google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 20, 2022

Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuweka Jitihada Usikose Pesa.

No comments :

Kukosa pesa ni kilema kikubwa sana katika huu ulimwengu tuliopo. Ukiwa huna pesa changamoto kwako ni nyingi na unakuwa upo kwenye ukilema mkubwa usioujua.

Maskini wa kipato kidogo hata akiwa na mawazo mazuri bado hatapewa kipaumbele katika jamii yake kama vile pumba za tajiri zinavyopewa kipaumbele kikubwa zaidi.

Mungu mwenyewe analijua hilo ndio maana baada ya mfalme sulemani kumuomba hekima, Mungu akaamua kumpatia na utajiri kama ziada ya maombi yake.

Maana alijua kuwa hekima ya maskini inadharauliwa, wala maneno yake hayasikilizwi.


Binafsi nawapongeza wote ambao wanahamasisha wengine kutafuta pesa, maana wakizipata wataheshimiwa.

Umaskini ni mbaya sana, na unapaswa kuchukiwa kwa nguvu zote, nami nasema hakuna mpumbavu duniani zaidi ya anae ona ufahari kuwa juu ya umaskini.

Umaskini sio baraka ni laana, ndani ya umaskini kuna ujinga mwingi, maradhi sugu, pamoja na kuonewa, nenda kwenye magereza au vituo vya polisi utakuta 90% ya walioshikiliwa ni maskini.

Nenda kwenye hizi hospital za kawaida, utakuta wanaoteseka wengi ni maskini, hata anaetumiwa mgambo waende kumkamata huyo ni maskini kwa sababu, wenye pesa hutumiwa barua ya wito na atajisalimisha mwenyewe maana utajiri unampa ujasiri wa kutokuogopa hovyo.

Ndugu yangu unaesoma ujumbe huu, anza kuuchukia umaskini kama unavyochukia harufu mbaya na uogope kama vile unavyoogopa magonjwa yasiyotibika, hiyo itakusaidia upate hamasa ya kutafuta pesa na kuwa tajiri katika siku zote za maisha yako.

Kila la kheri katika kufikia mafanikio makubwa.

Endelea kujifunza kupitia MafanikioApp na dirayamafanikio.blogspot.com kwa ajili ya kujifunza.

Kama unapenda kujiunga na kundi la mafanikio ili uweze kujifunza zaidi mambo mengi ya mafanikio. Tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER'S kwenda 0687449428 na utapewa utaratibu wa kuunganishwa.

Hakimiliki©2022 Imani Ngwangwalu. Haki zote zimehifadhiwa. Makala hizi hutolewa kwa ajili ya kuboresha maisha yako. Rukhsa 'kushare' na usibadili kitu chochote bila ruhusa ya mwandishi.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.