Atakuwa na malengo ya kuhakikisha anaibadili dunia na wala siyo kusubiri dunia imbadilishe. Ni kwa sababu, akisubiri dunia imbadili, atakuwa miongoni mwa watu wanaosubiri kutupwa kwenye shimo la sahau.

Hii ina maana kuwa, mjasiriamali hatakiwi kukumbuka changamoto za jana kwa lengo la kumpa huzuni na machungu yatakayomsababisha ashindwe kupiga hatua. Bali anatakiwa kuchukulia changamoto hizo kama somo, ambalo litamwezesha kufika anakoelekea pasipo kurudi katika hali yake ya jana, ambayo siyo taswira nzuri katika kichwa chake.
Kama nilivyowahi kusema katika makala zangu za mwaka jana, mwanzo ni mgumu. Leo narudia tena kusema kuwa mwanzo ni mgumu. Mwanzo wa shughuli za ujasiriamali, wakati mwingine utaona kama hakuna anayekujali.
Unaweza kuhangaika siku nzima na hata zaidi ya miezi kadhaa pasipo kupata kile ulichokusudia. Wakati mwingine unaweza kuwa unatafuta msaada fulani ili kukamilisha kile ulichokianzisha ukaambulia patupu! Unaweza kuchekwa na baadhi ya watu, wakiwamo wale uliowategemea kuwa wangekuunga mkono. Pia, unaweza kukutana na upinzani mkubwa kutoka kwa wajasiriamali wenzako, hata kwa wivu wake kana kwamba unapigana vita.
Hata hivyo, ukiamua kuona mbele utavuka vikwazo hivi vyote na kupata kile ulichokusudia. Kuona mbele ni pamoja na kuwa na dira au mweleko wa wapi unataka kuwa. Mjasiriamali mwenye dira huwa hakati tamaa na haogopi vita kutoka kwa wenzake au kwa baadhi ya watu. Ni mtu mwenye kuangalia ni njia zipi azitumie kufika pale anapotaka kufika.
Ikumbukwe kuwa ushindi huja kwa mtu mwenye kupambana kwa malengo ya kuiona kesho yenye nuru ya mafanikio.
Ushindi hupatikana na kujifunza kila hatua na njia anayoipita mjasiriamali ili kufika kwa mafanikio pale anapopata. Ili kufanikisha hili, mbali ya kuwa na maono, mjasiriamali anatakiwa kuwa mvumilivu na mwenye kuthubutu.
Uvumilivu na uthubutu ni miongoni mwa vitu muhimu sana kwa mjasiriamali. Ni vitu vinavyochangia suala zima la utekelezaji wa dira ya mjasiriamali, ambayo siku zote huwa ni kuona mbele. Kwa hiyo utakuja kutambua kuwa uvumilivu na uthubutu ndiyo silaha ya mjasiriamali kufikia kwenye mafanikio.
Watu wengi wameshindwa kufika popote kwa sababu ya kukosa uthubutu na uvumilivu wa kufanya yale wanayofikiria.
Kwa mjasiriamali anayethubutu na kuvumilia, ataiona kesho yake yenye neema na ambayo itamfaidisha yeye, jamii yake na Taifa kwa ujumla kwani mwendapole hajikwai, akijikwaa hataanguka wala kushindwa kuendelea na safari yake.
Makala hii imeandikwa na Chiraka Muhura wa Gazeti la Mwanachi.

Jul 6, 2020

Misingi 6 Muhimu Ya Kujiwekea, Ili Kujenga Mafanikio Ya Kudumu.

1 comment :
Ili uweze kufanikiwa, ni lazima kujiwekea misingi imara ya kimafanikio itakayokuwa ikukuongoza kila siku. Bila kuijua misingi hii mapema sitashangaa kuona maisha yako yakibaki kuwa yaleyale bila ya kubadilika sana. Kwa kujiwekea misingi hii, inauwezo wa kufanya maisha yako kubadilika kwa sehemu kubwa sana.
Kama misingi hiyo ipo, ni nini kinachokuzuia wewe kufanikiwa sasa? Bila shaka hakuna. Unachohitajika kukifanya ni kutumia misingi hiyo mpaka kufanikiwa. Uwezo na nguvu za kubadilisha maisha yako kwa kadri unavyotaka unao. Kwa kuijua misingi hii, kwako itakuwa chachu ya kukusaidia kuweza kusonga mbele na kujijengea maisha ya mafanikio makubwa:-
Je, misingi hiyo ni ipi?
Hii Ndiyo Misingi 6 Muhimu Ya Kujiwekea, Ili Kujenga Mafanikio Ya Kudumu.
1. Kaa mbali na watu hasi.
Kama vile ambavyo ilivyo kompyuta inaweza ikaharibiwa na virusi na kuharibika kabisa, hata wewe maisha yako yanaweza kuharibiwa vivyohivyo lakini ikiwa una watu hawa hasi wengi wanaokuzunguka. Unapokuwa na watu hasi inakuwa ni rahisi sana kwako kuweza kuua mipango na malengo mazuri uliyojiwekea.
Ninajua watu hawa wanaweza wakawa ni rafiki zako au ndugu kabisa, lakini hiyo haina namna tena kwako, zaidi ya kuachana nao. Ikiwa utaendelea kung’ang’ania kuwa na watu hawa hasi utarudishwa nyuma sana katika maisha yako. Ili kuokoa maisha yako ni lazima kukaa mbali nao na kutafuta marafiki chanya watakaokupa hamasa ya kufanikiwa zaidi. Kukaa mbali na watu hasi ni msingi mzuri kwako unaotakiwa kuujua.

