google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 1, 2020

MAMBO YA KUJUA KABLA HUJAACHA KAZI.

No comments :

Naamini umejifunza masomo ya kuyajua kabla hujaacha kazi, lakini pia mbali na masomo hayo hapa kuna mambo ya kuyajua kabla hujaacha kazi.


Haya ni mambo ambayo unatakiwa ujikumbushe ili kujenga msingi mzuri wa ujasiriamali. Naomba twende pamoja kujifunza mambo hayo;-

  Jambo #1. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa ujue, jinsi ya kubadilisha bahati mbaya na kuwa bahati nzuri.

Kama hujui jinsi ya kubadilisha bahati mbaya, na kuwa bahati nzuri, usijaribu kuacha kazi utajiumiza sana. Ujasiriamali una mambo mengi sana ya changamoto.

Hivyo kwa kadri unavyokutana na changamoto ngumu kabisa, unatakiwa ujue jinsi ya kuzibadilisha changamoto hizo na kuwa bahati nzuri. Kama ukishindwa, basi tulia na ajira.

 Jambo # 2. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kujua, ni shughuli zipi zinatengeneza biashara ya mafanikio.

Biashara haihusishi mauzo tu peke yake. Kama ndio umetoka kwenye ajira na una akili ya kuwaza mauzo peke yake, utakwama. Unatakiwa ujue biashara inahusisha mambo mengi.

Zipo shughuli nyingi zinazotengeneza mafanikio ya biashara kama huduma kwa wateja, usafi, au mawasiliano mazuri na wateja. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kuzingatia haya kwanza.


 Jambo  #  3.  Kabla  hujaacha kazi,  unatakiwa  ujue,  umuhimu  wa kujiendeleza binafsi.
Kama utaingia kwenye ujasiriamali na umegoma kujiendeleza, utashindwa sana, kwa sababu kwenye ujasiriamali zipo changamoto nyingi na zinazotaka kichwa chako kiwe kizuri.

Na kwa sababu ya changamoto hizo inatakiwa muda wote uwe bora na pia wanaokuzunguka wawe bora. Yote haya utayapata kwa wewe kuamua kujifunza na kujinoa.

 Jambo # 4. Kabla hujaacha kazi, jifunze kidogo elimu ya uhasibu.

Kwa kujifunza elimu hii, itakusaidia sana kujua mtiririko wa pesa katika biashara, pia itakusaidia kujua bajeti ya biashara na yako kitaalamu zaidi, tofauti na ungekuwa hujui.

Kama kwako ni ngumu kujifunza elimu hii, basi, biashara ikikua kidogo, ajiri angalau mhasibu anayejua vizuri na uwe unamlipa. Hii itakusaidia kujenga biashara yako kwa mafanikio.

 Jambo la #5. Kabla hujaacha kazi, kumbuka kuwa safari yako ya mafanikio inaanzia ndani ya moyo na roho yako.

Hapa kabla hujaacha kazi unatakiwa ujiulize, ndani mwako unaona mafanikio? Hii ikiwa na maana kwamba mafanikio yako lazima uyaone ndani kwanza kabla hayajaonekana kwa nje.

Hata kwa hatua unazochukua inatakiwa zidhihirishe kile kilicho moyoni mwako. Kama mafanikio moyoni huyaoni usijaribu kuacha kazi, maana hata kwenye ujasiriamali hutafanikiwa pia.

 Jambo #6. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa ujue, kitu chochote unachotaka kukiuza, kina bei tatu za msingi. Bei ya chini, bei ya kati na bei ya juu.

Kama utachagua kuuza kitu hicho kwenye bei ya chini, unatakiwa ujue pia dakika yoyote ataibuka mtu wa kushindana na wewe. Ili uwe mshindi katika kuuza kwa bei ya chini unatakiwa uwe na njia nzuri sana ya kuuza bidhaa yako.

