google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 17, 2015

Mambo 6 Unayotakiwa Kujua, Ili Kuboresha Biashara Yako.

4 comments :
Kuwa na kiu ama shauku ya kufikia ngazi kubwa ya kimafanikio kibiashara, ni hitaji ambalo kila mjasiriamali na mfanyabiashara wa kweli  huwa nalo ndani ya moyo wake. Pamoja na kiu hii ya kutaka kufikia mafanikio hayo makubwa kibiashara, wajasiriamali  wengi hujikuta wakikwama na kushindwa  kutimiza malengo yao. Kwa kawaida, huwa yapo mambo mengi yanayochangia kutokea kwa hali hii, ikiwemo na kufanya biashara kwa mazoea na matokeo yake kushindwa kuboresha biashara.

Unaposhindwa kuboresha biashara yako, sio tu kwamba itapelekea wewe kukosa wateja, bali pia itakusababishia kushindwa kufikia mafanikio makubwa uliyojiwekea katika maisha yako. Kwa kujua hilo, ni muhimu sana kwako kuiangalia na kuichunguza biashara yako mara kwa mara na kufanya marekebisho muhimu na ya lazima, ili kupata matokeo chanya unayoyahitaji na si vinginevyo. Lakini, hautaweza kufanya chochote au marekebisho yoyote kama hujui mambo haya.

Haya Mambo 6 Unayotakiwa Kujua, Ili Kuboresha Biashara Yako.

1. Kubali Kuwa Kuna ushindani.
Ni muhimu kujua hili mapema kuwa biashara unayoifanya hauko peke yako, wapo watu pia wanaofanya biashara kama ya kwako. Kwa kujua hilo hutakiwi kubweteka, kujiachia ama kulala na kusubiri wateja waje, utakuwa unapoteza muda na hutapata mafanikio makubwa kama unayoyataka. Badala yake, fanya kazi kwa bidii kuweza kukabiliana na upinzani ulionao na usiogope  wala kutishwa na chochote, hapo utakuwa umefanya kitu cha kuboresha biashara yako.


2. Kuwa na malengo na biashara yako.
Ili uweze kufikia mafanikio makubwa unayoyataka katika biashara yako, ni muhimu pia kujiwekea malengo maalum ya kibiashara. Malengo hayo yatakusaidia kujua ni wapi unapotakiwa kufika baada ya muda fulani na wapi ulipokwama. Unapokuwa na malengo juu ya biashara yako, ni lazima nidhamu yako itakuwa juu hasa katika mambo ya pesa na utahakikisha kufanya lolote ili biashara yako ikue. Biashara yoyote unayoifanya kama haina malengo maalumu haiwezi kukua na kufika mbali hata iweje.

3. Jitoe Kufanya kazi kwa bidii.
Kwa kuwa umeamua kuwa mjasiriamali, kitu pekee ambacho kinaweza kufanya biashara yako ing’ae ni kufanya kazi kwa bidii,  kwa ubunifu na maarifa makubwa. Nguvu nyingi, mawazo na mwelekeo mkubwa unatakiwa kuupeleka kwenye biashara yako ili ikuletee mafanikio makubwa na  si vinginevyo. Kumbuka, wewe ndiyo bosi na mkurugenzi wa biashara yako unayoifanya, ukilala au kusinzia ujue kabisa kila kitu kitaharibika na hutaweza kusonga mbele.


4Ishi na watu wenye mitazamo chanya.
Itakuwa ni ngumu sana kwako kufanikiwa kama utakuwa una watu wengi wanaokuzunguka ni wenye mitazamo hasi na biashara unayoifanya. Watu hawa watakukatisha tamaa kwa maneno na mienendo yao na utajikuta unashindwa kusonga mbele. Ili uweze kuboresha biashara yako na kufikia mafanikio makubwa, ni muhimu sana kuwa na watu chanya ambao wanauwezo wa kukusaidia kwa hali yoyote ile hata pale ambapo mambo yako yanakwenda hovyo. 

5. Badili jinsi unavyojitazama mara moja.
Kuwa na mtazamo chanya juu ya biashara yako ni kitu cha lazima sana kwako, ili iweze kuleta mabadiliko unayatarajia. Biashara yako haitafika popote kama utakuwa mtu wa kuitazama na kuona kuwa haitafanikiwa sana kama unavyoziona za wengine. Kutokana na mitazamo wako huo utaanza kufanya mambo kizembe hali itakayopelekea wewe kushindwa. Kama unataka kuboresha  biashara yako, badili jinsi unavyojitazama wewe na biashara kwa ujumla.

6. Jifunze zaidi kuhusu biashara.
Unatakiwa kujifunza na kuilewa vizuri biashara unayoifanya kila siku. Hiki ni kitu ambacho hutakiwi kukwepa kwani kitakusaidia kuiboresha biashara yako kwa sehemu kubwa sana. Kwa kadri jinsi utakavyozidi kujifunza juu ya biashara yako, utagundua mapungufu mengi ambayo ukija kufafanyia kazi, itakusaidia kuhama kutoka ngazi moja na kuelekea ngazi nyingine zaidi ya mafanikio kibiashara.

Kumbuka, ili tuweze kufanikiwa na kufikia mafanikio makubwa, tunalazimika kuboresha  biashara zetu kwa sehemu kubwa kila siku. Kama utashindwa kuboresha biashara yako, basi elewa tu hutafika mbali sana kimafanikio kama  unavyofikiri, kwani nguvu ya ushindani itakushinda na utajikuta umebaki pembeni na kuwa mtazamaji kwa wengine. Kwa kuanzia, hayo ndiyo mambo muhimu unayotakiwa kuyajua ili kuboresha biashara yako.

Nakutakia ushindi katika biashara yako iwe ya mafanikio, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kila siku kujifunza na kuhamasika, mpaka maisha yako yaimarike.

IMANI NGWANGWALU,


4 comments :

  1. Hbr, tunshukur kwa fursa hzo, ila nlipenda utupatie n Elim ya namna ya utengenezaj wa chaki

    ReplyDelete
  2. Shukrani Sana wangu kwa ushauri mzuri

    ReplyDelete
  3. Ahsante sana rafiki. Mungu akubariki

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.