2. Wekeza kila siku katika maisha yako.
Huu ni msingi muhimu sana kujiwekea ili kuwa na mafanikio ya viwango vya juu. Kama katika maisha yako unawekeza kila siku, tambua baada ya muda kidogo kuanzia sasa utakuwa mbali sana kimafanikio. Pengine unaweza ukaanza kusema ‘oooh mimi sasa sina pesa, sina mtaji hili halinihusu nitawekeza vipi sasa hapa?’
Sikiliza, hauhitaji kuwa na pesa ili kuwekeza. Anza na kuwekeza kwanza kwenye akili yako kwa kujifunza kupitia vitabu au semina mbalimbali. Maisha yako yatakuwa ya thamani sana kila utakavyozidi kufanya uwekezaji huu. Maarifa utakayoyapata huko kwani yataweza kukusaidia kuwekeza katika maeneo mengine na kufanikiwa zaidi pale utakapopata mtaji unaouhitaji.
3. Kuwa wewe kama wewe.
Kuna wakati wengi wetu huwa ni watu wa kutaka maisha ya kuwapendezesha wengine. Nikiwa na maana kutaka kuishi maisha kama wengine wanavyoishi. Hiki ni kitu hatari sana kwako kwa sababu unakuwa unaishi kwa kufuata bendera ama wengine wanavyoishi na kujikuta unakuwa mtu wa kupoteza mwelekeo.
Ili uweze kuishi kwa mafanikio ni vizuri ukajijengea msingi wa kuishi maisha yako ukiwa wewe kama wewe. Kwa kuishi wewe kama wewe itakulazimisha kutambua  unataka nini kwenye haya maisha, ni lini utafikia mipango yako uliyojiwekea na unataka kitu gani kikusaidie kufikia malengo yako. Huo ndiyo msingi muhimu pia kuujua kwa ajili ya mafanikio yako ya leo na kesho.
4. Jiwekee mipaka katika maisha yako.
Ishi maisha yako kwa kujiwekea mipaka. Usije ukaruhusu kila mtu kuingilia maisha yako kwa jinsi anavyotaka hata awe ndugu wa karibu kiasi gani. Bila shaka umeshawahi kuona watu ambao maisha yao yanaharibiwa kutokana na kuingiliwa na watu walio karibu nao. Na hii yote imekuwa ikitokea kutokana na wahusika kushindwa kujiwekea mipaka iliyoimara katika maisha yao.
Mipaka hii unatakiwa ujiwekee katika maeneo mabalimbali kama vile katika muda, kazi zako za kawaida na wakati mwingine kwenye biashara zako unazozifanya. Kwa kufanya hivyo watu wako wa karibu watakuwa hawako huru sana kuingilia yale maeneo uliyojiwekea mipaka maana wakifanya hivyo watajua utakuwa mkali au hutakubali kiurahisi. Hiyo itakusaidia kukujengea msingi mwingine imara wa mafanikio yako.
5. Kuwa king’ang’anizi wa mafanikio.
Kwenye maisha yako kitu ambacho hutakiwi kukiruhusu ni kushindwa kiurahisi. Kama ikitokea umeshindwa katika jambo kwa namna  moja au nyingne, jaribu kutafuta njia ya kulifanya jambo hilo kwa namna ya tofauti mpaka kufanikiwa. Unapokuwa king’anga’nizi wa mafanikio huo utakuwa msingi bora kwako unaojitengenezea wa kufikia mafaniko makubwa.
Maisha ni kusonga mbele. Ng’ang’ania mafanikio yako mpaka uyaone hata kwa gharama yoyote ile. Usiruhusu kitu kikakukatisha tamaa. Kama unafikira za nyuma unazoziweza kwa kudhani kuwa ulikosea eneo fulani ni bora ukaachana nazo fikra hizo kwa sasa, kwa sababu hazitakusaidi kitu chochote zaidi ya kukwamisha wewe. Yaliyopita yamepita, songa mbele.
6. Jijengee ukomavu wa fikra.
Ili uweze kufanikiwa inatakiwa ifike mahali fikra zako ziwe zimekomaa na kuweza kutambua kila hali inayojitokeza katika maisha na jinsi ya kuweza kukabiliana nayo. Kwa mfano, inapotokea kushindwa au ukakosea katika jambo fulani unakabiliana vipi na kushindwa huko bila kuumia au kujiona hufai na kisha kuendelea mbele.
Hakuna kingine zaidi ya wewe kuwa na ukomavu fulani wa fikra utakao kuwezesha kusonga mbele. Ukomavu huu ni rahisi kuupata, utaupata tu ikiwa wewe ni mtu wa kujifunza mambo mbalimbali ya kimafanikio kama unavyofanya sasa hivi. Bila kufanya hivyo hutaweza kuhimili mawimbi mengi ya maisha yanayojitokeza kwa upande wako.
Kumbuka hii ni sehemu ya misingi ambayo unaweza ukajiwekea kama nguzo ya mafanikio yako. Lakini, kwa kutumia kijitabu chako kidogo cha kujifunzia unaweza ukaongeza misingi mingine ambayo unaona kwako inafaa kukuongoza katika safari ya mafanikio. Bila kujiwekea misingi binafsi, utayumbishwa sana katika maisha kwa mambo mengi na itakuwa ngumu kufanikiwa.
Tunakutakia kila la kheri katika safari ya mafanikio, endelea kuwashirikisha wengine kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kila siku kwa kujifunza na kuhamasika zaidi.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 04 80 35,