Kama utachagua kuuza bidhaa zako kwa bei ya juu, pia jifunze kutoa huduma bora. Kama huelewi hili vizuri, nenda kwenye hotel zinazotoa huduma kwa bei ya juu uone vizuri kile wanachokifanya ni nini kwenye biashara zao.

  Jambo #7. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kujua na kukumbuka, mauzo=kipato.

Kama utakuwa unataka kuacha kazi na ukajigundua kwenye mauzo haupo vizuri., nikwambie tu, jifunze kuuza kwanza, halafu ndo uache kazi. Kama huwezi kuuza, hiyo ni shida kwako kufanikiwa.

Tunaambiwa asilimia kubwa ya watu wengi huwa tunazaliwa hatujui kuuza. Hata hivyo unaweza kujifunza kuuza ili uwe mjasiriamali mzuri, vinginevyo utakwama. Anza kujifunza kuuza, utafanikiwa.


 Jambo # 8. Kabla hujaacha kazi, unatakiwa kujua vizuri jinsi ya kutumia pesa zako vizuri.

Ni wazi wajasiriamali walio wengi, hawajui jinsi ya kutumia pesa zao vizuri. Wanajikuta wanatumia tu pesa hawajui zitarudi vipi. Sasa usiingie kwenye mtego huo.

Ili uwe mjasiriamali mwenye mafanikio, unatakiwa kujua kila shilingi ya pesa yako inakwenda wapi. Ukiona unafika sehemu unashangaa pesa zako zimeenda wapi, bado hujajua jinsi ya kuzitumia.

  Jambo #9. Kabla hujaacha kazi, anzisha biashara ya pembeni kwa ajili ya kujifunza ujasiriamali.

Hakuna ambae anaweza akaendesha baiskeli pasipo kujifunza. Hata kwenye biashara mambo yako hivyo, unatakiwa uwe na biashara ya mazoezi kabla hujaacha kazi na kuingia kwenye ujasiriamali.

Usije ukafanya kosa la kuacha kazi, wakati hata hujui ABC za ujasiriamali ziko vipi. Ukiwa unafanya biashara huku umeajiriwa, itakupa ukomavu wa wewe kufanikiwa kibiashara.

 Jambo   #10.   Kabla   hujaacha   kazi,    tafuta   mshauri   wa mafanikio/mentor.

Ni ngumu sana kwa wajasiriamali wengi, kuwa na mshauri wa mafanikio, lakini kabla hujaamua kuacha kazi, hakikisha una mshauri huyu wa mafanikio ambae atakuongoza katika njia sahihi.

Kama unaona kumpata mshauri wako wa mafanikio ni ngumu, basi amua kufanya vitabu viwe ndo mshauri wako. Kwenye vitabu unatakiwa kujifunza sana na itakusaidia kufanikiwa.

  Jambo #11. Kabla hujaacha kazi, tafuta mtandao wa wajasiriamali.

Usije ukakimbilia kwenye ulimwengu wa ujasiriamali, kama huna mtandao wa ujasiriamali. Kitendo cha kuwa na mtandao huu, kitakusaidia sana wewe katika safari yako ya kimafanikio.

Inakubidi utafute mtandao, ambao kwako unaona unakufaa na kukusaidia. Kila wakati jumuika katika mikutano yao ili kupata uzoefu utakaokujenga, kukulea na kukusaidia kufikia malengo.

   Jambo #12. Kabla hujaacha kazi, tazama mtazamo wako.

Ikiwa mtazamo wako unaona tu kwamba ukiingia kwenye ujasiriamali unapata mafanikio ya moja kwa moja, unajidanganya. Inakubidi ujue kwamba zipo changamoto na unatakiwa kuzifanyia kazi.

Ukijua hili, au ukaamua kuingia na mtazamo huu, wa kutambua changamoto za ujasiriamali, utakusaidia kupambana na changamoto zinazojitokeza.

Mwisho; kabla hujaacha kazi, unatakiwa uwe na imani sahihi kwenye ujasiriamali na kuielewa vizuri, misingi sahihi ya ujasiriamali.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.