google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 2, 2018

Aina Ya Watu Wanaoendelea Haraka Kwenye Maisha Yao.

No comments :
Kwenye maisha wapo watu ambao ukiwaangalia kwa haraka wanaonekana ni kama hawaendelei upesi yaani zile hatua za mafanikio kwao zinaonekana zinachelewa kabisa, na wapo watu ambao wanaonekana wanafanikiwa upesi sana.
Hili nafikiri umeshawahi kuliona, na kuna wakati labda ulijiuliza hawa wanaoendelea sana ni watu wa namna gani. Pia ukaendelea kujiuliza kwa nini wao waendelee upesi na wengine wasiendelee upesi? Je, kuna bahati au nini sababu?
Katika makala haya leo tutajifunza aina ya watu ambao wanaendelea sana. Watu hawa ni wa aina gani, karibu tujifunze.
1. Watu wenye mapenzi na kile wanachokifanya.
Watu hawa wenye mapenzi na kile wanachokifanya, ama ‘passionate people’ huwa ni watu wanaofanikiwa. Kwa nini kwao kufanikiwa kunakuwa nje nje ni kwa sababu watu hawa watafanya kila linawezekana hadi kuona wanafanikiwa.
Itafika mahali watu hawa watakosea, lakini kwa sababu wana mapenzi na kitu hicho watakifanya na hadi kuona wanafanikiwa tena kwa kiasi kikubwa kwenye maisha yao. Jaribu kuwatafuta  watu wa namna hii, utagundua wanaendelea kwa haraka sana.
2. Watu wenye nidhamu ya hali ya juu.
Pia kundi lingine la watu ambao wanaendelea kwa haraka ni hili la watu wenye nidhamu kubwa. Nidhamu inawafanya watu hawa wajitume kufanya kile wanachotakiwa kukifanya hata bila kujali kama wana hamasa au hawana hamasa.
Wakati watu wengine wana subiri wapate hamasa ndio wafanye kitu, watu hawa wanajituma tu, pasipo kujali hamasa hiyo. Kwa kifupi ni watu wanaofanya pasipo kujali wanajisikia au hawajisikii ila wao wanafanya, kwa sababu hiyo wanaendelea sana upesi.
3. Watu wanaojitoa mhanga.
Inasemekana pia watu wanaojitoa mhanga juu ya maisha yao, ‘risk taker’ pia ni watu wanaoendelea sana. Watu hawa kwanza hawaogopi kuchukua hatua yoyote, pia hata wakishindwa wanarudi upya tena upesi sana.
Mafanikio yoyote yanawafata watu wa namna hii bila kipingamizi. Mafanikio hayawezi kukwepeka ikiwa unajitoa kweli hata kwenye mazingira ambayo yanaonekana ni hatarishi kwa wengi. Kujitoa huko ndiko kunakowafanikisha sana watu hawa.
4. Watu wanaozingatia jambo moja.
Wale watu ambao mawazo yao wanaweka kwenye jambo moja na kulifanya kwa usahihi, watu hao wanafanikiwa moja kwa moja. Watu hawa mara nyingi hawataki kuzigawanya nguvu zao zikawa katika maeneo makubwa mawili.
Kwa sababu hiyo ya kuweka nguvu zao katika eneo moja hujikuta wakifanikisha mambo yao na kuendelea kwa upesi. Hawa ni watu ambao nasema wanazingatia sana PLAN A ya maisha yao kuliko ile PLAN B. Wanaamini mafanikio yao yapo kwenye ule mpango wa kwanza, hivyo kwa hili hufanikwa.
5. Watu wanaojua kuishi na watu vizuri.
Uzuri wa watu hawa, kwa sababu wanajua kuishi na watu vizuri, hilo linawasaidia kufanya biashara kwa ushirikiano mkubwa, hiyo haitoshi inawasaidia pia kuweza kuwajua wateja kwa wengi kila siku zinavyokwenda.
Unatakiwa kuelewa hivi kwenye maisha hatufanikiwi tukiwa sisi kama sisi, ni lazima tuwe na ushirikino na watu. Kwa kuwa na ushirikiano huo inasaidia sana kuweza kukuza mahusiano yetu kibiashara na hatimaye na sisi kuweza kufanikiwa kwa haraka.
Hizi ndizo aina za watu ambao kwenye maisha huwa ni watu wa mafanikio au kuendelea sana. Kama unataka kuwa miongoni mwao unaweza ukavuta tabia mojawapo hapo na wewe ukawa ni miongoni mwa watu wenye mafanikio ya kasi katika sayari hii.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.