Jul 5, 2020

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuachana Na Tabia Ya Kujihukumu.

No comments :
Kuna wakati katika maisha yako unaweza ukajiona umekosea hili ama lile na lile na kuhisi umeharibu maisha yako kabisa. Kukosea kwa mambo hayo ambayo unaona kabisa ulitakiwa kuyafanya kiusahihi lakini yamekuwa sivyo ndivyo, hali hii hupelekea kuumia moyo na kujihukumu kila wakati.
Ni hali ambayo huwa inatukuta wengi wetu nakujiona ni wakosefu kutokana na kuhukumiwa huko. Hali hii inapotokea kwa muda huwa siyo tatizo kubwa sana lakini inapozidi hapa ndipo ambapo inakulazimu kutafuta tiba ya kukutoa huko kwenye kujihukumu.
Inawezekana ukawa ni miongoni mwa watu ambao huwa wanajihukumu sana ama ulishaona watu wako wakaribu wakiwa hivyo. Kama ni hivyo unatakiwa kuchukua hatua zitakazo kufanya uachane na kujihukumu huko ambako kunakupotezea furaha.
Fuatana nasi katika makala hii kujua hatua muhimu unazotakiwa kuchukua ili kuachana na tabia ya kujihukumu:-
1. Acha kujilinganisha na wengine.
Kama una tabia ya kujilinganisha na wengine sana ni lazima utakuwa mtu wa kujihukumu ndani yako iwe kwa vibaya au vizuri. Ikiwa itatokea wale unaojilingisha nao wakawa wamekuzidi kimaisha kwa sehemu kubwa ni lazima utajihukumu vibaya na kujiona wewe pengine hufai na si chochote katika maisha yako.
Watu wengi ambao huwa wanatabia hii ya kujilinganisha na wengine, ni watu ambao huwa wanajihukumu sana tena kwa vibaya. Kwa kadri wanavyozidi kujihukumu badala ya kuboresha maisha yao ndivyo hujikuta wanaya bomoa zaidi. Na hiyo huwa inatokea kwa sababu huwa wanashindwa kuchukua hatua na kubaki kujihukumu.
Ili uweze kutoka hapo na kuweza kuishi maisha ya furaha na yasiyo ya majuto unalazimika wewe binafsi kuachana na tabia ya kutokujihukumu tena. Unatakiwa kuishi wewe kama wewe kwa kukimbia mbio zako mwenyewe na siyo kuiga maisha ya watu ambayo yanaweza yakakuumiza na kukutesa siku zote.

