google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Mar 11, 2019

Tabia Muhimu Zitakazokusaidia Kukupa Mafanikio Kwa Kiasi Kikubwa.

No comments :
Moja ya sheria ya msingi na ya muhimu katika mafanikio yoyote yale ni kuwa na tabia nzuri. Tabia ni moja ya kitu ambacho ni cha msingi sana katika kukupa mafanikio yale uyatakayo. Ukiangalia wengi wanaoshindwa, chanzo kinaanzia kwenye tabia zao.
Tuchukulie kwa mtu anayataka mafanikio, kuwa na malengo tu peke yake na kuyafanyia kazi haitoshi, lazima mtu huyu awe na tabia zinazoendana na malengo hayo, kama kuwa na matumizi mazuri ya pesa au utunzaji wa muda mzuri.
Unapokuwa na tabia mbaya na huku ukitaka mafaniko, ni wazi hutaweza kufanikiwa na utahangaika sana kufikia mafanikio hayo. Mpaka hapo unaona tabia ni kitu cha msingi sana katika kukufanikisha wewe kwenye maisha yako.
Unaweza ukawa na mafanikio makubwa sana, ikiwa utajenga tabia bora za kukusaidia kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kila wakati. Je, unataka kuzijua tabia hizi ni zipi za kukusaidia wewe kuweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa?

1. Tabia ya kutafuta msaada.
Hakuna mtu ambaye anaweza kufanikiwa akiwa peke yake. Kila mtu anahitaji msaada kwa mtu mwingine hata kama msaada huo ni kidogo sana lakini msaada huo unahitajika ili kuweza kujenga mafanikio ya kudumu.
Unapokuwa unawasiliana na wengine na wakajua changamoto zako, ni rahisi sana kwa wao kuweza kukusaidia wewe na kupiga hatua mbele za kimafanikio. Usijaribu kuishi kipeke yako yako, tafuta msaada kwa wengine na utafanikiwa pia.
2. Tabia ya kuchukua hatua.
Unayo nafasi kubwa sana ya kufikia mafanikio yoyote yale unayoyataka kwenye maisha, lakini kama huchukui hatua nikwambie tu, utakufa kwa msongo wa mawazo. Najua una mawazo mazuri lakini hayawezi kufanya kazi mpaka uchukue hatua.
Huhitaji kuwa na hamasa ili uchukue hatua, wewe chukua hatua kwa hali yoyote uliyonayo. Acha kuendelea kufikiria sana juu ya ndoto zako, chukua hatua. Soma vitu vya kukusaidia na kisha amua kuchukua hatua na ukijenga tabia hii itakusaidia sana.
3. Tabia ya kutokuishi kimazoea.
Maisha ya watu wengi yanakuwa mabaya kwa sababu ya kuishi sana kimazoea. Kuishi kimazoea ni sumu kubwa sana ya wewe kuweza kufikia mafanikio makubwa. Unatakiwa ujue namna ya kuishi nje ya mazoea yako ili uweze kufanikiwa zaidi.
Kila wakati tafuta namna ambayo itakusaidia wewe kuweza kuishi nje ya mazoea yako. Ikiwa lakini kila wakati unaishi kwenye mazea hayo hayo itakuwa ni ngumu sana kwako kuweza kusonga mbele na kupigia hatua hasa za kimafanikio.
4. Tabia ya kusema hapana.
Hii ni moja ya tabia nzuri sana kwako wewe kuindeleza ili kufikia mafamikio. Unatakiwa kujifunza kusema hapana kwa mambo mengi sana. Unatakiwa ujue kusema hapana kwa wanaokupotezea muda wako au kwa yale mambo usiyoyahitaji.
Ikiwa wewe utakuwa ni mtu wa kukubali kila kitu, kwamba kitu hiki kiwe hivi au vile ni ngumu sana kuweza kupiga hatua sahihi za kimafanikioo husika. Jifunze kusema hapana kwa kila kitu ambacho hakina manufaa kwako wewe.
5. Tabia ya kuchukua majukumu yako.
Unatakiwa ujue kila mtu ana changamoto zake za kimaisha, lakini kama unashindwa kuwajibika na majukumu hayo na kila wakati kutaka kulaumu tu watu wengine, hilo tu nikwambie utakuwa ni miongoni mwa watu ambao watashindwa sana.
Nikwambie tu, kubali kuwajibika kwa kila jambo linalokuhusu wewe. Wajibika kwenye ndoto zako, wajibika kwenye maisha yako ya kila siku. Kila wakati ujue jinsi ya kuwajibika na hapo utaweza kupiga hatua za mafanikio sahihi kwako.
Hivi ndivyo unavyoweza ukatumia tabia hizo vizuri na zikakusaidia wewe kuweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kwenye maisha yako kama unavyotaka iwe. Ni jukumu lako wewe sasa kuchukua hatua na kuhakikisha unasonga mbele.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,






No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.