google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 2, 2020

Ukifanyia Kazi Mambo Haya Mara Kwa Mara, Yatakufikisha Kwenye Ndoto Zako.

No comments :
Kila mtu anatamani kuzifikia ndoto za maisha yake ya mafanikio. Kwa sababu hiyo kila mtu huchukua hatua anazoziona yeye zinamfaa ili kutimiza malengo hayo. Je, ni wangapi wanajua kuwa huwa wanachukua hatua sahihi au la.?

Katika makala haya, ni lengo langu ni kukumbusha wewe, mambo ya msingi na kama utayazingatia mambo haya yatakusaidia wewe kuweza kukufikisjha kwenye ndoto zako za mafanikio. Je mambo hayo ni yapi?


1. Andika malengo yako.

Najua malengo yako unayajua vizuri tu, lakini kuna sababu muhimu sana kwa wewe kuyaandika malengo yako tena. Chukua kalamu na karatasi, na andika vitu vyote unavyotaka kuvifikia kwenye maisha yako.

Fikiria juu ya kitu ambacho unataka kufanya au unahitaji kukifanya. Inaweza kuwa kitu chochote kama malengo ya afya au malengo ya biashara yako. Orodhesha vitu vingi iwezekanavyo, lakini viwe vile unavyotaka kuvifanikisha.


2. Weka vipaumbele vya malengo yako.

Ndio, najua umeandika malengo mengi, lakini ukweli ni kwamba huwezi kuyatimiza yote. Ili uweze kuyafikia malengo hayo,  yagawawe kwa kuzingatia vipaumbele. Unapaswa kujua, malengo yapi uanze nayo na yapi uyaache.

Kwa kuweka vipaumbele itakupa nguvu wewe, ya kuweza kuyafikia malengo yako kwa urahisi. Na ukishaweka vipaumbele, usibabaishwe na malengo mengine yatakayotokea hapa katikati, vipaumbele vyako vinatosha, vitekeleze kwanza.

3. Vunja vunja malengo yako.

Vunja kila lengo kuwa dogo ambapo unajua unaweza kutimiza kwa urahisi. Hakikisha pia unajipa muda wa wewe kutekeleza malengo yako kulingana na wakati uliokadiriwa wa mradi huo uliojiwekea.

Kwa mfano, ikiwa lengo lako ni kusoma kitabu. Usijilazimishe kusoma kurasa mia moja, kwa mara moja, soma kurasa chache na zielewe. Fikiri kama unataka kujifunza kuogelea, je! Ungeingia ndani ya bahari au ungeanza kwanza kujifunza katika dimbwi?

4. Amua kuwajibika.

Lengo kuu ni kuishi maisha bora ya kufikia malengo yetu na kufanya hivyo lazima tuchukue hatua moja kwa wakati mmoja na kwa hiyo tunahitaji msimamo thabiti. Je! Unahakikisha vipi malengo yako yanatimia?

Hapa hakuna ujanja, unatakiwa kuwajibika. Fanya kila linalowezekana kwa wewe kuamua kuwajibika ili kuhakikisha malengo yako yanatimia. Ukikubali kuwajibika nakupa uhakika unaweza kufanikiwa na kufika mbali kimafanikio.

Fanyia kazi mambo hayo na hakikisha unachukua hatua kuona ndoto zako zinatimia.

Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kumbuka, ufalme hauji kwa maneno bali unakuja kwa vitendo,...chukua hatua. 
 Nikutakie kila la kheri,
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA NDOTO ZAKO ZITUMIE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
IMANI NGWANGWALU,
Mawasiliano, Whats app; 0713048035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.