2. Jiamini wewe kama wewe ulivyo.
Unapokuwa unajiamini wewe binafsi kuwa unaweza inakuwa siyo rahisi sana kwako kuweza kujihukumu bila sababu. Ni lazima utambue kuwa una uwezo mkubwa ndani yako usioweza kuzuiliwa na kitu chochote. Hivyo, ni muhimu kuutumia uwezo huo ulionao ndani yako kuweza kukufanikisha.
Jifunze kuchukua hatua mathubuti ambazo zitakupelekea wewe uweze kujiamini. Kama kuna kitu huna iwe maarifa au chochote kile weka utaratibu wa kujifunza au kupata kitu hicho. Kwa kuwa na maarifa hayo hiyo itakuwa ni chachu kwako mojawapo ya kuweza kukufanya ujiamini na hutoweza tena kujihukumu ndani yako.
Ukijaribu kuchunguza kidogo, utaelewa kwamba watu wengi ambao huwa hawajimini mara nyingi ni watu ambao ni wa kujihukumu sana kwa mabaya na kutilia shaka uwezo wao mkubwa walionao. Ili uweze kuachana na kujihukumu nguzo mojawapo muhimu kwako ni kujiamini.
3. Chukua hatua.
Badala ya kukaa na kuzidi kujihukumu chukua hatua za kuweza kukutoa hapo ulipo. Unaweza ukachukua hatua za kuachana na maneno ya wanaokuona huwezi, umeshindwa na pengine hutafanikiwa, hayo yote yanayokufanya uanze kujihukumu. Kama utaendelea kujihukumu tu, itakuwa ni ngumu sana kwako kuweza kufanikiwa.
Kwa kufuata hatua hizo tatu muhimu yaani kujiamini, kuacha kujilinganisha na wengine na kuchuua hatua ni njia muhimu sana ya kukusaidia kuondokana na kujihukumu.
Kwa makala nyingine nzuri zaidi endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza kila siku na kuboresha maisha yako.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048 035,

Jul 4, 2020

Watu Watano Hatari Ambao Hutakiwi Kufanya Nao Biashara.

No comments :
Ili uweze kufanikiwa katika biashara unayoifanya ni muhimu kufanya biashara na watu sahihi ambao wanaweza kukusaidia hata wewe kuweza kusonga mbele. Watu hawa wanaweza wakawa ni wateja wako ama timu nzima inayokuzunguka na kukusaidia kukua katika biashara yako unayoifanya.
Inapotokea ukajikuta ukawa na ‘timu’ au watu unayofanya nayo biashara ikawa siyo sahihi sana kwako hapo ndipo matatizo na kushindwa mara nyingi huweza kuanza kujitokeza. Watu hawa ndiyo ambao tutawajadili katika makala hii, wale wanaoweza kutukwamisha na kutufanya tushindwe kufikia ndoto zetu tulizojiwekea.
Ni watu ambao tunawajua na tunashirikiana nao mara kwa mara katika shughuli tunazozifanya kila wakati za kibiashara. Kitu cha msingi na cha kujiuliza ni watu gani hasa ambao unatakiwa kuwaepuka na ambao wanaweza wakawa ni hatari kwa maendeleo ya biashara yako leo na kesho?
Hawa Ndiyo Watu Watano Hatari Ambao Hutakiwi Kufanya Nao Biashara.
1. Watu wanaokubali kila kitu.
Hawa ni watu ambao kila kitu wanachoambiwa huwa ni wepesi wa kukubali. Mara nyingi ni watu ambao hawana misimamo na wakati wowote wanaweza kuyumbishwa. Unapokuwa na watu kama hawa katika timu yako ya biashara inakuwa ni rahisi hata kwako wewe kuweza kukuangusha wakati wowote bila kutegemea.
Inapotokea kidogo tu wakapewa ushawishi na mtu mwingine pia ni rahisi kwao kuweza kukubali kwa sababu hiyo ndiyo asili yao. Kama unataka kufanya kazi au biashara yako vizuri ikafanikiwa zaidi, hakikisha unafanya kazi na watu wenye misimamo imara ambayo haiyumbishwi hovyo. Ikiwa utafanya kazi na watu hawa ‘Yes Man’ ipo siku watakukwamisha tu.

SOMA; Sababu 10 Zinazofanya Biashara Nyingi Mpya Zishindwe Kuendelea.



