google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 15, 2018

Mafanikio Yako Yanatengenezwa Na Muda Huu Tu.

No comments :
Kati ya kitu ambacho huwezi kucheza nacho na ikitokea umekipoteza ndio imetoka hiyo, ni muda ulionao. Unaweza ukacheza na vyote kwenye maisha yako na ukavipoteza na ukaanza upya hadi kufanikiwa, lakini si muda wako, ukipoteza muda haurudi tena.

Upo uwezekano pesa ukaiweka ya akiba kama umeipata pesa nyingi na ya ziada. Hata hivyo inapotokea pesa imepotea, upo uwezekano pia wa kuweza kutafuta pesa zingine kwa baadae na ukawa tena na pesa kama kawaida utafikiri hukupoteza kitu.
Lakini uwezekano huo ambao upo kwenye pesa hauwezi kutokea hata kidogo kwenye muda wako. Muda ulionao ni kitu kingine ambapo thamani yake haipimiki kwa chochote. Unapochagua kupoteza muda wako ndio unapoteza maisha yako kabisa.

Unayo nafasi moja tu ya kufanya maisha yako ya kesho yawe bora ikiwa utaitumia leo kwa uhakika. Unayo nafasi moja ya kutumia fursa uliyonayo kwa uhakika hadi kufanikiwa kwa muda ulinao. Ikiwa utajichanganya na kutumia fursa hovyo huwezi kufanikiwa.
Muda ulionao leo unaweza kufanya maisha yako ya kesho yakawa mazuri sana au yakawa hovyo kabisa, kikubwa tu inategemea muda wako unautumiaje? Kama unautumia muda wako hovyo andika maumivu.
Ndio maana unatakiwa utambue leo yako ikipita, hiyo ndio imepita haiwezi kurudi tena. Kwa hiyo kama kuna jambo umeliahirisha na kuamua kulifanya kesho, basi ujue kabisa umesogeza mafanikio yako kesho.
Unachotakiwa kujua kitu kingine kinachowaangusha watu wengi kwenye maisha si kwa sababu hawana uwezo huo, bali kinachowaangusha ni kwamba wamekuwa ni watu wa kutumia muda wao hovyo sana kila siku.
Kama unajiona huna cha kufanya kwenye maisha yako, hebu tumia muda wako kidogo ulionao kuweza hata kujifunza juu ya maisha kupitia vitabu au semina ili uweze kubadilisha maisha yako. Usikubali kupoteza muda wako hovyo hiyo ni hatari kubwa sana kwako.
Juhudi zako lazima ziendane na kutambua umuhimu wa kutunza muda wako ili kufikia mafanikio makubwa. Ikiwa utakuwa unaishi tu kiholela na kuona muda kwako ni kitu ambacho hakina thamani kabisa utapotea.
Kumbuka kila wakati muda unaotengeneza maisha yako ni muda huo huo mdogo  ambao unaouna hauna thamani huo ndio unaofana maisha yako yawe bora au hovyo kabisa. Unatakiwa kuwa makini na muda wako ili kujenga maisha uyatakayo.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,


No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.