google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 18, 2018

Mambo Kumi Utakayofaidika Nayo Kupitia Kujifunza Kila Siku …

No comments :
Watu wanao anguka sana kwenye maisha na hawafiki mbali ni wale watu ambao hawajifunzi iwe kwa kusoma vitabu au kujifunza kwa wengine. Ipo faida kubwa sana ya kujifunza ambayo wengi hawaijui na kuchukulia mambo kwa kawaida tu.
Labda nikwambie hivi, ikiwa husomi vitabu ni kweli unaweza ukafanikiwa, lakini hutaweza kufikia mafanikio yale ya juu sana. Utaishia tu kwenye haya mafanikio ya kawaida. Sasa je, faida za kusoma vitabu ni zipi?
Hapa kwenye makala haya nimekuwekea faida kumi na kwa kifupi tu ambazo unaweza ukazipitia na kuchukua hatua.

1. Ukisoma vitabu, utakuwa unakua kila siku kimafanikio angalau kwa asilimia moja tu, kuliko ambavyo ungekaa  bila kujifunza kupitia vitabu.
2. Ukiamua kusoma vitabu, itakusaidia kuvunja baadhi ya tabia zako mbaya na zinakupeleka wewe ushindwe, na kutengeneza tabia zaidi za kimafanikio.
3. Vitabu vinakuepusha na kukwepa kufanya makosa , ambayo watu wengi wanayafanya karibu kila siku kwenye safari zao za mafanikio.
4. Kupitia kusoma vitabu, vinakupa hamasa na nguvu ya kusonga mbele zaidi hata pale ambapo kuna wakati unajiona unakosa hamasa, vitabu vinakupa nguvu hiyo.
5. Pia faida nyingine ya vitabu, vinakupa uwezo zaidi wa wewe kuweza kujiamini na kuona kwamba kumbe unaweza kufanya kitu kwenye maisha yako .
6. Vitabu vinasaidia kukutengenezea mfumo mpya wa maisha na ambao hata hukuwa nao, yaani unakuwa unajishangaa unakuwa mpya kila siku iitwapo leo.
7. Kujisomea vitabu pia inasaidia wewe kuweza kutengeneza mazingira ya wazi ambayo yatakusaidia sana kuweza kufanikiwa tofauti na ambavyo kama hujisomei kabisa.
8. Vitabu vinakusaidia wewe kuweza kufanya mabadiliko madogo madogo na kila siku, ambapo mwisho wa siku unashangaa unafika mbali sana kimafanikio.
9. Vitabu vinakupa msukumo wa kurudi kwenye njia kuu hasa pale unapokuwa umetoka kwenye njia kuu hii ni mojawapo ya faida kubwa sana kuijua.
10. Na muhimu zaidi, vitabu vinakufanya wewe unakuwa mtu wa kuchukua hatua zaidi kila siku. Kama ulikiwa unashindwa kuchukua hatua vitabu vinakusukuma kufanya hivyo.
Kwa uchache hizi ni faida ambazo wewe utakazopata kupitia kujisomea, unasubiri nini tena? Washa moto zaidi wa kujisomea.…
.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatimia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, KIENYEJI ASILIA na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.