 2. Watu wanaochochea maneno.
Ni mara nyingi sana hawa ni watu ambao huwa tunao katika kazi zetu na pengine katika timu zetu za biashara. Hawa ni watu ambao mara nyingi hujifanya ni watu wa kupeleka sana habari kwa bosi wakati mwingine habari hizo wanazozipeleka zinaweza kuwa hata siyo za kweli kwa namna moja au nyingine ilimradi tu wazifikishe.
Unapokuwa na watu wa namna hii hata kama ni wawili katika bishara yako hicho ni kitu cha hatari kwako. Watu hawa wanakuwa wanauwezo mkubwa wa kuweza kuiharibu ama kuibomoa ‘Staff’ yako kwa jinsi wanavyoweza. Watu hawa wakati mwingine hufahamika kama wambea ambao kila mara hutaka kujifanya wako karibu na bosi, hivyo ni muhimu kuwaepuka sana katika kazi zetu na biashara kwa ujumla.
3. Watu wanaojua kila kitu.
Ni watu ambao huwa hawapo tayari kuelekezwa kitu kutokana na wao kujifanya wanajua kila kitu. Kama katika biashara yako una watu wa namna hii iwe wateja au wafanyakazi wako ama wafanyakazi wenzako hii itakupa tabu na shida kubwa sana katika suala zima la utendaji wa kazi.
Kwa maana kila utakachotaka kumwambia mtu wa namna hii, hata kama kuna sehemu amekosea utashindwa kwa sababu yeye anajua kila kila kitu. Najua bila shaka kwa namna moja au nyingine umewahi kukutana na watu wa namna hii katika eneo ulipo na unajua vizuri usumbufu wa watu hawa kuwa ni mkubwa.

SOMA; Mambo 12 Ya Kuzingatia Kama Unataka Kujiajiri.

 4. Watu wanaobadilika badilika.
Katika biashara yoyote unayoifanya, moja ya watu hatari wa kuwaepuka ni watu hawa wanaobadilika badilika kila wakati. Watu hawa mara nyingi huweza kubadilika zaidi kutokana na mambo mengi waliyonayo ndani mwao. Kitu kimojawapo kinachoweza kuwapelekea wao kubadilika zaidi ni tamaa walizonazo na kutokuwa waaminifu.
Unapoamua kufanya biashara na watu wa namna hii inakuwa siyo rahisi kwako kuweza kufanikiwa. Hii ni kwa sababu dakika na muda wowote ule ni rahisi sana kwao kuweza kukugeuka na inakuwa ni rahisi kuweza kukupa hasara ambayo hukutegemea. Dawa pekee ya kuweza kukwepa matatizo hayo ni kuwaepuka watu hawa kwa namna yoyote ile unayoweza.
5. Watu wanaolalamika sana.
Unapokuwa unafanya biashara na watu wa namna hii watakufanya ujihisi au uone kuwa wewe unakosea katika kila kitu. Hawa ni watu wenye tabia ya kulalamikia mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na huduma, pengine kwa kuona kwao mbovu au wananyonywa kwa namna moja au nyingine lakini ilimradi tu walalamike.
Ni watu ambao kiuhalisia ukiwa nao pamoja katika eneo la biashara ni rahisi sana kuweza kukuvunja hata moyo. Upo wakati utafika ambao unaweza ukahisi kweli kwa wanayolalamikia inaweza ikawa ni kweli kumbe hakuna hata ukweli wa kitu hicho hata kidogo kama wao wanavyodai iko hivyo.
Kumbuka, kama nilivyosema mwanzo unapokuwa na watu hawa inakuwa ni vigumu kwako kuweza kufanikiwa katika eneo la biashara unallolifanyia hata ufanyaje. Lakini kwa kifupi, hao ndiyo watu ambao tunao katika maeneo yetu ya kazi na ni muhimu kuwaepuka ili kuweza kufanikiwa zaidi.
Tunakutakia kila la kheri, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika zaidi. Pia hakikisha unawashirikisha wengine waendelee kujifunza kupitia mtandao huu.
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
0713 04 80 35,


Jul 3, 2020

Ni Ipi Imani Yako Kuhusu Mipango Uliyonayo?

No comments :
Watu waliowengi ni kawaida kusikia wakisema jipe IMANI Mungu atakusaidia ufanikiwe au bora imani tu! utafanikiwa. 

Pengine hali hii inatokana na msukumo ambao wamekuwa wakiupata kutoka kwa viongozi wa dini, ambao mara zote wamesisitiza waumini wao kuwa na IMANI; lakini..pasipo kuwambia, ni jinsi gani ya kuwa na hiyo IMANI. 

Huwezi kuwa na IMANI hivihivi kutokea hewani tu! ni lazima IMANI yako ijengeke kutoka kwenye msingi fulani. 

Kwa mfano msingi wa IMANI juu ya kupata PESA au MAFANIKIO ni kuanza KUTAMANI kitu fulani, halafu unapanga MPANGO wa jinsi ya kupata hicho kitu unachokitamani. 

