google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 1, 2021

Hiki Ndicho Kitu Kinachokuzuia Kufanya Mabadiliko Kwenye Maisha Yako.

No comments :
Ikiwa kila wakati unajaribu kufanya mabadiliko ya kitu fulani na unashindwa kuleta mabadiliko hayo, basi tambua maumivu ya kushindwa hayajawa makubwa sana ndani yako hadi uweze kuleta mabadiliko hayo.
Kwa mfano, unataka kuwa na mtaji na unashindwa kila mara, basi elewa kabisa maumivu ya kushindwa kupata mtaji hayajawa makubwa vya kutosha. Tuchukulie leo hii, ukaambiwa usipokuwa na mtaji hadi mwaka huu unaisha, utapigwa risasi.
Jiulize utakubali kufa kwa sababu ya kukosa mtaji huo unaoutaka? Bila shaka haitawezekana, utafanya kila linalowezekana kufanikisha hilo. Hivyo, wakati mwingine mabadiliko yanakuja kwenye maisha yako kwa sababu ya kule kuumia sana.

Wakati ulipokuwa shule ulisoma sana na kuhakikisha unafaulu ili kukwepa maumivu ya kufeli. Pia kuna wakati umeweka juhudi nyingi sana ili kukwepa maumivu ya aina fulani na kutafuta mahala sahihi kwako.  

Tunaambiwa kitu chenye nguvu ya kubadili tabia yako na mafanikio ni maumivu. Waulize wote ambao wamefanikiwa na ambao wanafikiri chanya kuhusu mafanikio, watakwambia maumivu yamewasaidia sana kubadilika na kuweza kufika hapo walipo mpaka leo.
Kitu kinachokuzuia wewe kufanya mabadiliko kwenye maisha yako ni maumivu, hujawa na maumivu ya kutosha kuweza kubadilisha maisha yako. Ikiwa utakuwa na maumivu hayo, hutakubali, utafanya kila njia kubadilisha maisha yako.
Tunajua sote maumivu yanauma, kama maumivu yanauma, huwezi kukubali ukabaki na maumivu hayo kwako, lazima utatafuta njia ya kubadilisha maumivu hayo. Hivyo, kila wakati pambana kuweza kuleta mabadiliko juu ya maisha yako.
Mwisho kabisa niseme kwako hivi, utabadili maisha yako, ikiwa utakuwa una uchungu na maumivu ya kutosha, maumivu ya kuchoshwa na hali mbaya uliyonayo na kutaka kubadili maisha yako kabisa, hapo mabadiliko utayaona.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0687449428, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kumbuka, ufalme hauji kwa maneno bali unakuja kwa vitendo,...chukua hatua. 
Nikutakie kila la kheri,
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA NDOTO ZAKO ZITUMIE.


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.