google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 29, 2015

Kama Hupati Matokeo Mazuri Kwa Kile Unachokifanya, Soma Hapa Kujua Nini Cha Kufanya.

No comments :
Umewahi kuona ama kusikia kuhusu watu waliojaribu bidhaa au kufanya biashara hii na ile na kupata mafanikio makubwa lakini unapojaribu wewe hupati matokeo mazuri? Je, umekuwa mtu anayeona hakuna kitu kinachoweza kukusaidia kupata mafanikio makubwa katika maisha yako? Huenda umekuwa ukijaribu kutumia njia fulani za kuboresha maisha yako, inayoonekana  kuwa nzuri sana, lakini umechoshwa sana na kukwama kila wakati.

Mara kwa mara umekuwa ukijitahidi kufanya hiki na kile lakini umekuwa huoni matokeo hasa ya kile unachokitaka. Kuna wakati umekuwa ukijiuliza pengine una mkosi au nini shida? Na imekuwa ikifika wakati unaanza kujihisi kutaka kukata tamaa kwa kile unachokifanya na kuona kuwa maisha kwako tena basi hayawezekani. Hebu tutazame jinsi unavyoweza kuwa umefikia hatua hiyo uliyopo na sababu zinazoweza kupelekea mambo haya kukutokea.

Kwanza, huenda kuna wakati ulijaribu kitu ama kwa kufuata ushauri, ama maelezo uliyosoma, ama kwa kuona mafanikio ya mtu mwingine. Kimsingi, umejaribu njia hiyo kwa kufuata uzoefu mzuri wa mtu mwingine. Hata hivyo ulipojaribu, hukupata matokeo kama uliyotarajia, ukaamua kuamini kuwa haikukusaidia. Lakini mawazo haya ni kweli kiasi gani? Mara nyingi, tena mara nyingi sana, matokeo ya vitu vya aina moja kwa watu tofauti huwa tofauti na ni kosa kujihukumu na kujilinganisha na watu wengine. Pengine ulihitaji muda zaidi. Huenda mazingira yako ni tofauti kabisa.

Bila kujali hayo na jinsi ulivyofikia, ulijijengea ukweli ndani ya nafsi yako na ukweli huo ni kwamba ‘jambo hili halikukusaidia’ ingawa kwa ukweli wa ndani kabisa, ukweli wako huo uliegemea kwa juu kwenye ulinganifu wako na mtu mwingine na ambaye hauna uhusiano wowote wa moja kwa moja nawe na kile ambacho ni bora kwako. Ni vema ukafahamu pia kwamba matokeo na mafanikio yote hayo unayoyaona kuhusu mtu huyo mwingine, yalikuwa kwa wakati ule uliozungumziwa na hiyo haina maana kwamba sasa ni zamu yako kutumia njia ama ushauri huo na kwamba matokeo mazuri kama yale yatakutokea nawe.


Kuanzia hapo, kila kitu utakachokijaribu kitafananishwa na kuhusishwa na matokeo ya kile cha kwanza, huku ukiwa na ukweli ndani yako ambao mwangwi wake unazidi kuunguruma wa ‘hili halikunisadia mara ya kwanza ngoja tuone safari hii kama litaweza’ tayari unakuwa kama unajipiga vita. Inawezekana hukutarajia kushindwa kwa njia ya moja kwa moja, lakini tayari unauona uwezekano huo na uamuzi wako umeegemea kwenye matokeo mabaya ya mwanzo.

Kwa kadri unavyojaribu mambo mengi ukiwa na mawazo haya, ndivyo unavyozidi kuyajenga mawazo haya ndani yako. Hatimaye inakuwa ni dhana iliyojaa ‘hakuna kitu kitakachosaidia.’ Kabla ya kutambua hilo, hiyo ndiyo aina ya mtu utakayokuwa. Mtu unayejaribu kufikia malengo fulani maalumu ama kujaribu kitu hiki ama kile ama teknolojia ile na kuwa na kauli ndani yake kwamba, ‘wengine wanafanikiwa lakini si mimi’

Sasa nini cha kufanya kama hupati matokeo mazuri kwa kile unachokifanya ukilinganisha na wengine? Ni vipi utaweza kijitoa kutoka kwenye mzunguuko huu? Kwanza, fahamu jinsi ulivyofikia huko, kwa kuilinganisha nafsi yako na matokeo ya watu wengine walioko kwenye njia tofauti kabisa nawe, ingawa huenda walikuwa wakitafuta matokeo kama unayoyataka wewe hivi sasa.

Halafu ujijengee dhana yako. Iruhusu nafsi yako kupata mafanikio kimtindo wake, bila kuamua kwa kuangalia kile kilichowatokea watu wengine, au matakwa yaliyowekwa na watu wengine zaidi yako wewe. Na ni pale utakapoamini kwamba unayo haki ya kufanikiwa, na ni kwamba, na ni kwamba utafanikiwa, ndipo maisha yako yatakapobadilika. Kila utakachokijaribu, kitakusaidia kwa sababu, umefahamu kwamba kinatakiwa kukusaidia wewe na si mtu mwingine.

Subira yako ya ndani na kutokuwa na maamuzi ya kabla ya mafanikio unayotaka, yenye kuegemea nje ya nafsi yako, itafanya kazi kwako kwa nguvu kubwa na utarudiwa na uwezo wako na kuweza kudhibiti mwelekeo wa mambo yako. Lakini kikubwa, jiwekee na wewe malengo yako na kuwa tofauti na kufanya mabadiliko kwa kile unachokifanya ukilinganisha na wengine uliwaona, hii itakusaidia kukuletea matokeo tofatuti katika maisha yako.

Nakutakia kila la kheri katika safari yako ya mafanikio, endelea kutembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kupata maarifa bora, yakayokuwa msaada mkubwa kwa maisha yako.

DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,

IMANI NGWANGWALU,

0713048035/dirayamafanikio@gmail.com






No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.