google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 24, 2015

Nguzo Tatu Muhimu Za Mafanikio Ambazo Ni Lazima Uwe Nazo.

1 comment :
Umefika sasa wakati wa kila mmoja wetu kutambua kuwa ana uwezo mkubwa wa kutumia vipaji vilivyo ndani mwake kuweza kumletea mafanikio makubwa  maishani. Hii  nikiwa na maana kuwa inakulazimu kuweza kujua kuwa hiki kipindi tulichonacho sasa ni kipindi cha maarifa ambayo kwa sehemu kubwa yanahusisha vipaji na ubunifu mkubwa zaidi ili kuweza kufanikiwa.

Katika kipindi hiki mtu anayefanya chochote kwa sababu yoyote hawezi kufika popote. Watakaoweza kumudu mashindano ya dunia hii ya sasa, ambayo imefanywa kuwa ndogo zaidi, ni wale tu walio na maaarifa maaalum na kwa sababu maalum na siyo tu maarifa. Ninasema hivi sio kwa kukutisha na pia si maanishi uwe na elimu ya chuo kikuu ndiyo uwe na maarifa haya, unaweza kuyapata hata kama hukwenda shule.

Kwa kulijua hilo kuwa tupo kwenye dunia ya ushindani ambayo inatulazimisha kuwa na maarifa, vipaji na ubunifu ni muhimu kwetu kujipanga ili kuhakikisha mambo hayo yote matatu tunayo ili kuweza kujihakikishia kufanikiwa, kwani mambo hayo ni nguzo muhimu sana kwetu sisi na kizazi kijacho ili kujenga taifa imara lililofanikiwa.


Pamoja na umuhimu wa maarifa, ubunifu na vipaji katika suala zima la mafanikio yetu, lakini kwa bahati mbaya wazazi wengi hapa nchini hawajui au hawajali sana kuhusu vipaji. Hii hupelekea wazazi wengi kuweza kukandamiza vipaji vingi vya watoto wao bila kujua kuwa wanaua vipaji hivi vya watoto.

 
Kuna wazazi ambao huwakataza watoto wao wasiimbe kwa maelezo kwamba, kuimba ni ibilisi. Kuna wazazi wengine huweza kuwavunja nguvu  watoto wanacheza mpira, kuchora na shughuli nyingine za kisanii kwa maelezo kwamba mambo hayo huwapotezea muda wa masomo. Wasichokifahamu wazazi hao ni kwamba, huenda  hivyo wanavyofanya watoto ndivyo vipaji vyao, yaani ndiyo makusudi ya wao kuletwa hapa duniani.

Kwa watu wengi ikiwemo wazazi kama ambavyo nawaongelea hapa wanapenda au wanataka watoto wao wawe ama wafanye yale ambayo wao wazazi ndiyo wanayoyapenda bila kujali upendeleo na uwezo wa watoto. Hali hiyo ndiyo ambayo inawafanya wasomi wengi wa nchi hii kwa wasomi wa sifa na pato, badala ya kuwa wasomi wa ubunifu kwa faida ya jamii.


Kuna wasomi ambao hawakujua tangu awali kwa nini wanasoma kile walichokisoma, kwa sababu hata uchaguzi wa wasome kitu gani, ulifanywa na wazi wao, wakati mwingine, kwa kuwalazimisha. Kuna vijana wengi wenye vipaji vikubwa ambao wameshindwa kuvitumia kabisa au kuvitumia vizuri, kwa sababu vilikandamizwa utotoni.

Kama tulivyosema, umefika muda sasa ambapo wazi wanapaswa kama siyo kulazimishwa na mazingira, kujua kwa makusudi vipaji vya watoto wao ili waweze kuwasaidia kujenga kesho yenye mkabala thabiti zaidi wa kimafanikio.

Mtoto anapoonesha kipaji fulani, sisi wazazi tusikikandamize kwa sababu, hatukitaki. Anapoonyesha kipaji tumpe moyo  ili aweze kukiendeleza kwa faida yake na ya kwa wengine. Kukandamiza vipaji vya watoto na kujaribu kuwaingizia kile ambacho hakiko ndani mwao kwa hakika ni kuwaumiza bure tu.

Ifike mahali na sisi tukubali kwamba, hata sisi huenda vipaji vyetu huenda vilikandamizwa au hatukuoneshwa kwa namna nzuri ya kuvibaini na ndiyo maana pengine wengi wetu hatufurahii shughuli tunazizifanya maishani mwetu. Kwa nini nasi tulee watoto ambao watakuwa na utapiamulo wa ufahamu na matumizi ya vipaji.


Pia tutambue kuwa, tupo kwenye kipindi cha zama za maarifa ni jukumu lako kutumia nguzo tatu hizo muhimu kuweza kutufanikisha nikiwa na maana Maarifa, ubunifu na vipaji tulivyo navyo ili kufikia mafanikio makubwa. Vitu hivi vikikaa pamoja na kufanyiwa kazi vinaleta matokeo makubwa na ya kushangaza. Kwani hizo ndizo nguzo tatu muhimu za mafanikio kwako na kizazi kijacho unazotakiwa kuzijua.

Tunakutakia kila la kheri, endelea kujifunza kila siku bila kuchoka kwa kupitia mtandao huu wa DIRA YA MAFANIKIO lakini hakikisha unawashirikisha wengine ili kuweza kujifunza zaidi.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,

1 comment :

Note: Only a member of this blog may post a comment.