google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 3, 2015

Hatua Tano Muhimu Za Kuelekea Kwenye Mafanikio.

No comments :
Mara nyingi sana katika maisha yetu tumesikia maneno kama “nipe tano” “chukua tano” maneno hayo yamekuwa maarufu na katika mazingira tofauti, yamekuwa yakiashiria ushindi , au hali ya mafanikio au furaha baada ya hali fulani.
Vivyo hivyo katika maisha yetu ya kutafuta kufanikiwa katika yale yote tunayoyafanya kila siku viko vitu au hatua ambazo huwa zinatulazimu kuzijua au kuzipitia kama kweli tunamaanisha na tunadhamiria hayo mafanikio tunayoyatafuta.
Watu wengi hutamani mafanikio na kuyazungumzia sana katika maneno yao ya kila siku lakini hawajawahi kuyaishi mafanikio hayo kwa sababu ya kutokuwa na dhamira madhubuti katika kuyaelekea. Je, unajua ni hatua zipi muhimu za kuelekea kwenye maisha ya mafaniko?
1.Kuwa na uwezo binafsi wa kuvikagua vile ulivyo ndani yako.
katika maisha yetu ya kila siku hatuna budi namna ya kujifunza kujikagua sisi wenyewe, kuvikagua vile tulivyonavyo ndani yetu kwa sababu ni ukwelli kwamba pasipo kujikagua sisi wenyewe basi hatutaweza kuyatambua mapungufu tulionayo na kama hatutoyatambua mapungufu hayo hayatoweza kushughulikiwa na kuondelewa, maana yake ni kwamba tutazidi kushi na upungufu wetu na hivyo kuathiri ufanisi wetu na mwisho wake mafanikio yetu kwa ujumla yataathirika.
Labda nikupe mfano wa mtu mwenye duka , mara kwa mara huwa na muda wa kuvikagua vitu au mali aliyo nayo dukani kwake na hapa huweza kutambua nini kimepungua , nini hakipo kabisa na nini hakipo kwa wingi. Katika kujikagua sisi wenyewe sio tu tutapata uhakika  wa vile tusivyonavyo bali pia tutapata kufahamu vile tulivyonavyo kwa wingi. Jifunze kufanya tathmini ya maisha yako kila wakati, tathmini matendo yako ya kila siku, maneno yako ya kila siku, mitazamo yako ya kila siku, halafu angalia wapi kuna upungufu na wapi kuna fursa.

 2. Uwezo wa kuwa na msimamo.
Wengi wetu tumeshindwa kuyafikia malengo tuliyowahi kujiwekea kwa sababu tu hatuna msimamo katika vile tunavyoviamini kwa hiyo inakuwa ni rahisi kuyumbishwa na kupeperushwa na kila upepo unaokuja upande wetu. Ili kufikia mafanikio tunayoyatamani hatuna budi kuwa na misimamo fulani katika maisha. Naupenda msemo unaosema kama huwezi kuwa na msimamo na chochote basi utachukuliwa na chochote.
Kama wewe ni kijana na huna msimamo katika baadhi ya mambo basi ni rahisi kujikuta unabebwa na mengi kama vile rushwa na ubadhilifu. Ni vyema kufahamu kila wakati maishani kuwa kama huna msimamo katika ufanisi basi utaangukia katika uzembe na kutokuwajibika na kama hautakuwa na msimamo katika kuhakikisha unafanikiwa basi utaangukia katika umaskini.
3. Uwezo wa kupiga hatua.
Yamkini unatamani sana kufanikiwa na kila siku unaongelea sana mafanikio, ni vyema kujua kwamba mafanikio yetu hayaji kwa kuyatamani au kuyaongelea bali katika uwezo binafsi wa kuamua kupiga hatua. Yawezekana upo katika chombo kizuri tu cha usafiri lakini utajikuta unapitwa na kila mtu, hata wale wenye vyombo vibovu vya usafiri nao watakupita kama utakuwa umekaa tu kwenye chombo chako pasipo kuruhusu mwendo.
Chukua hatua kuelekea mustakabali wako, angalia mbele yako unaona nini? Niniambacho unakiona kwenye mustakabali wako? Nini  ungetamani ukipate kwenye mustakabali wako? Anza kufanya kila kinachohusika ili kuona hiyo ndoto yako ikiwa dhahiri.
Anza kupiga hatua ya kwanza na hatua nyingine zitakuwa ni rahisi kufuatia. Kamwe usitishike na umbali unaouona kuelekea mustakabali wako, jinsi unavyopiga hatua ujasiri wako unafunguka na kukua, kumbuka kuwa kila hatua unayoipiga hata kama ni ndogo kiasi gani inakusogeza karibu na mustakabali wako.

4. Uwezo wa kujitengenezea sura ya maisha yako.
Katika maisha yetu ya kila siku ni ama uamue kuitengeneza sura ya maisha yako au kuibomoa sura hiyo, wengine wetu maisha yetu hayajawahi kuwa na sura nzuri ya kuvutia.
Sisi wenyewe ndiyo wenye uwezo wa kuamua kuitengeneza sura hiyo kuwa kama vile tunataka iwe, ukiamua kukaa tu pasipo kufanya chochote basi umekusudia kwa dhamiri halisi kuiharibu sura  ya maisha yako mwenyewe.
Ulimwengu wa leo unabadilika kwa kasi sana, ili kuweza kubakia kwenye maana na wenye umuhimu basi hatunabudi kuwezana na mabadiliko hayo. Kama hutoweza kuyaweza mabadiliko ya karne hii basi mabadiliko hayo yatatuweza.
 5. Uwezo wa kukikalia kiti na kuyaongoza maisha yako mwenyewe.
Ziko nyakati ambazo wengi wetu hatuwezi kufika tunapotamani kufika kwa sababu dereva anayeendesha chombo chako siyo wewe, wakati huohuo unafikiria kuelekea pale unapopatamani wewe.
Ni ngumu katika maisha kama unaifahamu ndoto yako na unaiona kesho yako na unaitamani sana kuifikia  basi amua kukaa kwenye kiti cha dereva wewe mwenyewe na kuendesha chombo kuelekea huko.
Watu wengi siyo kwamba tumewakabidhi wengine udereva wa safari yetu kwa kujua bali ni kwa kutokujua, mara unaona muelekeo wa safari siyo ule unaoutarajia, yamkini sasa dereva uliyemkabidhi kiti anakupeleka kwenye ndoto yake na siyo ya kwako tena.
Sasa amua kuingia kwenye kiti cha dereva wewe mwenyewe, hayo ni maisha yako na siyo mwingine. Kamwe usiache furaha ya mafanikio yako katika mikono ya mwingine. Kubali na kuwa tayari kubeba majukumu. Kama unatokea unafanya makosa basi usijitetee na kukwepa, chukua tano!
Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza na kuhamasika zaidi.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA MTAALAMU WA SAIKOLOJIA,

CHRIS MAUKI WA GAZETI LA MWANANCHI.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.