google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 1, 2019

Kama Una Tabia Hizi, Mafanikio Kwako Yatabaki Kuwa Ndoto.

2 comments :
Adui wa kwanza wa mafanikio katika maisha yako ni wewe mwenyewe. Wewe ndiye unayeamua,ufanikiwe au usifanikiwe. Ninaposema hivi nina maana kwamba ziko tabia ambazo ukiwa nazo unafanikiwa na zipo tabia  mbazo ukiwa nazo utaishia kuona wenzako wanafanikiwa wewe unabaki palepale.Tabia hizi ni adui mkubwa wa mafanikio yako. Kwa hiyo usianze kutafuta mchawi wa mafanikio yako,mchawi wa kwanza ni wewe. Wewe ndiye mwenye maamuzi ya mwisho juu ya maisha yako unataka yaweje.

Hizi ni tabia ambazo umekuwa nazo kwa muda mrefu na hutaki kuziachia. Kwa jinsi unavyoendelea kuwa nazo ndivyo ambapo unajikuta maisha yako yanazidi kuwa magumu na wakati huo huo mafanikio kwako yataishia kuwa ndoto ya saa sita mchana, ndoto ya alinacha na mara nyingi utajikuta ukiishi maisha ya wasiwasi huku ukiwa hauna uhuru katika maisha yako. Unapojifunza tabia hizi fanya mabadiliko, chukua hatua sahihi za kubadili maisha yako na utafanikiwa.

Hizi ndizo tabia ambazo ukiwa nazo, mafanikio kwako yataishia kuwa ndoto za mchana:-

1.Kutokuwa na malengo.
Ili mtu afanikiwe lazima awe na malengo. Malengo ndio chanzo cha mafanikio, mafanikio hayaji kwa bahatí mbaya. Watu wote waliofankiwa unaowafahamu na usiowafahamu walikuwa na malengo, wakayaweka katika vitendo na kufanikiwa. Kama wewe ni mwanafunzi weka lengo unataka kuwa nani baadaye, vinginevyo utaishia kusoma na kubaki huna kazi ya kufanya; unakuwa umepoteza muda bure katika maisha yako.

Kama wewe ni mfanyabiashara weka lengo la kuwa mfanyabiashara mkubwa. Zingatia kwamba malengo ndiyo yanakupa dira na muelekeo katika maisha yako. Kupitia malengo unajua unatakiwa uanzie wapi na uishie wapi kulingana na lengo ulilojiwekea kwa wakati huo. Kutokuwa na malengo katika maisha ni sawa sawa na kusafiri bila kujua unaenda wapi. Hii ni hatari sana kwako.



2 .Kutokuwa na malengo  maalum yanayoeleweka.
Kuwa na malengo haitoshi, ni lazima uwe na malengo yanayoeleweka na kufikika. Ni kosa Kubwa kuwa na malengo mengi Ambayo hayafikiki na kutaka kuyatekeleza kwa wakati mmoja. Kuwa na malengo mengi  humfanya mtu achanganyikiwe. Mtu mwenye malengo mengi ana hatari ya; Kuchanganyikiwa na kushindwa kuamua aanze na lipi, amalize na lipi,pia ana hatari ya kutekeleza mambo nusunusu na hatimaye kushindwa kuendelea kabisa na mipango hiyo.

Weka malengo machache ambayo una uwezo wa kuyatekeleza kwa muda uliopanga kisha anza kutekeleza mpango mmoja hadi mwingine. Ukishafanikiwa kutekeleza mipango hiyo weka lengo lingine na utazidi kupiga hatua moja hadi nyingine na kuzidi kufanikiwa siku hadi siku.

3. Kukosa uvumilivu.
Mafanikio ni safari ndefu sana katika maisha ya binadamu. Mafanikio ya kweli yanachukua muda mrefu kupatikana, hayachukui muda mfupi kama wengi tunavyotaka. Kutaka mafanikio kwa muda mfupi ni tatizo ambalo limetukumba wengi katika dunia ya leo yenye changamoto nyingi za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Watu wengi tunaiogopa safari ndefu ya mafanikio, tunataka mafanikio ya muda mfupi.

WatuWengi wanakata tamaa mapema kwa kwa sababu wanataka mafanikio kwa mnuda mfupi jambo ambalo haliwezekani. Matokeo yake wanaamua kupita njia za mkato ili kufikia malengo wanayojiwekea. Usiogope kuchukua muda mrefu hadi kufanikiwa,hayo ndiyo mafanikio ya kweli. Ikiwa unataka kufikia mafanikio, usiogope kupita jangwani.


