google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Dec 3, 2018

Marafiki Ambao Hutakiwi Kuwa Nao Kama Unataka Kufika Mbali Kimafanikio.

No comments :
Upo mchango mkubwa sana wa marafiki katika kutufikisha kwenye mafanikio. Lakini hata hivyo ieleweke hivi si kila rafiki ni rafiki mwema katika kutusaidia kutufikisha kwenye mafanikio yetu. Wapo marafiki ambao hawafai kuambatana nasi hata kidogo kama tunataka kufanikiwa na kuweza kufika mbali kabisa kimafanikio.
Hapa kati makala haya nataka nikuonyeshe rafiki  ambao hutakiwi kuambatana nao katika safari yako ya kimafanikio. Kama utaamua kuambatana na marafiki hawa ujue kabisa utakuwa unafanya kazi ya ‘makitaimu’ yaani utakuwa huendi mbali sana kimafanikio. Twende sasa pamoja kujifunza aina hii ya marafiki unaotakiwa kuwaepuka.

1. Marafiki wakosoaji.
Aina hii ya marafiki watakakukosoa kila kitu unachokifanya au kile ulichonacho. Watakosoa kwamba ukifanyacho hakifai. Watakosoa utendaji wako wa kazi na hata pia wanaweza kukosoa aina ya maisha unayoishi.
Kuwa na marafiki wa namna hii ambao ni wakosoaji ni sawa na kujitafutia majanga. Hawa ni marafiki ambao unatakiwa uwakwepe sana. Kuendelea kukaa na marafiki hawa huko ni kujipotezea muda wako wewe, kwani hawatakusaidia kufanikiwa.
2. Marafiki wasio na malengo ya kimaisha.
Hawa pia ni aina ya marafiki wabaya sana kwenye maisha yako. Unapokuwa na marafiki wa aina hii unatakiwa kuelewa kwamba upo uwezekano mkubwa hata wewe ukaanza kuishi mfumo wa maisha yao yaani ukaishi bila malengo yoyote.
Marafiki hawa kwa sababu hawana malengo, basi hata muda wao wanautumia hovyo sana. Muda ambao ungetumika kufanya vitu vya msingi wao wanaoupoteza, ukifatilia sababu hasa, utagundua hawana malengo maishani mwao.
3. Marafiki watumiaji.
Hii ni aina ya marafiki ambao muda wao mwingi sana wanawaza juu ya kutumia. Marafiki hawa hawako tayari kuweka pesa kwa ajili ya kuwekeza bali ni kuzitumia. Kila ikifika ijumaa wao ni sherehe kwa kujirusha huku na kule.
Epuka sana marafiki hawa kwani watakufanya wewe ushindwe kuwekeza pesa zako kwa ajili ya kesho. Pia marafiki hawa watakufanya utumie sana pesa zako hovyo bila mpangilio. Kama ukiweza kuwaepuka marafiki hawa basi utajenga mwelekeo wa kufanikiwa.
4. Marafiki wanaopenda ushindani usio na maana.
Hawa ni marafiki ambao kila kitu ukifanya wanataka kushindana na wewe. Kwa mfano, ukinunua kitu hiki na wao wanataka kununua. Ukiwekeza kwenye mradi huu na wao wanataka kuwekeza. Kama unataka kufika mbali kimafanikio, hawa ni marafiki ambao pia hawakufai kabisa
Kuendelea kuwa na marafiki hawa, inabidi utambue wanakupotezea sana nguvu zako nyingi ambazo ungezitumia kuweza kufanikiwa. Kwa kifupi hawa ni marafiki wasumbufu kwako na hawakufai katika kukufikisha kwenye ndoto zako.
Kwa kuhitimisha makala haya, hizi ndizo aina za marafiki unaotakiwa kuwaepuka sana katika maisha yako. Ni jukumu lako sasa kuchagua marafiki waliobora kwako na kuachana na marafiki watakaokurudisha nyuma kimafanikio.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.