google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Feb 13, 2015

Kama Unaendeshwa Na Kitu Hiki, Maisha Yako Ni Magumu Sana.

No comments :
Mtu mwenye hisia nyingi ambaye anaongozwa na hisia, ni yule ambaye huweza kuathiriwa au kutikiswa kwa urahisi zaidi na hisia. Ni jambo zuri kujijua sisi wenyewe na haiba zetu na hata kutambua hisia zetu. Ninapozungumzia hisia nikiwa na maana ya hali kama kuwa na furaha, huzuni, chuki na hata wakati mwingine kijicho hizo ni baadhi tu ya hisia.

Baadhi ya watu ni wenye kuongozwa sana na hisia wakati ambapo wengine hawako hivyo na kwa  kuutambua ukweli huu tutaweza kuzuia na kuepuka kuumiza vichwa vyetu na hata kupata maumivu mengine katika maisha yetu. Hata kama hatumo katika kundi la wale wenye hisia nyingi, bado kila mmoja wetu anazo hisia na yuko katika hatari ya kuongozwa na hisia hizo.

Tunaweza kuamka mapema sana asubuhi siku moja, huku tukiwa tumejazwa na hisia za huzuni na kwa siku hiyo nzima tukaongozwa na kufuata hisia hizo. Siku inayofuata tunaweza tukaamka pia tukiwa tumechukia, huku tukihisi au kutaka kuona kila mmoja wetu pale nyumbani kwetu aondoke machoni petu, hivyo tukajikuta tukaishia kufanya vituko vya ajabu tu.

Wakati mwingine tunaweza kuamka na hisia za kujisikitikia sisi wenyewe na kujuta sana na hata kuamua kukaa kwenye kona tukiugulia kwa siku nzima huku tukiwa tumeshika tama. Na kujiuliza maswali mengi ambayo hayana majibu na huku tukiwa hatutaki kabisa kuongea na mtu. Na inapotekea mtu akatuongelesha tunakuwa wakali sana kiasi cha kwamba tunaweza kumjibu vibaya kama sio sisi tuliozoeleka.


Hivyo basi, iwapo tutaamua kuziachia hisia zetu zifanye vile zinavyotaka, basi ni wazi kabisa hisia hizi zitachochea matatizo ambayo yatasababisha tutoke nje ya makusudio yetu mema na kutupeleka kwenye makusudio au matakwa ya kutuangusha. Hapa ndipo pale tunapoanza kusema, ‘ilikuwa ni ibilisi tu’. Ndio maana katika maisha yako, kama bado ni mtumwa na unaendelea kuendeshwa na hisia zako, maisha yako ni magumu sana. Ni magumu kwa sababu kila wakati utakuwa unaishi maisha yanayokuumiza wewe tu.


Nimetumia miaka mingi ya maisha yangu katika kufuata vile nilivyokuwa nikijihisi. Kama niliamka asubuhi nikiwa mwenye huzuni, basi nilihuzunika siku nzima. Kwa wakati huo sikuweza kujua kwamba, ningeweza kuzizuia hisia za aina hiyo. Sasa nimetambua kwamba, ninaweza kupambana kikamilifu na hisia zote mbaya na zilizo hasi ambazo zinatamani kuniongoza siku nzima.

Ni lazima tujifunze kuwa wenye tahadhari kuhusiana na hisia zetu mwenyewe na kuweza kuelewa jinsi tutakavyoweza kuziongoza na kuzisimamia kwa usahihi na uhakika zaidi. Njia mojawapo ya kufanya hivyo, ni kuzijua aina tofauti za haiba au tabia na kujua namna zinavyoitikia kwa njia tofauti, hali au mazingira yanayofanana.

Nimejifunza kwamba, ninapoamka asubuhi nikiwa na kisirani, sipaswi kuendelea kukilea kisirani hicho. Ninapaswa badala yake kuamua kuwa mimi, kuamua kuwa na mkabala tofauti wa kimaisha kwa siku hiyo. Ni mimi ninayepaswa kusema ninataka nijisikie vipi, siyo mazingira au hali inayonizunguka.

Ninapojikuta nimenyong’onyea, ni lazima nijiulize haraka kama ni lazima ninyong’onyee. Ni wazi wazi kwamba, huwa ninapata jibu la hapana. Kwa hiyo, kuanzia hapo hutafuta sababu ya kunyong’onyea kwangu. Nikishaipata hutafuta sababu iliyo kinyume na hiyo, ambapo hunisaidia kuondokewa na kunyong’onyea huko sana.

Nakutakia maisha mema yawe ya furaha kwako, endelea kutembelea mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO kujifunza na kuhamasika kila siku, karibu sana.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,

IMANI NGWANGWALU,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.