google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 22, 2019

Kama Utakosa Kitu Hiki Sahau Kuishi Maisha Ya Uhuru, Furaha Na Mafanikio.

No comments :
Kama upo kwenye chombo cha usafiri, halafu ni usiku  na tena unataka kusafiri mbali na kwa haraka zaidi, kitu cha kwanza unachotakiwa kuhakikisha chombo hicho inacho ni mwanga wa uhakika. Pasipo mwanga wa uhakika safari yako itakuwa ni ya shida kidogo, unaweza ukaenda lakini si kwa kasi na mwendo ule unaoutaka wewe.
Hata kwenye maisha yako ukitaka kufika mbali kimafanikio kitu kimojawapo unachotakiwa kuwa nacho ni kujifunza kuwa na msamaha. Unapokuwa na msamaha, inakusaidia kuondoa uchungu, hasira, visasi vyote unakuwa umeweka pembeni na matokeo yake unakuwa huru kufanya mambo mengine na kusonga mbele.
Kuishi maisha ya kutokuwa na msamaha, ni sawa na kuendesha gari huku ukiwa umeshikilia breki, kwani kwa kufanya hivyo mwendo wako hautakuwa mzuri, ni rahisi kukosa mwelekeo na hata kupotea kabisa. Unatakiwa kukumbuka unapokuwa na msamaha hiyo inakuweka huru sana wewe kuweza kufikia mafanikio yako.

Unapoamua kuishi maisha ya kutokuwa na msamaha kitu kitakachofatia hapo kwako ni kwa wewe kuishi maisha ya kisasi. Inapotokea ukaishi maisha ya kisasi mwanzo inaweza ikaonekana ni maisha mazuri, lakini nikwambie maisha hayo yanakuwa ni mabaya sana kwako kwani yatakuzuia wewe kuweza kuendelea mbele sana.
Unapokosa msamaha kabisa ujue unakuwa maisha ambayo yanakuwa ya uchungu karibu wakati wote. Unatakiwa kujua ufunguo mojawapo wa furaha ni wewe kujijengea tabia ya kuwa na msamaha. Kama hautakuwa na msamaha sahau kabisa kwa wewe kuweza kuishi maisha ya furaha au maisha ya uhuru.
Kwa mujibu wa wataalumu wa saikolojia na mafanikio, inasemekana moja ya siri muhimu ya kuishi maisha marefu na yenye faida kila siku ni kwamba kabla hujalala, jifunze kumsamehe kila mtu ambae amekukosea. Unapowasamehe watu hao ambao wamekukosea hiyo ni njia ya wewe kuendelea kufanikiwa kwenye mambo yako.
Ni bora ukasamehe na kusahau kuliko ukashindwa kusamehe na kukumbuka. Elewa, kusamehe kila wakati kunaendana na Baraka, lakini kutokusamehe kunakuumiza wewe na kunakupotezea sana milango mikubwa ya Baraka ambayo inatakiwa itokee kwako. Kwa hiyo ipo haja ya wewe kuweza kusamehe kwa namna yoyote ile.
Kabla hujamaliza  siku yako unatakiwa ujue ni watu gani ambao wanahitaji msamaha wako na wasamehe hata usipowaambia. Usichome daraja moto mara baada ya kuvuka mto. Nikwambie huwezi kujua utatumia daraja hilo mara ngapi tena kwa usafiri. Ipo faida ya kuishi maisha ya msamaha, hebu anza leo kuishi maisha hayo uone faida zake.
Jiulize ni wapi unakwama hadi ushindwe kutoa msamaha, je msamaha unaotaka kuutoa kwani unalipiwa? Kama msamaha unaotaka kuutoa ni bure, hebu samehe na kisha baki huru na maisha yako. Maisha yako hayatakuwa mabaya kisa umemeshindwa kusamehe, zaidi utajenga maisha ya mafanikio makubwa kwako.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,











No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.