google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 22, 2022

WAZO LA KUJIAJIRI: Biashara Ya Vikombe Vya Chai Vyenye kubadili Rangi Vikiwekwa Chai Au Maji Ya Moto.

No comments :

Naam, wala usishangae najua tumezoea kunywa chai kwa kutumia vikombe hivi vya kawaida ambavyo havina kitu cha kushangaza pindi utuamiapo. Sasa katika wazo letu la kujiajiri tunakuleta wazo jipya ambalo kwa baadhi ya watu huenda likawa ni geni kabisa. Wazo hili si jingine bali ni vikombe vya udongo ambavyo hubadili mwonekano hasa pale vinapowekwa maji ya moto au chai.
Vikombe hivi ni vizuri sana ndugu yangu kwa sababu ya uimara wake lakini najua pindi utakapoamua kuifanya biashara ya vikombe hivi utawashangaza wengi sana na kiukweli utapata wateja wengi sana. Chukua sekunde chache wawaze mamantile waliopo mtaani kwako, usiishie hapo endelea kuwaza mahotel ambayo upo nayo karibu.
Endelea kuwaza wale watoto ambao hawapendi kunywa chai, vipi ukimpa mtoto huyo chai kwenye kikombe ambacho kitaonesha sura yake pamoja na jina lake bila shaka mtoto huyo hata kusumbua tena kwenye suala la kunywa chai na uji pia, kwa sababu mtoto huyo atashangaa majabu ya kikombe hicho pia hivyo atakunywa tu.
Endelea kuwaza kwa sauti ya chini, Vipi mumeo anaamka asubuhi kabla ya kwenda kazini anakuta umemuwekea maziwa kwenye kikombe kimeandikwa “ I love you Benson” na hilo ndilo jina la mumeo na akimaliza kunywa chai hiyo hayo maandishi yanatopea hadi kesho tena kikombe hicho kikiwekewa chai, bila shaka mumeo huyo atafarijika na michepuko haitakuwa  nafasi tena na utafurahia ndoa yako.
Kwa mifano hiyo michache utaona ni kwa namna gani vikombe hivo jinsi vitakavyokupa hela nyingi kwa sababu kwa hapa nchini kwetu havipo kwa wingi, hivyo bado ni fursa ambayo ni mbichi kabisa. Hivyo ni nafasi yako mwafaka wa kukamatia fursa hii na kuanza kuifanyia kazi ili uanze pia kujitengenezea pesa.
Kumbuka; Vikombe hivi  hubadilisha rangi, picha, maneno  kila vinapowekwa chai au maji ya moto hivyo ni fursa sana kama utaifikiria  kwa jicho la tatu.
-------------------------------------------------------------------------------------------------
MUHIMU: Kama utakuwa  upo tayari na unahitaji kufanya biashara hii wasiliana na uongozi wa DIRA YA MAFANIKIO kwa nambari 0757 909 942 au bofya namba hii tuwasiliane kupigia whatsapp wa.me/+255757909942  hii au email yetu ya dirayamafanikio@gmail.com
------------------------------------------------------------------------------------------------
Makala hii  imeandikwa; Benson Chonya
------------------------------------------------------------------------------------------------

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.