google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 3, 2021

Weka Umakini Wako Wote Kwenye Vitu Hivi Na Utafanikiwa.

1 comment :
Kila wakati zingatia kile kinacholeta mabadiliko sana kwenye maisha na unatakiwa kuachana na kile ambacho hakileti mabadiliko kwenye maisha yako. Kama unaendelea kufanya vitu ambavyo havileti matokeo chanya kwako huko ni kujipoteza.
Kwa maana hiyo, kama kuna kitu unataka kukifanya unatakiwa ujiulize je, kitu hiki kina mchango kiasi gani katika kuweza kufanikisha ndoto zangu. Kama unaona kitu hicho hakina machango wowote ni jukumu lako kuweza kuachana nacho mara moja.
Kila wakati weka nguvu zako, muda wako na umakini wako wote kwenye vile vitu ambavyo vinaleta matokeo kwako ya mafanikio tu. Haina maana kupoteza nguvu zako nyingi kwa kufanya kitu ambacho hakina msaada kwako, utakuwa unapotea sana.
Kila wakati ijaze akili yako  mawazo chanya yatakayokusaidia wewe kuweza kufikia ndoto zako. Kila wakati weka juhudi sahihi za kukusaidia kuweza kufanikiwa kwa kufanya vitu vinavyoendana na ndoto yako unayoitaka kuifanikisha.

Usijaribu kupoteza nguvu zako kwa kufanya mambo ambayo hayakusaidii kuweza kutimiza ndoto zako. Ishi kwa faida kwa kufanya mambo ambayo yanakusaidia kuweza kutimiza ndoto zako, kinyume cha hapo hutaweza kufikia ndoto zako.
Tatizo la watu wengi wanapoelekea kwenye kufikia ndoto zao, wanakuwa wanaweka umakini wao kwenye vitu ambavyo hata haviwasaidii. Kwa kufanya vitu hivyo watu hao ndio hujikuta wakipotea karibu kila wakati kwenye kufanikisha ndoto zao.
Ili uweze kufikia ndoto zako, fanya ufanyalo, lakini hakikisha unaweka umakini wako wote kwenye vitu vya msingi vinavyokusaidia kutimiza ndoto zako. Kwa kufanya vitu hivyo ni kweli ndoto zako utaweza kuzifikia hata kama unakutana na changamoto nyingi.
Usiendelee kusita, usiendelee kusubiri, kama unataka kufanikiwa weka nguvu zako zote kwenye mambo yanayoweza kukupa mafanikio. Kama nilivyosema watu wengi hawaweki sana nguvu zao kwenye mambo yaletayo mafanikio yao, zingatia hilo.

Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.


1 comment :

Note: Only a member of this blog may post a comment.