Kutokana na MPANGO, utatengeneza mchakato wa utekelezaji (mpango kazi) na hapa utatambua majukumu yako ya kufanya kila siku. 

dirayamafanikio@gmail.com


MPANGO ambao umejiwekea utaratibu wa kuupitia kila siku, utakujengea IMANI kwamba siku moja utafanikiwa kupata hicho unachotamani, kwasababu mpango utakuonyesha njia inayokwenda kufikia kile unachokitaka. 

IMANI yako iliyojengwa katika msingi huu, inakufanya uweze kuwapuuza wakatisha tamaa wote ambao wamejaa sana mitaani kwetu. 

Kwa hiyo, tunajifunza kwamba ni lazima tupange MIPANGO ya kupata PESA au kile tunachotamani kuwanacho. Japokuwa kuna imani kwamba mipango yote inapangwa na MUNGU, hivyo wasiojua ukweli huu hawaoni haja ya kupanga MIPANGO. Watu wengi wanadai kwamba wao wanaishi kwa IMANI na wanaichukulia siku kama ilivyokuja. Hii inamaanisha kwamba watu hawa huwa hawapangi siku yao, mwezi na hata mwaka. 

Mungu wetu amekwishatupatia akili ya kutambua baya na zuri na pia tumepewa zawadi ya uwezo wa kupiga picha ya akili, ili kusudi tuweze kushiriki kwenye mchakato wa uumbaji na kutengeneza vitu mbalimbali kupitia MIPANGO. 

Kwa kifupi ni kwamba, unahitaji MPANGO kuamini katika IMANI na ukweli ni kwamba: 
“yeyote asiyekuwa na MPANGO wa kupata pesa hana IMANI ya kupata PESA”

Unahitaji Mpango kazi wa kuamini kuwa utapata siku moja kile unachotamani kukipata. Kumbuka kuwa IMANI ya kweli inayojionyesha katika vitu viwili; yaani MPANGO na MATARAJIO. 

IMANI siku zote, inatanguliwa na mawazo ya kitu Fulani (KUTAMANI), na baadae MPANGO KAZI (utekelezaji), ambao unakufanya upate kutambua majukumu ya kutimiza kila siku. 

Utekelezaji wa majukumu yako ya kila siku unakupa MATARAJIO ya kufanikiwa. Matarajio ndiyo yanakujengea IMANI ya kwamba utafanikiwa siku moja. 

Kwahiyo, MPANGO kwa maandishi juu ya kupata PESA au mafanikio yoyote, ndiyo inaonyesha matendo makuu ya kwamba UNAAMINI utapata pesa au mafanikio. 

Jul 2, 2020

Ukifanyia Kazi Mambo Haya Mara Kwa Mara, Yatakufikisha Kwenye Ndoto Zako.

No comments :
Kila mtu anatamani kuzifikia ndoto za maisha yake ya mafanikio. Kwa sababu hiyo kila mtu huchukua hatua anazoziona yeye zinamfaa ili kutimiza malengo hayo. Je, ni wangapi wanajua kuwa huwa wanachukua hatua sahihi au la.?

Katika makala haya, ni lengo langu ni kukumbusha wewe, mambo ya msingi na kama utayazingatia mambo haya yatakusaidia wewe kuweza kukufikisjha kwenye ndoto zako za mafanikio. Je mambo hayo ni yapi?


1. Andika malengo yako.

Najua malengo yako unayajua vizuri tu, lakini kuna sababu muhimu sana kwa wewe kuyaandika malengo yako tena. Chukua kalamu na karatasi, na andika vitu vyote unavyotaka kuvifikia kwenye maisha yako.

Fikiria juu ya kitu ambacho unataka kufanya au unahitaji kukifanya. Inaweza kuwa kitu chochote kama malengo ya afya au malengo ya biashara yako. Orodhesha vitu vingi iwezekanavyo, lakini viwe vile unavyotaka kuvifanikisha.


2. Weka vipaumbele vya malengo yako.

Ndio, najua umeandika malengo mengi, lakini ukweli ni kwamba huwezi kuyatimiza yote. Ili uweze kuyafikia malengo hayo,  yagawawe kwa kuzingatia vipaumbele. Unapaswa kujua, malengo yapi uanze nayo na yapi uyaache.

Kwa kuweka vipaumbele itakupa nguvu wewe, ya kuweza kuyafikia malengo yako kwa urahisi. Na ukishaweka vipaumbele, usibabaishwe na malengo mengine yatakayotokea hapa katikati, vipaumbele vyako vinatosha, vitekeleze kwanza.

3. Vunja vunja malengo yako.

Vunja kila lengo kuwa dogo ambapo unajua unaweza kutimiza kwa urahisi. Hakikisha pia unajipa muda wa wewe kutekeleza malengo yako kulingana na wakati uliokadiriwa wa mradi huo uliojiwekea.