 4. Kukosa nidhamu.
Nidhamu ndicho chanzo cha mafanikio. Ukitaka kufanikiwa ni lazima ujitambue wewe ni nani una lengo gani na unapaswa kufanya nini ili kufanikisha lengo lako. Si hivyo tu unapaswa kuwa na mipaka katika utendaji wako. Unapaswa kujua lipi la kufanya na lipi si la kufanya, LAZIMA UWE NA NIDHAMU. Nidhamu ni uwezo wa kujitawala na kujizuia, kujiwekea  mipaka ya utendaji wewe mwenyewe bila kusimamiwa.
Unaweza kuiga na kufanya karibú kila kitu unachokiona na kukisikia, lakini si lazima uige na kufanya, mambo mengine siyo ya kuiga. Jiheshimu mwenyewe, pia  heshimu na kazi yako.Usiache kazi na  kufanya mambo mengine yasiyo ya msingi ambayo hayakusaidii kufikia lengo lako.

5. Kukosa shukurani.
Hakuna mtu anayefanikiwa katika maisha yake kwa juhudi zake mwenyewe bila kuwategemea wengine kwa namana yeyote ile, hayupo dunia hii. Tambua mchango wa wengine katika mafanikio yako. Kuna njia  nyingi za kuonyesha kwamba unatambua mchango wa jamii inayokuzunguka katika mafanikio yako. Baadhi ya mashirika na taasisi huamua kuchangia huduma za jamii kama elimu na afya kwa kutoa vitendea kazi kwa shule au hospitali.

Baadhi ya watu huamua kuwasaidia wengine katika shughuli zao   kiuchumi. Yapomambo mengi unayoweza kufanya ili kuonyesha kwamba unatambua mchango wa wengine katika mafanikio yako. Si vyema kutokufanya jambo kwa ajili ya wengine ikiwa wapo ambao walifanya kitu fulani na wengine wanaendelea kufanya kwa ajili ya mafanikio yako. Kwa hakika kuna watu wamefanya kitu fulani kuchangia mafanikio yako, wewe unafanya nini kwa ajili ya wengine?

6. Kuwa na hofu sana.
Watu  wengi huwa wanaogopa kujaribu kufanya kazi fulani kwa sababu watachekwa au kujishushia hadhi mbele ya jamii. Baadhi ya watu wanaogopa kujaribu  kwa sababu wakishindwa watachekwa na kujisikia vibaya. Wengine wanaogopa kupoteza fedha baada ya kupata hasara. Ni bora kujaribu ukashindwa kuliko kutokujaribu    kabisa. Mafanikio huja kwa kujaribu na kushindwa bila kukata tamaa. Katika ugunduzi wa gropu,Thomas Edison alishindwa zaidi ya mara elfu moja, hatimaye alifanikiwa mpaka leo hii tunasimulia habarí zake na kujifunza kutoka kwake.

Thomas Edison anasema,Udhaifu wetu mkubwa upo kwenye kukata tamaa. Njia ya hakika ya kuweza kufanikiwa ni kujaribu mara nyingine  tena. Kupata matokeo Ambayo hukuyatarajia na huyataki katika jambo ulilolifanya, haina maana kwamba matokeo hayo hayana faida.Wakati umejaribu njia zote na kushindwa, kumbuka hili-HUJASHINDWA. Kumbuka, kujaribu na kushindwa ni sehemu ya mafanikio.


Nakutakia mafanikio mema, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kila siku, karibu sana.

  • Makala hii imeandikwa na DEOGRATIUS GUNJU WA MBEYA TANZANIA
  • Mawasiliano 0718 610022






2 comments :

  1. Ok...

    What I'm going to tell you might sound really weird, maybe even kind of "supernatural"

    HOW would you like it if you could simply hit "PLAY" to listen to a short, "musical tone"...

    And miraculously attract MORE MONEY to your life??

    And I'm talking about hundreds... even thousands of dollars!!!

    Sounds way too EASY?? Think it couldn't possibly be REAL?!?

    Well then, I'll be the one to tell you the news.

    Sometimes the most magical miracles life has to offer are also the EASIEST!!!

    Honestly, I'm going to provide you with PROOF by letting you listen to a REAL "miracle money-magnet tone" I've produced...

    (And COMPLETELY RISK FREE).

    YOU simply hit "PLAY" and watch money coming right into your life... starting almost INSTANTLY...

    CLICK here NOW to experience the magical "Miracle Wealth Building Tone" - it's my gift to you!!!

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.