google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 30, 2020

Kama Utazingatia Mambo Haya Mawili, Umefanikiwa.

No comments :
Kama unataka kujenga maisha yako ya mafanikio, na ukajikuta mbali sana, unaweza ukazingatia sana mambo haya mawili tu. Haya ni mambo ambayo yamewasaidia sana wengi kufanikiwa;-

 #1. Linda kazi yako ya siku na anzisha biashara ya muda.

Kama umeajiriwa anza na kulinda kazi yako kwanza, na kama umejiajiri, chunga sana kipato chako, hiyo inakusaidia sana, kujifunza biashara, na kuchukua uzoefu mkubwa wa biashara. Pia inakusaidia kuchukua umiliki wa maisha yako ya baadae, ya kwamba utakuwa wapi mara baada ya muda fulani.

Kwa kadri unavyokuwa kwenye ajira au biashara yako na huku unafanya biashara nyingine ya pembeni itakusaidia sana kujifunza mengi ambayo usingeweza  kujifunza kama usingeanza kabisa biashara hiyo.


 #2. Wekeza katika nyumba.

Ukiwekeza katika nyumba, ama "real estate" ni rahisi kwa benki kukupa mkopo na ukasonga mbele sana kimafanikio. Hivyo kazana kujenga nyumba hata kama ni ndogo ndogo tu, kwa ajili ya mikopo.

Wawekezaji wengi, wanafanikiwa kwa sababu ya kutumia mikopo ya nyumba. Unasubiri nini, anza kuwekeza kidogo kidogo kwenye nyumba ili ikusaidie kuchukulia mkopo, ila hakikisha isiwe nyumba yako ya kuishi.

Kila la kheri,
Imani ngwangwalu,
dirayamafanikio@gmail.com

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.