google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 19, 2015

Hatua Tano Muhimu Za Kufikia Malengo Uliyojiwekea.

No comments :
Habari ya leo mpenzi msomaji wa mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO. Nimatumaini yangu ya kuwa umzima wa afya na unaendelea vizuri na harakati za kuboresha maisha yako ya kila siku. Ninakukaribisha sana katika siku nyingine tena, ambapo tunakutana kujadili maisha, lengo likiwa ni kuhakikisha tunapata maarifa bora yatakayoweza kutusaidia kuweza kuboresha maisha yetu na kuwa ya kiwango cha juu kabisa cha mafanikio kama tunavyotaka iwe.

Katika makala yetu ya leo tutaangalia hasa juu ya malengo na jinsi ambavyo tunaweza kufikia malengo tuliyojiwekea bila kizuiliwa na kitu chochote. Mara nyingi wengi wetu kuna wakati huwa ni watu wa kujiuliza, nitawezaje kufikia lengo hili ama lile katika maisha yangu. Ni maswali ambayo huwa yanakuja pengine kutokana  na mtu huyo kugundua kuwa kuna uwezekano wa yeye kutotimiza malengo yake kwa sababu anazozijua yeye, ikiwa ni pamoja na wasiwasi ama kushindwa kujiamini.

Wengine kutokana na wasiwasi ama kushindwa kujiamini kama nilivyosema, hujikuta ni watu wa kuamini kuwa labda wanaotimiza malengo ya aina fulani ni watu wenye vipaji, wamejaaliwa na pia ni watu wenye bahati sana katika maisha yao, kitu ambacho sio kweli hata kidogo. Kiukweli, unaouwezo mkubwa wa kutimiza malengo yoyote unayojiwekea katika maisha yako, kama utaamua iwe hivyo kwako. Hakuna kitu ama mtu mwenye uwezo wa kukuzuia wala huhitaji nguvu za ziada kufanikisha hilo.


Unaweza ukawa unaanza kujiuliza nifanye nini au ni kipi cha kufanya ili niweze kutimiza malengo yangu muhimu niliyojiwekea? Ni vizuri kujiuliza hivyo maana hiyo nayo ni hatua ya kuonyesha kuwa una nia na mafanikio unayoyataka na wala hutanii. Kipo kitu muhimu ambacho wewe unatakiwa ufanye ili kutimiza malengo yako, kitu hiki nikufatilia na kufanyia kazi hatua hizi tano za kufikia malengo yako na si vinginevyo.   Ukifanya hivyo uwe na uhakika utafikia malengo yako bila wasiwasi. Unajua hatua hizo ni zipi?

Hizi Ndizo Hatua Tano Muhimu Za Kufikia Malengo Uliyojiwekea.

1. Ni lazima uwe na hamasa ya kutaka kufanikiwa.
Hautaweza kufanikiwa kama huna njaa na kiu kubwa ya mafanikio ndani mwako. Ili uweze kufanikiwa hasa kwa malengo uliyojiwekea ni lazima uwe na hasira kubwa ya mafanikio. Ukiwa na hasira hii, itakusaidia wewe kupita eneo lolote, hata katikati vizuizi ama vikwazo ambavyo huwa tunakutana navyo katika safari ya mafanikio. Watu wengi wenye mafanikio makubwa duniani ni watu ambao walikuwa na hasira na malengo yao waliyojiwekea.



2. Anza kuchukua hatua mapema.
Kuongea sana juu ya mipango na malengo mazuri uliyonayo hakutakusaidia kitu, zaidi ya kuchukua hatua muhimu za kuelekea kwenye utekelezaji. Anza kuchukua hatua mapema za kutekeleza ndoto zako hata kwa kidogo kidogo ipo siku utafika. Ni bora ukafanya kwa kidogo hiyo itakusaidia sana tofauti na ambavyo ungekaa na kusubiri, hiyo ingekuwa inakupotezea muda sana katika maisha yako.

3. Unahitaji kujifunza zaidi.
Hii ni hatua muhimu pia ya kufikia malengo unayoyahitaji katika maisha yako. Ni muhimu kujifunza na ukapata maarifa yanayoendana na malengo unayoyahitaji katika maisha yako. Hiyo itakusaidia kujua vitu vya msingi vinavyoendana na malengo uliyojiwekea. Kwa mfano, kama malengo yako ni kuwa millionea baada ya miaka 20 kuanzia sasa ni lazima uanze kujifunza kuishi maisha wanayoishi mamilionea kwa kujisomea kila siku.

4. Unahitaji kuwa na mitazamo chanya.
Mara nyingi kuna wakati huwa tunashindwa kufikia malengo yetu tuliyojiwekea kutokana na mitazamo tuliyonayo juu ya malengo yetu. Kama unajiona huwezi kufikia malengo yako, huo ndio ukweli hutaweza kuyafikia. Jenga mitazamo chanya ambayo itakusaidia kufikia malengo muhimu uliyojiwekea. Achana na fikra ama imani za kuwa huwezi kufanikiwa kwa sababu hii na hii, jiwekee mitazamo chanya na utaweza kufikia malengo yako.

5. Jifunze kutokana na makosa.
Kuna wakati huwa tunafikia mafanikio kwa yale tunayoyahitaji baada ya kukosea sana hiki na kile. Hautaweza kufikia mafanikio au malengo yako kwa urahisi kama unavyofikiri, kuna wakati ni lazima ukosee. Unapokosea huo ndio huwa wakati muhimu kwako wa kujifunza kutokana na makosa uliyoyafanya.  Acha kusononeka wala kulia kama kuna sehemu umekosea, hiyo hatakusadia kitu. Badala yake, chukua hatua muhimu ya kunyanyuka pale ulipoanguka, jifunze na kisha songa mbele.

Mwisho, unaposhindwa kufikia malengo yako kwa namna yoyote ile acha kulaumu vitu ambavyo viko nje ya wewe kuwa ndiyo vimesababisha ushindwe kufikia malengo uliyojiwekea. Mara nyingi sisi wenyewe huwa ndio huwa vizuizi wa malengo yetu. Jifunze hatua hizo tano muhimu zikusaidie kufikia malengo muhimu uliyojiwekea katika maisha yako.

Nakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio. Ansante kwa kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO na endelea kuwashirikisha wengine kujifunza mambo mazuri yanayoendelea humu.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,

  IMANI NGWANGWALU,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.