google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Apr 24, 2019

Usipoteze Muda Wako, NI Utajiri Wa Kesho Yako.

No comments :
Muda ni mchache, maisha uliyonayo au maisha tuliyonayo ni mafupi, kwa hiyo kila muda na fursa unayoipata hata kama ni ndogo sana, tafadhari itumie vizuri na kwa uhakika mkubwa. Kutumia muda wako hovyo, hakuna tofauti na wewe kuamua kupoteza fursa za mafanikio yako tena kwa makusudi.
Ili kutumia muda wako vizuri, unatakiwa kufanya kile kinachotakiwa kufanyika kwa wakati ule  hata kama mwili wako uwe unataka au hutaki.  Moja ya kanuni ambayo inatumika na watu ambao hawafanyi kitu katika maisha, ni kutokuchukulia leo katika umuhimu wake. Kama leo yako unaiona ipo ipo tu, upo kwenye wakati wa kupoteza.
Maisha ya mafanikio yanatengemezwa na hatua ndogo ndogo sana za kila siku. Inapotokea wengine wanasita kuchukua hatua wewe unatakiwa kuchukua hatua na si kupoteza muda na kusema nitafanya siku nyingine. Muda ulionao ni wa dhahabu, ukipotea umepotea, kama ukijua thamani ya muda wako hutaweza kuupoteza tena.

Moja ya siri ya kufikia mafanikio yako ni kutumia kwa usahihi kila fursa ambayo unaipata. Muda unakwenda na kupaa, unatakiwa kuwa rubani kuendesha muda wako kwa usahihi. Jiulize,  usipotumia leo fursa za mafanikio unazozipata unataka kutumia fursa hizo lini au wakati gani, naamini unanipata vyema.
Mwanamafanikio William Ward moja katui ya maandiko anasema, “unatakiwa ujifunze kujiendeleza kwa kusoma wakati wengine wamelala, unatakiwa kuwekeza wakati wengine hawaoni fursa, unatakiwa kujiandaa kwa kila kitu wakati wengine wanacheza”. Acha kupoteza muda wa maisha yako kwa chochote, utumie vizuri.
Elewa hakuna muda bora kama huu ulionao kwa sasa. Kama utakuwa ni mtu kupoteza muda wako na kusubiri, hicho unachosubiri upo uwezekano hutaweza kukifanya tena au utakifanya kwa tabu. Wengi wanaoahirisha mambo ukumbuke huja kuyafanya tena mara nyingi huwa ni ngumu sana kwao kuweza kutokea.







No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.