google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 18, 2015

Mambo 5 Yanakuzuia Wewe Kuwa Tajiri.

No comments :
Watu wengi huwa ni watu wakijirudisha nyuma  katika maisha yao pasipo kujua hasa kutokana na vitendo, mienendo, hulka na hata tabia walizonazo kwa ujumla. Hayo ni mambo machache kati ya mengi ambayo yamekuwa yakisimamisha ndoto za watu wengi katika safari nzima ya kuelekea kwenye utajiri. Kiuhalisia, ili uweze kufikia ngazi kubwa ya mafanikio na hatimaye kuwa tajiri unahitaji kujifunza vitu vingi sana vitakavyoweza kukusaidia kusonga mbele, ikiwa na pamoja nakujua vitu vinavyokuzuia wewe kuwa tajiri. Leo katika makala hii tutazungumzia mambo yanayokuzuia wewe kuwa tajiri katika maisha yako.

Yafuatayo Ni Mambo 5 Yanakuzuia Wewe Kuwa Tajiri.

1. Umekuwa ukiathiriwa sana na mazingira uliyopo.
Hii ndiyo sababu kubwa mojawapo inayokufanya ushindwe kufikia mafanikio makubwa na hatimaye kuwa tajiri. Hili limekuwa likitokea kwako pasipo kujua na pengine umekuwa ukiona kama jambo la kawaida tu kwako, bila kugundua kitu. Inawezekana ukawa umekulia katika jamii maskini ambapo muda mwingi tokea unasoma shule na mpaka sasa uko mtaani umekuwa ukiona watu wengi wanaokuzunguka ni maskini. Picha utakayokuwa inakujia kichwani kwako ni kuwa haiwezekani kuwa tajiri. Unaamini hivyo ni kwa sababu ya mazingira yanayokuzunguka unaona wengi ni maskini na ni kitu ambacho kimekuwa kikikuathiri na kukuzuia wewe kuwa tajiri.


2. Hujaamua kuwa tajiri katika maisha yako.
Maamuzi ni kitu cha muhimu sana katika maisha yako. Hata kama utakuwa unasoma vitabu vya mafanikio kwa wingi, kuhudhuria warsha na semina mbalimbali za mafanikio, kama hujafanya maamuzi mazito ya kutaka kuwa tajiri katika maisha yako, huwezi kuwa tajiri. Mafanikio makubwa ya maisha yako yanategemea sana na maamuzi unayoyafanya leo kila siku. Ukiamua kuwa tajiri kisha ukajitoa kulipia gharama za kuwa tajiri, hilo linawezekana. Maamuzi utakayochukua yana nguvu ya kukutoa kwenye umaskini na kukufanya kuwa tajiri. Mpaka sasa hujawa tajiri moja ya kitu kinachokuzuia ni maamuzi yako mwenyewe.

 3. Umekuwa mtu wa kuahirisha sana mambo yako.
Unashindwa kufikia ndoto zao kubwa kwa sababu ya tabia yako hii ya kuahirisha mipango yako mara kwa mara, hali ambayo imekuwa ikisababisha uzidi kukosa fursa nyingi kila kukicha. Kama kuna jambo umeamua kulifanya na kulitekeleza ni vizuri ukalifanya leo ili uweze kufikia mafanikio yako unayoyataka. Kama ni kesho ambayo unasema kila siku utafanya hutaweza kuja kuipata mpaka unazeeka. Jifunze kufanya mambo yako leo leo na achana na kesho utapoteza muda wako bure kuisubiri na kesho haitafika.

4. Umekuwa ukitumia pesa zako vibaya.
Hili ndilo kosa kubwa ambalo umekuwa ukilifanya na limekuwa likikugharimu na kukuzuia kuwa tajiri. Mara nyingi umekuwa ukitumia nguvu nyingi kutafuta pesa zako, lakini unapozipata umekuwa ukizitumia hovyo sana hali inayosababisha ushindwe kuweka hata fedha kidogo kwa ajili ya akiba yako. Na umekuwa ukifanya hivi kwa sababu ya kukosa nidhamu binafsi juu ya pesa zako na umejikuta umekuwa mtumwa wa pesa. Kama unaendelea na maisha haya ya kutumia pesa zako bila ya utaratibu maalumu, tambua kabisa utabaki kuwa maskini siku zote na hili halina ubishi.

5. Umekuwa ni mtu wa kupoteza muda sana.
Ni jambo ambalo nimekuwa nikilisema mara kwa mara kuwa, kama unaishi na unaendelea kuishi maisha ya kupoteza muda, elewa huna kabisa maisha ama kwa maneno rahisi huwezi kufanikiwa tena katika maisha yako. Muda ni kila kitu katika maisha yako unapocheza na muda, inakuwa ni sawa na kuchezea maisha yako mwenyewe. Ubaya wa muda ukiupoteza ndio haurudi tena hata ufanye nini. Jifunze kutumia muda wako vizuri, ili ukuzalishie na  ukuletee mafanikio makubwa.

Hayo ndiyo mambo yanayokuzuia wewe kuwa tajiri katika maisha yako, nakutakia kila kheri katika safari yako ya mafanikio. Nakusihi endelea kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika kila siku. Usisite pia kuwashirikisha wengine ili tujifunze wote kwa pamoja mambo mazuri yatakayoboresha maisha yetu.

IMANI NGWANGWALU,








No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.