google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 17, 2018

Kila Wakati Zitumie Kanuni Hizi Muhimu Kwa Ajili Ya Mafanikio Yako.

No comments :
Leo nitaomba nichukue walau dakika chache ili niweze kukumbusha kanuni sita za kukupa mafanikio unayoyahitaji. Hizi ni kanuni ambazo ukizitumia na kuzifanyia kazi ni lazima zikupe matokeo makubwa kwa ajili ya mafanikio yako.

Wengi wanaozitumia kanuni hizo zinawasaidia sana kupiga hatua na kuwafanikisha. Kila wakati jaribu kuzitumia kanuni hizi kwa ajili ya manufaa yako na ya wengine pia. Usitoke hapo ulipo twende pamoja katika somo letu la leo tujifunze kanuni hizi;-

1. Kanuni ya 1; Chukua hatua stahiki.

Miongoni mwa vitu vitakuvyofanya uzidi kufanikiwa zaidi ya hapo ulipo sasa ni pamoja na kuendelea kuchukua hatua stahiki kwa hicho unachokifanya au kile unachotaka kufanya. Kushindwa kuchukua hatua huko ni kuchagua kujiangusha wewe mwenyewe.

2. Kanuni ya 2;Tumia siku yako vizuri na kwa uhakika.

Mafanikio siku zote ni matokeo ya vile unavyoitumia siku yako vyema, hivyo ulivyo leo ni matokeo ya hatua ulizozichukua siku ya jana. Hivyo jifunze kuitumia leo yako vyema ili uishe kesho yako yenye mafanikio na furaha tele.


 3. Kanuni ya 3; Jenga mtazamo sahihi kila wakati.

Hivyo ulivyo leo katika suala la mafanikio ni matokeo ya mawazo yako. Kama mawazo yako ni hasi basi hata maisha yake yatakuwa vivyo hivyo. Kama unataka unataka kubadili maisha yako, basi badili na mawazo yako na kuwa chanya.

4. Kanuni ya 4; Tafuta njia ya mafanikio yako.

Kama tutaamua kutafuta mafanikio ya kweli ni lazima tutafuta njia ya kuyapata mafanikio hayo, ila kama hatuhitaji mafanikio ni lazima tutafuta visingizio. Hivyo ili tuweze kufika katika kilele cha mafanikio tunatakiwa kutafuta njia ya kupata mafanikio hayo.

5. Kanuni ya 5; Jenga uwezo wa kutatua changamoto;

Katika maisha haya kila kitu kinawezekana, kama kuna jambo unaliona ni changamoto na haliwezekani basi mahala hapo ndipo palipo na fursa lukuki zilizojificha, hivyo jifinze kushughulika na kila changamoto zilipo katika jamii yako kwani hapo ndipo palipo na fursa.

6.  Kanuni ya 6; Toa hofu zako.

Siraha hatari zaidi duniani si bunduki wala mabomu ya nyuklia kama wengi wadhanivyo, bali siraha hatari zaidi duniani ni hofu. Hofu ndio chanzo kikubwa cha kuua ndoto za walio wengi, wengi wetu tunashindwa kuthubutu kufanya jambo fulani eti kwa sababu ya kwamba tunaogopa kitu fulani.

Hivyo kama kweli unataka kupiga hatua za kusonga mbele tunatakiwa kuhakikisha ya kwamba tunaondokana na hofu, kwani hofu ni adui nambari moja wa mafanikio.

Asante sana kwa kusoma makala haya kupitia mtandao huu wa Dira Ya Mafanikio, nikutakie siku njema na mafanikio mema.

Ndimi: Afisa Mipango Benson Chonya
bensonchonya23@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.