google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 20, 2018

Sababu Tano (5) Kwa Nini Unaogopa Sana Kushindwa.

No comments :
Kati ya kitu ambacho watu wengi sana wanakiogopa ni kule kushindwa. Ukiwauliza watu hao kwa nini wanaogopa sana kushindwa kwenye kile kitu wanachataka kufanya, sana sana watakwambia sababu moja tu kwamba wanaogopa kupata hasara.
Watu hawa wanakuwa hawana sababu zingine makini za kwa nini wao wanaogopa kushindwa, na hali ambayo inawasababishia wao hata washindwe kuchukua hatua. Suala la kuogopa kushindwa lipo kwa watu wengi sana, na unaweza ukawa miongoni mwao.
Hebu tuulizane mimi na wewe, au nikuulize je, unajua hasa kwa nini watu wanaogopa sana kushindwa, iwe kuogopa kushindwa kwenye mradi, kwenye masomo, au kwenye usaili, lakini woga huo upo tena kwa sehemu kubwa tu, naamini unalijua hilo.
Sina shaka unafikiri na kujiuliza aisee ni kweli watu tunaogopa kushindwa na una hamu ya kutaka kujua sababu zake ni zipi hasa zinazofanya watu waogope sana kushindwa. Tulia hapo hapo, nikupe sababu yakinifu  za kwa nini watu wengi wanaogopa kushindwa.

1. Ufinyu wa mawazo.
Watu wanaogopa kushindwa kwa sababu ya ufinyu wa mawazo au akili zao zinakuwa  kama vile zimefikia ukomo. Kivipi? Mtu anakuwa anaogopa kushindwa kwa kuamini kwamba akishindwa ndio hana nafasi tena ya kujaribu, kwa hiyo hawezi kufanikiwa hata iweje.
Ukiwa una mawazo haya yanayoamini nafasi pekee ya hicho ukifanyacho ni moja tu na haitajirudia kwako tena, basi utaogopa sana kushindwa. Hutaweza kufanya biashara kwa usahihi au chochote kwa sababu utaogopa kama ukishindwa ndio umepoteza na kupotea.
Maisha hayana nafasi moja kama unavyofikiri. Ukishindwa leo, kuna nafasi ya kujaribu tena na tena mpaka utafanikiwa. Ukiondoa ufinyu wa mawazo au ‘limited mind’ ya kuamini kwamba ukishindwa ndio basi, hutaogopa kushindwa tena, upo?
2. Kutaka kuonekana sahihi wakati wote.
Leo kila mtu akifikiria kufanya jambo anataka kuwa sahihi sana mbele ya watu. Anataka kufanya jambo lake huku akiwa amekamilika kwa asilimia mia moja. Mtu huyu anasahau kabisa kwamba hata wale anaowaona wamekamilika walianza wakiwa hawajakamilika.
Kwa mawazo hayo ni lazima, piga ua garagaza, mtu huyu ataogopa kushindwa. Kila wakati akitaka kufanya jambo anakuwa anajiuliza je, nikishindwa itakuwaje, si nitachekwa na watu na nitaonekana sifai.
Kwa hiyo hapa na kwa kifupi, kinachowapoteza watu wengi na kuogopa kushindwa ni kwa sababu ya kutaka kuanza kwa ukamili, ukiwa sawa kila kitu. Kwa sababu hiyo kuogopa kushindwa huwezi kukwepa hata iweje, umeidaka hiyo?
3. Athari mbaya tulizofundishwa shuleni.
Tokea tukiwa shule au tukiwa wadogo tumefundishwa na kukaririshwa na kwa bahati mbaya na sisi tukameza kama kasuku na kujua kwamba kushindwa ni kitu kibaya. Hakuna ambaye kafundishwa kushindwa ni kitu kizuri.
Ili kukuhakikishia kushindwa ni kitu kibaya, tena tukawekewa na viboko, ukizingua  tu kwa kushindwa unacharazwa bakora zako ili kesho usishindwe. Kwa hiyo kila wakati ulikuwa ukiwaza mmh nikishindwa tu, kimenuka.
Sasa nikuulize, je, uliyepitia mazingira kama haya utakwepa kuogopa kushindwa? Hapa ni lazima utaogopa kushindwa tu na utakuwa unaona kushindwa ni kosa kubwa sana. Hivyo utafanya kila linawezekana usishindwe, kumbe ndio umepotea, umeiona hiyo?
4. Kuhofia kuchekwa.
Eti unaogopa kushindwa kwa sababu ya kuogopa kuchekwa, unasema daah, hivi nikishindwa watu watasema nini, si watanicheka sana na itakuwaje. Kwa sababu hii tu, aloo, lazima uogope kushindwa na hutaweza kuchukua hatua.
Unajua kila mtu anataka kuonekana simba, anataka kuonekana anafanikiwa kwenye jamii, sasa kwa mawazo hayo mtu anataka mambo yake yaonekane yamewaka hakuna kushindwa, hapo ndipo hofu inapoanza kuzalishwa sasa.
Kwa mtu mwenye mawazo kama hayo ya kuogopa kuchekwa, wee, utamwambia nini, badala ya kuweka nguvu zake kwenye kuchukua hatua, yeye anakomaa na kuogopa kushindwa kwa kile anachotaka kukifanya, hatari hiyo umeisoma eeh?
5. Kutokujiamini.
Sababu  nyingine ya kiufundi ya kuogopa kwetu kushindwa ni kwa sababu hatujiamini. Hauamini kwamba eti unaweza ukatoka kwenye kushindwa hadi kufanikiwa. Haumini kama ndani yako unao uwezo mkubwa wa kukusaidia kufanikiwa.
Kama hujiamini kuogopa kushindwa kunakuhusu sana tu na tena sana. Kama huamini uwezo wako, basi hiyo kwako itakuwa ni sababu ya msingi sana itakayokufanya uogope sana kushindwa kwa chochote kile, unachotaka kukifanya.
Kwa kujifunza sababu hizi zinakufanya uogope kushindwa naamini zimekuondolea hofu kwa kiasi, lakini elewa hivi, huwezi kufanikiwa pasipo kushindwa, kwani kushindwa ni sehemu ya mafanikio. Hivyo usiogope sana kushindwa, bali kushindwa huko kufanye kuwa ngazi ya mafanikio yako. Na piga marufuku kuogopa kushindwa maishani mwako kabisa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 713 048 035,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.