Kwa mfano, ikiwa lengo lako ni kusoma kitabu. Usijilazimishe kusoma kurasa mia moja, kwa mara moja, soma kurasa chache na zielewe. Fikiri kama unataka kujifunza kuogelea, je! Ungeingia ndani ya bahari au ungeanza kwanza kujifunza katika dimbwi?

4. Amua kuwajibika.

Lengo kuu ni kuishi maisha bora ya kufikia malengo yetu na kufanya hivyo lazima tuchukue hatua moja kwa wakati mmoja na kwa hiyo tunahitaji msimamo thabiti. Je! Unahakikisha vipi malengo yako yanatimia?

Hapa hakuna ujanja, unatakiwa kuwajibika. Fanya kila linalowezekana kwa wewe kuamua kuwajibika ili kuhakikisha malengo yako yanatimia. Ukikubali kuwajibika nakupa uhakika unaweza kufanikiwa na kufika mbali kimafanikio.

Fanyia kazi mambo hayo na hakikisha unachukua hatua kuona ndoto zako zinatimia.

Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kumbuka, ufalme hauji kwa maneno bali unakuja kwa vitendo,...chukua hatua. 
 Nikutakie kila la kheri,
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA NDOTO ZAKO ZITUMIE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
Mawasiliano, Whats app; 0713048035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com




Jul 1, 2020

MAMBO YA KUJUA KABLA HUJAACHA KAZI.

No comments :

Naamini umejifunza masomo ya kuyajua kabla hujaacha kazi, lakini pia mbali na masomo hayo hapa kuna mambo ya kuyajua kabla hujaacha kazi.


Haya ni mambo ambayo unatakiwa ujikumbushe ili kujenga msingi mzuri wa ujasiriamali. Naomba twende pamoja kujifunza mambo hayo;-

  Jambo #1. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa ujue, jinsi ya kubadilisha bahati mbaya na kuwa bahati nzuri.

Kama hujui jinsi ya kubadilisha bahati mbaya, na kuwa bahati nzuri, usijaribu kuacha kazi utajiumiza sana. Ujasiriamali una mambo mengi sana ya changamoto.

Hivyo kwa kadri unavyokutana na changamoto ngumu kabisa, unatakiwa ujue jinsi ya kuzibadilisha changamoto hizo na kuwa bahati nzuri. Kama ukishindwa, basi tulia na ajira.

 Jambo # 2. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kujua, ni shughuli zipi zinatengeneza biashara ya mafanikio.

Biashara haihusishi mauzo tu peke yake. Kama ndio umetoka kwenye ajira na una akili ya kuwaza mauzo peke yake, utakwama. Unatakiwa ujue biashara inahusisha mambo mengi.

Zipo shughuli nyingi zinazotengeneza mafanikio ya biashara kama huduma kwa wateja, usafi, au mawasiliano mazuri na wateja. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kuzingatia haya kwanza.


 Jambo  #  3.  Kabla  hujaacha kazi,  unatakiwa  ujue,  umuhimu  wa kujiendeleza binafsi.
Kama utaingia kwenye ujasiriamali na umegoma kujiendeleza, utashindwa sana, kwa sababu kwenye ujasiriamali zipo changamoto nyingi na zinazotaka kichwa chako kiwe kizuri.

Na kwa sababu ya changamoto hizo inatakiwa muda wote uwe bora na pia wanaokuzunguka wawe bora. Yote haya utayapata kwa wewe kuamua kujifunza na kujinoa.

 Jambo # 4. Kabla hujaacha kazi, jifunze kidogo elimu ya uhasibu.

Kwa kujifunza elimu hii, itakusaidia sana kujua mtiririko wa pesa katika biashara, pia itakusaidia kujua bajeti ya biashara na yako kitaalamu zaidi, tofauti na ungekuwa hujui.

Kama kwako ni ngumu kujifunza elimu hii, basi, biashara ikikua kidogo, ajiri angalau mhasibu anayejua vizuri na uwe unamlipa. Hii itakusaidia kujenga biashara yako kwa mafanikio.

 Jambo la #5. Kabla hujaacha kazi, kumbuka kuwa safari yako ya mafanikio inaanzia ndani ya moyo na roho yako.

Hapa kabla hujaacha kazi unatakiwa ujiulize, ndani mwako unaona mafanikio? Hii ikiwa na maana kwamba mafanikio yako lazima uyaone ndani kwanza kabla hayajaonekana kwa nje.

