google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jul 1, 2015

Huyu Ndiye Mtu Pekee Anayekufanya Ushindwe Katika Maisha Yako.

No comments :
Habari za siku ya leo ndugu msomaji wa mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO. Ni matarajio yetu ya kuwa umzima wa afya na karibu sana katika siku nyingie ambapo unapata nafasi ya kujifunza mambo muhimu ya kimafanikio. Katika makala ya leo tutaangalia jambo muhimu la kujifunza kupitia simulizi liliyotolewa na mwandishi nguli wa vitabu John Mason.
Katika kitabu chake cha ‘Limitation is Imitation’ mwandishi huyu anaelezea hadithi ya kijana mmoja ambaye siku moja aliweza kutoka na baba yake na kwenda kutalii katika eneo moja la mlimani ambapo wote kwa pamoja waliweza kupata nafasi ya kupanda juu ya mlima huo.
Wakiwa juu ya mlima ule kijana yule mdogo pengine kutokana na uchovu ilifika mahali alitaka kudondoka yaani nikiwa na maana aliteleza na kutaka kuanguka chini. Kutokana na hofu hiyo ya kutaka kudondoka chini kijana yule alijikuta akipiga kelele  ‘Yaaaa! Yaaaa!’. Kwa mshangao tena, kutokana na kelele hizo alizozipiga alishangaa tena kelele hizo hizo za kwake zinasikika upande mwingine.
Kijana yule kitu hicho kilimshangaza sana na kujikuta akimuuliza baba yake nini hicho alichokisikia ambacho kilitoa sauti kama yake. Lakini kabla hajajibiwa na baba yake swali lake, kijana huyu alishangaa tena maongezi hayohayo anayomuulizia baba yake yanasikika upande wa pili tena. Hali hiyo ilizidi kumtia hofu zaidi na wasiwasi mwingi na kuwa na kulikoni nyingi kwenye kichwa chake.
Baba yake baada ya kuona hivyo aliamua kumwambia mtoto wake kuwa kitu hicho anachokisikia kinafahamika kama mwangwi na kisha akamfafanuliwa jinsi inavyokuwa na kwa sababu gani huo mwangwi huo unatokea na kisha mwisho kabisa akasisitiza kwa kijana wake kuwa hivyo ndivyo maisha yetu huwa yako hivyo kama mwangwi.

Kijana alistaajabu na kushangaa, lakini aliambiwa na baba yake huo ndiyo ukweli anaotakiwa aujue kuwa maisha  yetu yanakuwa kama mwangwi ama sauti inayojirudiarudia kwa sababu yanatupa kila kitu kama tulivyokitoa. Kama utatoa upendo jiandae kupokea upendo, kama huwa unatoa mafanikio na kufanya kila kinachoendana na mafanikio jiandae kupokea mafanikio pia katika maisha yako. Kwa tafsiri hiyo maisha yako ni mrejesho wa vitendo vyetu tunavyovifanya katika maishayetu.
Maisha uliyonayo siyo ajali kama unavyofikiria, ni matokeo ya mrejesho wa yale mambo unayoyafanya. Jaribu kuangalia na kujichunguza kidogo utagundua ukweli wa hilo kuwa unavuna ulichokipanda huo ndiyo mrejesho ninao taka kukwambia. Hivyo kama unajiona maisha yako ni mabaya acha kulaumu watu wengine, mtu wa kwanza kumlaumu ni wewe mwenyewe kwani huyu ndiye mtu pekee anayekufanya ushindwe katika maisha yako.
Kuna wakati pia mwandishi  Stewart Johnson aliwahi kusema kuwa kitu kikubwa katika maisha yetu ni siyo kushindana na wengine ni bali kushindana sisi wenyewe na kuwa bora zaidi na zaidi siku hadi siku, hili ndilo jukumu na lengo kubwa ambalo tunatakiwa tuwe nalo katika maisha yetu. Na huu ndiyo ukweli usiopingika unaotakiwa uujue ili kuboresha maisha yako.
Katika maisha yako kama unataka mafanikio zaidi jifunze kutambua kwamba maisha yako ni kama mwangwi. Ukishajua hilo lipia gharama za mafanikio hayo kwa kufanya vitendo ambavyo vitakufanya lazima ufanikiwe. Acha kujidanganya wewe mwenyewe na kuamini kuwa yupo ‘mchawi’ anayeweza kukwamisha mipango na malengo yako.
Hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kukuharibia maisha yako ni wewe mwenyewe kutokana na vitendo vyako. Jifunze sasa kutokuwaangalia wengine kama chanzo cha matatizo yako, badala yake anza kujiangalia wewe kwanza kuwa ndiye unayesababisha ushindwe kufanikiwa. Hakuna mtu anayekufanya ushindwe zaidi ya wewe mwenyewe kujiaminisha kuwa huwezi na unajikuta umeshindwa kweli.
Kumbuka siku zote maisha yako yapo hivo kutokana na mambo yale uliyoyapanda, ama uliyoyatoa. Hakuna kujuta wala kulalamika kwa kuwa tunapata vitu vinavyotokana na sisi wenyewe ni matokeo ya matendo yetu ambayo tunayafanya mara kwa mara na kila siku. Hivyo ni rahisi kusema kuwa katika maisha yetu tunavuna kile tulichokipanda na siyo vinginevyo.

Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio na endelea kutembelea mtandao huu wa DIRA YAMAFANIKIO kwa kujifunza na kuelimika zaidi.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.