google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 1, 2018

Kitu Kimoja Ambacho Unatakiwa Kukijua Kuhusu Mafanikio.

No comments :
Kila mtu anataka kufanikiwa. Kila mtu ana kiu, hamasa na nia kubwa ya kuona anafanikiwa kwenye maisha yake. Japokuwa, pamoja na kiu hiyo kipo kitu kimoja ambacho unalazimika ukijue ili uweze kufikia mafanikio hayo.
Kama hutaweza kukijua kitu hicho na huku ukitafuta mafanikio yako, kitakachotokea kwako ni kwamba utakuwa unapata tabu sana kwenye safari ya mafanikio. Kwa lugha rahisi kuna wakati utakuwa huelewi elewi jinsi mambo yanavyokwenda.
Najua safari ya mafanikio ina anza na watu wengi sana, lakini kwa bahati mbaya wengi wanakuwa ni watu wa kuishia njiani. Unajua ni kwa nini, ni kwa sababu ya wengi kushindwa kukujia kitu hicho muhimu katika mafanikio.
Kitu hicho ambacho wewe unalazimika sana kukijua kwenye safari yako ya mafanikio ni kwamba mafanikio yanatumia muda mrefu sana kuyafikia. Hiki ndicho kitu unatakiwa ukiweke kwenye akili yako na kutambua mafanikio hayafikiwi siku moja, yanahitaji muda ili uweze kuyafikia.
Kuna kipindi, wakati naanza kuandika kwenye blog hii nilikuwa nashangaa sana kwa nini inachukua muda mrefu kwa blog hii kuwa na wasomaji wengi. Kwa sababu hii niliamua kujifunza muda halisi wa mafanikio kwa watu waliofanikiwa hasa ni upi.
Nilichokuja kugundua ni kwamba mafanikio yanatumia muda mrefu na si mfupi kama unavyofikiri ili kuweza kuyafikia. Kwa chochote kile unachokifanya, inatakiwa utenge muda wa kutosha ili mpaka kuanza kuona matunda yake.

Kwa mfano, ilichukua muda wa miaka 11 hadi program ya ‘Microsoft’ ya bilionea mkubwa duniani kuanza kufanya kazi na kuleta mafanikio makubwa. Mafanikio yake hayakutokea tu ghafla kuna miaka ilikataika hapa katikati.
Pia ilimchukua miaka 29 kwa Abraham Lincoln hadi kuweza kuwa Rais wa marekani. Ipo mifano mingi inayoonyesha kwamba mafanikio si kitu cha mara moja tu, unatakiwa kuwekeza muda ili uweze kufanikiwa kwenye mafanikio hayo uyatakayo.
Kama utakuwa ni mtu wa kutaka mafanikio na halafu ukategemea mafanikio hayo yakatokea ghafla ghafla kwa muda mchache ni rahisi sana kwako kuweza kukata tamaa na kuona ni kitu ambacho hakiwezekani au mafanikio ni ya watu wa aina fulani tu lakini si wewe.
Kwenye akili yako sasa weka wazi, mafanikio ni safari ya muda mrefu. Unatakiwa kabisa utenge miaka angalau kuanzia 5 hadi 15 ya kutafafuta mafanikio yako  ya kweli na ya kudumu. Ukikurupuka na kutaka mafanikio ya chapu chapu utakwama.
Watu wengi wanakata tamaa kwenye safari ya mafanikio kwa sababu ya kutokujua kwamba mafanikioo yanataka muda mrefu. Katika kipindi cha kutafuta mafanikio yako unatakiwa ujitoe hasa, kuvumilia na kutoa kila ulichonacho hadi ufanikiwe.
Nimekundikia makala haya si kukatisha tamaa bali kukupa ukweli na uhalisia ulivyo. Kama una bisha chunguza mwenyewe kwa watu waliofanikiwa, utagundua wametumia muda mrefu ili kuweza kufanikiwa kwao kwa uhakika.
Kwa kifupi, hakuna mafanikio ya ghafla, hakuna mafanikio ya chapu chapu, unatakiwa kutumia muda na nguvu kujenga mafanikio yako pasipo kukata tamaa, kila siku unatakiwa ujitume kwa kutenga miaka 5 hadi 15 ya mafanikio yako.
Unatakiwa kujua hakuna ambaye atashindwa kama ataamua kufanya kazi kwa bidiii na pasipo kukata tamaa. Kwa mtu wa namna hii ushindi upo mbele yake na unamsubiri kwa hamu kubwa na wewe unaweza kuamua ikawa hivyo kwako.
Kitu cha msingi hapa ambacho unatakiwa kuelewa kwenye makala haya ni kwamba, mafanikio yanatumia muda mrefu kuweza kuyafikia. Hiki ndicho kitu unatakiwa ukiweke akilini mwako wakati unatafuta mafanikio. Ukijua hili mapema hutakata tamaa na  kikubwa kwako endelea kupambana na utafanikiwa.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,










No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.