google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jun 29, 2015

Kama Unataka Kuishi Maisha Ya Furaha Na Mafanikio? Hakikisha Unafanya Uchaguzi Huu Katika Maisha Yako.

No comments :
Maisha uliyonayo yanaweza yakawa mazuri sana ama mabaya kutokana na aina ya uchaguzi unaofanya juu ya maisha yako kila siku. Mara nyingi uchaguzi tunaofanya katika maisha yetu ndiyo huwa unaamua zaidi maisha yetu yaweje. Kama uchaguzi unaofanya ni mbaya, ni wazi maisha yako yatakuwa mabaya na kama uchaguzi wako ni mzuri basi maisha yako yatakuwa mazuri hivyohivyo hakuna atakayezuia hilo.
Kwa kuwa uchaguzi wowote tunaofanya katika maisha yetu unakuwa una athari ni vizuri tukawa makini kidogo na uchaguzi wa mambo tunayofanya kila siku. Nikiwa na maana kuwa inatakiwa tujue kama kuna jambo tunalifanya ni muhimu kutambua lina athari zipi kwetu. Kama tumeamua kufanya kitu fulani tuanze kwa kutafakari matokeo yake kwanza. Hivyo ndivo tunavyotakiwa kufanya ili kuwa na uchaguzi sahihi katika maisha yetu.
Kwa uchaguzi sahihi tutazidi kufanya maisha yetu kuwa bora siku hadi siku. Ikumbukwe pia kila kunapokucha tunanya aina nyingi sana za chaguzi ambazo zinaamua hatima ya maisha yetu. Mara nyingi huwa ni watu wa kuchagua mavazi, nguo za kuvaa, njia na mambo mengineyo mengi. Sasa ikiwa tunachagua mambo haya, kwanini tusiwe na uchaguzi juu ya maisha yetu? Je, unajua ni aina gani ya uchaguzi sahihi tunaotakiwa kuufanya katika maisha yetu ili kufanikiwa zaidi?
 1. Chagua kuishi sasa.
Hii ndiyo siri ya wewe kuweza kufurahia maisha yako. Hautaweza kufurahia maisha yako na kuyaona katika uzuri wake halisi ikiwa unaishi kwa fikra sana za siku ziliyopita ama siku za nyuma zaidi. Kwa kuishi kwako sasa, kuishi kwa kutokuwa na hofu sana juu ya kesho yako, hapo utakuwa unafanya uchaguzi sahihi utakao weza kubadilisha maisha yako na kuwa ya furaha na yenye mafanikio kwako pia.

2. Chagua kuishi maisha yasiyokuumiza.
Acha kuishi maisha ya kuumiza utaumia sana. Ili kufanikwa kwa hili, jifunze kutokuyachukulia mambo kwa ujumla ili usiweze kuumia zaidi. Ikiwa mtu atakwambia wewe ni mbaya, hufai hiyo yote inaweza ikawa sawa kulingana na mtazamo wake. Hapo lakini wewe usije ukachukulia huo ndiyo ukweli na kuanza kuumia na kujiona kweli hufai. Fuata ukweli ulio ndani yako kuhusu wewe na siyo vinginevyo.
 3. Chagua kuishi maisha ya ukarimu.
Haijalishi mtu amekufanyia nini katika maisha yako kitu kikubwa cha kujifunza nikuwa mkarimu kwa wetu wengine. Unapokuwa mkarimu unakuwa unaishi maisha ya utulivu ambayo mara nyingi yanakuwa hayana msuguano zaidina wengine katika maisha yako. Kwa kuishi maisha hayo yatakusaidia kukupa furaha na nguvu ya kufanikiwa. Hivi ndivyo unavyotakiwa kuishi na kuwa hivyo.

4. Chagua kuishi kwa kufanya mambo yako kwa uchache.
Ikiwa utajifunza kumudu tabia hii basi utaweza kuishi maisha safi ya furaha ambayo wewe mwenyewe utakuwa ni wazi unayafurahia kwa vyovyote vile iwavyo. Jifunze katika maisha yako kuongea kidogo na kuwa msikilizaji sana. Jifunze pia kula chakula kiasi ili kukujengea afya bora zaidi. Mambo mengi jaribu kuyafanya kwa kiasi hiyo itakuwa ni siri mojawapo ya kuweza kukupeleka kwenye mafanikio.
 5. Chagua kufanya mambo mapya.
Hautaweza kufanikiwa kama utakuwa unafanya mambo yaleyale siku zote. Ili kuweza kufanikiwa unalazimika kuchagua kufanya mambo mapya ambayo hujayazoea. Katika kufanya mambo mapya ni lazima kujitoa mhanga na kukabiliana na kila aina ya changamoto ili kuweza kufanikiwa, vinginevyo itakuwa ni ngumu sana kuweza kumudu kuleta mafanikio tunayoyataka katika maisha yetu.
Tunakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio na endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza na kuhamasika zaidi.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
IMANI NGWANGWALU,
0713 048035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.