google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 23, 2019

Kama Utapoteza Jambo Hili, Hutalipata Tena Maishani Mwako.

No comments :
Katika kijiji kimoja kulikuwako na watu watatu ambao walikuwa na safari ndefu sana ya kuelekea mbali na mahali walipokuwa wanaishi, safari hii ilikuwa ni mahususi kwa ajili ya kujitafutia  riziki zao za kila siku ambazo zilipatikana katika msitu fulani uliokuwa  mkubwa sana.
Watu hawa walitembea kwa umbali mrefu sana ikafika mahala wakawa wapo  katikati ya pori ambapo walianza kuingia na hofu ndani mwao, watu hawa majina yao ni, mtu wa kwanza alikuwa akifahamika kama moto, mtu wa pili alikuwa akifahamika kama maji na mtu wa tatu alikuwa hajulikani ni nani.
Wakiwa katikati ya pori wakiwa wamejawa na  wasiwasi na wanakokwenda  huku wakiwa hawaelewi watafika lini na muda gani, mmoja wao  akawambia wenzake “ jamani eeh hebu tusimame tuelezane kitu kimoja,  huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni moto, huku tukokwenda  nahisi tunaweza tukapotea.

Kama tunaweza tukapotea inabidi tuambiane ishara mapesa kabisa kwamba je, kama ukipotea utawezaje kujulikana sehemu uliyopo? yeye moto akasema  ikitokea tumeenda mahali na tukagawana kila mtu njia yake na ikawa haileweki mtu mwingine yupo wapi,  mimi kama moto ikatokea nimepotea basi msisumbuke kunitafuta ninyi angalieni ishara ya moshi popote utakapouona moshi unapotokea basi  hapo ndipo nitakapokuwepo.
Wakati huo wote moto anazungumza maji na yule mwingine ambaye hajulikani wakasema sawa mkuu sisi tumekuelewa.
Ikafika zamu ya maji naye kuzungumza, maji akasema “ moto mimi nakubaliana na wewe hata mimi nahisi kabisa kuna kila dalili zote za kupotea katika msitu huu, hivyo kama ikitokeo tumegawanyika na mimi nikapotea, mimi ili niweze kuonekana wala usisumbuke wewe angalia ishara ya kijani, ukiona sehemu ya kijani hapo ndipo utakaponipata.
Baada ya moto na maji kuzungumza hayo ikafika zamu ya mtu wa tatu ambaye hajulikani  kuzungumza, yeye akasema “jamani mimi mwenzenu sitabiriki”  mimi nikipotea sielewi mtanipataje kwa kweli maana mimi sina ishara yeyote ile nitakayoifanya ili mnione.
Sasa mimi na wewe tujiulize huyo mtu wa tatu alikuwa ni nani? Ambaye alisema hana ishara yeyote ile endapo atakuwa apotea? Endele kutafakari kisha unipe jibu.
Ila kwa kuwa umekuwa mzembe wa kuumiza kichwa basi ngoja nikupe jibu, mtu wa tatu alikwa ni muda.
Fundisho la hadithi hii ni:
Katika maisha yako poteza vitu vyote utavipata lakini usije ukapoteza muda wako huwezi kuupata, tumeona kuwa moto ukipotea ishara yake huwa ni moshi,  pia tumeona maji yakipotea ishara unaweza kuona ni ukijani katika uoto lakini muda ukipotea basi andika umeumia kwasababu muda huo hauwezi kurudi tena.
Kwahiyo tunafundishwa poteza  vingine kwenye maisha ila usithubutu kuja hata siku moja kuja kupoteza  muda wako, kwani ukipoteza muda hakuna ishara itakayokuonesha namna ya kupata ule muda ulioupoteza.
Hivyo fundisho kubwa hapa ni kuhakikisha unatumia muda wako vizuri ila kwa baadae usije ukajuta kwamba ulikuwa mjinga kwa kupoteza muda wako kwa kiasi hicho.
Nikutakie kila la kheri na tafakari njema ya hadithi hii, byee.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA AFISA MIPANGO BENSON CHONYA.


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.