Hata kwa hatua unazochukua inatakiwa zidhihirishe kile kilicho moyoni mwako. Kama mafanikio moyoni huyaoni usijaribu kuacha kazi, maana hata kwenye ujasiriamali hutafanikiwa pia.

 Jambo #6. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa ujue, kitu chochote unachotaka kukiuza, kina bei tatu za msingi. Bei ya chini, bei ya kati na bei ya juu.

Kama utachagua kuuza kitu hicho kwenye bei ya chini, unatakiwa ujue pia dakika yoyote ataibuka mtu wa kushindana na wewe. Ili uwe mshindi katika kuuza kwa bei ya chini unatakiwa uwe na njia nzuri sana ya kuuza bidhaa yako.

Kama utachagua kuuza bidhaa zako kwa bei ya juu, pia jifunze kutoa huduma bora. Kama huelewi hili vizuri, nenda kwenye hotel zinazotoa huduma kwa bei ya juu uone vizuri kile wanachokifanya ni nini kwenye biashara zao.

  Jambo #7. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kujua na kukumbuka, mauzo=kipato.

Kama utakuwa unataka kuacha kazi na ukajigundua kwenye mauzo haupo vizuri., nikwambie tu, jifunze kuuza kwanza, halafu ndo uache kazi. Kama huwezi kuuza, hiyo ni shida kwako kufanikiwa.

Tunaambiwa asilimia kubwa ya watu wengi huwa tunazaliwa hatujui kuuza. Hata hivyo unaweza kujifunza kuuza ili uwe mjasiriamali mzuri, vinginevyo utakwama. Anza kujifunza kuuza, utafanikiwa.


 Jambo # 8. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kujua vizuri jinsi ya kutumia pesa zako vizuri.

Ni wazi wajasiriamali walio wengi, hawajui jinsi ya kutumia pesa zao vizuri. Wanajikuta wanatumia tu pesa hawajui zitarudi vipi. Sasa usiingie kwenye mtego huo.

Ili uwe mjasiriamali mwenye mafanikio, unatakiwa kujua kila shilingi ya pesa yako inakwenda wapi. Ukiona unafika sehemu unashangaa pesa zako zimeenda wapi, bado hujajua jinsi ya kuzitumia.

  Jambo #9. Kabla hujaacha kazi, anzisha biashara ya pembeni kwa ajili ya kujifunza ujasiriamali.

Hakuna ambae anaweza akaendesha baiskeli pasipo kujifunza. Hata kwenye biashara mambo yako hivyo, unatakiwa uwe na biashara ya mazoezi kabla hujaacha kazi na kuingia kwenye ujasiriamali.

Usije ukafanya kosa la kuacha kazi, wakati hata hujui ABC za ujasiriamali ziko vipi. Ukiwa unafanya biashara huku umeajiriwa, itakupa ukomavu wa wewe kufanikiwa kibiashara.

 Jambo   #10.   Kabla   hujaacha   kazi,    tafuta   mshauri   wa mafanikio/mentor.

Ni ngumu sana kwa wajasiriamali wengi, kuwa na mshauri wa mafanikio, lakini kabla hujaamua kuacha kazi, hakikisha una mshauri huyu wa mafanikio ambae atakuongoza katika njia sahihi.

Kama unaona kumpata mshauri wako wa mafanikio ni ngumu, basi amua kufanya vitabu viwe ndo mshauri wako. Kwenye vitabu unatakiwa kujifunza sana na itakusaidia kufanikiwa.

  Jambo #11. Kabla hujaacha kazi, tafuta mtandao wa wajasiriamali.

Usije ukakimbilia kwenye ulimwengu wa ujasiriamali, kama huna mtandao wa ujasiriamali. Kitendo cha kuwa na mtandao huu, kitakusaidia sana wewe katika safari yako ya kimafanikio.

Inakubidi utafute mtandao, ambao kwako unaona unakufaa na kukusaidia. Kila wakati jumuika katika mikutano yao ili kupata uzoefu utakaokujenga, kukulea na kukusaidia kufikia malengo.

   Jambo #12. Kabla hujaacha kazi, tazama mtazamo wako.

Ikiwa mtazamo wako unaona tu kwamba ukiingia kwenye ujasiriamali unapata mafanikio ya moja kwa moja, unajidanganya. Inakubidi ujue kwamba zipo changamoto na unatakiwa kuzifanyia kazi.

Ukijua hili, au ukaamua kuingia na mtazamo huu, wa kutambua changamoto za ujasiriamali, utakusaidia kupambana na changamoto zinazojitokeza.

Mwisho; kabla hujaacha kazi, unatakiwa uwe na imani sahihi kwenye ujasiriamali na kuielewa vizuri, misingi sahihi ya ujasiriamali.